< Mwanzo 44 >

1 Kisha Yosefu akampa yule msimamizi wa nyumbani mwake maagizo haya: “Jaza magunia ya watu hawa kiasi cha chakula ambacho wanaweza kuchukua, na uweke fedha ya kila mtu kwenye mdomo wa gunia lake.
I zapovjedi Josif èovjeku što upravljaše kuæom njegovom govoreæi: naspi ovijem ljudima u vreæe žita koliko mogu ponijeti, i svakome u vreæu metni ozgo novce njegove.
2 Kisha weka kikombe changu kile cha fedha kwenye mdomo wa gunia la yule mdogo wa wote pamoja na fedha zake ambazo angenunulia nafaka yake.” Naye akafanya kama Yosefu alivyosema.
I èašu moju, èašu srebrnu, metni najmlaðemu u vreæu ozgo i novce za njegovo žito. I uèini kako mu Josif reèe.
3 Kulipopambazuka, hao watu wakaruhusiwa kuondoka pamoja na punda zao.
A ujutru kad svanu, otpustiše ljude s magarcima njihovijem.
4 Kabla hawajafika mbali kutoka mjini, Yosefu akamwambia mtumishi wake, “Wafuatilie wale watu mara moja, utakapowakuta, waambie, ‘Kwa nini mmelipiza wema kwa ubaya?
A kad izaðoše iz mjesta i još ne bijahu daleko, reèe Josif èovjeku što upravljaše kuæom njegovom: ustani, idi brže za onijem ljudima, i kad ih stigneš reci im: zašto vraæate zlo za dobro?
5 Je, kikombe hiki sicho anachonywea bwana wangu na pia hukitumia kwa kutabiri mambo yajayo? Hili ni jambo ovu mlilolitenda.’”
Nije li to èaša iz koje pije moj gospodar? i neæe li po njoj zacijelo poznati kakvi ste? zlo ste radili što ste to uèinili.
6 Alipowafikia, akarudia maneno haya kwao.
I on ih stiže, i reèe im tako.
7 Lakini wakamwambia mtumishi, “Kwa nini bwana wangu anasema maneno kama haya? Liwe mbali na watumishi wako wasije wakafanya jambo kama hilo!
A oni mu rekoše: zašto govoriš, gospodaru, take rijeèi? Saèuvaj Bože da sluge tvoje uèine tako što!
8 Hata hivyo tulikurudishia zile fedha kutoka nchi ya Kanaani ambazo tulizikuta kwenye midomo ya magunia yetu. Hivyo kwa nini tuibe fedha au dhahabu kutoka nyumbani kwa bwana wako?
Eno smo ti donijeli natrag iz zemlje Hananske novce koje naðosmo ozgo u vreæama svojim, pa kako bismo ukrali iz kuæe gospodara tvojega srebro ili zlato?
9 Ikiwa yeyote miongoni mwa watumishi wako atapatikana nacho, auawe, na sisi wengine tutakuwa watumwa wa bwana wangu.”
U kojega se izmeðu sluga tvojih naðe, onaj neka pogine, i svrh toga mi æemo biti robovi gospodaru mojemu.
10 Akajibu, “Vema sana; na iwe kama msemavyo. Yeyote atakayekutwa nacho atakuwa mtumwa wangu, lakini ninyi wengine mtakuwa hamna lawama.”
A on reèe: neka bude kako rekoste; ali u koga se naðe, onaj da mi bude rob, a vi ostali neæete biti krivi.
11 Kila mmoja wao akafanya haraka kushusha gunia lake chini na kulifungua.
I brže poskidaše svi na zemlju vreæe svoje, i razdriješiše svaki svoju vreæu.
12 Ndipo msimamizi akaendelea kutafuta, akianzia kwa mkubwa wa wote na akaishia kwa mdogo wa wote. Basi kikombe kikapatikana katika gunia la Benyamini.
A on stade tražiti poèev od najstarijega, i kad doðe na najmlaðega, naðe se èaša u vreæi Venijaminovoj.
13 Kwa jambo hili, wakararua nguo zao. Ndipo wote wakapakiza mizigo yao juu ya punda zao na kurudi mjini.
Tada razdriješe haljine svoje, i natovarivši svaki svoj tovar na svojega magarca vratiše se u grad.
14 Yosefu alikuwa bado yuko nyumbani mwake wakati Yuda na kaka zake walipoingia, wote wakajitupa chini mbele yake.
I doðe Juda s braæom svojom Josifu u kuæu, dok on još bijaše kod kuæe, i padoše pred njim na zemlju.
15 Yosefu akawaambia, “Ni jambo gani hili mlilolifanya? Hamjui kuwa mtu kama mimi anaweza kufahamu mambo kwa njia ya kutabiri?”
A Josif im reèe: šta ste to uèinili? zar nijeste znali da èovjek kao što sam ja može zacijelo doznati?
16 Yuda akajibu, “Tutaweza kusema nini kwa bwana wangu? Tutaweza kuzungumza nini? Tutawezaje kuthibitisha kwamba hatuna hatia? Mungu amefunua hatia ya watumishi wako. Sasa sisi tu watumwa wa bwana wangu, sisi wenyewe pamoja na yule aliyepatikana na kikombe.”
Tada reèe Juda: šta da ti reèemo, gospodaru? šta da govorimo? kako li da se pravdamo? Bog je otkrio zloèinstvo tvojih sluga. Evo, mi smo svi robovi tvoji, gospodaru, i mi i ovaj u koga se našla èaša.
17 Lakini Yosefu alisema, “Liwe mbali nami kufanya jambo kama hili! Mtu yule tu aliyekutwa na kikombe ndiye atakayekuwa mtumwa wangu. Ninyi wengine, rudini kwa baba yenu kwa amani.”
