< Mwanzo 44 >

1 Kisha Yosefu akampa yule msimamizi wa nyumbani mwake maagizo haya: “Jaza magunia ya watu hawa kiasi cha chakula ambacho wanaweza kuchukua, na uweke fedha ya kila mtu kwenye mdomo wa gunia lake.
Og han befalede den, som forestod hans Hus, og sagde: Fyld Mændenes Poser med Spise, efter som de kunne føre, og læg hvers Penge øverst i hans Pose!
2 Kisha weka kikombe changu kile cha fedha kwenye mdomo wa gunia la yule mdogo wa wote pamoja na fedha zake ambazo angenunulia nafaka yake.” Naye akafanya kama Yosefu alivyosema.
Og min Skaal, den Sølvskaal, skal du lægge øverst i den yngstes Pose og Pengene for hans Korn; og han gjorde efter Josefs Ord, som han havde sagt.
3 Kulipopambazuka, hao watu wakaruhusiwa kuondoka pamoja na punda zao.
Om Morgenen, der det blev lyst, bleve Mændene sendte bort, de og deres Asener.
4 Kabla hawajafika mbali kutoka mjini, Yosefu akamwambia mtumishi wake, “Wafuatilie wale watu mara moja, utakapowakuta, waambie, ‘Kwa nini mmelipiza wema kwa ubaya?
Der de vare dragne ud af Staden og ikke vare komne langt, sagde Josef til den, som forestod hans Hus: Staa op, forfølg Mændene, og naar du naar dem, da skal du sige til dem: hvorfor have I betalt ondt for godt?
5 Je, kikombe hiki sicho anachonywea bwana wangu na pia hukitumia kwa kutabiri mambo yajayo? Hili ni jambo ovu mlilolitenda.’”
Er det ikke den, som min Herre drikker af? og hvorved han spaar? I have gjort ilde i, hvad I have gjort.
6 Alipowafikia, akarudia maneno haya kwao.
Og han naaede dem og talede disse Ord til dem.
7 Lakini wakamwambia mtumishi, “Kwa nini bwana wangu anasema maneno kama haya? Liwe mbali na watumishi wako wasije wakafanya jambo kama hilo!
Og de sagde til ham: Hvi taler min Herre saadanne Ord? det være langt fra dine Tjenere at gøre saadan Gerning.
8 Hata hivyo tulikurudishia zile fedha kutoka nchi ya Kanaani ambazo tulizikuta kwenye midomo ya magunia yetu. Hivyo kwa nini tuibe fedha au dhahabu kutoka nyumbani kwa bwana wako?
Se, de Penge, som vi fandt oven i vore Poser, have vi bragt til dig igen fra Kanaans Land; hvorledes skulde vi da stjæle af din Herres Hus Sølv eller Guld?
9 Ikiwa yeyote miongoni mwa watumishi wako atapatikana nacho, auawe, na sisi wengine tutakuwa watumwa wa bwana wangu.”
Hos hvem af dine Tjenere den findes, han skal dø; dertil ville vi ogsaa være min Herres Trælle.
10 Akajibu, “Vema sana; na iwe kama msemavyo. Yeyote atakayekutwa nacho atakuwa mtumwa wangu, lakini ninyi wengine mtakuwa hamna lawama.”
Og han sagde: Ja nu, det skal saa være efter eders Ord: hos hvem den findes, han skal være min Træl, og I skulle være frie.
11 Kila mmoja wao akafanya haraka kushusha gunia lake chini na kulifungua.
Saa hastede de, og hver lagde sin Pose ned paa Jorden, og hver oplod sin Pose.
12 Ndipo msimamizi akaendelea kutafuta, akianzia kwa mkubwa wa wote na akaishia kwa mdogo wa wote. Basi kikombe kikapatikana katika gunia la Benyamini.
Og han ransagede; han begyndte med den ældste og endte med den yngste, og Skaalen fandtes udi Benjamins Pose.
