< Mwanzo 46 >
1 Hivyo Israeli akaondoka na vyote vilivyokuwa mali yake, naye alipofika Beer-Sheba, akamtolea dhabihu Mungu wa Isaki baba yake.
And Israel took his journey with all that he had, and came to Beer-sheba; and he offered sacrifices to the God of his father Isaac.
2 Mungu akanena na Israeli katika maono usiku na kusema, “Yakobo! Yakobo!” Akajibu, “Mimi hapa.”
And God spoke to Israel in the visions of the night and said, Jacob, Jacob! And he said, Here am I.
3 Mungu akamwambia, “Mimi ndimi Mungu wa baba yako, usiogope kushuka Misri, kwa maana huko nitakufanya taifa kubwa.
And he said, I am God, the God of thy father: fear not to go down to Egypt; for I will there make of thee a great nation.
4 Nitashuka Misri pamoja nawe, nami hakika nitakurudisha tena Kanaani. Mikono ya Yosefu mwenyewe ndiyo itakayofunga macho yako.”
I will go down with thee to Egypt, and I will also certainly bring thee up; and Joseph shall put his hand on thine eyes.
5 Ndipo Yakobo akaondoka Beer-Sheba nao wana wa Israeli wakamchukua baba yao Yakobo na watoto wao na wake zao katika magari ya kukokotwa yale Farao aliyokuwa amempelekea kumsafirisha.
And Jacob rose up from Beer-sheba; and the sons of Israel carried Jacob their father, and their little ones, and their wives, on the waggons that Pharaoh had sent to carry him.
6 Wakachukua pia mifugo yao na mali walizokuwa wamezipata Kanaani, Yakobo na uzao wake wote wakashuka Misri.
And they took their cattle, and their goods which they had acquired in the land of Canaan, and came to Egypt, Jacob and all his seed with him;
7 Akawachukua wanawe na binti zake, wajukuu wake wa kiume na wa kike, yaani uzao wake wote mpaka Misri.
his sons and his sons' sons with him, his daughters and his sons' daughters and all his seed he brought with him to Egypt.
8 Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli (Yakobo na wazao wake), waliokwenda Misri: Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Yakobo.
And these are the names of the sons of Israel who came into Egypt: Jacob and his sons. Jacob's firstborn, Reuben.
9 Wana wa Reubeni ni: Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi.
And the sons of Reuben: Enoch, and Phallu, and Hezron, and Carmi.
10 Wana wa Simeoni ni: Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Shauli mwana wa mwanamke Mkanaani.
— And the sons of Simeon: Jemuel, and Jamin, and Ohad, and Jachin, and Zohar, and Saul the son of a Canaanitish woman.
11 Wana wa Lawi ni: Gershoni, Kohathi na Merari.
— And the sons of Levi: Gershon, Kohath, and Merari.
12 Wana wa Yuda ni: Eri, Onani, Shela, Peresi na Zera (lakini Eri na Onani walifariki katika nchi ya Kanaani). Wana wa Peresi ni: Hesroni na Hamuli.
— And the sons of Judah: Er, and Onan, and Shelah, and Pherez, and Zerah; but Er and Onan died in the land of Canaan. And the sons of Pherez were Hezron and Hamul.
13 Wana wa Isakari ni: Tola, Puva, Yashubu na Shimroni.
— And the sons of Issachar: Tola, and Puah, and Job, and Shimron.
14 Wana wa Zabuloni ni: Seredi, Eloni na Yaleeli.
— And the sons of Zebulun: Sered, and Elon, and Jahleel.
15 Hawa ndio wana wa Lea aliomzalia Yakobo huko Padan-Aramu pamoja na binti yake Dina. Jumla ya wanawe na binti zake walikuwa thelathini na watatu.
— These are the sons of Leah, whom she bore to Jacob in Padan-Aram; and his daughter, Dinah. All the souls of his sons and his daughters were thirty-three.
16 Wana wa Gadi ni: Sefoni, Hagi, Shuni, Esboni, Eri, Arodi na Areli.
And the sons of Gad: Ziphion and Haggi, Shuni and Ezbon, Eri, and Arodi, and Areli.
17 Wana wa Asheri ni: Imna, Ishva, Ishvi na Beria. Dada yao alikuwa Sera. Wana wa Beria ni: Heberi na Malkieli.
— And the sons of Asher: Jimnah, and Jishvah, and Jishvi, and Beriah; and Serah their sister; and the sons of Beriah: Heber and Malchiel.
18 Hawa ndio watoto Zilpa aliomzalia Yakobo, ambao Labani alimpa binti yake Lea; jumla yao walikuwa kumi na sita.
— These are the sons of Zilpah, whom Laban gave to Leah his daughter; and she bore these to Jacob: sixteen souls.
