< Mwanzo 44 >

1 Kisha Yosefu akampa yule msimamizi wa nyumbani mwake maagizo haya: “Jaza magunia ya watu hawa kiasi cha chakula ambacho wanaweza kuchukua, na uweke fedha ya kila mtu kwenye mdomo wa gunia lake.
And he commanded [the one] who [was] over household his saying fill [the] sacks of the men food just as they are able! to carry and put [the] silver of each man in [the] mouth of sack his.
2 Kisha weka kikombe changu kile cha fedha kwenye mdomo wa gunia la yule mdogo wa wote pamoja na fedha zake ambazo angenunulia nafaka yake.” Naye akafanya kama Yosefu alivyosema.
And cup my [the] cup of silver you will put in [the] mouth of [the] sack of the young [brother] and [the] silver of grain his and he did according to [the] word of Joseph which he had spoken.
3 Kulipopambazuka, hao watu wakaruhusiwa kuondoka pamoja na punda zao.
The morning it was light and the men they were sent off they and donkeys their.
4 Kabla hawajafika mbali kutoka mjini, Yosefu akamwambia mtumishi wake, “Wafuatilie wale watu mara moja, utakapowakuta, waambie, ‘Kwa nini mmelipiza wema kwa ubaya?
They they came out the city not they had gone far and Joseph he said to [the one] who [was] over household his arise pursue after the men and you will overtake them and you will say to them why? have you repaid evil for good.
5 Je, kikombe hiki sicho anachonywea bwana wangu na pia hukitumia kwa kutabiri mambo yajayo? Hili ni jambo ovu mlilolitenda.’”
¿ Not [is] this [that] which he drinks master my in it and he indeed he practices divination by it you have done evil [that] which you have done.
6 Alipowafikia, akarudia maneno haya kwao.
And he overtook them and he spoke to them the words these.
7 Lakini wakamwambia mtumishi, “Kwa nini bwana wangu anasema maneno kama haya? Liwe mbali na watumishi wako wasije wakafanya jambo kama hilo!
And they said to him why? does he speak master my according to the words these far be it to servants your from doing according to the manner this.
8 Hata hivyo tulikurudishia zile fedha kutoka nchi ya Kanaani ambazo tulizikuta kwenye midomo ya magunia yetu. Hivyo kwa nini tuibe fedha au dhahabu kutoka nyumbani kwa bwana wako?
Here! silver which we found in [the] mouth of sacks our we brought back to you from [the] land of Canaan and how? will we steal from [the] house of master your silver or gold.
9 Ikiwa yeyote miongoni mwa watumishi wako atapatikana nacho, auawe, na sisi wengine tutakuwa watumwa wa bwana wangu.”
[anyone] whom It is found with him of servants your and he will die and also we we will be[long] to lord my to slaves.
10 Akajibu, “Vema sana; na iwe kama msemavyo. Yeyote atakayekutwa nacho atakuwa mtumwa wangu, lakini ninyi wengine mtakuwa hamna lawama.”
And he said also now according to words your [will be] so it [anyone] whom it is found with him he will be of me slave and you you will be innocent.
11 Kila mmoja wao akafanya haraka kushusha gunia lake chini na kulifungua.
And they hurried and they brought down each man sack his [the] ground towards and they opened each man sack his.
12 Ndipo msimamizi akaendelea kutafuta, akianzia kwa mkubwa wa wote na akaishia kwa mdogo wa wote. Basi kikombe kikapatikana katika gunia la Benyamini.
And he searched with the old [brother] he began and with the young [brother] he finished and it was found the cup in [the] sack of Benjamin.
13 Kwa jambo hili, wakararua nguo zao. Ndipo wote wakapakiza mizigo yao juu ya punda zao na kurudi mjini.
And they tore clothes their and he loaded each man on donkey his and they went back the city towards.
14 Yosefu alikuwa bado yuko nyumbani mwake wakati Yuda na kaka zake walipoingia, wote wakajitupa chini mbele yake.
And he came Judah and brothers his [the] house of towards Joseph and he still he [was] there and they fell before him [the] ground towards.
15 Yosefu akawaambia, “Ni jambo gani hili mlilolifanya? Hamjui kuwa mtu kama mimi anaweza kufahamu mambo kwa njia ya kutabiri?”
And he said to them Joseph what? [is] the deed this which you have done ¿ not do you know that indeed he practices divination a man who [is] like me.
16 Yuda akajibu, “Tutaweza kusema nini kwa bwana wangu? Tutaweza kuzungumza nini? Tutawezaje kuthibitisha kwamba hatuna hatia? Mungu amefunua hatia ya watumishi wako. Sasa sisi tu watumwa wa bwana wangu, sisi wenyewe pamoja na yule aliyepatikana na kikombe.”
And he said Judah what? will we say to lord my what? will we speak and what? will we justify ourselves God he has found [the] guilt of servants your here we [are] slaves of lord my both we as well as [the one] who it was found the cup in hand his.
17 Lakini Yosefu alisema, “Liwe mbali nami kufanya jambo kama hili! Mtu yule tu aliyekutwa na kikombe ndiye atakayekuwa mtumwa wangu. Ninyi wengine, rudini kwa baba yenu kwa amani.”
