< Mwanzo 46 >

1 Hivyo Israeli akaondoka na vyote vilivyokuwa mali yake, naye alipofika Beer-Sheba, akamtolea dhabihu Mungu wa Isaki baba yake.
Tako Izrael krene na put sa svim što bijaše njegovo i stigne u Beer Šebu te prinese žrtvu Bogu svoga oca Izaka.
2 Mungu akanena na Israeli katika maono usiku na kusema, “Yakobo! Yakobo!” Akajibu, “Mimi hapa.”
U noćnom viđenju zovne Bog Izraela: “Jakove! Jakove!” On odgovori: “Evo me!”
3 Mungu akamwambia, “Mimi ndimi Mungu wa baba yako, usiogope kushuka Misri, kwa maana huko nitakufanya taifa kubwa.
“Ja sam Bog, Bog tvoga oca. Ne boj se sići u Egipat, jer ću ondje od tebe proizvesti velik narod.
4 Nitashuka Misri pamoja nawe, nami hakika nitakurudisha tena Kanaani. Mikono ya Yosefu mwenyewe ndiyo itakayofunga macho yako.”
Ja ću sići u Egipat s tobom i sam ću te vratiti ovamo; a Josip će ti svojom rukom oči zaklopiti.”
5 Ndipo Yakobo akaondoka Beer-Sheba nao wana wa Israeli wakamchukua baba yao Yakobo na watoto wao na wake zao katika magari ya kukokotwa yale Farao aliyokuwa amempelekea kumsafirisha.
I Jakov krene iz Beer Šebe. Sinovi Izraelovi postave svoga oca Jakova, svoju djecu i svoje žene u kola što ih je faraon poslao da ga prevezu.
6 Wakachukua pia mifugo yao na mali walizokuwa wamezipata Kanaani, Yakobo na uzao wake wote wakashuka Misri.
Uzmu sa sobom svoje blago i dobra što ih bijahu stekli u zemlji kanaanskoj te stignu Jakov i sve njegovo potomstvo u Egipat.
7 Akawachukua wanawe na binti zake, wajukuu wake wa kiume na wa kike, yaani uzao wake wote mpaka Misri.
Sa sobom je u Egipat poveo svoje sinove i unuke, svoje kćeri i kćeri svojih sinova, sve svoje potomstvo.
8 Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli (Yakobo na wazao wake), waliokwenda Misri: Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Yakobo.
Ovo su imena Izraelaca - Jakova i njegovih potomaka - koji su stigli u Egipat: Jakovljev prvorođenac Ruben.
9 Wana wa Reubeni ni: Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi.
Rubenovi sinovi: Henok, Falu, Hesron i Karmi.
10 Wana wa Simeoni ni: Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Shauli mwana wa mwanamke Mkanaani.
Sinovi Šimunovi: Jemuel, Jamin, Ohad, Jakin, Sohar i Šaul, sin Kanaanke.
11 Wana wa Lawi ni: Gershoni, Kohathi na Merari.
Sinovi Levijevi: Geršon, Kehat i Merari.
12 Wana wa Yuda ni: Eri, Onani, Shela, Peresi na Zera (lakini Eri na Onani walifariki katika nchi ya Kanaani). Wana wa Peresi ni: Hesroni na Hamuli.
Sinovi Judini: Er, Onan, Šela, Peres i Zerah. Er i Onan umrli su u zemlji kanaanskoj. Peresovi sinovi bili su Hesron i Hamul.
13 Wana wa Isakari ni: Tola, Puva, Yashubu na Shimroni.
Sinovi Jisakarovi: Tola, Fuva, Jašub i Šimron.
14 Wana wa Zabuloni ni: Seredi, Eloni na Yaleeli.
Sinovi Zebulunovi: Sered, Elon i Jahleel.
15 Hawa ndio wana wa Lea aliomzalia Yakobo huko Padan-Aramu pamoja na binti yake Dina. Jumla ya wanawe na binti zake walikuwa thelathini na watatu.
To su sinovi koje je Lea imala s Jakovom u Padan Aramu i još kćerka Dina. U svemu je, dakle, imao sinova i kćeri trideset i troje.
16 Wana wa Gadi ni: Sefoni, Hagi, Shuni, Esboni, Eri, Arodi na Areli.
Sinovi Gadovi: Sifjon, Hagi, Šuni, Esbon, Eri, Arodi i Areli.
17 Wana wa Asheri ni: Imna, Ishva, Ishvi na Beria. Dada yao alikuwa Sera. Wana wa Beria ni: Heberi na Malkieli.
Sinovi Ašerovi: Jimna, Jišva, Jišvi, Berija i sestra im Serah. Sinovi Berijini: Heber i Malkiel.
18 Hawa ndio watoto Zilpa aliomzalia Yakobo, ambao Labani alimpa binti yake Lea; jumla yao walikuwa kumi na sita.
To su bili potomci Zilpe, koju je Laban darovao svojoj kćeri Lei. Ona je tako rodila Jakovu šesnaest duša.
