< Mwanzo 46 >

1 Hivyo Israeli akaondoka na vyote vilivyokuwa mali yake, naye alipofika Beer-Sheba, akamtolea dhabihu Mungu wa Isaki baba yake.
Israel viajou com tudo o que tinha, e veio a Beersheba, e ofereceu sacrifícios ao Deus de seu pai, Isaac.
2 Mungu akanena na Israeli katika maono usiku na kusema, “Yakobo! Yakobo!” Akajibu, “Mimi hapa.”
Deus falou a Israel nas visões da noite, e disse: “Jacó, Jacó! Ele disse: “Aqui estou eu”.
3 Mungu akamwambia, “Mimi ndimi Mungu wa baba yako, usiogope kushuka Misri, kwa maana huko nitakufanya taifa kubwa.
Ele disse: “Eu sou Deus, o Deus de seu pai”. Não tenha medo de descer ao Egito, pois lá eu farei de você uma grande nação”.
4 Nitashuka Misri pamoja nawe, nami hakika nitakurudisha tena Kanaani. Mikono ya Yosefu mwenyewe ndiyo itakayofunga macho yako.”
Eu descerei com vocês no Egito. Certamente também o trarei novamente para cima. A mão de José fechará seus olhos”.
5 Ndipo Yakobo akaondoka Beer-Sheba nao wana wa Israeli wakamchukua baba yao Yakobo na watoto wao na wake zao katika magari ya kukokotwa yale Farao aliyokuwa amempelekea kumsafirisha.
Jacó se levantou de Berseba, e os filhos de Israel carregaram Jacó, seu pai, seus pequenos e suas esposas, nos vagões que o Faraó havia enviado para carregá-lo.
6 Wakachukua pia mifugo yao na mali walizokuwa wamezipata Kanaani, Yakobo na uzao wake wote wakashuka Misri.
Levaram seu gado e seus bens, que haviam conseguido na terra de Canaã, e entraram no Egito-Jacob e toda sua descendência com ele,
7 Akawachukua wanawe na binti zake, wajukuu wake wa kiume na wa kike, yaani uzao wake wote mpaka Misri.
seus filhos, e os filhos de seus filhos com ele, suas filhas e as filhas de seus filhos, e ele trouxe toda sua descendência com ele para o Egito.
8 Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli (Yakobo na wazao wake), waliokwenda Misri: Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Yakobo.
Estes são os nomes dos filhos de Israel, que vieram para o Egito, Jacó e seus filhos: Reuben, o primogênito de Jacó.
9 Wana wa Reubeni ni: Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi.
Os filhos de Rúben: Hanoch, Pallu, Hezron e Carmi.
10 Wana wa Simeoni ni: Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Shauli mwana wa mwanamke Mkanaani.
Os filhos de Simeão: Jemuel, Jamin, Ohad, Jachin, Zohar, e Shaul, filho de uma mulher cananéia.
11 Wana wa Lawi ni: Gershoni, Kohathi na Merari.
Os filhos de Levi: Gershon, Kohath, e Merari.
12 Wana wa Yuda ni: Eri, Onani, Shela, Peresi na Zera (lakini Eri na Onani walifariki katika nchi ya Kanaani). Wana wa Peresi ni: Hesroni na Hamuli.
Os filhos de Judá: Er, Onan, Shelah, Perez e Zerah; mas Er e Onan morreram na terra de Canaã. Os filhos de Perez eram Hezron e Hamul.
13 Wana wa Isakari ni: Tola, Puva, Yashubu na Shimroni.
Os filhos de Issachar: Tola, Puvah, Iob, e Shimron.
14 Wana wa Zabuloni ni: Seredi, Eloni na Yaleeli.
Os filhos de Zebulun: Sered, Elon, e Jahleel.
15 Hawa ndio wana wa Lea aliomzalia Yakobo huko Padan-Aramu pamoja na binti yake Dina. Jumla ya wanawe na binti zake walikuwa thelathini na watatu.
Estes são os filhos de Leah, que ela levou a Jacob em Paddan Aram, com sua filha Dinah. Todas as almas de seus filhos e de suas filhas eram trinta e três.
16 Wana wa Gadi ni: Sefoni, Hagi, Shuni, Esboni, Eri, Arodi na Areli.
Os filhos de Gad: Ziphion, Haggi, Shuni, Ezbon, Eri, Arodi, e Areli.
17 Wana wa Asheri ni: Imna, Ishva, Ishvi na Beria. Dada yao alikuwa Sera. Wana wa Beria ni: Heberi na Malkieli.
Os filhos de Asher: Imnah, Ishvah, Ishvi, Beriah, e Serah, sua irmã. Os filhos de Beriah: Heber e Malchiel.
18 Hawa ndio watoto Zilpa aliomzalia Yakobo, ambao Labani alimpa binti yake Lea; jumla yao walikuwa kumi na sita.
Estes são os filhos de Zilpah, que Laban deu a Leah, sua filha, e estes ela deu a Jacob, até mesmo dezesseis almas.
