< Mwanzo 46 >

1 Hivyo Israeli akaondoka na vyote vilivyokuwa mali yake, naye alipofika Beer-Sheba, akamtolea dhabihu Mungu wa Isaki baba yake.
Da brød Israel op med alt, hvad han havde, og drog til Be'ersjeba, og han slagtede Ofre for sin Fader Isaks Gud.
2 Mungu akanena na Israeli katika maono usiku na kusema, “Yakobo! Yakobo!” Akajibu, “Mimi hapa.”
Men Gud sagde i et Nattesyn til Israel: "Jakob, Jakob!" Og han svarede: "Se, her er jeg!"
3 Mungu akamwambia, “Mimi ndimi Mungu wa baba yako, usiogope kushuka Misri, kwa maana huko nitakufanya taifa kubwa.
Da sagde han: "Jeg er Gud, din Faders Gud, vær ikke bange for at drage ned til Ægypten, thi jeg vil gøre dig til et stort Folk der;
4 Nitashuka Misri pamoja nawe, nami hakika nitakurudisha tena Kanaani. Mikono ya Yosefu mwenyewe ndiyo itakayofunga macho yako.”
jeg vil selv drage med dig til Ægypten, og jeg vil også føre dig tilbage, og Josef skal lukke dine Øjne!"
5 Ndipo Yakobo akaondoka Beer-Sheba nao wana wa Israeli wakamchukua baba yao Yakobo na watoto wao na wake zao katika magari ya kukokotwa yale Farao aliyokuwa amempelekea kumsafirisha.
Da brød Jakob op fra Be'ersjeba; og Israels Sønner satte deres Fader Jakob og deres Børn og Kvinder på de Vogne, Farao havde sendt til at hente ham på.
6 Wakachukua pia mifugo yao na mali walizokuwa wamezipata Kanaani, Yakobo na uzao wake wote wakashuka Misri.
Og de tog deres Kvæg og al deres Ejendom, som de havde erhvervet sig i Kana'ans Land, og drog til Ægypten, Jakob og alt hans Afkom med ham;
7 Akawachukua wanawe na binti zake, wajukuu wake wa kiume na wa kike, yaani uzao wake wote mpaka Misri.
således bragte han sine Sønner og Sønnesønner, sine Døtre og Sønnedøtre og alt sit Afkom med sig til Ægypten.
8 Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli (Yakobo na wazao wake), waliokwenda Misri: Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Yakobo.
Følgende er Navnene på Israels Sønner, der kom til Ægypten, Jakob og hans Sønner: Ruben, Jakobs førstefødte;
9 Wana wa Reubeni ni: Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi.
Rubens Sønner Hanok, Pallu. Hezron og Karmi;
10 Wana wa Simeoni ni: Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Shauli mwana wa mwanamke Mkanaani.
Simeons Sønner Jemuel, Jamin, Ohad, Jakin, Zohar og Kana'anæerkvindens Søn Sjaul;
11 Wana wa Lawi ni: Gershoni, Kohathi na Merari.
Leois Sønner Gerson, Kehat og Merari;
12 Wana wa Yuda ni: Eri, Onani, Shela, Peresi na Zera (lakini Eri na Onani walifariki katika nchi ya Kanaani). Wana wa Peresi ni: Hesroni na Hamuli.
Judos Sønner Er, Onan, Sjela, Perez og Zera; men Er og Onan døde i Kana'ans Land. Perezs Sønner var Hezron og Hamul.
13 Wana wa Isakari ni: Tola, Puva, Yashubu na Shimroni.
Issakars Sønner Tola, Pua, Jasjub og Sjimron;
14 Wana wa Zabuloni ni: Seredi, Eloni na Yaleeli.
Zedulons Sønner Sered, Eloo og Jalel;
15 Hawa ndio wana wa Lea aliomzalia Yakobo huko Padan-Aramu pamoja na binti yake Dina. Jumla ya wanawe na binti zake walikuwa thelathini na watatu.
det var Leos Sønner, som hun fødte Jakob i Paddan-Aram; desuden fødte hun ham Datteren Dina; det samlede Tal på hans Sønner og Døtre var tre og tredive.
16 Wana wa Gadi ni: Sefoni, Hagi, Shuni, Esboni, Eri, Arodi na Areli.
Gods Sønner Zifjon, Haggi. Sjuni, Ezbon, Eri, Arodi og Areli.