19 Wana wa Raheli mke wa Yakobo ni: Yosefu na Benyamini.
Sinovi Jakovljeve žene Rahele: Josip i Benjamin.
20 Huko Misri, Asenathi binti wa Potifera, aliyekuwa kuhani wa mji wa Oni, alimzalia Yosefu wana wawili, Manase na Efraimu.
Josipu su se u egipatskoj zemlji rodili Manaše i Efrajim. Rodila mu ih je kći onskog svećenika Poti-Fere.
21 Wana wa Benyamini ni: Bela, Bekeri, Ashbeli, Gera, Naamani, Ehi, Roshi, Mupimu, Hupimu na Ardi.
Sinovi Benjaminovi: Bela, Beker, Ašbel, Gera, Naaman, Ehi, Roš, Mupim, Hupim i Ard.
22 Hawa ndio wana wa Raheli aliomzalia Yakobo; jumla yao ni kumi na wanne.
To su bili potomci Rahelini koje je rodila Jakovu - u svemu njih četrnaest.
23 Mwana wa Dani ni: Hushimu.
Danov je sin Hušim.
24 Wana wa Naftali ni: Yaseeli, Guni, Yeseri na Shilemu.
Sinovi Naftalijevi: Jahseel, Guni, Jeser i Šilem.
25 Hawa walikuwa wana wa Bilha aliomzalia Yakobo, ambaye Labani alikuwa amempa Raheli binti yake; jumla yao walikuwa saba.
To su bili potomci Bilhe, koju je Laban dao svojoj kćeri Raheli. Ona je Jakovu rodila sedam potomaka.
26 Wote waliokwenda Misri pamoja na Yakobo, waliokuwa wazao wake hasa pasipo kuhesabu wakwe zake, walikuwa watu sitini na sita.
Tako je sve Jakovljeve čeljadi što je od njega poteklo i u Egipat doselilo - ne uključujući žena Jakovljevih sinova - u svemu šezdeset i šest osoba.
27 Pamoja na wana wawili waliozaliwa na Yosefu huko Misri, jumla yote ya jamaa ya Yakobo, waliokwenda Misri, walikuwa sabini.
I k tome dva sina Josipova što su mu se rodila u Egiptu. Prema tome, sve čeljadi Jakovljeva doma što se naseli u Egiptu bijaše sedamdeset duša.
28 Basi Yakobo akamtanguliza Yuda aende kwa Yosefu ili amwelekeze njia ya Gosheni. Walipofika nchi ya Gosheni,
Izrael posla Judu naprijed k Josipu da se pred njim pojavi u Gošenu. Kad stignu u gošenski kraj,
29 gari kubwa zuri la Yosefu liliandaliwa, naye akaenda Gosheni kumlaki baba yake Israeli. Mara Yosefu alipofika mbele yake, alimkumbatia baba yake, akalia kwa muda mrefu.
Josip upregne svoja kola i zaputi se u Gošen - u susret svome ocu Izraelu. Stupivši preda nj, pade mu oko vrata i dugo je tako plakao.
30 Israeli akamwambia Yosefu, “Sasa niko tayari kufa, kwa kuwa nimejionea mwenyewe kwamba bado uko hai.”
Onda Izrael reče Josipu: “Sada, pošto sam rođenim očima vidio da si još živ, mogu umrijeti.”
31 Ndipo Yosefu akawaambia ndugu zake na watu wa nyumbani mwa baba yake, “Nitapanda kwa Farao na kumwambia, ‘Ndugu zangu na watu wa nyumbani mwa baba yangu, waliokuwa wakiishi katika nchi ya Kanaani, wamekuja kwangu.
Zatim Josip reče svojoj braći i očevoj obitelji: “Otići ću i obavijestiti faraona; reći ću mu: 'Moja braća i obitelj moga oca, koji su bili u zemlji kanaanskoj, došli su k meni.
32 Watu hao ni wachunga mifugo, huchunga mifugo, wamekuja na makundi ya kondoo, mbuzi na ngʼombe pamoja na kila kitu walicho nacho.’
Oni su ljudi pastiri, uvijek su se bavili stočarstvom; dotjerali su sa sobom svoja stada i sve što im pripada.'
33 Farao atakapowaita na kuwaulizeni, ‘Kazi yenu ni nini?’
Tako, kad vas faraon pozove i zapita: 'Čime se bavite?'
34 Mjibuni, ‘Watumwa wako wamekuwa wachunga mifugo tangu ujana wetu mpaka sasa, kama baba zetu walivyofanya.’ Ndipo mtakaporuhusiwa kukaa katika nchi ya Gosheni, kwa kuwa wachunga mifugo wote ni chukizo kwa Wamisri.”
odgovorite: 'Ljudi smo, sluge tvoje, koji se od početka do sad bavimo stočarstvom; i mi i naši preci', tako da se možete naseliti u gošenskom kraju. Svi su, naime, pastiri Egipćanima mrski.”

< Mwanzo 46 >