< Mwanzo 44 >

1 Kisha Yosefu akampa yule msimamizi wa nyumbani mwake maagizo haya: “Jaza magunia ya watu hawa kiasi cha chakula ambacho wanaweza kuchukua, na uweke fedha ya kila mtu kwenye mdomo wa gunia lake.
Il donna cet ordre à l'intendant de sa maison: « Remplissez de nourriture les sacs des hommes, autant qu'ils peuvent en porter, et mettez l'argent de chacun dans l'ouverture de son sac.
2 Kisha weka kikombe changu kile cha fedha kwenye mdomo wa gunia la yule mdogo wa wote pamoja na fedha zake ambazo angenunulia nafaka yake.” Naye akafanya kama Yosefu alivyosema.
Mets ma coupe, la coupe d'argent, dans l'ouverture du sac du plus jeune, avec son argent. » Il fit selon la parole que Joseph avait dite.
3 Kulipopambazuka, hao watu wakaruhusiwa kuondoka pamoja na punda zao.
Dès que le matin se leva, les hommes partirent, eux et leurs ânes.
4 Kabla hawajafika mbali kutoka mjini, Yosefu akamwambia mtumishi wake, “Wafuatilie wale watu mara moja, utakapowakuta, waambie, ‘Kwa nini mmelipiza wema kwa ubaya?
Lorsqu'ils sortirent de la ville et qu'ils ne furent pas encore loin, Joseph dit à son intendant: « Monte, suis les hommes. Quand tu les auras rattrapés, demande-leur: Pourquoi avez-vous rendu le mal pour le bien?
5 Je, kikombe hiki sicho anachonywea bwana wangu na pia hukitumia kwa kutabiri mambo yajayo? Hili ni jambo ovu mlilolitenda.’”
N'est-ce pas là ce que boit mon seigneur et ce par quoi il devine? Vous avez fait le mal en agissant ainsi ».
6 Alipowafikia, akarudia maneno haya kwao.
Il les rattrapa et leur adressa ces paroles.
7 Lakini wakamwambia mtumishi, “Kwa nini bwana wangu anasema maneno kama haya? Liwe mbali na watumishi wako wasije wakafanya jambo kama hilo!
Ils lui dirent: « Pourquoi mon seigneur tient-il de tels propos? Loin de tes serviteurs l'idée de faire une telle chose!
8 Hata hivyo tulikurudishia zile fedha kutoka nchi ya Kanaani ambazo tulizikuta kwenye midomo ya magunia yetu. Hivyo kwa nini tuibe fedha au dhahabu kutoka nyumbani kwa bwana wako?
Voici, l'argent que nous avons trouvé dans la bouche de nos sacs, nous te l'avons rapporté du pays de Canaan. Comment donc voler de l'argent ou de l'or dans la maison de ton seigneur?
9 Ikiwa yeyote miongoni mwa watumishi wako atapatikana nacho, auawe, na sisi wengine tutakuwa watumwa wa bwana wangu.”
Chez celui de tes serviteurs chez qui on le trouvera, qu'il meure, et nous aussi nous serons les esclaves de mon seigneur. »
10 Akajibu, “Vema sana; na iwe kama msemavyo. Yeyote atakayekutwa nacho atakuwa mtumwa wangu, lakini ninyi wengine mtakuwa hamna lawama.”
Il dit: « Qu'il en soit maintenant ainsi selon vos paroles. Celui chez qui elle sera trouvée sera mon esclave; et toi, tu seras irréprochable. »
11 Kila mmoja wao akafanya haraka kushusha gunia lake chini na kulifungua.
Ils se hâtèrent alors de descendre leur sac à terre, et chacun ouvrit son sac.
12 Ndipo msimamizi akaendelea kutafuta, akianzia kwa mkubwa wa wote na akaishia kwa mdogo wa wote. Basi kikombe kikapatikana katika gunia la Benyamini.
