< Mwanzo 45 >
1 Hapo Yosefu hakuweza kujizuia zaidi mbele ya wote waliokuwa wamesimama karibu naye, akapaza sauti, akasema, “Mwondoeni kila mtu mbele yangu!” Kwa hiyo hapakuwepo mtu yeyote pamoja na Yosefu alipojitambulisha kwa ndugu zake.
And Joseph hath not been able to refrain himself before all those standing by him, and he calleth, 'Put out every man from me;' and no man hath stood with him when Joseph maketh himself known unto his brethren,
2 Naye akalia kwa sauti kubwa kiasi kwamba Wamisri walimsikia, hata watu wa nyumbani mwa Farao wakapata hizo habari.
and he giveth forth his voice in weeping, and the Egyptians hear, and the house of Pharaoh heareth.
3 Yosefu akawaambia ndugu zake, “Mimi ni Yosefu! Je, baba yangu angali hai bado?” Lakini ndugu zake hawakuweza kumjibu, kwa sababu walipatwa na hofu kuu mbele yake.
And Joseph saith unto his brethren, 'I [am] Joseph, is my father yet alive?' and his brethren have not been able to answer him, for they have been troubled at his presence.
4 Ndipo Yosefu akawaambia ndugu zake, “Sogeeni karibu nami.” Waliposogea, akasema, “Mimi ni ndugu yenu Yosefu, yule ambaye mlimuuza Misri!
And Joseph saith unto his brethren, 'Come nigh unto me, I pray you,' and they come nigh; and he saith, 'I [am] Joseph, your brother, whom ye sold into Egypt;
5 Sasa, msihuzunike wala msijichukie wenyewe kwa kuniuza huku, kwa sababu ilikuwa ni ili kuokoa maisha ya watu ndiyo sababu Mungu alinituma niwatangulie ninyi.
and now, be not grieved, nor let it be displeasing in your eyes that ye sold me hither, for to preserve life hath God sent me before you.
6 Kwa miaka miwili sasa imekuwepo njaa katika nchi, pia kwa miaka mitano ijayo hapatakuwepo kulima wala kuvuna.
'Because these two years the famine [is] in the heart of the land, and yet [are] five years, [in] which there is neither ploughing nor harvest;
7 Lakini Mungu alinitanguliza mbele yenu ili kuhifadhi mabaki kwa ajili yenu katika nchi, na kuokoa maisha yenu kwa wokovu mkuu.
and God sendeth me before you, to place of you a remnant in the land, and to give life to you by a great escape;
8 “Kwa hiyo basi, si ninyi mlionileta huku, bali ni Mungu. Alinifanya kuwa baba kwa Farao, bwana wa watu wa nyumbani mwake wote, na mtawala wa Misri yote.
and now, ye — ye have not sent me hither, but God, and He doth set me for a father to Pharaoh, and for lord to all his house, and ruler over all the land of Egypt.
9 Sasa rudini haraka kwa baba yangu na mwambieni, ‘Hili ndilo mwanao Yosefu asemalo: Mungu amenifanya mimi kuwa bwana wa Misri yote. Shuka uje kwangu, wala usikawie.
'Haste, and go up unto my father, then ye have said to him, Thus said Joseph thy son, God hath set me for lord to all Egypt; come down unto me, stay not,
10 Nawe utaishi katika nchi ya Gosheni na kuwa karibu nami, wewe, watoto wako na wajukuu wako, makundi yako ya kondoo, mbuzi na ngʼombe, pamoja na vyote ulivyo navyo.
and thou hast dwelt in the land of Goshen, and been near unto me, thou and thy sons, and thy son's sons, and thy flock, and thy herd, and all that thou hast,
11 Nitawatunza huko, kwa sababu bado iko miaka mingine mitano inayokuja ya njaa. La sivyo, wewe na nyumba yako na wote ulio nao mtakuwa fukara.’
and I have nourished thee there — for yet [are] five years of famine — lest thou become poor, thou and thy household, and all that thou hast.
12 “Mnaweza kujionea wenyewe, hata ndugu yangu Benyamini, kwamba hakika ni mimi ninayezungumza nanyi.
'And lo, your eyes are seeing, and the eyes of my brother Benjamin, that [it is] my mouth which is speaking unto you;
13 Mwambieni baba yangu juu ya heshima yote niliyopewa huku Misri, na kuhusu kila kitu mlichokiona. Mleteni baba yangu huku haraka.”
and ye have declared to my father all my honour in Egypt, and all that ye have seen, and ye have hasted, and have brought down my father hither.'
