< Mwanzo 45 >

1 Hapo Yosefu hakuweza kujizuia zaidi mbele ya wote waliokuwa wamesimama karibu naye, akapaza sauti, akasema, “Mwondoeni kila mtu mbele yangu!” Kwa hiyo hapakuwepo mtu yeyote pamoja na Yosefu alipojitambulisha kwa ndugu zake.
and not be able Joseph to/for to refrain to/for all [the] to stand upon him and to call: call out to come out: come all man from upon me and not to stand: stand man: anyone with him in/on/with to know Joseph to(wards) brother: male-sibling his
2 Naye akalia kwa sauti kubwa kiasi kwamba Wamisri walimsikia, hata watu wa nyumbani mwa Farao wakapata hizo habari.
and to give: cry out [obj] voice his in/on/with weeping and to hear: hear Egyptian and to hear: hear house: household Pharaoh
3 Yosefu akawaambia ndugu zake, “Mimi ni Yosefu! Je, baba yangu angali hai bado?” Lakini ndugu zake hawakuweza kumjibu, kwa sababu walipatwa na hofu kuu mbele yake.
and to say Joseph to(wards) brother: male-sibling his I Joseph still father my alive and not be able brother: male-sibling his to/for to answer [obj] him for to dismay from face his
4 Ndipo Yosefu akawaambia ndugu zake, “Sogeeni karibu nami.” Waliposogea, akasema, “Mimi ni ndugu yenu Yosefu, yule ambaye mlimuuza Misri!
and to say Joseph to(wards) brother: male-sibling his to approach: approach please to(wards) me and to approach: approach and to say I Joseph brother: male-sibling your which to sell [obj] me Egypt [to]
5 Sasa, msihuzunike wala msijichukie wenyewe kwa kuniuza huku, kwa sababu ilikuwa ni ili kuokoa maisha ya watu ndiyo sababu Mungu alinituma niwatangulie ninyi.
and now not to hurt and not to be incensed in/on/with eye: appearance your for to sell [obj] me here/thus for to/for recovery to send: depart me God to/for face: before your
6 Kwa miaka miwili sasa imekuwepo njaa katika nchi, pia kwa miaka mitano ijayo hapatakuwepo kulima wala kuvuna.
for this year [the] famine in/on/with entrails: among [the] land: country/planet and still five year which nothing plowing and harvest
7 Lakini Mungu alinitanguliza mbele yenu ili kuhifadhi mabaki kwa ajili yenu katika nchi, na kuokoa maisha yenu kwa wokovu mkuu.
and to send: depart me God to/for face: before your to/for to set: put to/for you remnant in/on/with land: country/planet and to/for to live to/for you to/for survivor great: large
8 “Kwa hiyo basi, si ninyi mlionileta huku, bali ni Mungu. Alinifanya kuwa baba kwa Farao, bwana wa watu wa nyumbani mwake wote, na mtawala wa Misri yote.
and now not you(m. p.) to send: depart [obj] me here/thus for [the] God and to set: make me to/for father to/for Pharaoh and to/for lord to/for all house: household his and to rule in/on/with all land: country/planet Egypt
9 Sasa rudini haraka kwa baba yangu na mwambieni, ‘Hili ndilo mwanao Yosefu asemalo: Mungu amenifanya mimi kuwa bwana wa Misri yote. Shuka uje kwangu, wala usikawie.
to hasten and to ascend: rise to(wards) father my and to say to(wards) him thus to say son: child your Joseph to set: make me God to/for lord to/for all Egypt to go down [emph?] to(wards) me not to stand: stand
10 Nawe utaishi katika nchi ya Gosheni na kuwa karibu nami, wewe, watoto wako na wajukuu wako, makundi yako ya kondoo, mbuzi na ngʼombe, pamoja na vyote ulivyo navyo.
and to dwell in/on/with land: country/planet Goshen and to be near to(wards) me you(m. s.) and son: child your and son: child son: child your and flock your and cattle your and all which to/for you
11 Nitawatunza huko, kwa sababu bado iko miaka mingine mitano inayokuja ya njaa. La sivyo, wewe na nyumba yako na wote ulio nao mtakuwa fukara.’
and to sustain [obj] you there for still five year famine lest to possess: poor you(m. s.) and house: household your and all which to/for you
12 “Mnaweza kujionea wenyewe, hata ndugu yangu Benyamini, kwamba hakika ni mimi ninayezungumza nanyi.
and behold eye your to see: see and eye brother: male-sibling my Benjamin for lip my [the] to speak: speak to(wards) you
13 Mwambieni baba yangu juu ya heshima yote niliyopewa huku Misri, na kuhusu kila kitu mlichokiona. Mleteni baba yangu huku haraka.”
