< Mwanzo 45 >
1 Hapo Yosefu hakuweza kujizuia zaidi mbele ya wote waliokuwa wamesimama karibu naye, akapaza sauti, akasema, “Mwondoeni kila mtu mbele yangu!” Kwa hiyo hapakuwepo mtu yeyote pamoja na Yosefu alipojitambulisha kwa ndugu zake.
And Ioseph coude no longer refrayne before all them that stode aboute him but commaunded that they shuld goo all out from him and that there shuld be no man with him whyle he vttred him selfe vnto his brethern.
2 Naye akalia kwa sauti kubwa kiasi kwamba Wamisri walimsikia, hata watu wa nyumbani mwa Farao wakapata hizo habari.
And he wepte alowde so that the Egiptians and the house of Pharao herde it.
3 Yosefu akawaambia ndugu zake, “Mimi ni Yosefu! Je, baba yangu angali hai bado?” Lakini ndugu zake hawakuweza kumjibu, kwa sababu walipatwa na hofu kuu mbele yake.
And he sayde vnto his brethern: I am Ioseph: doth my father yet lyue? But his brethern coude not answere him for they were abasshed at his presence.
4 Ndipo Yosefu akawaambia ndugu zake, “Sogeeni karibu nami.” Waliposogea, akasema, “Mimi ni ndugu yenu Yosefu, yule ambaye mlimuuza Misri!
And Ioseph sayde vnto his brethern: come nere to me and they came nere. And he sayde: I am Ioseph youre brother whom ye sold in to Egipte.
5 Sasa, msihuzunike wala msijichukie wenyewe kwa kuniuza huku, kwa sababu ilikuwa ni ili kuokoa maisha ya watu ndiyo sababu Mungu alinituma niwatangulie ninyi.
And now be not greued therwith nether let it seme a cruel thinge in youre eyes that ye solde me hither. For God dyd send me before you to saue lyfe.
6 Kwa miaka miwili sasa imekuwepo njaa katika nchi, pia kwa miaka mitano ijayo hapatakuwepo kulima wala kuvuna.
For this is the seconde yere of derth in the lande and fyue moo are behynde in which there shall nether be earynge nor hervest.
7 Lakini Mungu alinitanguliza mbele yenu ili kuhifadhi mabaki kwa ajili yenu katika nchi, na kuokoa maisha yenu kwa wokovu mkuu.
Wherfore God sent me before you to make prouision that ye myghte continue in the erth and to save youre lyues by a greate delyuerance.
8 “Kwa hiyo basi, si ninyi mlionileta huku, bali ni Mungu. Alinifanya kuwa baba kwa Farao, bwana wa watu wa nyumbani mwake wote, na mtawala wa Misri yote.
So now it was not ye that sent me hither but God: and he hath made me father vnto Pharao and lorde ouer all his house and rueler in all the land of Egipte.
9 Sasa rudini haraka kwa baba yangu na mwambieni, ‘Hili ndilo mwanao Yosefu asemalo: Mungu amenifanya mimi kuwa bwana wa Misri yote. Shuka uje kwangu, wala usikawie.
Hast you ad goo to my father and tell him this sayeth thy sonne Ioseph: God hath made me lorde ouer all Egipte. Come downe vnto me and tarye not
10 Nawe utaishi katika nchi ya Gosheni na kuwa karibu nami, wewe, watoto wako na wajukuu wako, makundi yako ya kondoo, mbuzi na ngʼombe, pamoja na vyote ulivyo navyo.
And thou shalt dwell in the londe of Gosan and be by me: both thou and thi childern and thi childerns childern: and thy shepe and beestes and all that thou hast.
11 Nitawatunza huko, kwa sababu bado iko miaka mingine mitano inayokuja ya njaa. La sivyo, wewe na nyumba yako na wote ulio nao mtakuwa fukara.’
There will I make provision for the: for there remayne yet v yeres of derth lest thou and thi houshold and all that thou hast perish.
12 “Mnaweza kujionea wenyewe, hata ndugu yangu Benyamini, kwamba hakika ni mimi ninayezungumza nanyi.
Beholde youre eyes do se and the eyes also of my brother Ben Iamin that I speake to you by mouth.
13 Mwambieni baba yangu juu ya heshima yote niliyopewa huku Misri, na kuhusu kila kitu mlichokiona. Mleteni baba yangu huku haraka.”
Therfore tell my father of all my honoure which I haue in Egipte and of all that ye haue sene ad make hast and brynge in father hither.