19 Wana wa Raheli mke wa Yakobo ni: Yosefu na Benyamini.
Os filhos de Raquel, a esposa de Jacó: José e Benjamim.
20 Huko Misri, Asenathi binti wa Potifera, aliyekuwa kuhani wa mji wa Oni, alimzalia Yosefu wana wawili, Manase na Efraimu.
A José na terra do Egito nasceram Manassés e Efraim, que Asenath, filha de Potiphera, sacerdote de On, lhe deu à luz.
21 Wana wa Benyamini ni: Bela, Bekeri, Ashbeli, Gera, Naamani, Ehi, Roshi, Mupimu, Hupimu na Ardi.
Os filhos de Benjamin: Bela, Becher, Ashbel, Gera, Naaman, Ehi, Rosh, Muppim, Huppim e Ard.
22 Hawa ndio wana wa Raheli aliomzalia Yakobo; jumla yao ni kumi na wanne.
Estes são os filhos de Raquel, que nasceram de Jacob: todas as almas eram catorze.
23 Mwana wa Dani ni: Hushimu.
O filho de Dan: Hushim.
24 Wana wa Naftali ni: Yaseeli, Guni, Yeseri na Shilemu.
Os filhos de Naftali: Jahzeel, Guni, Jezer, e Shillem.
25 Hawa walikuwa wana wa Bilha aliomzalia Yakobo, ambaye Labani alikuwa amempa Raheli binti yake; jumla yao walikuwa saba.
Estes são os filhos de Bilhah, que Laban deu a Raquel, sua filha, e estes ela deu a Jacó: todas as almas eram sete.
26 Wote waliokwenda Misri pamoja na Yakobo, waliokuwa wazao wake hasa pasipo kuhesabu wakwe zake, walikuwa watu sitini na sita.
Todas as almas que vieram com Jacó para o Egito, que foram sua descendência direta, além das esposas dos filhos de Jacó, todas as almas eram sessenta e seis.
27 Pamoja na wana wawili waliozaliwa na Yosefu huko Misri, jumla yote ya jamaa ya Yakobo, waliokwenda Misri, walikuwa sabini.
Os filhos de José, que nasceram para ele no Egito, eram duas almas. Todas as almas da casa de Jacó, que entraram no Egito, eram setenta.
28 Basi Yakobo akamtanguliza Yuda aende kwa Yosefu ili amwelekeze njia ya Gosheni. Walipofika nchi ya Gosheni,
Jacó enviou Judá antes dele para José, para mostrar o caminho diante dele para Gósen, e eles vieram para a terra de Gósen.
29 gari kubwa zuri la Yosefu liliandaliwa, naye akaenda Gosheni kumlaki baba yake Israeli. Mara Yosefu alipofika mbele yake, alimkumbatia baba yake, akalia kwa muda mrefu.
José preparou sua carruagem, e subiu ao encontro de Israel, seu pai, em Gósen. Apresentou-se a ele, caiu sobre seu pescoço e chorou um bom tempo no pescoço.
30 Israeli akamwambia Yosefu, “Sasa niko tayari kufa, kwa kuwa nimejionea mwenyewe kwamba bado uko hai.”
Israel disse a José: “Agora deixe-me morrer, já que vi seu rosto, que você ainda está vivo”.
31 Ndipo Yosefu akawaambia ndugu zake na watu wa nyumbani mwa baba yake, “Nitapanda kwa Farao na kumwambia, ‘Ndugu zangu na watu wa nyumbani mwa baba yangu, waliokuwa wakiishi katika nchi ya Kanaani, wamekuja kwangu.
Joseph disse a seus irmãos, e à casa de seu pai: “Subirei, e falarei com o Faraó, e lhe direi: 'Meus irmãos, e a casa de meu pai, que estavam na terra de Canaã, vieram até mim'.
32 Watu hao ni wachunga mifugo, huchunga mifugo, wamekuja na makundi ya kondoo, mbuzi na ngʼombe pamoja na kila kitu walicho nacho.’
Estes homens são pastores, pois foram criadores de gado, e trouxeram seus rebanhos, e seus rebanhos, e tudo o que eles têm”.
33 Farao atakapowaita na kuwaulizeni, ‘Kazi yenu ni nini?’
Acontecerá, quando o Faraó o convocar, e dirá: “Qual é a sua ocupação?
34 Mjibuni, ‘Watumwa wako wamekuwa wachunga mifugo tangu ujana wetu mpaka sasa, kama baba zetu walivyofanya.’ Ndipo mtakaporuhusiwa kukaa katika nchi ya Gosheni, kwa kuwa wachunga mifugo wote ni chukizo kwa Wamisri.”
que você dirá: 'Seus servos têm sido criadores de gado desde nossa juventude até agora, tanto nós como nossos pais:' para que você possa habitar na terra de Gósen; pois cada pastor é uma abominação para os egípcios'.

< Mwanzo 46 >