13 Kwa jambo hili, wakararua nguo zao. Ndipo wote wakapakiza mizigo yao juu ya punda zao na kurudi mjini.
Da sønderreve de deres Klæder, og hver lagde paa sit Asen, og de fore til Staden igen.
14 Yosefu alikuwa bado yuko nyumbani mwake wakati Yuda na kaka zake walipoingia, wote wakajitupa chini mbele yake.
Og Juda og hans Brødre kom til Josefs Hus, og han selv var endnu der, og de faldt til Jorden for hans Ansigt.
15 Yosefu akawaambia, “Ni jambo gani hili mlilolifanya? Hamjui kuwa mtu kama mimi anaweza kufahamu mambo kwa njia ya kutabiri?”
Da sagde Josef til dem: Hvad er dette for en Gerning, som I have gjort? vide I ikke, at en Mand, som jeg er, kunde spaa det?
16 Yuda akajibu, “Tutaweza kusema nini kwa bwana wangu? Tutaweza kuzungumza nini? Tutawezaje kuthibitisha kwamba hatuna hatia? Mungu amefunua hatia ya watumishi wako. Sasa sisi tu watumwa wa bwana wangu, sisi wenyewe pamoja na yule aliyepatikana na kikombe.”
Og Juda sagde: Hvad skulle vi sige til min Herre? hvad skulle vi tale, og hvormed ville vi retfærdiggøre os? Gud har fundet dine Tjeneres Misgerning; se, vi ere min Herres Trælle, baade vi, saa og den, i som Skaalen er funden hos.
17 Lakini Yosefu alisema, “Liwe mbali nami kufanya jambo kama hili! Mtu yule tu aliyekutwa na kikombe ndiye atakayekuwa mtumwa wangu. Ninyi wengine, rudini kwa baba yenu kwa amani.”
Og han sagde: Det være langt fra mig at gøre dette; den Mand, som Skaalen er funden hos, skal være min Træl; men drager I op med Fred til eders Fader!
18 Ndipo Yuda akamwendea na kumwambia: “Tafadhali bwana wangu, mruhusu mtumishi wako aseme neno kwa bwana wangu. Usimkasirikie mtumishi wako, ingawa wewe ni sawa na Farao mwenyewe.
Da gik Juda frem til ham og sagde: Hør mig, min Herre! kære, lad din Tjener tale et Ord for min Herres Øren, og lad din Vrede ikke forhaste sig paa din I Tjener; thi du er ligesom Farao.
19 Bwana wangu aliwauliza watumishi wake, ‘Mnaye baba au ndugu?’
Min Herre spurgte sine Tjenere ad og sagde: Have I Fader eller Broder?
20 Nasi tukakujibu, ‘Tunaye baba yetu ambaye ni mzee; pia yupo mwanawe mdogo aliyezaliwa katika uzee wake. Ndugu yake amekufa, na huyu mdogo ndiye mwana pekee kwa mama yake aliyebaki, naye baba yake anampenda.’
Da sagde vi til min Herre: Vi have en gammel Fader, og han har en ung Søn, han avlede i sin Alderdom; og hans Broder er død, og han er alene bleven igen efter sin Moder, og hans Fader har ham kær.
21 “Ndipo ulipowaambia watumishi wako, ‘Mleteni kwangu ili niweze kumwona kwa macho yangu mwenyewe.’
Da sagde du til dine Tjenere: Fører ham ned til mig, at jeg kan se ham.
22 Nasi tukamwambia bwana wangu, ‘Kijana hawezi kumwacha baba yake; akimwacha, baba yake atakufa.’
Da sagde vi til min Herre: Den unge Mand kan ikke forlade sin Fader, dersom han forlader sin Fader, da dør denne.