14 Ndipo akamkumbatia Benyamini ndugu yake na kulia, naye Benyamini akamkumbatia akilia.
And he falleth on the neck of Benjamin his brother, and weepeth, and Benjamin hath wept on his neck;
15 Pia akawabusu ndugu zake wote, huku akilia. Baada ya hayo ndugu zake wakazungumza naye.
and he kisseth all his brethren, and weepeth over them; and afterwards have his brethren spoken with him.
16 Habari zilipofika kwenye jumba la Farao kwamba ndugu zake Yosefu wamefika, Farao na maafisa wake wote wakafurahi.
And the sound hath been heard in the house of Pharaoh, saying, 'Come have the brethren of Joseph;' and it is good in the eyes of Pharaoh, and in the eyes of his servants,
17 Farao akamwambia Yosefu, “Waambie ndugu zako, ‘Fanyeni hivi: Pakieni wanyama wenu mrudi mpaka nchi ya Kanaani,
and Pharaoh saith unto Joseph, 'Say unto thy brethren, This do ye: lade your beasts, and go, enter ye the land of Canaan,
18 mkamlete baba yenu na jamaa zenu kwangu. Nitawapa sehemu nzuri sana ya nchi ya Misri nanyi mtafurahia unono wa nchi.’
and take your father, and your households, and come unto me, and I give to you the good of the land of Egypt, and eat ye the fat of the land.
19 “Mnaagizwa pia kuwaambia, ‘Fanyeni hivi: Chukueni magari ya kukokotwa kutoka Misri, kwa ajili ya watoto wenu na wake zenu, mkamchukue baba yenu mje.
'Yea, thou — thou hast been commanded: this do ye, take for yourselves out of the land of Egypt, waggons for your infants, and for your wives, and ye have brought your father, and come;
20 Msijali kamwe kuhusu mali zenu, kwa sababu mema yote ya Misri yatakuwa yenu.’”
and your eye hath no pity on your vessels, for the good of all the land of Egypt [is] yours.'
21 Hivyo wana wa Israeli wakafanya hivyo. Yosefu akawapa magari ya kukokotwa, kama Farao alivyoagiza, pia akawapa mahitaji kwa ajili ya safari yao.
And the sons of Israel do so, and Joseph giveth waggons to them by the command of Pharaoh, and he giveth to them provision for the way;
22 Kila mmoja mavazi mapya, lakini Benyamini akampa shekeli 300 za fedha, na jozi tano za nguo.
to all of them hath he given — to each changes of garments, and to Benjamin he hath given three hundred silverlings, and five changes of garments;
23 Hivi ndivyo vitu alivyotuma kwa baba yake: punda kumi waliochukua vitu vizuri vya Misri, punda wake kumi waliobeba nafaka, mikate na mahitaji mengine ya safari.
and to his father he hath sent thus: ten asses bearing of the good things of Egypt, and ten she-asses bearing corn and bread, even food for his father for the way.
24 Akaagana na ndugu zake walipokuwa wakiondoka, akawaambia, “Msigombane njiani!”
And he sendeth his brethren away, and they go; and he saith unto them, 'Be not angry in the way.'
25 Basi wakatoka Misri na kufika kwa baba yao Yakobo katika nchi ya Kanaani.
And they go up out of Egypt, and come in to the land of Canaan, unto Jacob their father,
26 Wakamwambia baba yao, “Yosefu angali hai! Ukweli ni kwamba yeye ndiye mtawala wa Misri yote.” Yakobo akapigwa na bumbuazi; hakuwasadiki.
and they declare to him, saying, 'Joseph [is] yet alive,' and that he [is] ruler over all the land of Egypt; and his heart ceaseth, for he hath not given credence to them.
27 Lakini walipokwisha kumweleza kila kitu ambacho Yosefu alikuwa amewaambia, na alipoona magari ya kukokotwa Yosefu aliyokuwa amempelekea ya kumchukua aende Misri, roho ya baba yao Yakobo ikahuishwa.
And they speak unto him all the words of Joseph, which he hath spoken unto them, and he seeth the waggons which Joseph hath sent to bear him away, and live doth the spirit of Jacob their father;
28 Ndipo Israeli akasema, “Nimesadiki! Mwanangu Yosefu bado yu hai. Nitakwenda nikamwone kabla sijafa.”
and Israel saith, 'Enough! Joseph my son [is] yet alive; I go and see him before I die.'