and to tell to/for father my [obj] all glory my in/on/with Egypt and [obj] all which to see: see and to hasten and to go down [obj] father my here/thus
14 Ndipo akamkumbatia Benyamini ndugu yake na kulia, naye Benyamini akamkumbatia akilia.
and to fall: fall upon neck Benjamin brother: male-sibling his and to weep and Benjamin to weep upon neck his
15 Pia akawabusu ndugu zake wote, huku akilia. Baada ya hayo ndugu zake wakazungumza naye.
and to kiss to/for all brother: male-sibling his and to weep upon them and after so to speak: speak brother: male-sibling his with him
16 Habari zilipofika kwenye jumba la Farao kwamba ndugu zake Yosefu wamefika, Farao na maafisa wake wote wakafurahi.
and [the] voice: message to hear: hear house: household Pharaoh to/for to say to come (in): come brother: male-sibling Joseph and be good in/on/with eye: appearance Pharaoh and in/on/with eye: appearance servant/slave his
17 Farao akamwambia Yosefu, “Waambie ndugu zako, ‘Fanyeni hivi: Pakieni wanyama wenu mrudi mpaka nchi ya Kanaani,
and to say Pharaoh to(wards) Joseph to say to(wards) brother: male-sibling your this to make: do to load [obj] cattle your and to go: went to come (in): come land: country/planet [to] Canaan
18 mkamlete baba yenu na jamaa zenu kwangu. Nitawapa sehemu nzuri sana ya nchi ya Misri nanyi mtafurahia unono wa nchi.’
and to take: take [obj] father your and [obj] house: household your and to come (in): come to(wards) me and to give: give to/for you [obj] goodness land: country/planet Egypt and to eat [obj] fat [the] land: country/planet
19 “Mnaagizwa pia kuwaambia, ‘Fanyeni hivi: Chukueni magari ya kukokotwa kutoka Misri, kwa ajili ya watoto wenu na wake zenu, mkamchukue baba yenu mje.
and you(m. s.) to command this to make: do to take: take to/for you from land: country/planet Egypt cart to/for child your and to/for woman: wife your and to lift: bear [obj] father your and to come (in): come
20 Msijali kamwe kuhusu mali zenu, kwa sababu mema yote ya Misri yatakuwa yenu.’”
and eye your not to pity upon article/utensil your for goodness all land: country/planet Egypt to/for you he/she/it
21 Hivyo wana wa Israeli wakafanya hivyo. Yosefu akawapa magari ya kukokotwa, kama Farao alivyoagiza, pia akawapa mahitaji kwa ajili ya safari yao.
and to make: do so son: child Israel and to give: give to/for them Joseph cart upon lip: word Pharaoh and to give: give to/for them provision to/for way: journey
22 Kila mmoja mavazi mapya, lakini Benyamini akampa shekeli 300 za fedha, na jozi tano za nguo.
to/for all their to give: give to/for man: anyone change mantle and to/for Benjamin to give: give three hundred silver: money and five change mantle
23 Hivi ndivyo vitu alivyotuma kwa baba yake: punda kumi waliochukua vitu vizuri vya Misri, punda wake kumi waliobeba nafaka, mikate na mahitaji mengine ya safari.
and to/for father his to send: depart like/as this ten donkey to lift: bear from goodness Egypt and ten she-ass to lift: bear grain and food: bread and food to/for father his to/for way: journey
24 Akaagana na ndugu zake walipokuwa wakiondoka, akawaambia, “Msigombane njiani!”
and to send: depart [obj] brother: male-sibling his and to go: went and to say to(wards) them not to tremble in/on/with way: journey
25 Basi wakatoka Misri na kufika kwa baba yao Yakobo katika nchi ya Kanaani.
and to ascend: rise from Egypt and to come (in): come land: country/planet Canaan to(wards) Jacob father their
26 Wakamwambia baba yao, “Yosefu angali hai! Ukweli ni kwamba yeye ndiye mtawala wa Misri yote.” Yakobo akapigwa na bumbuazi; hakuwasadiki.
and to tell to/for him to/for to say still Joseph alive and for he/she/it to rule in/on/with all land: country/planet Egypt and be numb heart his for not be faithful to/for them
27 Lakini walipokwisha kumweleza kila kitu ambacho Yosefu alikuwa amewaambia, na alipoona magari ya kukokotwa Yosefu aliyokuwa amempelekea ya kumchukua aende Misri, roho ya baba yao Yakobo ikahuishwa.
and to speak: speak to(wards) him [obj] all word Joseph which to speak: speak to(wards) them and to see: see [obj] [the] cart which to send: depart Joseph to/for to lift: bear [obj] him and to live spirit Jacob father their
28 Ndipo Israeli akasema, “Nimesadiki! Mwanangu Yosefu bado yu hai. Nitakwenda nikamwone kabla sijafa.”
and to say Israel many still Joseph son: child my alive to go: went and to see: see him in/on/with before to die

< Mwanzo 45 >