23 Lakini ukawaambia watumishi wako, ‘Ndugu yenu mdogo asiposhuka pamoja nanyi, hamtauona uso wangu tena.’
Da sagde du til dine Tjenere: Dersom ikke eders yngste Broder kommer ned med eder, skulle I ikke se mit Ansigt mere.
24 Tuliporudi nyumbani kwa mtumwa wako baba yangu, tulimwambia lile bwana wangu alilokuwa amesema.
Og det skete, at vi i fore op til din Tjener, min Fader, i og vi gave ham min Herres Tale i til Kende.
25 “Ndipo baba yetu aliposema, ‘Rudini Misri mkanunue chakula kingine.’
Da sagde vor Fader: Drager hen igen, køber os lidt Spise!
26 Lakini tukamwambia, ‘Hatuwezi kushuka Misri mpaka ndugu yetu mdogo awe pamoja nasi ndipo tutakapokwenda. Hatutaweza kuuona uso wa yule mtu mpaka ndugu yetu mdogo awe pamoja nasi.’
Da sagde vi: Vi kunne ikke I fare ned; dersom vor yngste Broder er med os, da ville vi rejse ned; thi vi kunne ikke se den Mands Ansigt, dersom vor yngste Broder ikke er med os.
27 “Mtumwa wako baba yangu alituambia, ‘Mnajua mke wangu alinizalia wana wawili.
Da sagde din Tjener, min Fader, til os: I vide, at min Hustru har født mig to.
28 Mmojawapo alipotea, nami nikasema, “Hakika ameraruliwa vipande vipande.” Nami sijamwona tangu wakati huo.
Og den ene gik bort fra mig, og jeg sagde: Han er vist reven ihjel, og jeg har ikke set ham hidindtil.
29 Ikiwa mtaniondolea huyu tena na akapatwa na madhara, mtashusha kichwa changu chenye mvi kaburini nikiwa mwenye huzuni.’ (Sheol h7585)
Dersom I toge ogsaa denne fra mit Ansigt, og han kom til Ulykke, da førte I mine graa Haar med Kummer ned i Graven. (Sheol h7585)
30 “Hivyo sasa, kama kijana hatakuwa pamoja nasi nitakaporudi kwa mtumishi wako baba yangu, na kama baba yangu, ambaye maisha yake yamefungamanishwa na uhai wa kijana huyu,
Og nu, dersom jeg kommer til din Tjener, min Fader, og den unge Mand ikke er med os, efterdi hans Sjæl er bunden til den unge Mands Sjæl,
31 akiona kijana hayupo nasi, atakufa. Watumishi wako watashusha kichwa chenye mvi cha baba yetu kaburini kwa huzuni. (Sheol h7585)
da sker det, naar han ser, at den unge Mand ikke er der, at han dør, og dine Tjenere ville bringe din Tjeners, vor Faders, graa Haar med Sorg til Graven. (Sheol h7585)
32 Mtumwa wako alimhakikishia baba yangu usalama wa kijana. Nikamwambia, ‘Kama sikumrudisha kwako nitakuwa mwenye lawama mbele yako, baba yangu, maisha yangu yote!’
Thi din Tjener blev ansvarlig for den unge Mand hos min Fader og sagde: Dersom jeg ikke bringer dig ham igen, da vil jeg bære Skyld for min Fader alle Dage.
33 “Sasa basi, tafadhali mruhusu mtumishi abaki hapa kama mtumwa wa bwana wangu badala ya kijana, naye kijana umruhusu arudi na ndugu zake.
Og nu, kære, lad din Tjener blive min Herres Træl i Stedet for den unge Mand, men den unge Mand drage op med sine Brødre.
34 Ninawezaje kurudi kwa baba yangu kama kijana hatakuwa pamoja nami? La hasha! Usiniache nikaone huzuni ile itakayompata baba yangu.”
Thi hvorledes skulde jeg fare op til min Fader, uden at den unge Mand er med mig? jeg maatte da se paa det onde, som skulde ramme min Fader.

< Mwanzo 44 >