14 Ndipo akamkumbatia Benyamini ndugu yake na kulia, naye Benyamini akamkumbatia akilia.
And he fell on his brother Ben Iamis necke and wepte and Ben Iamin wepte on his necke.
15 Pia akawabusu ndugu zake wote, huku akilia. Baada ya hayo ndugu zake wakazungumza naye.
Moreouer he fylled all his brethern and wepte apon them. And after that his brethern talked with him.
16 Habari zilipofika kwenye jumba la Farao kwamba ndugu zake Yosefu wamefika, Farao na maafisa wake wote wakafurahi.
And when the tidynges was come vnto Pharaos housse that Iosephes brethern were come it pleased Pharao well and all his seruauntes.
17 Farao akamwambia Yosefu, “Waambie ndugu zako, ‘Fanyeni hivi: Pakieni wanyama wenu mrudi mpaka nchi ya Kanaani,
And Pharao spake vnto Ioseph: saye vnto thy brethern this do ye: lade youre beestes ad get you hence And when ye be come vnto the londe of Canaan
18 mkamlete baba yenu na jamaa zenu kwangu. Nitawapa sehemu nzuri sana ya nchi ya Misri nanyi mtafurahia unono wa nchi.’
take youre father and youre housholdes and come vnto me and I will geue you the beste of the lande of Egipte and ye shall eate the fatt of the londe.
19 “Mnaagizwa pia kuwaambia, ‘Fanyeni hivi: Chukueni magari ya kukokotwa kutoka Misri, kwa ajili ya watoto wenu na wake zenu, mkamchukue baba yenu mje.
And commaunded also. This do ye: take charettes with you out of the lande of Egipte for youre childern and for youre wyues: and brynge youre father and come.
20 Msijali kamwe kuhusu mali zenu, kwa sababu mema yote ya Misri yatakuwa yenu.’”
Also regarde not youre stuff for the goodes of all the londe of Egipte shalbe youres.
21 Hivyo wana wa Israeli wakafanya hivyo. Yosefu akawapa magari ya kukokotwa, kama Farao alivyoagiza, pia akawapa mahitaji kwa ajili ya safari yao.
And the childern of Israell dyd euen so And Ioseph gaue them charettes at the commaundment of Pharao and gaue them vitayle also to spende by the waye.
22 Kila mmoja mavazi mapya, lakini Benyamini akampa shekeli 300 za fedha, na jozi tano za nguo.
And he gaue vnto eche of them chaunge of rayment: but vnto Ben Iamin he gaue. iij. hundred peces of syluer and. v. chaunge of rayment.
23 Hivi ndivyo vitu alivyotuma kwa baba yake: punda kumi waliochukua vitu vizuri vya Misri, punda wake kumi waliobeba nafaka, mikate na mahitaji mengine ya safari.
And vnto his father he sent after the same maner: x. he asses laden with good out of Egipte and. x. she asses laden with corne bred and meate: to serue his father by the waye.
24 Akaagana na ndugu zake walipokuwa wakiondoka, akawaambia, “Msigombane njiani!”
So sent he his brethern awaye and they departed. And he sayde vnto them: se that ye fall nor out by the waye.
25 Basi wakatoka Misri na kufika kwa baba yao Yakobo katika nchi ya Kanaani.
And they departed from Egipte and came in to the land of Canaan vnto Iacob their father and told him saynge.
26 Wakamwambia baba yao, “Yosefu angali hai! Ukweli ni kwamba yeye ndiye mtawala wa Misri yote.” Yakobo akapigwa na bumbuazi; hakuwasadiki.
Ioseph is yet a lyue and is gouerner ouer all the land of Egipte. And Iacobs hert wauered for he beleued tho not.
27 Lakini walipokwisha kumweleza kila kitu ambacho Yosefu alikuwa amewaambia, na alipoona magari ya kukokotwa Yosefu aliyokuwa amempelekea ya kumchukua aende Misri, roho ya baba yao Yakobo ikahuishwa.
And they tolde him all the wordes of Ioseph which he had sayde vnto them. But when he sawe the charettes which Ioseph had sent to carie him then his sprites reviued.
28 Ndipo Israeli akasema, “Nimesadiki! Mwanangu Yosefu bado yu hai. Nitakwenda nikamwone kabla sijafa.”
And Israel sayde. I haue ynough yf Ioseph my sonne be yet alyue: I will goo and se him yer that I dye.