< Mwanzo 46 >

1 Hivyo Israeli akaondoka na vyote vilivyokuwa mali yake, naye alipofika Beer-Sheba, akamtolea dhabihu Mungu wa Isaki baba yake.
Israël donc partit avec tout ce qu’il avait, vint au Puits du Serment; et là, des victimes immolées au Dieu de son père Isaac,
2 Mungu akanena na Israeli katika maono usiku na kusema, “Yakobo! Yakobo!” Akajibu, “Mimi hapa.”
Il l’entendit dans une vision de la nuit, l’appelant et lui disant: Jacob, Jacob. Il lui répondit: Me voici.
3 Mungu akamwambia, “Mimi ndimi Mungu wa baba yako, usiogope kushuka Misri, kwa maana huko nitakufanya taifa kubwa.
Dieu lui dit: Je suis le Dieu très fort de ton père; ne crains point, descends en Égypte, parce que je te ferai père d’une grande nation en ce pays.
4 Nitashuka Misri pamoja nawe, nami hakika nitakurudisha tena Kanaani. Mikono ya Yosefu mwenyewe ndiyo itakayofunga macho yako.”
Moi-même je descendrai là avec toi, et moi-même je t’en ramènerai, lorsque tu en reviendras: et Joseph posera ses mains sur tes yeux.
5 Ndipo Yakobo akaondoka Beer-Sheba nao wana wa Israeli wakamchukua baba yao Yakobo na watoto wao na wake zao katika magari ya kukokotwa yale Farao aliyokuwa amempelekea kumsafirisha.
Jacob donc se leva du Puits du Serment, et ses fils le portèrent avec leurs petits enfants et leurs femmes sur les chars que Pharaon avait envoyés pour transporter le vieillard.
6 Wakachukua pia mifugo yao na mali walizokuwa wamezipata Kanaani, Yakobo na uzao wake wote wakashuka Misri.
Et tout ce qu’il possédait dans la terre de Chanaan: il arriva donc en Égypte avec toute sa lignée,
7 Akawachukua wanawe na binti zake, wajukuu wake wa kiume na wa kike, yaani uzao wake wote mpaka Misri.
Ses fils, ses petits-fils, ses filles et toute sa race ensemble.
8 Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli (Yakobo na wazao wake), waliokwenda Misri: Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Yakobo.
Or voici les noms des fils d’Israël, qui entrèrent en Égypte, lorsqu’il vint avec ses enfants. Le premier-né était Ruben.
9 Wana wa Reubeni ni: Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi.
Les fils de Ruben: Hénoch, Phallu, Hesron et Charmi.
10 Wana wa Simeoni ni: Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Shauli mwana wa mwanamke Mkanaani.
Les fils de Siméon: Jamuel, Jamin, Ahod, Jachin, Sohar et Saül fils d’une Chananéenne.
11 Wana wa Lawi ni: Gershoni, Kohathi na Merari.
Les fils de Lévi: Gerson, Caath et Mérari.
12 Wana wa Yuda ni: Eri, Onani, Shela, Peresi na Zera (lakini Eri na Onani walifariki katika nchi ya Kanaani). Wana wa Peresi ni: Hesroni na Hamuli.
Les fils de Juda: Her, Onan, Séla, Pharès et Zara; mais Her et Onan moururent dans le pays de Chanaan. Et naquirent à Pharès, les fils Hesron et Hamul.
13 Wana wa Isakari ni: Tola, Puva, Yashubu na Shimroni.
Les fils d’Issachar: Thola, Phua, Job et Semron.
14 Wana wa Zabuloni ni: Seredi, Eloni na Yaleeli.
Les fils de Zabulon: Sared, Elon et Jahélel.
15 Hawa ndio wana wa Lea aliomzalia Yakobo huko Padan-Aramu pamoja na binti yake Dina. Jumla ya wanawe na binti zake walikuwa thelathini na watatu.
Ce sont là les fils de Lia qu’elle enfanta en Mésopotamie de Syrie, avec Dina sa fille; toutes les âmes de ses fils et de ses filles furent trente-trois.
16 Wana wa Gadi ni: Sefoni, Hagi, Shuni, Esboni, Eri, Arodi na Areli.
Les fils de Gad: Séphion, Haggi, Suni, Esébon, Héri, Arodi et Aréli.
17 Wana wa Asheri ni: Imna, Ishva, Ishvi na Beria. Dada yao alikuwa Sera. Wana wa Beria ni: Heberi na Malkieli.
Les fils d’Aser: Jamné, Jésua, Jessui et Béria, et aussi Sara leur sœur. Les fils de Béria: Héber et Melchiel.
18 Hawa ndio watoto Zilpa aliomzalia Yakobo, ambao Labani alimpa binti yake Lea; jumla yao walikuwa kumi na sita.
Ce sont là les fils de Zelpha que donna Laban à Lia sa fille, et qui les enfanta à Jacob: seize âmes.
19 Wana wa Raheli mke wa Yakobo ni: Yosefu na Benyamini.
Les fils de Rachel femme de Jacob: Joseph et Benjamin.
