< Mwanzo 44 >
1 Kisha Yosefu akampa yule msimamizi wa nyumbani mwake maagizo haya: “Jaza magunia ya watu hawa kiasi cha chakula ambacho wanaweza kuchukua, na uweke fedha ya kila mtu kwenye mdomo wa gunia lake.
Och Joseph befallde honom, som var öfver hans hus, och sade: Fyll dessa männernas säckar med spisning, så mycket de kunna föra, och lägg hvarjom sina penningar ofvan i hans säck:
2 Kisha weka kikombe changu kile cha fedha kwenye mdomo wa gunia la yule mdogo wa wote pamoja na fedha zake ambazo angenunulia nafaka yake.” Naye akafanya kama Yosefu alivyosema.
Och mina silfskål ofvan i dens yngstas säck med penningarna för sädena. Han gjorde, som Joseph honom sade.
3 Kulipopambazuka, hao watu wakaruhusiwa kuondoka pamoja na punda zao.
Om morgonen, då ljust vardt, läto de männerna fara med sina åsnar.
4 Kabla hawajafika mbali kutoka mjini, Yosefu akamwambia mtumishi wake, “Wafuatilie wale watu mara moja, utakapowakuta, waambie, ‘Kwa nini mmelipiza wema kwa ubaya?
Då de nu voro ut af stadenom, och icke långt komne, sade Joseph till honom, som var öfver hans hus: Up och far efter männerna, och när du får dem, så säg till dem: Hvi hafven I lönt godt med ondo?
5 Je, kikombe hiki sicho anachonywea bwana wangu na pia hukitumia kwa kutabiri mambo yajayo? Hili ni jambo ovu mlilolitenda.’”
Är icke det der min herre dricker utaf, och der han spår med? I hafven illa gjort.
6 Alipowafikia, akarudia maneno haya kwao.
Och som han beslog dem, sade han sådan ord till dem.
7 Lakini wakamwambia mtumishi, “Kwa nini bwana wangu anasema maneno kama haya? Liwe mbali na watumishi wako wasije wakafanya jambo kama hilo!
De svarade honom: Hvi talar min herre sådana ord? Bort det, att dine tjenare skulle så göra.
8 Hata hivyo tulikurudishia zile fedha kutoka nchi ya Kanaani ambazo tulizikuta kwenye midomo ya magunia yetu. Hivyo kwa nini tuibe fedha au dhahabu kutoka nyumbani kwa bwana wako?
Si, penningarna, som vi funnom ofvan uti våra säckar, hafvom vi fört till dig igen af Canaans lande: Och hvi skulle vi då hafva stulit silfver eller guld af dins herras huse?
9 Ikiwa yeyote miongoni mwa watumishi wako atapatikana nacho, auawe, na sisi wengine tutakuwa watumwa wa bwana wangu.”
När hvilken det varder funnit ibland dina tjenare, han må dö: Dertill vilje vi ock vara mins herras trälar.
10 Akajibu, “Vema sana; na iwe kama msemavyo. Yeyote atakayekutwa nacho atakuwa mtumwa wangu, lakini ninyi wengine mtakuwa hamna lawama.”
Han sade: Ja, vare som I hafven sagt: När hvilkom det finnes, han vare min träl: men I skolen vara löse.
11 Kila mmoja wao akafanya haraka kushusha gunia lake chini na kulifungua.
Och då de hastade sig, och lade hvar sin säck af ned på jordena, och hvar lät upp sin säck.
12 Ndipo msimamizi akaendelea kutafuta, akianzia kwa mkubwa wa wote na akaishia kwa mdogo wa wote. Basi kikombe kikapatikana katika gunia la Benyamini.
Och han sökte, och begynte på den första, in till den yngsta; då fans skålen i BenJamins säck.
13 Kwa jambo hili, wakararua nguo zao. Ndipo wote wakapakiza mizigo yao juu ya punda zao na kurudi mjini.
Då refvo de sin kläder, och ladde hvar uppå sin åsna, och foro åter in i staden.
14 Yosefu alikuwa bado yuko nyumbani mwake wakati Yuda na kaka zake walipoingia, wote wakajitupa chini mbele yake.
Och Juda gick med sina bröder in i Josephs hus; ty han var ändå der, och de föllo ned på jordena för honom.
15 Yosefu akawaambia, “Ni jambo gani hili mlilolifanya? Hamjui kuwa mtu kama mimi anaweza kufahamu mambo kwa njia ya kutabiri?”
Joseph sade till dem: Hvi torden I det göra? Veten I icke, att en sådana man, som jag är, kunde spå till?
16 Yuda akajibu, “Tutaweza kusema nini kwa bwana wangu? Tutaweza kuzungumza nini? Tutawezaje kuthibitisha kwamba hatuna hatia? Mungu amefunua hatia ya watumishi wako. Sasa sisi tu watumwa wa bwana wangu, sisi wenyewe pamoja na yule aliyepatikana na kikombe.”
Juda sade: Hvad skole vi säga minom herra, eller huru skole vi bära före? Gud hafver funnit dina tjenares missgerningar: Si, vi och den, som skålen är funnen när, äre min herras trälar.
17 Lakini Yosefu alisema, “Liwe mbali nami kufanya jambo kama hili! Mtu yule tu aliyekutwa na kikombe ndiye atakayekuwa mtumwa wangu. Ninyi wengine, rudini kwa baba yenu kwa amani.”
Men han sade: Bort det, att jag skulle så göra. Den mannen, som skålen är funnen när, han skall vara min träl: Men I farer med frid upp till edar fader.
