< Mwanzo 43 >
1 Wakati huu njaa ilikuwa bado ni kali mno katika nchi.
A ciężki głód [panował] w tej ziemi.
2 Hivyo wakati walikuwa wamemaliza kula nafaka yote waliyoileta kutoka Misri, Yakobo baba yao akawaambia, “Rudini Misri mkatununulie chakula kingine zaidi.”
I gdy zużyli zboże, które przynieśli z Egiptu, ich ojciec powiedział do nich: Idźcie znowu [i] kupcie nam trochę żywności.
3 Lakini Yuda akamwambia, “Mtu yule alituonya kwa msisitizo, ‘Hamtauona uso wangu tena mpaka mje na ndugu yenu.’
Juda powiedział do niego: Ten człowiek uroczyście nam oświadczył: Nie zobaczycie mojej twarzy, jeśli nie będzie z wami waszego brata.
4 Kama utakubali ndugu yetu aende pamoja nasi, tutakwenda kuwanunulia chakula.
Jeśli [więc] poślesz naszego brata z nami, pojedziemy i nakupimy ci żywności;
5 Lakini ikiwa hutamruhusu aende, hatutakwenda, kwa sababu mtu yule alituambia, ‘Hamtauona uso wangu tena mpaka mje pamoja na ndugu yenu.’”
Ale jeśli nie poślesz, nie pojedziemy, bo ten człowiek mówił do nas: Nie zobaczycie mojej twarzy, jeśli nie będzie z wami waszego brata.
6 Israeli akauliza, “Kwa nini mkaniletea taabu hii kwa kumwambia yule mtu mlikuwa na ndugu mwingine?”
Izrael zapytał: Dlaczego sprawiliście mi ból, mówiąc temu człowiekowi, że macie jeszcze brata?
7 Wakamjibu, “Yule mtu alituhoji kwa undani sana habari zetu na za jamaa yetu. Alituuliza, ‘Je, baba yenu bado yungali hai? Je mnaye ndugu mwingine?’ Sisi tulimjibu maswali yake tu. Tungewezaje kujua kwamba angesema, ‘Mleteni mdogo wenu hapa’?”
Odpowiedzieli: Ten człowiek dokładnie się wypytał o nas i naszą rodzinę: Żyje jeszcze wasz ojciec? Macie [jeszcze jakiegoś] brata? I odpowiedzieliśmy mu na jego pytania. Skąd mogliśmy wiedzieć, że powie: Przyprowadźcie mi tu waszego brata?
8 Ndipo Yuda akamwambia baba yake Israeli, “Mtume kijana pamoja nami, nasi tutaondoka mara, ili sisi na wewe pamoja na watoto wetu tuweze kuishi, wala tusife.
I Juda powiedział do swego ojca Izraela: Poślij chłopca ze mną. Powstaniemy i pojedziemy, abyśmy żyli, a nie pomarli [z głodu], tak my, jak i ty, i nasze dzieci.
9 Mimi mwenyewe nitakuhakikishia usalama wake, mimi mwenyewe nitawajibika kumrudisha. Ikiwa sitamrudisha kwako na kumweka mbele yako, nitakuwa mwenye lawama mbele yako maisha yangu yote.
Ja biorę odpowiedzialność za niego, ode mnie się go domagaj. Jeśli nie przyprowadzę go do ciebie i nie stawię go przed tobą, na zawsze będę ponosił [za to] winę.
10 Hakika, kama hatukuchelewa kuondoka, tungekuwa tumekwenda na kurudi mara mbili.”
Gdybyśmy bowiem nie zwlekali, wrócilibyśmy już dwa razy.
11 Basi baba yao Israeli akawaambia, “Kama ni lazima iwe hivyo, basi fanyeni hivi: Wekeni baadhi ya mazao bora ya nchi katika mifuko yenu na mpelekeeni yule mtu kama zawadi, zeri kidogo, asali kidogo, vikolezo, manemane, kungu na lozi.
Wtedy Izrael, ich ojciec, powiedział do nich: Jeśli tak [musi być], zróbcie w ten sposób: weźcie z najlepszych owoców ziemi w wasze naczynia i zanieście je temu człowiekowi w darze – trochę balsamu, trochę miodu, wonności, mirry, orzechów i migdałów.