And he said far be it to me from doing this the man whom it was found the cup in hand his he he will be of me slave and you go up to peace to father your.
18 Ndipo Yuda akamwendea na kumwambia: “Tafadhali bwana wangu, mruhusu mtumishi wako aseme neno kwa bwana wangu. Usimkasirikie mtumishi wako, ingawa wewe ni sawa na Farao mwenyewe.
And he drew near to him Judah and he said pardon me O lord my may he speak please servant your a word in [the] ears of lord my and may not it burn anger your on servant your for as you as Pharaoh.
19 Bwana wangu aliwauliza watumishi wake, ‘Mnaye baba au ndugu?’
Lord my he asked servants his saying ¿ [does] there [belong] to you a father or a brother.
20 Nasi tukakujibu, ‘Tunaye baba yetu ambaye ni mzee; pia yupo mwanawe mdogo aliyezaliwa katika uzee wake. Ndugu yake amekufa, na huyu mdogo ndiye mwana pekee kwa mama yake aliyebaki, naye baba yake anampenda.’
And we said to lord my there [belongs] to us a father old and a child of old age young and brother his he died and he was left he to only him to mother his and father his he loves him.
21 “Ndipo ulipowaambia watumishi wako, ‘Mleteni kwangu ili niweze kumwona kwa macho yangu mwenyewe.’
And you said to servants your bring down him to me so let me set eye my on him.
22 Nasi tukamwambia bwana wangu, ‘Kijana hawezi kumwacha baba yake; akimwacha, baba yake atakufa.’
And we said to lord my not he will be able the young man to leave father his and he will leave father his and he will die.
23 Lakini ukawaambia watumishi wako, ‘Ndugu yenu mdogo asiposhuka pamoja nanyi, hamtauona uso wangu tena.’
And you said to servants your if not he will come down brother your young with you not you will repeat! to see face my.
24 Tuliporudi nyumbani kwa mtumwa wako baba yangu, tulimwambia lile bwana wangu alilokuwa amesema.
And it was that we went up to servant your father my and we told to him [the] words of lord my.
25 “Ndipo baba yetu aliposema, ‘Rudini Misri mkanunue chakula kingine.’
And he said father our go back buy for us a little of food.
26 Lakini tukamwambia, ‘Hatuwezi kushuka Misri mpaka ndugu yetu mdogo awe pamoja nasi ndipo tutakapokwenda. Hatutaweza kuuona uso wa yule mtu mpaka ndugu yetu mdogo awe pamoja nasi.’
And we said not we are able to go down if there [is] brother our young with us and we will go down for not we will be able to see [the] face of the man and brother our young not he [is] with us.
27 “Mtumwa wako baba yangu alituambia, ‘Mnajua mke wangu alinizalia wana wawili.
And he said servant your father my to us you you know that two [sons] she bore to me wife my.
28 Mmojawapo alipotea, nami nikasema, “Hakika ameraruliwa vipande vipande.” Nami sijamwona tangu wakati huo.
And he went out the one from with me and I said surely certainly he has been torn to pieces and not I have seen him until now.
29 Ikiwa mtaniondolea huyu tena na akapatwa na madhara, mtashusha kichwa changu chenye mvi kaburini nikiwa mwenye huzuni.’ (Sheol h7585)
And you will take also this [one] from with presence my and it will happen to him harm and you will cause to go down gray hair my in calamity Sheol towards. (Sheol h7585)
30 “Hivyo sasa, kama kijana hatakuwa pamoja nasi nitakaporudi kwa mtumishi wako baba yangu, na kama baba yangu, ambaye maisha yake yamefungamanishwa na uhai wa kijana huyu,
And therefore when come I to servant your father my and the lad not [is] he with us and life his [is] bound up with life his.
31 akiona kijana hayupo nasi, atakufa. Watumishi wako watashusha kichwa chenye mvi cha baba yetu kaburini kwa huzuni. (Sheol h7585)
And it will be when sees he that there not [is] the young man and he will die and they will bring down servants your [the] gray hair of servant your father our in sorrow Sheol towards. (Sheol h7585)
32 Mtumwa wako alimhakikishia baba yangu usalama wa kijana. Nikamwambia, ‘Kama sikumrudisha kwako nitakuwa mwenye lawama mbele yako, baba yangu, maisha yangu yote!’
For servant your he stood surety for the young man from with father my saying if not I will bring him to you and I will be culpable to father my all the days.
33 “Sasa basi, tafadhali mruhusu mtumishi abaki hapa kama mtumwa wa bwana wangu badala ya kijana, naye kijana umruhusu arudi na ndugu zake.
And therefore let him remain please servant your in place of the young man a slave of lord my and the lad let him go up with brothers his.
34 Ninawezaje kurudi kwa baba yangu kama kijana hatakuwa pamoja nami? La hasha! Usiniache nikaone huzuni ile itakayompata baba yangu.”
For how? will I go up to father my and the lad not [is] he with me lest I should look on the calamity which it will find father my.

< Mwanzo 44 >