17 Wana wa Asheri ni: Imna, Ishva, Ishvi na Beria. Dada yao alikuwa Sera. Wana wa Beria ni: Heberi na Malkieli.
Asers Sønner Jimna, Jisjva. Jisjvi og Beria, og deres Søster Sera; og Berias Sønner Heber og Mallkiel;
18 Hawa ndio watoto Zilpa aliomzalia Yakobo, ambao Labani alimpa binti yake Lea; jumla yao walikuwa kumi na sita.
det var Sønnerne af Zilpo, som Laban gav sin Datter Lea, og som fødte Jakob dem, seksten i alt;
19 Wana wa Raheli mke wa Yakobo ni: Yosefu na Benyamini.
Rakels, Jakobs Hustrus, Sønner Josef og Benjamin;
20 Huko Misri, Asenathi binti wa Potifera, aliyekuwa kuhani wa mji wa Oni, alimzalia Yosefu wana wawili, Manase na Efraimu.
og Josef fik Børn i Ægypten med Asenat, en Datter af Potifera, Præsten i On: Manasse og Efraim;
21 Wana wa Benyamini ni: Bela, Bekeri, Ashbeli, Gera, Naamani, Ehi, Roshi, Mupimu, Hupimu na Ardi.
Benjomins Sønner Bela, Beker, Asjbel, Gera, Nåman, Ebi, Rosj, Muppim, Huppim og Ard;
22 Hawa ndio wana wa Raheli aliomzalia Yakobo; jumla yao ni kumi na wanne.
det var Rakels Sønner, som hun fødte Jakob, fjorten i alt;
23 Mwana wa Dani ni: Hushimu.
Dons Søn Husjim;
24 Wana wa Naftali ni: Yaseeli, Guni, Yeseri na Shilemu.
Noffolis Sønner Jazeel, Guni, Jezer og Sjillem;
25 Hawa walikuwa wana wa Bilha aliomzalia Yakobo, ambaye Labani alikuwa amempa Raheli binti yake; jumla yao walikuwa saba.
det var Sønnerne af Bilha, som Laban gav Rakel, og som fødte Jakob dem, syv i alt.
26 Wote waliokwenda Misri pamoja na Yakobo, waliokuwa wazao wake hasa pasipo kuhesabu wakwe zake, walikuwa watu sitini na sita.
Hele Jakobs Familie, der kom til Ægypten med ham, fraregnet Jakobs Sønnekoner, udgjorde tilsammen seks og tresindstyve;
27 Pamoja na wana wawili waliozaliwa na Yosefu huko Misri, jumla yote ya jamaa ya Yakobo, waliokwenda Misri, walikuwa sabini.
og Josefs Sønner, der fødtes ham i Ægypten, var to; alle de af Jakobs Hus, der kom til Ægypten, udgjorde halvfjerdsindstyve.
28 Basi Yakobo akamtanguliza Yuda aende kwa Yosefu ili amwelekeze njia ya Gosheni. Walipofika nchi ya Gosheni,
Men Juda sendte han i Forvejen til Josef, for at man skulde vise ham Vej til Gosen, og de kom til Gosens Land.
29 gari kubwa zuri la Yosefu liliandaliwa, naye akaenda Gosheni kumlaki baba yake Israeli. Mara Yosefu alipofika mbele yake, alimkumbatia baba yake, akalia kwa muda mrefu.
Da lod Josef spænde for sin Vogn og rejste sin Fader i Møde til Gosen; og da han traf ham, omfavnede han ham og græd længe i hans Arme;
30 Israeli akamwambia Yosefu, “Sasa niko tayari kufa, kwa kuwa nimejionea mwenyewe kwamba bado uko hai.”
og Israel sagde til Josef: "Lad mig nu kun dø, da jeg har set dit Ansigt, at du endnu lever!"
31 Ndipo Yosefu akawaambia ndugu zake na watu wa nyumbani mwa baba yake, “Nitapanda kwa Farao na kumwambia, ‘Ndugu zangu na watu wa nyumbani mwa baba yangu, waliokuwa wakiishi katika nchi ya Kanaani, wamekuja kwangu.
Men Josef sagde til sine Brødre og sin Faders Hus: "Jeg vil drage hen og melde det til Farao og sige til ham: Mine Brødre og min Faders Hus i Kana'an er kommet til mig;
32 Watu hao ni wachunga mifugo, huchunga mifugo, wamekuja na makundi ya kondoo, mbuzi na ngʼombe pamoja na kila kitu walicho nacho.’
disse Mænd er Hyrder, thi de driver Kvægavl, og de har bragt deres Småkvæg og Hornkvæg og alt, hvad de ejer, med.
33 Farao atakapowaita na kuwaulizeni, ‘Kazi yenu ni nini?’
Når så Farao lader eder kalde og spørger eder, hvad I er,
34 Mjibuni, ‘Watumwa wako wamekuwa wachunga mifugo tangu ujana wetu mpaka sasa, kama baba zetu walivyofanya.’ Ndipo mtakaporuhusiwa kukaa katika nchi ya Gosheni, kwa kuwa wachunga mifugo wote ni chukizo kwa Wamisri.”
skal I sige: Dine Trælle har drevet Kvægavl fra Barnsben af ligesom vore Fædre! for at I kan komme til at bo i Gosens Land. Thi enhver Hyrde er Ægypterne en Vederstyggelighed."

< Mwanzo 46 >