12 Chukueni fedha mara mbili, kwa kuwa mtazirudisha zile fedha zilizowekwa midomoni mwa magunia yenu. Labda ziliwekwa kwa makosa.
Weźcie też ze sobą podwójną sumę pieniędzy, a pieniądze wrzucone na wierzch waszych worów zabierzcie ze sobą, bo może to była pomyłka.
13 Mchukueni ndugu yenu pia mrudi kwa huyo mtu mara moja.
Weźcie także waszego brata, wstańcie i jedźcie znowu do tego człowieka;
14 Naye Mungu Mwenyezi awajalieni rehema mbele ya huyo mtu ili apate kumwachia yule ndugu yenu na Benyamini mweze kurudi pamoja. Kwangu mimi kama nikufiwa nimefiwa.”
A niech Bóg Wszechmogący da wam miłosierdzie przed tym człowiekiem, aby wam wypuścił waszego drugiego brata i Beniamina. A jeśli mam stracić swoje dzieci, to je stracę.
15 Basi hao watu wakazichukua zile zawadi na zile fedha mara mbili pamoja na Benyamini. Wakafanya haraka kwenda Misri na walipofika wakajionyesha kwa Yosefu.
Mężczyźni wzięli więc ten dar, zabrali ze sobą podwójną sumę pieniędzy oraz Beniamina, wstali i pojechali do Egiptu, i stanęli przed Józefem.
16 Yosefu alipomwona Benyamini pamoja nao, akamwambia msimamizi wa nyumba yake, “Wachukue watu hawa nyumbani kwangu, mchinje mnyama na kuandalia chakula kwa kuwa watakula chakula cha mchana pamoja nami.”
A gdy Józef zobaczył z nimi Beniamina, powiedział do zarządcy jego domu: Wprowadź tych ludzi do domu, zabij [bydlę] i przyrządź, bo ci ludzie w południe będą jedli ze mną.
17 Yule Msimamizi akafanya kama Yosefu alivyomwambia na akawachukua wale watu nyumbani kwa Yosefu.
Człowiek ten zrobił, jak mu Józef rozkazał, i wprowadził tych ludzi do domu Józefa.
18 Basi watu hao wakaogopa walipopelekwa nyumbani kwa Yosefu. Wakafikiri, “Tumeletwa hapa kwa ajili ya zile fedha zilizorudishwa katika magunia yetu mara ile ya kwanza. Anataka kutushambulia na kutushinda, atuchukue sisi kama watumwa, na atwae hawa punda zetu.”
Gdy zostali wprowadzeni do domu Józefa, bali się i mówili: Wprowadzono nas tu z powodu tych pieniędzy, które za pierwszym razem włożono do naszych worów, aby rzucić na nas [oszczerstwo], napaść na nas i wziąć w niewolę nas i nasze osły.
19 Hivyo wakamwendea msimamizi wa nyumba wa Yosefu na kuzungumza naye kwenye ingilio la nyumbani.
Podeszli do zarządcy domu Józefa i rozmawiali z nim w drzwiach domu.
20 Wakasema, “Tafadhali bwana, tulikuja hapa mara ya kwanza kununua chakula.
I powiedzieli: [Pozwól], panie. Przyjechaliśmy za pierwszym razem kupić żywności.
21 Lakini mahali pale tulipotua wakati wa jioni tulifungua magunia yetu, na kila mmoja wetu akakuta fedha zake, kwenye mdomo wa gunia lake kiasi kile kile tulicholeta. Kwa hiyo tumezirudisha.
A gdy przyjechaliśmy do gospody i rozwiązaliśmy nasze wory, pieniądze każdego [były] na wierzchu jego wora, nasze pieniądze w pełnej wadze. Przywieźliśmy je więc ze sobą.
22 Pia tumeleta fedha nyingine kwa ajili ya kununulia chakula. Hatujui ni nani aliziweka fedha hizo katika magunia yetu.”
Przywieźliśmy też inne pieniądze ze sobą, aby nakupić żywności. Nie wiemy, kto włożył nasze pieniądze do naszych worów.
23 Akawaambia, “Vema, msiogope. Mungu wenu, Mungu wa baba yenu, amewapa ninyi hazina katika magunia yenu; mimi nilipokea fedha yenu.” Ndipo akawaletea Simeoni.