19 Wana wa Raheli mke wa Yakobo ni: Yosefu na Benyamini.
The sons of Rachel Jacob's wife: Joseph and Benjamin.
20 Huko Misri, Asenathi binti wa Potifera, aliyekuwa kuhani wa mji wa Oni, alimzalia Yosefu wana wawili, Manase na Efraimu.
And to Joseph in the land of Egypt were born Manasseh and Ephraim, whom Asnath bore to him, the daughter of Potipherah the priest in On.
21 Wana wa Benyamini ni: Bela, Bekeri, Ashbeli, Gera, Naamani, Ehi, Roshi, Mupimu, Hupimu na Ardi.
— And the sons of Benjamin: Belah, and Becher, and Ashbel, Gera and Naaman, Ehi and Rosh, Muppim, and Huppim, and Ard.
22 Hawa ndio wana wa Raheli aliomzalia Yakobo; jumla yao ni kumi na wanne.
— These are the sons of Rachel who were born to Jacob: all the souls were fourteen.
23 Mwana wa Dani ni: Hushimu.
And the sons of Dan: Hushim.
24 Wana wa Naftali ni: Yaseeli, Guni, Yeseri na Shilemu.
— And the sons of Naphtali: Jahzeel, and Guni, and Jezer, and Shillem.
25 Hawa walikuwa wana wa Bilha aliomzalia Yakobo, ambaye Labani alikuwa amempa Raheli binti yake; jumla yao walikuwa saba.
— These are the sons of Bilhah, whom Laban gave to Rachel his daughter; and she bore these to Jacob: all the souls were seven.
26 Wote waliokwenda Misri pamoja na Yakobo, waliokuwa wazao wake hasa pasipo kuhesabu wakwe zake, walikuwa watu sitini na sita.
All the souls that came with Jacob to Egypt, that had come out of his loins, besides Jacob's sons' wives: all the souls were sixty-six.
27 Pamoja na wana wawili waliozaliwa na Yosefu huko Misri, jumla yote ya jamaa ya Yakobo, waliokwenda Misri, walikuwa sabini.
And the sons of Joseph who were born to him in Egypt, were two souls. All the souls of the house of Jacob that came to Egypt were seventy.
28 Basi Yakobo akamtanguliza Yuda aende kwa Yosefu ili amwelekeze njia ya Gosheni. Walipofika nchi ya Gosheni,
And he sent Judah before him to Joseph, to give notice before he came to Goshen. And they came into the land of Goshen.
29 gari kubwa zuri la Yosefu liliandaliwa, naye akaenda Gosheni kumlaki baba yake Israeli. Mara Yosefu alipofika mbele yake, alimkumbatia baba yake, akalia kwa muda mrefu.
Then Joseph yoked his chariot, and went up to meet Israel his father, to Goshen, and he presented himself to him; and he fell on his neck, and wept on his neck a good while.
30 Israeli akamwambia Yosefu, “Sasa niko tayari kufa, kwa kuwa nimejionea mwenyewe kwamba bado uko hai.”
And Israel said to Joseph, Now let me die, after I have seen thy face, since thou still livest.
31 Ndipo Yosefu akawaambia ndugu zake na watu wa nyumbani mwa baba yake, “Nitapanda kwa Farao na kumwambia, ‘Ndugu zangu na watu wa nyumbani mwa baba yangu, waliokuwa wakiishi katika nchi ya Kanaani, wamekuja kwangu.
And Joseph said to his brethren and to his father's house, I will go up, and tell Pharaoh, and say to him, My brethren and my father's house, who were in the land of Canaan, are come to me;
32 Watu hao ni wachunga mifugo, huchunga mifugo, wamekuja na makundi ya kondoo, mbuzi na ngʼombe pamoja na kila kitu walicho nacho.’
and the men are shepherds, for they have been occupied with cattle; and they have brought their sheep, and their cattle, and all that they have.
33 Farao atakapowaita na kuwaulizeni, ‘Kazi yenu ni nini?’
And it shall come to pass that when Pharaoh shall call you and say, What is your occupation?
34 Mjibuni, ‘Watumwa wako wamekuwa wachunga mifugo tangu ujana wetu mpaka sasa, kama baba zetu walivyofanya.’ Ndipo mtakaporuhusiwa kukaa katika nchi ya Gosheni, kwa kuwa wachunga mifugo wote ni chukizo kwa Wamisri.”
then ye shall say, Thy servants are men that have been occupied with cattle from our youth even until now, both we and our fathers; in order that ye may dwell in the land of Goshen; for every shepherd is an abomination to the Egyptians.