< Mwanzo 46 >
1 Hivyo Israeli akaondoka na vyote vilivyokuwa mali yake, naye alipofika Beer-Sheba, akamtolea dhabihu Mungu wa Isaki baba yake.
Israël partit avec tout ce qui lui appartenait. Arrivé à Bersabée, il offrit des sacrifices au Dieu de son père Isaac.
2 Mungu akanena na Israeli katika maono usiku na kusema, “Yakobo! Yakobo!” Akajibu, “Mimi hapa.”
Et Dieu parla à Israël dans une vision de nuit, et il dit: « Jacob! Jacob! » Israël répondit: « Me voici. »
3 Mungu akamwambia, “Mimi ndimi Mungu wa baba yako, usiogope kushuka Misri, kwa maana huko nitakufanya taifa kubwa.
Et Dieu dit: « Je suis le Dieu fort, le Dieu de ton père. Ne crains point de descendre en Égypte, car là je te ferai devenir une grande nation.
4 Nitashuka Misri pamoja nawe, nami hakika nitakurudisha tena Kanaani. Mikono ya Yosefu mwenyewe ndiyo itakayofunga macho yako.”
Moi-même je descendrai avec toi en Égypte, et moi-même aussi je t’en ferai sûrement remonter; et Joseph posera sa main sur tes yeux. »
5 Ndipo Yakobo akaondoka Beer-Sheba nao wana wa Israeli wakamchukua baba yao Yakobo na watoto wao na wake zao katika magari ya kukokotwa yale Farao aliyokuwa amempelekea kumsafirisha.
Jacob, se levant, quitta Bersabée; et les fils d’Israël mirent Jacob, leur père, ainsi que leurs femmes et leurs enfants, sur les chariots que Pharaon avait envoyés pour le transporter.
6 Wakachukua pia mifugo yao na mali walizokuwa wamezipata Kanaani, Yakobo na uzao wake wote wakashuka Misri.
Ils prirent aussi leurs troupeaux et leurs biens qu’ils avaient acquis dans le pays de Chanaan. Et Jacob se rendit en Égypte avec toute sa famille.
7 Akawachukua wanawe na binti zake, wajukuu wake wa kiume na wa kike, yaani uzao wake wote mpaka Misri.
Il emmena avec lui en Égypte ses fils et les fils de ses fils, ses filles et les filles de ses fils, et toute sa famille.
8 Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli (Yakobo na wazao wake), waliokwenda Misri: Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Yakobo.
Voici les noms des fils d’Israël qui vinrent en Égypte: Jacob et ses fils. — Premier-né de Jacob, Ruben. —
9 Wana wa Reubeni ni: Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi.
Fils de Ruben: Hénoch, Phallu, Hesron et Charmi. —
10 Wana wa Simeoni ni: Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Shauli mwana wa mwanamke Mkanaani.
Fils de Siméon: Jamuel, Jamin, Ahod, Jachin et Sohar, et Saul, fils de la Chananéenne. —
11 Wana wa Lawi ni: Gershoni, Kohathi na Merari.
Fils de Lévi: Gerson, Caat et Mérari. —
12 Wana wa Yuda ni: Eri, Onani, Shela, Peresi na Zera (lakini Eri na Onani walifariki katika nchi ya Kanaani). Wana wa Peresi ni: Hesroni na Hamuli.
Fils de Juda: Her, Onan, Séla, Pharès et Zara; mais Her et Onan étaient morts au pays de Chanaan. Les fils de Pharès furent Hesron et Hamul. —
13 Wana wa Isakari ni: Tola, Puva, Yashubu na Shimroni.
Fils d’Issachar: Thola, Phua, Job et Semron. —
14 Wana wa Zabuloni ni: Seredi, Eloni na Yaleeli.
Fils de Zabulon: Sared, Elon et Jahélel —
15 Hawa ndio wana wa Lea aliomzalia Yakobo huko Padan-Aramu pamoja na binti yake Dina. Jumla ya wanawe na binti zake walikuwa thelathini na watatu.
Ce sont là les fils que Lia enfanta à Jacob à Paddan-Aram, avec sa fille Dina. Ses fils et ses filles étaient en tout trente-trois personnes.
16 Wana wa Gadi ni: Sefoni, Hagi, Shuni, Esboni, Eri, Arodi na Areli.
Fils de Gad: Séphion, Haggi, Suni, Esebon, Heri, Arodi et Aréli. —
17 Wana wa Asheri ni: Imna, Ishva, Ishvi na Beria. Dada yao alikuwa Sera. Wana wa Beria ni: Heberi na Malkieli.
Fils d’Aser: Jamné, Jésua, Jessui et Béria, et Sara, leur sœur. Les fils de Béria furent Héber et Melchiel. —
18 Hawa ndio watoto Zilpa aliomzalia Yakobo, ambao Labani alimpa binti yake Lea; jumla yao walikuwa kumi na sita.
Ce sont là les fils de Zelpha, que Laban avait donnée à Lia, sa fille; et elle les enfanta à Jacob: en tout seize personnes.
