< Mwanzo 46 >
1 Hivyo Israeli akaondoka na vyote vilivyokuwa mali yake, naye alipofika Beer-Sheba, akamtolea dhabihu Mungu wa Isaki baba yake.
and to set out Israel and all which to/for him and to come (in): come Beersheba [to] Beersheba and to sacrifice sacrifice to/for God father his Isaac
2 Mungu akanena na Israeli katika maono usiku na kusema, “Yakobo! Yakobo!” Akajibu, “Mimi hapa.”
and to say God to/for Israel in/on/with vision [the] night and to say Jacob Jacob and to say behold I
3 Mungu akamwambia, “Mimi ndimi Mungu wa baba yako, usiogope kushuka Misri, kwa maana huko nitakufanya taifa kubwa.
and to say I [the] God God father your not to fear from to go down Egypt [to] for to/for nation great: large to set: make you there
4 Nitashuka Misri pamoja nawe, nami hakika nitakurudisha tena Kanaani. Mikono ya Yosefu mwenyewe ndiyo itakayofunga macho yako.”
I to go down with you Egypt [to] and I to ascend: establish you also to ascend: establish and Joseph to set: put hand: power his upon eye your
5 Ndipo Yakobo akaondoka Beer-Sheba nao wana wa Israeli wakamchukua baba yao Yakobo na watoto wao na wake zao katika magari ya kukokotwa yale Farao aliyokuwa amempelekea kumsafirisha.
and to arise: rise Jacob from Beersheba Beersheba and to lift: bear son: child Israel [obj] Jacob father their and [obj] child their and [obj] woman: wife their in/on/with cart which to send: depart Pharaoh to/for to lift: bear [obj] him
6 Wakachukua pia mifugo yao na mali walizokuwa wamezipata Kanaani, Yakobo na uzao wake wote wakashuka Misri.
and to take: take [obj] livestock their and [obj] property their which to gather in/on/with land: country/planet Canaan and to come (in): come Egypt [to] Jacob and all seed: children his with him
7 Akawachukua wanawe na binti zake, wajukuu wake wa kiume na wa kike, yaani uzao wake wote mpaka Misri.
son: child his and son: child son: child his with him daughter his and daughter son: child his and all seed: children his to come (in): bring with him Egypt [to]
8 Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli (Yakobo na wazao wake), waliokwenda Misri: Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Yakobo.
and these name son: descendant/people Israel [the] to come (in): come Egypt [to] Jacob and son: child his firstborn Jacob Reuben
9 Wana wa Reubeni ni: Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi.
and son: child Reuben Hanoch and Pallu and Hezron and Carmi
10 Wana wa Simeoni ni: Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Shauli mwana wa mwanamke Mkanaani.
and son: child Simeon Jemuel and Jamin and Ohad and Jachin and Zohar and Shaul son: child [the] Canaanitess
11 Wana wa Lawi ni: Gershoni, Kohathi na Merari.
and son: child Levi Gershon Kohath and Merari
12 Wana wa Yuda ni: Eri, Onani, Shela, Peresi na Zera (lakini Eri na Onani walifariki katika nchi ya Kanaani). Wana wa Peresi ni: Hesroni na Hamuli.
and son: child Judah Er and Onan and Shelah and Perez and Zerah and to die Er and Onan in/on/with land: country/planet Canaan and to be son: child Perez Hezron and Hamul
13 Wana wa Isakari ni: Tola, Puva, Yashubu na Shimroni.
and son: child Issachar Tola and Puah and Yob and Shimron
14 Wana wa Zabuloni ni: Seredi, Eloni na Yaleeli.
and son: child Zebulun Sered and Elon and Jahleel
15 Hawa ndio wana wa Lea aliomzalia Yakobo huko Padan-Aramu pamoja na binti yake Dina. Jumla ya wanawe na binti zake walikuwa thelathini na watatu.
these son: child Leah which to beget to/for Jacob in/on/with Paddan (Paddan)-aram and with Dinah daughter his all soul: person son: child his and daughter his thirty and three
16 Wana wa Gadi ni: Sefoni, Hagi, Shuni, Esboni, Eri, Arodi na Areli.
and son: child Gad Ziphion and Haggi Shuni and Ezbon Eri and Arodi and Areli
17 Wana wa Asheri ni: Imna, Ishva, Ishvi na Beria. Dada yao alikuwa Sera. Wana wa Beria ni: Heberi na Malkieli.
and son: child Asher Imnah and Ishvah and Ishvi and Beriah and Serah sister their and son: child Beriah Heber and Malchiel
18 Hawa ndio watoto Zilpa aliomzalia Yakobo, ambao Labani alimpa binti yake Lea; jumla yao walikuwa kumi na sita.
these son: child Zilpah which to give: give Laban to/for Leah daughter his and to beget [obj] these to/for Jacob six ten soul: person
19 Wana wa Raheli mke wa Yakobo ni: Yosefu na Benyamini.
son: child Rachel woman: wife Jacob Joseph and Benjamin
20 Huko Misri, Asenathi binti wa Potifera, aliyekuwa kuhani wa mji wa Oni, alimzalia Yosefu wana wawili, Manase na Efraimu.