A Josif reèe: Bože saèuvaj! neæu ja to; u koga se našla èaša on neka mi bude rob, a vi idite s mirom ocu svojemu.
18 Ndipo Yuda akamwendea na kumwambia: “Tafadhali bwana wangu, mruhusu mtumishi wako aseme neno kwa bwana wangu. Usimkasirikie mtumishi wako, ingawa wewe ni sawa na Farao mwenyewe.
Ali Juda pristupiv k njemu reèe: èuj me, gospodaru; dopusti da progovori sluga tvoj gospodaru svojemu, i neka se gnjev tvoj ne raspali na slugu tvojega, jer si ti kao sam Faraon.
19 Bwana wangu aliwauliza watumishi wake, ‘Mnaye baba au ndugu?’
Gospodar moj zapita sluge svoje govoreæi: imate li oca ili brata?
20 Nasi tukakujibu, ‘Tunaye baba yetu ambaye ni mzee; pia yupo mwanawe mdogo aliyezaliwa katika uzee wake. Ndugu yake amekufa, na huyu mdogo ndiye mwana pekee kwa mama yake aliyebaki, naye baba yake anampenda.’
A mi rekosmo gospodaru svojemu: imamo stara oca i brata najmlaðega, koji mu se rodi u starosti; a njegov je brat umro, i on osta sam od matere svoje, i otac ga pazi.
21 “Ndipo ulipowaambia watumishi wako, ‘Mleteni kwangu ili niweze kumwona kwa macho yangu mwenyewe.’
A ti reèe slugama svojim: dovedite mi ga da ga vidim svojim oèima.
22 Nasi tukamwambia bwana wangu, ‘Kijana hawezi kumwacha baba yake; akimwacha, baba yake atakufa.’
I rekosmo gospodaru svojemu: neæe moæi dijete ostaviti oca svojega; da ostavi oca svojega, odmah æe otac umrijeti.
23 Lakini ukawaambia watumishi wako, ‘Ndugu yenu mdogo asiposhuka pamoja nanyi, hamtauona uso wangu tena.’
A ti reèe slugama svojim: ako ne doðe s vama brat vaš najmlaði, neæete više vidjeti lica mojega.
24 Tuliporudi nyumbani kwa mtumwa wako baba yangu, tulimwambia lile bwana wangu alilokuwa amesema.
A kad se vratismo k sluzi tvojemu a ocu mojemu, kazasmo mu rijeèi gospodara mojega.
25 “Ndipo baba yetu aliposema, ‘Rudini Misri mkanunue chakula kingine.’
Poslije reèe nam otac: idite opet, kupite nam hrane.
26 Lakini tukamwambia, ‘Hatuwezi kushuka Misri mpaka ndugu yetu mdogo awe pamoja nasi ndipo tutakapokwenda. Hatutaweza kuuona uso wa yule mtu mpaka ndugu yetu mdogo awe pamoja nasi.’
A mi rekosmo: ne možemo iæi, osim ako bude brat naš najmlaði s nama, onda æemo iæi, jer ne možemo vidjeti lica onoga èovjeka, ako ne bude s nama brat naš najmlaði.
27 “Mtumwa wako baba yangu alituambia, ‘Mnajua mke wangu alinizalia wana wawili.
A sluga tvoj, otac moj, reèe nam: znate da mi je žena rodila dva sina.
28 Mmojawapo alipotea, nami nikasema, “Hakika ameraruliwa vipande vipande.” Nami sijamwona tangu wakati huo.
I jedan od njih otide od mene, i rekoh: zacijelo ga je raskinula zvjerka; i do sada ga ne vidjeh.
29 Ikiwa mtaniondolea huyu tena na akapatwa na madhara, mtashusha kichwa changu chenye mvi kaburini nikiwa mwenye huzuni.’ (Sheol h7585)
Ako i ovoga odvedete od mene i zadesi ga kakvo zlo, svaliæete me stara u grob s tugom. (Sheol h7585)
30 “Hivyo sasa, kama kijana hatakuwa pamoja nasi nitakaporudi kwa mtumishi wako baba yangu, na kama baba yangu, ambaye maisha yake yamefungamanishwa na uhai wa kijana huyu,
Pa sada da otidem k sluzi tvojemu, ocu svojemu, a ovo dijete da ne bude s nama, kako je duša onoga vezana za dušu ovoga,
31 akiona kijana hayupo nasi, atakufa. Watumishi wako watashusha kichwa chenye mvi cha baba yetu kaburini kwa huzuni. (Sheol h7585)
Umrijeæe kad vidi da nema djeteta, te æe sluge tvoje svaliti staroga slugu tvojega a oca svojega s tugom u grob. (Sheol h7585)
32 Mtumwa wako alimhakikishia baba yangu usalama wa kijana. Nikamwambia, ‘Kama sikumrudisha kwako nitakuwa mwenye lawama mbele yako, baba yangu, maisha yangu yote!’
A tvoj se sluga podjemèio za dijete ocu svojemu rekav: ako ti ga ne dovedem natrag, da sam kriv ocu svojemu dovijeka.
33 “Sasa basi, tafadhali mruhusu mtumishi abaki hapa kama mtumwa wa bwana wangu badala ya kijana, naye kijana umruhusu arudi na ndugu zake.
Zato neka sluga tvoj ostane mjesto djeteta da bude rob gospodaru mojemu a dijete neka ide s braæom svojom.
34 Ninawezaje kurudi kwa baba yangu kama kijana hatakuwa pamoja nami? La hasha! Usiniache nikaone huzuni ile itakayompata baba yangu.”
Jer kako bih se vratio k ocu svojemu bez djeteta, da gledam jade koji bi mi oca zadesili?

< Mwanzo 44 >