18 Ndipo Yuda akamwendea na kumwambia: “Tafadhali bwana wangu, mruhusu mtumishi wako aseme neno kwa bwana wangu. Usimkasirikie mtumishi wako, ingawa wewe ni sawa na Farao mwenyewe.
Då gick Juda till honom, och sade: Min herre, låt din tjenare tala ett ord i dina öron, min herre, och din vrede harmes icke öfver din tjenare; ty du äst såsom Pharao.
19 Bwana wangu aliwauliza watumishi wake, ‘Mnaye baba au ndugu?’
Min herre frågade sina tjenare, och sade: Hafven I ock någon fader, eller broder?
20 Nasi tukakujibu, ‘Tunaye baba yetu ambaye ni mzee; pia yupo mwanawe mdogo aliyezaliwa katika uzee wake. Ndugu yake amekufa, na huyu mdogo ndiye mwana pekee kwa mama yake aliyebaki, naye baba yake anampenda.’
Då svarade vi: Vi hafve en fader, och han är gammal, och en ung dräng föddan i hans ålderdom, och hans broder är död, och han är allena blifven igen af sine moder, och hans fader hafver honom kär.
21 “Ndipo ulipowaambia watumishi wako, ‘Mleteni kwangu ili niweze kumwona kwa macho yangu mwenyewe.’
Då sade du till dina tjenare: Hafver honom hit ned till mig, och jag vill göra honom godt.
22 Nasi tukamwambia bwana wangu, ‘Kijana hawezi kumwacha baba yake; akimwacha, baba yake atakufa.’
Men vi svarade minom herra: Pilten kan icke komma ifrå sinom fader; hvar han komme honom ifrå, dödde han.
23 Lakini ukawaambia watumishi wako, ‘Ndugu yenu mdogo asiposhuka pamoja nanyi, hamtauona uso wangu tena.’
Då sade du till dina tjenare: Hvar edar yngste broder icke kommer här med eder, skolen I icke mera komma för min ögon.
24 Tuliporudi nyumbani kwa mtumwa wako baba yangu, tulimwambia lile bwana wangu alilokuwa amesema.
Då forom vi upp till din tjenare, min fader, och sadom honom mins herras tal.
25 “Ndipo baba yetu aliposema, ‘Rudini Misri mkanunue chakula kingine.’
Då sade vår fader: Farer åter bort, och köper oss någon spisning.
26 Lakini tukamwambia, ‘Hatuwezi kushuka Misri mpaka ndugu yetu mdogo awe pamoja nasi ndipo tutakapokwenda. Hatutaweza kuuona uso wa yule mtu mpaka ndugu yetu mdogo awe pamoja nasi.’
Men vi sade: Vi kunne icke fara der ned, med mindre vår yngste broder är med oss, så vilje vi fara derned; ty vi kunne icke komma för dens mansens ögon, hvar vår yngste broder icke är med oss.
27 “Mtumwa wako baba yangu alituambia, ‘Mnajua mke wangu alinizalia wana wawili.
Då sade din tjenare, min fader, till oss: I veten, att min hustru hafver födt mig två:
28 Mmojawapo alipotea, nami nikasema, “Hakika ameraruliwa vipande vipande.” Nami sijamwona tangu wakati huo.
Den ene gick bort ifrån mig, och det sades, att han skulle vara ihjälrifven; och jag hafver ej sett honom allt härtill.
29 Ikiwa mtaniondolea huyu tena na akapatwa na madhara, mtashusha kichwa changu chenye mvi kaburini nikiwa mwenye huzuni.’ (Sheol )
Skolen I ock taga denna ifrå mig, och honom vederfars något ondt, så varden I drifvande min grå hår med sorg ned i grafvena. (Sheol )
30 “Hivyo sasa, kama kijana hatakuwa pamoja nasi nitakaporudi kwa mtumishi wako baba yangu, na kama baba yangu, ambaye maisha yake yamefungamanishwa na uhai wa kijana huyu,
Om jag nu komme hem till din tjenare, min fader, och pilten vore icke med oss, efter hans själ hänger intill desses själ;
31 akiona kijana hayupo nasi, atakufa. Watumishi wako watashusha kichwa chenye mvi cha baba yetu kaburini kwa huzuni. (Sheol )
Så sker det, då han ser, att pilten icke är tillstädes, att han dör: Så vorde vi dine tjenare, dins tjenares, vårs faders grå hår förande med jämmer ned i grafvena. (Sheol )
32 Mtumwa wako alimhakikishia baba yangu usalama wa kijana. Nikamwambia, ‘Kama sikumrudisha kwako nitakuwa mwenye lawama mbele yako, baba yangu, maisha yangu yote!’
Ty jag, din tjenare, hafver varit minom fader god för pilten, och sagt: Hafver jag icke honom till dig igen, så vill jag hafva skuld i alla mina lifsdagar.
33 “Sasa basi, tafadhali mruhusu mtumishi abaki hapa kama mtumwa wa bwana wangu badala ya kijana, naye kijana umruhusu arudi na ndugu zake.
Derföre, låt din tjenare blifva här qvar minom herra för en träl i piltens stad; och låt pilten fara upp med sina bröder.
34 Ninawezaje kurudi kwa baba yangu kama kijana hatakuwa pamoja nami? La hasha! Usiniache nikaone huzuni ile itakayompata baba yangu.”
Förty, huru skulle jag fara upp till min fader, när pilten är icke med mig? Jag finge se den jämmer, som min fader uppå komme.