< Mwanzo 44 >

1 Kisha Yosefu akampa yule msimamizi wa nyumbani mwake maagizo haya: “Jaza magunia ya watu hawa kiasi cha chakula ambacho wanaweza kuchukua, na uweke fedha ya kila mtu kwenye mdomo wa gunia lake.
And he commaunded the rueler of his house saynge: fyll the mens sackes with food as moch as they can carie
2 Kisha weka kikombe changu kile cha fedha kwenye mdomo wa gunia la yule mdogo wa wote pamoja na fedha zake ambazo angenunulia nafaka yake.” Naye akafanya kama Yosefu alivyosema.
and put euery mans money in his bagge mouth and put my syluer cuppe in the sackes mouth of the yongest and his corne money also. And he dyd as Ioseph had sayde.
3 Kulipopambazuka, hao watu wakaruhusiwa kuondoka pamoja na punda zao.
And in ye mornynge as soone as it was lighte the me were let goo with their asses.
4 Kabla hawajafika mbali kutoka mjini, Yosefu akamwambia mtumishi wake, “Wafuatilie wale watu mara moja, utakapowakuta, waambie, ‘Kwa nini mmelipiza wema kwa ubaya?
And when they were out of the cytie and not yet ferre awaye Ioseph sayde vnto the ruelar of his house: vp and folowe after the men and ouertake them and saye vnto them: wherefore haue ye rewarded euell for good?
5 Je, kikombe hiki sicho anachonywea bwana wangu na pia hukitumia kwa kutabiri mambo yajayo? Hili ni jambo ovu mlilolitenda.’”
is that not the cuppe of which my lorde drynketh ad doth he not prophesie therin? ye haue euell done that ye haue done.
6 Alipowafikia, akarudia maneno haya kwao.
And he ouertoke them and sayde the same wordes vnto them.
7 Lakini wakamwambia mtumishi, “Kwa nini bwana wangu anasema maneno kama haya? Liwe mbali na watumishi wako wasije wakafanya jambo kama hilo!
And they answered him: wherfore sayth my lorde soch wordes? God forbydd that thy servauntes shulde doo so.
8 Hata hivyo tulikurudishia zile fedha kutoka nchi ya Kanaani ambazo tulizikuta kwenye midomo ya magunia yetu. Hivyo kwa nini tuibe fedha au dhahabu kutoka nyumbani kwa bwana wako?
Beholde the money which we founde in oure sackes mouthes we brought agayne vnto the out of the lande of Canaa: how then shulde we steale out of my lordes house ether syluer or golde?
9 Ikiwa yeyote miongoni mwa watumishi wako atapatikana nacho, auawe, na sisi wengine tutakuwa watumwa wa bwana wangu.”
with whosoeuer of thy seruauntes it be founde let him dye and let vs also be my lordes bondmen.
10 Akajibu, “Vema sana; na iwe kama msemavyo. Yeyote atakayekutwa nacho atakuwa mtumwa wangu, lakini ninyi wengine mtakuwa hamna lawama.”
And he sayde: Now therfore acordynge vnto youre woordes he with whom it is found shalbe my seruaunte: but ye shalbe harmelesse.
11 Kila mmoja wao akafanya haraka kushusha gunia lake chini na kulifungua.
And attonce euery man toke downe his sacke to the grounde ad every man opened his sacke.
12 Ndipo msimamizi akaendelea kutafuta, akianzia kwa mkubwa wa wote na akaishia kwa mdogo wa wote. Basi kikombe kikapatikana katika gunia la Benyamini.
And he serched and began at the eldest and left at the yongest. And the cuppe was founde in Ben Iamins sacke.
13 Kwa jambo hili, wakararua nguo zao. Ndipo wote wakapakiza mizigo yao juu ya punda zao na kurudi mjini.
Then they rent their clothes and laded euery man his asse and went agayne vnto the cytie.
14 Yosefu alikuwa bado yuko nyumbani mwake wakati Yuda na kaka zake walipoingia, wote wakajitupa chini mbele yake.
And Iuda and his brethre came to Iosephs house for he was yet there ad they fell before him on the grounde.
15 Yosefu akawaambia, “Ni jambo gani hili mlilolifanya? Hamjui kuwa mtu kama mimi anaweza kufahamu mambo kwa njia ya kutabiri?”
And Ioseph sayde vnto the: what dede is this which ye haue done? wist ye not that soch a man as I can prophesie?
16 Yuda akajibu, “Tutaweza kusema nini kwa bwana wangu? Tutaweza kuzungumza nini? Tutawezaje kuthibitisha kwamba hatuna hatia? Mungu amefunua hatia ya watumishi wako. Sasa sisi tu watumwa wa bwana wangu, sisi wenyewe pamoja na yule aliyepatikana na kikombe.”
Then sayde Iuda: what shall we saye vnto my lorde what shall we speake or what excuse can we make? God hath founde out ye wekednesse of thy seruauntes. Beholde both we and he with whom the cuppe is founde are thy seruauntes.
17 Lakini Yosefu alisema, “Liwe mbali nami kufanya jambo kama hili! Mtu yule tu aliyekutwa na kikombe ndiye atakayekuwa mtumwa wangu. Ninyi wengine, rudini kwa baba yenu kwa amani.”