20 Huko Misri, Asenathi binti wa Potifera, aliyekuwa kuhani wa mji wa Oni, alimzalia Yosefu wana wawili, Manase na Efraimu.
Et il naquit à Joseph dans la terre d’Égypte des fils que lui enfanta Aseneth, fille de Putiphar, prêtre d’Héliopolis: Manassé et Ephraïm.
21 Wana wa Benyamini ni: Bela, Bekeri, Ashbeli, Gera, Naamani, Ehi, Roshi, Mupimu, Hupimu na Ardi.
Les fils de Benjamin: Béla, Béchor, Asbel, Géra, Naaman, Echi, Ros, Mophim, Ophim, et Ared.
22 Hawa ndio wana wa Raheli aliomzalia Yakobo; jumla yao ni kumi na wanne.
Ce sont là les fils de Rachel qu’elle engendra à Jacob: en tout quatorze âmes.
23 Mwana wa Dani ni: Hushimu.
Les fils de Dan: Husim.
24 Wana wa Naftali ni: Yaseeli, Guni, Yeseri na Shilemu.
Les fils de Nephtali: Jasiel, Guni, Jéser et Sallem.
25 Hawa walikuwa wana wa Bilha aliomzalia Yakobo, ambaye Labani alikuwa amempa Raheli binti yake; jumla yao walikuwa saba.
Ce sont là les fils de Bala que donna Laban à Rachel sa fille, et qu’elle enfanta à Jacob en tout sept âmes.
26 Wote waliokwenda Misri pamoja na Yakobo, waliokuwa wazao wake hasa pasipo kuhesabu wakwe zake, walikuwa watu sitini na sita.
Toutes les âmes qui entrèrent avec Jacob en Égypte, et qui étaient issues de lui, sans les femmes de ses fils, furent soixante-six;
27 Pamoja na wana wawili waliozaliwa na Yosefu huko Misri, jumla yote ya jamaa ya Yakobo, waliokwenda Misri, walikuwa sabini.
Mais les fils de Joseph qui lui naquirent dans la terre d’Égypte, deux âmes. Toutes les âmes de la maison de Jacob qui entrèrent en Égypte, furent soixante-dix.
28 Basi Yakobo akamtanguliza Yuda aende kwa Yosefu ili amwelekeze njia ya Gosheni. Walipofika nchi ya Gosheni,
Or Jacob envoya Juda devant lui vers Joseph, afin qu’on l’avertît, et qu’il vînt à sa rencontre dans la terre de Gessen.
29 gari kubwa zuri la Yosefu liliandaliwa, naye akaenda Gosheni kumlaki baba yake Israeli. Mara Yosefu alipofika mbele yake, alimkumbatia baba yake, akalia kwa muda mrefu.
Lorsqu’il y fut arrivé, Joseph, son char attelé, monta au même lieu à la rencontre de son père; et le voyant, il se jeta à son cou, et, au milieu des embrassements, il pleura.
30 Israeli akamwambia Yosefu, “Sasa niko tayari kufa, kwa kuwa nimejionea mwenyewe kwamba bado uko hai.”
Et le père dit à Joseph: Maintenant je mourrai joyeux, puisque j’ai vu ta face, et que je te laisse vivant après moi.
31 Ndipo Yosefu akawaambia ndugu zake na watu wa nyumbani mwa baba yake, “Nitapanda kwa Farao na kumwambia, ‘Ndugu zangu na watu wa nyumbani mwa baba yangu, waliokuwa wakiishi katika nchi ya Kanaani, wamekuja kwangu.
Mais Joseph dit à ses frères et à toute la maison de son père: Je monterai et je porterai la nouvelle à Pharaon, et je lui dirai: Mes frères et la maison de mon père qui étaient dans la terre de Chanaan, sont venus vers moi.
32 Watu hao ni wachunga mifugo, huchunga mifugo, wamekuja na makundi ya kondoo, mbuzi na ngʼombe pamoja na kila kitu walicho nacho.’
Ce sont des hommes pasteurs de brebis, et ils ont soin d’élever des troupeaux; leur menu et leur gros bétail et tout ce qu’ils pouvaient avoir, ils l’ont amené avec eux.
33 Farao atakapowaita na kuwaulizeni, ‘Kazi yenu ni nini?’
Lors donc qu’il vous appellera et demandera: Quelle est votre occupation?
34 Mjibuni, ‘Watumwa wako wamekuwa wachunga mifugo tangu ujana wetu mpaka sasa, kama baba zetu walivyofanya.’ Ndipo mtakaporuhusiwa kukaa katika nchi ya Gosheni, kwa kuwa wachunga mifugo wote ni chukizo kwa Wamisri.”
Vous répondrez: Nous vos serviteurs, nous sommes des hommes pasteurs depuis notre enfance jusqu’à présent, et nous et nos pères. Or vous direz cela, afin que vous puissiez demeurer dans la terre de Gessen; car les Égyptiens détestent tous les pasteurs de brebis.

< Mwanzo 46 >