< Mwanzo 43 >

1 Wakati huu njaa ilikuwa bado ni kali mno katika nchi.
La famine s'appesantissait sur le pays.
2 Hivyo wakati walikuwa wamemaliza kula nafaka yote waliyoileta kutoka Misri, Yakobo baba yao akawaambia, “Rudini Misri mkatununulie chakula kingine zaidi.”
Quand ils eurent fini de manger le blé qu'ils avaient apporté d'Egypte, leur père leur dit: " Retournez nous acheter un peu de vivres. "
3 Lakini Yuda akamwambia, “Mtu yule alituonya kwa msisitizo, ‘Hamtauona uso wangu tena mpaka mje na ndugu yenu.’
Juda lui répondit: " Cet homme nous a fait cette déclaration formelle: Vous ne verrez point ma face que votre frère ne soit avec vous.
4 Kama utakubali ndugu yetu aende pamoja nasi, tutakwenda kuwanunulia chakula.
Si donc tu laisses venir notre frère avec nous, nous descendrons et nous t'achèterons des vivres.
5 Lakini ikiwa hutamruhusu aende, hatutakwenda, kwa sababu mtu yule alituambia, ‘Hamtauona uso wangu tena mpaka mje pamoja na ndugu yenu.’”
Mais si tu ne le laisses pas venir, nous ne descendrons point; car cet homme nous a dit: Vous ne verrez pas ma face que votre frère ne soit avec vous. "
6 Israeli akauliza, “Kwa nini mkaniletea taabu hii kwa kumwambia yule mtu mlikuwa na ndugu mwingine?”
Et Israël dit: " Pourquoi m'avez-vous causé cette peine, de dire à cet homme que vous aviez encore un frère? "
7 Wakamjibu, “Yule mtu alituhoji kwa undani sana habari zetu na za jamaa yetu. Alituuliza, ‘Je, baba yenu bado yungali hai? Je mnaye ndugu mwingine?’ Sisi tulimjibu maswali yake tu. Tungewezaje kujua kwamba angesema, ‘Mleteni mdogo wenu hapa’?”
Ils dirent: " Cet homme nous a adressé beaucoup de questions sur nous et sur notre famille, en disant: Votre père vit-il encore? Avez-vous un autre frère? Et nous avons répondu selon ces questions. Pouvions-nous savoir qu'il dirait: Faites descendre votre frère? "
8 Ndipo Yuda akamwambia baba yake Israeli, “Mtume kijana pamoja nami, nasi tutaondoka mara, ili sisi na wewe pamoja na watoto wetu tuweze kuishi, wala tusife.
Et Juda dit à Israël, son père: " Laisse partir l'enfant avec moi, afin que nous nous levions et nous mettions en route, et nous vivrons et ne mourrons point, nous, toi et nos petits enfants.
9 Mimi mwenyewe nitakuhakikishia usalama wake, mimi mwenyewe nitawajibika kumrudisha. Ikiwa sitamrudisha kwako na kumweka mbele yako, nitakuwa mwenye lawama mbele yako maisha yangu yote.
C'est moi qui réponds de lui, tu le redemanderas de ma main. Si je ne le ramène pas auprès de toi, si je ne le mets pas devant toi, je serai coupable envers toi à tout jamais.
10 Hakika, kama hatukuchelewa kuondoka, tungekuwa tumekwenda na kurudi mara mbili.”
Car si nous n'avions pas tant tardé, nous serions maintenant deux fois de retour. "
11 Basi baba yao Israeli akawaambia, “Kama ni lazima iwe hivyo, basi fanyeni hivi: Wekeni baadhi ya mazao bora ya nchi katika mifuko yenu na mpelekeeni yule mtu kama zawadi, zeri kidogo, asali kidogo, vikolezo, manemane, kungu na lozi.
Israël, leur père, leur dit: " Eh bien, puisqu'il le faut, faites ceci: Prenez dans vos vaisseaux des meilleures productions du pays et portez à cet homme un présent: un peu de baume et un peu de miel, de l'astragale, du ladanum, des pistaches et des amandes.
12 Chukueni fedha mara mbili, kwa kuwa mtazirudisha zile fedha zilizowekwa midomoni mwa magunia yenu. Labda ziliwekwa kwa makosa.