A [on] powiedział: Pokój wam, nie bójcie się. Bóg wasz, Bóg waszego ojca, dał wam skarb do waszych worów. Wasze pieniądze doszły do mnie. I wyprowadził do nich Symeona.
24 Msimamizi akawapeleka wale watu katika nyumba ya Yosefu, akawapa maji ya kunawa miguu na kuwapa punda wao majani.
Człowiek ten wprowadził tych ludzi do domu Józefa, dał im wody, aby umyli sobie nogi; dał też karmę ich osłom.
25 Wakaandaa zawadi zao ili wampe Yosefu wakati atakapofika adhuhuri, kwa kuwa walikuwa wamesikia kwamba watakula chakula huko.
Potem przygotowali dar, zanim Józef przyszedł w południe. Słyszeli bowiem, że tam mieli jeść chleb.
26 Yosefu alipokuja nyumbani, walimkabidhi zile zawadi walizokuwa nazo, ambazo walikuwa wamezileta mle nyumbani, nao wakamsujudia hadi nchi.
A gdy Józef wszedł do domu, przynieśli mu dar, który [mieli] ze sobą w tym domu, i pokłonili mu się aż do ziemi.
27 Akawauliza kuhusu hali yao, kisha akawaambia, “Yule baba yenu mzee mliyeniambia habari zake, yu hali gani? Je, bado yu hai?”
I dowiadywał się, jak się im powodzi, i zapytał: Czy wasz ojciec jest zdrowy, ten starzec, o którym mi opowiadaliście? Czy jeszcze żyje?
28 Wakamjibu, “Mtumishi wako baba yetu bado anaishi na ni mzima.” Kisha wakainama chini kumpa heshima.
A oni odpowiedzieli: Twój sługa, nasz ojciec, jest zdrowy, jeszcze żyje. I uklękli, i pokłonili mu się.
29 Alipotazama na kumwona Benyamini ndugu yake, mwana wa mama yake hasa, akauliza, “Je, huyu ndiye ndugu yenu wa mwisho, ambaye mlinieleza habari zake?” Ndipo akasema, “Mungu na akufadhili, mwanangu.”
Wtedy podniósł swe oczy i zobaczył swego brata Beniamina, syna swej matki, i zapytał: Czy to [jest] wasz najmłodszy brat, o którym mi opowiadaliście? I powiedział mu: Niech Bóg będzie ci miłosierny, miły synu.
30 Akiwa ameguswa sana kwa kumwona ndugu yake, Yosefu akatoka nje kwa haraka na kutafuta mahali pa kulilia. Akaingia kwenye chumba chake cha pekee na kulilia humo.
I nagle Józef [wyszedł], bo wzruszył się do głębi swym bratem, i szukał [miejsca], gdzie mógłby zapłakać. Wszedł więc do komnaty i tam płakał.
31 Baada ya kunawa uso wake, akatoka nje na huku akijizuia akasema, “Pakueni chakula.”
Potem umył swoją twarz, wyszedł i gdy się opanował, powiedział: Kładźcie chleb.
32 Wakampakulia Yosefu peke yake, ndugu zake peke yao na Wamisri waliokula pamoja naye peke yao, kwa sababu Wamisri wasingeweza kula pamoja na Waebrania, kwa maana ilikuwa ni chukizo kwa Wamisri.
Położono jemu osobno, im osobno i osobno Egipcjanom, którzy z nim jedli. Egipcjanie bowiem nie mogą jeść chleba z Hebrajczykami, gdyż to budzi odrazę u Egipcjan.
33 Watu hao walikuwa wameketi mbele yake kwa mfuatano wa umri wao, kuanzia mzaliwa wa kwanza hadi mzaliwa wa mwisho, wakatazamana wao kwa wao kwa mshangao.
I usiedli przed nim, pierworodny według swego pierworództwa, a młodszy według swej młodości. I dziwili się ci mężczyźni, [patrząc] jeden na drugiego.
34 Wakati walipelekewa sehemu ya chakula kutoka mezani mwa Yosefu, sehemu ya Benyamini ilikuwa mara tano zaidi ya sehemu ya wale wengine. Kwa hiyo wakanywa na kufurahi pamoja naye.
Potem brał potrawy sprzed siebie i kazał im zanieść. A porcja Beniamina była pięciokrotnie większa od porcji ich wszystkich. Pili i podpili sobie z nim.