And he answered: God forbyd ye I shulde do so the man with whom the cuppe is founde he shalbe my seruaunte: but goo ye in peace vn to youre father.
18 Ndipo Yuda akamwendea na kumwambia: “Tafadhali bwana wangu, mruhusu mtumishi wako aseme neno kwa bwana wangu. Usimkasirikie mtumishi wako, ingawa wewe ni sawa na Farao mwenyewe.
Then Iuda went vnto him and sayde: oh my lorde let thy servaunte speake a worde in my lordes audyence and be not wrooth with thi servaunte: for thou art euen as Pharao.
19 Bwana wangu aliwauliza watumishi wake, ‘Mnaye baba au ndugu?’
My lorde axed his seruaunte sainge: haue ye a father or a brother?
20 Nasi tukakujibu, ‘Tunaye baba yetu ambaye ni mzee; pia yupo mwanawe mdogo aliyezaliwa katika uzee wake. Ndugu yake amekufa, na huyu mdogo ndiye mwana pekee kwa mama yake aliyebaki, naye baba yake anampenda.’
And we answered my lord we haue a father that is old and a yonge lad which he begat in his age: ad the brother of the sayde lad is dead and he is all that is left of that mother. And his father loueth him.
21 “Ndipo ulipowaambia watumishi wako, ‘Mleteni kwangu ili niweze kumwona kwa macho yangu mwenyewe.’
Then sayde my lorde vnto his seruauntes brynge him vnto me that I maye sett myne eyes apon him.
22 Nasi tukamwambia bwana wangu, ‘Kijana hawezi kumwacha baba yake; akimwacha, baba yake atakufa.’
And we answered my lorde that the lad coude not goo from his father for if he shulde leaue his father he were but a deed man.
23 Lakini ukawaambia watumishi wako, ‘Ndugu yenu mdogo asiposhuka pamoja nanyi, hamtauona uso wangu tena.’
Than saydest thou vnto thy servauntes: excepte youre yongest brother come with you loke that ye se my face no moare.
24 Tuliporudi nyumbani kwa mtumwa wako baba yangu, tulimwambia lile bwana wangu alilokuwa amesema.
And when we came vnto thy servaunt oure father we shewed him what my lorde had sayde.
25 “Ndipo baba yetu aliposema, ‘Rudini Misri mkanunue chakula kingine.’
And when oure father sayde vnto vs goo agayne and bye vs a litle fode:
26 Lakini tukamwambia, ‘Hatuwezi kushuka Misri mpaka ndugu yetu mdogo awe pamoja nasi ndipo tutakapokwenda. Hatutaweza kuuona uso wa yule mtu mpaka ndugu yetu mdogo awe pamoja nasi.’
we sayd yt we coude not goo. Neverthelesse if oure youngeste brother go with vs then will we goo for we maye not see the mannes face excepte oure yongest brother be with vs.
27 “Mtumwa wako baba yangu alituambia, ‘Mnajua mke wangu alinizalia wana wawili.
Then sayde thy servaunt oure father vnto vs. Ye knowe that my wyfe bare me. ij. sonnes.
28 Mmojawapo alipotea, nami nikasema, “Hakika ameraruliwa vipande vipande.” Nami sijamwona tangu wakati huo.
And the one went out from me and it is sayde of a suertie that he is torne in peaces of wyld beastes and I sawe him not sence.
29 Ikiwa mtaniondolea huyu tena na akapatwa na madhara, mtashusha kichwa changu chenye mvi kaburini nikiwa mwenye huzuni.’ (Sheol h7585)
Yf ye shall take this also awaye fro me and some mysfortune happen apon him then shall ye brynge my gray heed with sorow vnto the grave. (Sheol h7585)
30 “Hivyo sasa, kama kijana hatakuwa pamoja nasi nitakaporudi kwa mtumishi wako baba yangu, na kama baba yangu, ambaye maisha yake yamefungamanishwa na uhai wa kijana huyu,
Now therfore whe I come to thy servaunt my father yf the lad be not with me: seinge that his lyfe hageth by the laddes lyfe
31 akiona kijana hayupo nasi, atakufa. Watumishi wako watashusha kichwa chenye mvi cha baba yetu kaburini kwa huzuni. (Sheol h7585)
then as soone as he seeth that the lad is not come he will dye. So shall we thy servautes brynge the gray hedde of thy servaunt oure father with sorow vnto the grave. (Sheol h7585)
32 Mtumwa wako alimhakikishia baba yangu usalama wa kijana. Nikamwambia, ‘Kama sikumrudisha kwako nitakuwa mwenye lawama mbele yako, baba yangu, maisha yangu yote!’
For I thy servaunt became suertie for the lad vnto my father and sayde: yf I bringe him not vnto the agayne. I will bere the blame all my life loge.
33 “Sasa basi, tafadhali mruhusu mtumishi abaki hapa kama mtumwa wa bwana wangu badala ya kijana, naye kijana umruhusu arudi na ndugu zake.
Now therfore let me thy servaunt byde here for ye lad and be my lordes bondman: and let the lad goo home with his brethern.
34 Ninawezaje kurudi kwa baba yangu kama kijana hatakuwa pamoja nami? La hasha! Usiniache nikaone huzuni ile itakayompata baba yangu.”
For how can I goo vnto my father and the lad not wyth me: lest I shulde see the wretchednes that shall come on my father.

< Mwanzo 44 >