Il chercha, en commençant par le plus âgé et en terminant par le plus jeune. La coupe fut trouvée dans le sac de Benjamin.
13 Kwa jambo hili, wakararua nguo zao. Ndipo wote wakapakiza mizigo yao juu ya punda zao na kurudi mjini.
Puis ils déchirèrent leurs vêtements, chargèrent chacun leur âne et retournèrent à la ville.
14 Yosefu alikuwa bado yuko nyumbani mwake wakati Yuda na kaka zake walipoingia, wote wakajitupa chini mbele yake.
Juda et ses frères arrivèrent à la maison de Joseph, et il était encore là. Ils se jetèrent à terre devant lui.
15 Yosefu akawaambia, “Ni jambo gani hili mlilolifanya? Hamjui kuwa mtu kama mimi anaweza kufahamu mambo kwa njia ya kutabiri?”
Joseph leur dit: « Quelle est cette action que vous avez commise? Ne savez-vous pas qu'un homme tel que moi peut effectivement faire de la divination? ».
16 Yuda akajibu, “Tutaweza kusema nini kwa bwana wangu? Tutaweza kuzungumza nini? Tutawezaje kuthibitisha kwamba hatuna hatia? Mungu amefunua hatia ya watumishi wako. Sasa sisi tu watumwa wa bwana wangu, sisi wenyewe pamoja na yule aliyepatikana na kikombe.”
Juda dit: « Que dirons-nous à mon seigneur? Que dirons-nous? Comment allons-nous nous disculper? Dieu a découvert l'iniquité de tes serviteurs. Voici, nous sommes les esclaves de mon seigneur, nous et celui dans la main duquel se trouve la coupe. »
17 Lakini Yosefu alisema, “Liwe mbali nami kufanya jambo kama hili! Mtu yule tu aliyekutwa na kikombe ndiye atakayekuwa mtumwa wangu. Ninyi wengine, rudini kwa baba yenu kwa amani.”
Il répondit: « Loin de moi l'idée de faire cela. L'homme dans la main duquel se trouve la coupe sera mon esclave; quant à toi, monte en paix vers ton père. »
18 Ndipo Yuda akamwendea na kumwambia: “Tafadhali bwana wangu, mruhusu mtumishi wako aseme neno kwa bwana wangu. Usimkasirikie mtumishi wako, ingawa wewe ni sawa na Farao mwenyewe.
Alors Juda s'approcha de lui, et dit: « Oh, mon seigneur, permets à ton serviteur de dire une parole aux oreilles de mon seigneur, et ne laisse pas ta colère s'enflammer contre ton serviteur, car tu es comme Pharaon.
19 Bwana wangu aliwauliza watumishi wake, ‘Mnaye baba au ndugu?’
Mon seigneur a demandé à ses serviteurs: « Avez-vous un père ou un frère? »
20 Nasi tukakujibu, ‘Tunaye baba yetu ambaye ni mzee; pia yupo mwanawe mdogo aliyezaliwa katika uzee wake. Ndugu yake amekufa, na huyu mdogo ndiye mwana pekee kwa mama yake aliyebaki, naye baba yake anampenda.’
Nous avons répondu à mon seigneur: « Nous avons un père, un vieillard, et un enfant de sa vieillesse, un petit garçon; son frère est mort, et il reste seul de sa mère; et son père l'aime.
21 “Ndipo ulipowaambia watumishi wako, ‘Mleteni kwangu ili niweze kumwona kwa macho yangu mwenyewe.’
Tu as dit à tes serviteurs: « Faites-le descendre vers moi, afin que je pose mes yeux sur lui.
22 Nasi tukamwambia bwana wangu, ‘Kijana hawezi kumwacha baba yake; akimwacha, baba yake atakufa.’
Nous avons dit à mon seigneur: « Le garçon ne peut pas quitter son père, car s'il le quittait, son père mourrait. »
23 Lakini ukawaambia watumishi wako, ‘Ndugu yenu mdogo asiposhuka pamoja nanyi, hamtauona uso wangu tena.’
Tu as dit à tes serviteurs: « Si ton plus jeune frère ne descend pas avec vous, vous ne verrez plus ma face.