Prenez dans vos mains de l'argent en double, et reportez celui qui a été mis à l'entrée de vos sacs, peut-être par erreur.
13 Mchukueni ndugu yenu pia mrudi kwa huyo mtu mara moja.
Prenez votre frère, levez-vous et retournez vers cet homme.
14 Naye Mungu Mwenyezi awajalieni rehema mbele ya huyo mtu ili apate kumwachia yule ndugu yenu na Benyamini mweze kurudi pamoja. Kwangu mimi kama nikufiwa nimefiwa.”
Que le Dieu tout-puissant vous fasse trouver grâce devant cet homme, afin qu'il laisse revenir avec vous votre autre frère, ainsi que Benjamin! Pour moi, si je dois être privé de mes enfants, que j'en sois privé! "
15 Basi hao watu wakazichukua zile zawadi na zile fedha mara mbili pamoja na Benyamini. Wakafanya haraka kwenda Misri na walipofika wakajionyesha kwa Yosefu.
Les hommes prirent ce présent, et ils prirent dans leurs mains de l'argent au double, ainsi que Benjamin; et, s'étant levés, ils descendirent en Egypte et se présentèrent devant Joseph.
16 Yosefu alipomwona Benyamini pamoja nao, akamwambia msimamizi wa nyumba yake, “Wachukue watu hawa nyumbani kwangu, mchinje mnyama na kuandalia chakula kwa kuwa watakula chakula cha mchana pamoja nami.”
Dès que Joseph vit Benjamin avec eux, il dit à son intendant: " Fais entrer ces gens dans la maison, tue des victimes et apprête un repas, car ces gens mangeront avec moi à midi. "
17 Yule Msimamizi akafanya kama Yosefu alivyomwambia na akawachukua wale watu nyumbani kwa Yosefu.
Cet homme fit ce que Joseph avait ordonné, et il conduisit ces gens dans la maison de Joseph.
18 Basi watu hao wakaogopa walipopelekwa nyumbani kwa Yosefu. Wakafikiri, “Tumeletwa hapa kwa ajili ya zile fedha zilizorudishwa katika magunia yetu mara ile ya kwanza. Anataka kutushambulia na kutushinda, atuchukue sisi kama watumwa, na atwae hawa punda zetu.”
Pendant qu'on les conduisait à la maison de Joseph, les hommes eurent peur, et ils dirent: " C'est à cause de l'argent rapporté l'autre fois dans nos sacs qu'on nous emmène; c'est pour nous assaillir, tomber sur nous, nous prendre comme esclaves avec nos ânes. "
19 Hivyo wakamwendea msimamizi wa nyumba wa Yosefu na kuzungumza naye kwenye ingilio la nyumbani.
S'étant approchés de l'intendant de la maison de Joseph, ils lui adressèrent la parole, à l'entrée de la maison,
20 Wakasema, “Tafadhali bwana, tulikuja hapa mara ya kwanza kununua chakula.
en disant: " Pardon, mon seigneur. Nous sommes déjà descendus une fois pour acheter des vivres.
21 Lakini mahali pale tulipotua wakati wa jioni tulifungua magunia yetu, na kila mmoja wetu akakuta fedha zake, kwenye mdomo wa gunia lake kiasi kile kile tulicholeta. Kwa hiyo tumezirudisha.
Au retour, quand nous arrivâmes à l'endroit où nous devions passer la nuit, nous avons ouvert nos sacs, et voici, l'argent de chacun était à l'entrée de son sac, notre argent selon son poids: nous le rapportons avec nous;
22 Pia tumeleta fedha nyingine kwa ajili ya kununulia chakula. Hatujui ni nani aliziweka fedha hizo katika magunia yetu.”
et en même temps nous avons apporté d'autre argent pour acheter des vivres. Nous ne savons pas qui a mis notre argent dans nos sacs. "
23 Akawaambia, “Vema, msiogope. Mungu wenu, Mungu wa baba yenu, amewapa ninyi hazina katika magunia yenu; mimi nilipokea fedha yenu.” Ndipo akawaletea Simeoni.
Il leur dit: " Que la paix soit avec vous! Ne craignez rien. C'est votre Dieu, le Dieu de votre père, qui vous a donné un trésor dans vos sacs. Votre argent m'a été remis. " Et il leur amena Siméon.