19 Wana wa Raheli mke wa Yakobo ni: Yosefu na Benyamini.
Fils de Rachel, femme de Jacob: Joseph et Benjamin.
20 Huko Misri, Asenathi binti wa Potifera, aliyekuwa kuhani wa mji wa Oni, alimzalia Yosefu wana wawili, Manase na Efraimu.
Il naquit à Joseph, au pays d’Égypte, des fils que lui enfanta Aseneth, fille de Putiphar, prêtre d’On, savoir Manassé et Ephraïm. —
21 Wana wa Benyamini ni: Bela, Bekeri, Ashbeli, Gera, Naamani, Ehi, Roshi, Mupimu, Hupimu na Ardi.
Fils de Benjamin: Béla, Bochor, Asbel, Géra, Naaman, Echi, Ros, Mophim, Ophim et Ared. —
22 Hawa ndio wana wa Raheli aliomzalia Yakobo; jumla yao ni kumi na wanne.
Ce sont là les fils de Rachel, qui naquirent à Jacob: en tout quatorze personnes.
23 Mwana wa Dani ni: Hushimu.
Fils de Dan: Husim. —
24 Wana wa Naftali ni: Yaseeli, Guni, Yeseri na Shilemu.
Fils de Nephtali: Jasiel, Guni, Jéser et Salem. —
25 Hawa walikuwa wana wa Bilha aliomzalia Yakobo, ambaye Labani alikuwa amempa Raheli binti yake; jumla yao walikuwa saba.
Ce sont là les fils de Bala, que Laban avait donnée à Rachel, sa fille; et elle les enfanta à Jacob: en tout sept personnes.
26 Wote waliokwenda Misri pamoja na Yakobo, waliokuwa wazao wake hasa pasipo kuhesabu wakwe zake, walikuwa watu sitini na sita.
Toutes les personnes qui vinrent avec Jacob en Égypte, issues de lui, sans compter les femmes des fils de Jacob, étaient au nombre de soixante-six en tout.
27 Pamoja na wana wawili waliozaliwa na Yosefu huko Misri, jumla yote ya jamaa ya Yakobo, waliokwenda Misri, walikuwa sabini.
Les fils de Joseph qui lui étaient nés en Égypte étaient deux. — Le total des personnes de la famille de Jacob qui vinrent en Égypte était de soixante-dix.
28 Basi Yakobo akamtanguliza Yuda aende kwa Yosefu ili amwelekeze njia ya Gosheni. Walipofika nchi ya Gosheni,
Jacob avait envoyé Juda devant lui vers Joseph pour préparer son arrivée en Gessen. Lorsque Jacob et les siens furent entrés en Gessen,
29 gari kubwa zuri la Yosefu liliandaliwa, naye akaenda Gosheni kumlaki baba yake Israeli. Mara Yosefu alipofika mbele yake, alimkumbatia baba yake, akalia kwa muda mrefu.
Joseph fit atteler son char et y monta, pour aller en Gessen, à la rencontre d’Israël, son père. Il se montra à lui et, s’étant jeté à son cou, il pleura longtemps sur son cou.
30 Israeli akamwambia Yosefu, “Sasa niko tayari kufa, kwa kuwa nimejionea mwenyewe kwamba bado uko hai.”
Israël dit à Joseph: « Je puis mourir maintenant, puisque j’ai vu ton visage et que tu vis encore! »
31 Ndipo Yosefu akawaambia ndugu zake na watu wa nyumbani mwa baba yake, “Nitapanda kwa Farao na kumwambia, ‘Ndugu zangu na watu wa nyumbani mwa baba yangu, waliokuwa wakiishi katika nchi ya Kanaani, wamekuja kwangu.
Joseph dit à ses frères et à la famille de son père: « Je vais avertir Pharaon et je lui dirai: Mes frères et la famille de mon père, qui étaient au pays de Chanaan, sont venus vers moi.
32 Watu hao ni wachunga mifugo, huchunga mifugo, wamekuja na makundi ya kondoo, mbuzi na ngʼombe pamoja na kila kitu walicho nacho.’
Ces hommes font paître des brebis, car ce sont des propriétaires de troupeaux; ils ont amené leurs brebis et leurs bœufs, et tout ce qui leur appartient.
33 Farao atakapowaita na kuwaulizeni, ‘Kazi yenu ni nini?’
Et quand Pharaon vous appellera et dira: Quelle est votre occupation?
34 Mjibuni, ‘Watumwa wako wamekuwa wachunga mifugo tangu ujana wetu mpaka sasa, kama baba zetu walivyofanya.’ Ndipo mtakaporuhusiwa kukaa katika nchi ya Gosheni, kwa kuwa wachunga mifugo wote ni chukizo kwa Wamisri.”
vous répondrez: Nous, tes serviteurs, sommes des propriétaires de troupeaux depuis notre jeunesse jusqu’à présent comme l’étaient nos pères. De cette manière vous habiterez dans le pays de Gessen, car tous les bergers sont en abomination aux Égyptiens. »