24 Tuliporudi nyumbani kwa mtumwa wako baba yangu, tulimwambia lile bwana wangu alilokuwa amesema.
Lorsque nous sommes montés vers ton serviteur, mon père, nous lui avons rapporté les paroles de mon seigneur.
25 “Ndipo baba yetu aliposema, ‘Rudini Misri mkanunue chakula kingine.’
Notre père nous dit: « Retourne acheter un peu de nourriture.
26 Lakini tukamwambia, ‘Hatuwezi kushuka Misri mpaka ndugu yetu mdogo awe pamoja nasi ndipo tutakapokwenda. Hatutaweza kuuona uso wa yule mtu mpaka ndugu yetu mdogo awe pamoja nasi.’
Nous avons répondu: « Nous ne pouvons pas descendre. Si notre plus jeune frère est avec nous, nous descendrons, car nous ne verrons peut-être pas le visage de cet homme, à moins que notre plus jeune frère ne soit avec nous.
27 “Mtumwa wako baba yangu alituambia, ‘Mnajua mke wangu alinizalia wana wawili.
Ton serviteur, mon père, nous a dit: « Vous savez que ma femme m'a enfanté deux fils.
28 Mmojawapo alipotea, nami nikasema, “Hakika ameraruliwa vipande vipande.” Nami sijamwona tangu wakati huo.
L'un d'eux est sorti de chez moi, et j'ai dit: « Certainement, il est déchiré en morceaux »; et je ne l'ai pas revu depuis.
29 Ikiwa mtaniondolea huyu tena na akapatwa na madhara, mtashusha kichwa changu chenye mvi kaburini nikiwa mwenye huzuni.’ (Sheol h7585)
Si tu m'enlèves aussi celui-ci, et qu'il lui arrive malheur, tu feras descendre mes cheveux blancs avec tristesse au séjour des morts'. (Sheol h7585)
30 “Hivyo sasa, kama kijana hatakuwa pamoja nasi nitakaporudi kwa mtumishi wako baba yangu, na kama baba yangu, ambaye maisha yake yamefungamanishwa na uhai wa kijana huyu,
Maintenant, quand j'arriverai chez ton serviteur, mon père, et que le garçon ne sera pas avec nous, puisque sa vie est liée à celle du garçon,
31 akiona kijana hayupo nasi, atakufa. Watumishi wako watashusha kichwa chenye mvi cha baba yetu kaburini kwa huzuni. (Sheol h7585)
il arrivera, quand il verra que le garçon n'est plus, qu'il mourra. Tes serviteurs feront descendre avec douleur au séjour des morts les cheveux blancs de ton serviteur, notre père. (Sheol h7585)
32 Mtumwa wako alimhakikishia baba yangu usalama wa kijana. Nikamwambia, ‘Kama sikumrudisha kwako nitakuwa mwenye lawama mbele yako, baba yangu, maisha yangu yote!’
Car ton serviteur s'est porté garant de l'enfant auprès de mon père, en disant: « Si je ne te l'amène pas, c'est moi qui en porterai la responsabilité auprès de mon père pour toujours ».
33 “Sasa basi, tafadhali mruhusu mtumishi abaki hapa kama mtumwa wa bwana wangu badala ya kijana, naye kijana umruhusu arudi na ndugu zake.
Maintenant donc, que ton serviteur reste à la place du garçon, esclave de mon seigneur, et que le garçon monte avec ses frères.
34 Ninawezaje kurudi kwa baba yangu kama kijana hatakuwa pamoja nami? La hasha! Usiniache nikaone huzuni ile itakayompata baba yangu.”
Car comment monterai-je vers mon père, si le garçon n'est pas avec moi? de peur que je ne voie le malheur qui frappera mon père. »

< Mwanzo 44 >