24 Msimamizi akawapeleka wale watu katika nyumba ya Yosefu, akawapa maji ya kunawa miguu na kuwapa punda wao majani.
Cet homme, les ayant fait entrer dans la maison de Joseph, leur donna de l'eau et ils se lavèrent les pieds; il donna aussi du fourrage à leurs ânes.
25 Wakaandaa zawadi zao ili wampe Yosefu wakati atakapofika adhuhuri, kwa kuwa walikuwa wamesikia kwamba watakula chakula huko.
Ils préparèrent leur présent, en attendant que Joseph vint à midi; car on leur avait annoncé qu'ils mangeraient chez lui.
26 Yosefu alipokuja nyumbani, walimkabidhi zile zawadi walizokuwa nazo, ambazo walikuwa wamezileta mle nyumbani, nao wakamsujudia hadi nchi.
Quand Joseph fut arrivé chez lui, ils lui apportèrent dans la maison le présent qu'ils avaient dans la main, et se prosternèrent par terre devant lui.
27 Akawauliza kuhusu hali yao, kisha akawaambia, “Yule baba yenu mzee mliyeniambia habari zake, yu hali gani? Je, bado yu hai?”
Il leur demanda comment ils se portaient, puis il dit: " Votre vieux père, dont vous avez parlé, est-il en bonne santé? vit-il encore? "
28 Wakamjibu, “Mtumishi wako baba yetu bado anaishi na ni mzima.” Kisha wakainama chini kumpa heshima.
Ils répondirent: " Ton serviteur, notre père, est en bonne santé; il vit encore "; et ils s'inclinèrent et se prosternèrent.
29 Alipotazama na kumwona Benyamini ndugu yake, mwana wa mama yake hasa, akauliza, “Je, huyu ndiye ndugu yenu wa mwisho, ambaye mlinieleza habari zake?” Ndipo akasema, “Mungu na akufadhili, mwanangu.”
Joseph leva les yeux, et il vit Benjamin, son frère, fils de sa mère; il dit: " Est-ce là votre jeune frère dont vous m'avez parlé? " Et il dit: " Que Dieu te soit favorable, mon fils! "
30 Akiwa ameguswa sana kwa kumwona ndugu yake, Yosefu akatoka nje kwa haraka na kutafuta mahali pa kulilia. Akaingia kwenye chumba chake cha pekee na kulilia humo.
Alors, en toute hâte, car ses entrailles étaient émues pour son frère, Joseph chercha un endroit pour pleurer; il entra dans sa chambre et il y pleura.
31 Baada ya kunawa uso wake, akatoka nje na huku akijizuia akasema, “Pakueni chakula.”
Après s'être lavé le visage, il sortit et, faisant des efforts pour se contenir, il dit: " Servez à manger. "
32 Wakampakulia Yosefu peke yake, ndugu zake peke yao na Wamisri waliokula pamoja naye peke yao, kwa sababu Wamisri wasingeweza kula pamoja na Waebrania, kwa maana ilikuwa ni chukizo kwa Wamisri.
On le servit à part, et ses frères à part, à part aussi les Egyptiens qui mangeaient avec lui, car les Egyptiens ne peuvent prendre leurs repas avec les Hébreux: c'est une abomination pour les Egyptiens.
33 Watu hao walikuwa wameketi mbele yake kwa mfuatano wa umri wao, kuanzia mzaliwa wa kwanza hadi mzaliwa wa mwisho, wakatazamana wao kwa wao kwa mshangao.
Les frères de Joseph s'assirent devant lui, le premier-né selon son droit d'aînesse, et le plus jeune selon son âge; et ils se regardaient les uns les autres avec étonnement.
34 Wakati walipelekewa sehemu ya chakula kutoka mezani mwa Yosefu, sehemu ya Benyamini ilikuwa mara tano zaidi ya sehemu ya wale wengine. Kwa hiyo wakanywa na kufurahi pamoja naye.
Il leur fit porter des portions de devant lui, et la portion de Benjamin était cinq fois plus forte que les portions d'eux tous. Ils burent joyeusement avec lui.

< Mwanzo 43 >