and to beget to/for Joseph in/on/with land: country/planet Egypt which to beget to/for him Asenath daughter Potiphera Potiphera priest On [obj] Manasseh and [obj] Ephraim
21 Wana wa Benyamini ni: Bela, Bekeri, Ashbeli, Gera, Naamani, Ehi, Roshi, Mupimu, Hupimu na Ardi.
and son: child Benjamin Bela and Becher and Ashbel Gera and Naaman Ehi and Rosh Muppim and Huppim and Ard
22 Hawa ndio wana wa Raheli aliomzalia Yakobo; jumla yao ni kumi na wanne.
these son: child Rachel which to beget to/for Jacob all soul: person four ten
23 Mwana wa Dani ni: Hushimu.
and son: child Dan Hushim
24 Wana wa Naftali ni: Yaseeli, Guni, Yeseri na Shilemu.
and son: child Naphtali Jahzeel and Guni and Jezer and Shillem
25 Hawa walikuwa wana wa Bilha aliomzalia Yakobo, ambaye Labani alikuwa amempa Raheli binti yake; jumla yao walikuwa saba.
these son: child Bilhah which to give: give Laban to/for Rachel daughter his and to beget [obj] these to/for Jacob all soul: person seven
26 Wote waliokwenda Misri pamoja na Yakobo, waliokuwa wazao wake hasa pasipo kuhesabu wakwe zake, walikuwa watu sitini na sita.
all [the] soul: person [the] to come (in): come to/for Jacob Egypt [to] to come out: produce thigh his from to/for alone: besides woman: wife son: child Jacob all soul: person sixty and six
27 Pamoja na wana wawili waliozaliwa na Yosefu huko Misri, jumla yote ya jamaa ya Yakobo, waliokwenda Misri, walikuwa sabini.
and son: child Joseph which to beget to/for him in/on/with Egypt soul: person two all [the] soul: person to/for house: household Jacob [the] to come (in): come Egypt [to] seventy
28 Basi Yakobo akamtanguliza Yuda aende kwa Yosefu ili amwelekeze njia ya Gosheni. Walipofika nchi ya Gosheni,
and [obj] Judah to send: depart to/for face: before his to(wards) Joseph to/for to show to/for face: before his Goshen [to] and to come (in): come land: country/planet [to] Goshen
29 gari kubwa zuri la Yosefu liliandaliwa, naye akaenda Gosheni kumlaki baba yake Israeli. Mara Yosefu alipofika mbele yake, alimkumbatia baba yake, akalia kwa muda mrefu.
and to bind Joseph chariot his and to ascend: rise to/for to encounter: meet Israel father his Goshen [to] and to see: see to(wards) him and to fall: fall upon neck his and to weep upon neck his still
30 Israeli akamwambia Yosefu, “Sasa niko tayari kufa, kwa kuwa nimejionea mwenyewe kwamba bado uko hai.”
and to say Israel to(wards) Joseph to die [the] beat after to see: see I [obj] face your for still you alive
31 Ndipo Yosefu akawaambia ndugu zake na watu wa nyumbani mwa baba yake, “Nitapanda kwa Farao na kumwambia, ‘Ndugu zangu na watu wa nyumbani mwa baba yangu, waliokuwa wakiishi katika nchi ya Kanaani, wamekuja kwangu.
and to say Joseph to(wards) brother: male-sibling his and to(wards) house: household father his to ascend: rise and to tell to/for Pharaoh and to say to(wards) him brother: male-sibling my and house: household father my which in/on/with land: country/planet Canaan to come (in): come to(wards) me
32 Watu hao ni wachunga mifugo, huchunga mifugo, wamekuja na makundi ya kondoo, mbuzi na ngʼombe pamoja na kila kitu walicho nacho.’
and [the] human to pasture flock for human livestock to be and flock their and cattle their and all which to/for them to come (in): bring
33 Farao atakapowaita na kuwaulizeni, ‘Kazi yenu ni nini?’
and to be for to call: call to to/for you Pharaoh and to say what? deed: work your
34 Mjibuni, ‘Watumwa wako wamekuwa wachunga mifugo tangu ujana wetu mpaka sasa, kama baba zetu walivyofanya.’ Ndipo mtakaporuhusiwa kukaa katika nchi ya Gosheni, kwa kuwa wachunga mifugo wote ni chukizo kwa Wamisri.”
and to say human livestock to be servant/slave your from youth our and till now also we also father our in/on/with for the sake of to dwell in/on/with land: country/planet Goshen for abomination Egyptian all to pasture flock