< Mwanzo 43 >

1 Wakati huu njaa ilikuwa bado ni kali mno katika nchi.
And the famine [was] heavy in the land.
2 Hivyo wakati walikuwa wamemaliza kula nafaka yote waliyoileta kutoka Misri, Yakobo baba yao akawaambia, “Rudini Misri mkatununulie chakula kingine zaidi.”
And it was just when they finished to eat the grain which they had brought from Egypt and he said to them father their go back buy for us a little of food.
3 Lakini Yuda akamwambia, “Mtu yule alituonya kwa msisitizo, ‘Hamtauona uso wangu tena mpaka mje na ndugu yenu.’
And he said to him Judah saying certainly he warned us the man saying not you will see face my except brother your [is] with you.
4 Kama utakubali ndugu yetu aende pamoja nasi, tutakwenda kuwanunulia chakula.
If there you [are] sending brother our with us we will go down and we will buy for you food.
5 Lakini ikiwa hutamruhusu aende, hatutakwenda, kwa sababu mtu yule alituambia, ‘Hamtauona uso wangu tena mpaka mje pamoja na ndugu yenu.’”
And if not you [are] sending [him] not we will go down for the man he said to us not you will see face my except brother your [is] with you.
6 Israeli akauliza, “Kwa nini mkaniletea taabu hii kwa kumwambia yule mtu mlikuwa na ndugu mwingine?”
And he said Israel why? did you do harm to me by telling to the man ¿ still [belong] to you [does] a brother.
7 Wakamjibu, “Yule mtu alituhoji kwa undani sana habari zetu na za jamaa yetu. Alituuliza, ‘Je, baba yenu bado yungali hai? Je mnaye ndugu mwingine?’ Sisi tulimjibu maswali yake tu. Tungewezaje kujua kwamba angesema, ‘Mleteni mdogo wenu hapa’?”
And they said carefully he asked the man of us and of kindred our saying ¿ still [is] father your living ¿ [does] there [belong] to you a brother and we told to him on [the] mouth of the words these ¿ really did we know that he will say bring down brother your.
8 Ndipo Yuda akamwambia baba yake Israeli, “Mtume kijana pamoja nami, nasi tutaondoka mara, ili sisi na wewe pamoja na watoto wetu tuweze kuishi, wala tusife.
And he said Judah to Israel father his send! the young man with me so let us arise and we will go and we may live and not we will die both we as well as you as well as little one[s] our.
9 Mimi mwenyewe nitakuhakikishia usalama wake, mimi mwenyewe nitawajibika kumrudisha. Ikiwa sitamrudisha kwako na kumweka mbele yako, nitakuwa mwenye lawama mbele yako maisha yangu yote.
I I will stand surety for him from hand my you will require him if not I have brought him to you and I will set him before you and I will be culpable to you all the days.
10 Hakika, kama hatukuchelewa kuondoka, tungekuwa tumekwenda na kurudi mara mbili.”
For if not we had delayed for now we have returned this two times.
11 Basi baba yao Israeli akawaambia, “Kama ni lazima iwe hivyo, basi fanyeni hivi: Wekeni baadhi ya mazao bora ya nchi katika mifuko yenu na mpelekeeni yule mtu kama zawadi, zeri kidogo, asali kidogo, vikolezo, manemane, kungu na lozi.
And he said to them Israel father their if so - then this do take some of [the] best products of the land in vessels your and take down to the man a gift a little of balm and a little of honey spice and myrrh pistachio nuts and almonds.
12 Chukueni fedha mara mbili, kwa kuwa mtazirudisha zile fedha zilizowekwa midomoni mwa magunia yenu. Labda ziliwekwa kwa makosa.
And silver double take in hand your and the silver that was returned in [the] mouth of sacks your you will take back in hand your perhaps [was] a mistake it.
13 Mchukueni ndugu yenu pia mrudi kwa huyo mtu mara moja.
And brother your take and arise go back to the man.
14 Naye Mungu Mwenyezi awajalieni rehema mbele ya huyo mtu ili apate kumwachia yule ndugu yenu na Benyamini mweze kurudi pamoja. Kwangu mimi kama nikufiwa nimefiwa.”
And God Almighty may he give to you compassion before the man and he will let go to you brother your other and Benjamin and I just when I have been bereaved I have been bereaved.
15 Basi hao watu wakazichukua zile zawadi na zile fedha mara mbili pamoja na Benyamini. Wakafanya haraka kwenda Misri na walipofika wakajionyesha kwa Yosefu.
And they took the men the gift this and double money they took in hand their and Benjamin and they arose and they went down Egypt and they stood before Joseph.
16 Yosefu alipomwona Benyamini pamoja nao, akamwambia msimamizi wa nyumba yake, “Wachukue watu hawa nyumbani kwangu, mchinje mnyama na kuandalia chakula kwa kuwa watakula chakula cha mchana pamoja nami.”
And he saw Joseph with them Benjamin and he said to [the one] who [was] over household his bring the men the house towards and slaughter a slaughter and prepare [it] for with me they will eat the men at noon.
17 Yule Msimamizi akafanya kama Yosefu alivyomwambia na akawachukua wale watu nyumbani kwa Yosefu.
And he did the man just as he said Joseph and he brought the man the men [the] house of towards Joseph.
18 Basi watu hao wakaogopa walipopelekwa nyumbani kwa Yosefu. Wakafikiri, “Tumeletwa hapa kwa ajili ya zile fedha zilizorudishwa katika magunia yetu mara ile ya kwanza. Anataka kutushambulia na kutushinda, atuchukue sisi kama watumwa, na atwae hawa punda zetu.”
And they were afraid the men that they were brought [the] house of Joseph and they said on [the] matter of the silver which returned in sacks our at the beginning we [are] being brought to roll himself on us and to throw himself on us and to take us to slaves and donkeys our.
19 Hivyo wakamwendea msimamizi wa nyumba wa Yosefu na kuzungumza naye kwenye ingilio la nyumbani.
And they approached the man who [was] over [the] household of Joseph and they spoke to him [the] entrance of the house.
20 Wakasema, “Tafadhali bwana, tulikuja hapa mara ya kwanza kununua chakula.
And they said pardon us O lord my certainly we came down at the beginning to buy food.
21 Lakini mahali pale tulipotua wakati wa jioni tulifungua magunia yetu, na kila mmoja wetu akakuta fedha zake, kwenye mdomo wa gunia lake kiasi kile kile tulicholeta. Kwa hiyo tumezirudisha.
And it was that we came to the lodging place and we opened! sacks our and there! [the] silver of each man [was] in [the] mouth of sack his silver our in weight its and we have brought back it in hand our.
22 Pia tumeleta fedha nyingine kwa ajili ya kununulia chakula. Hatujui ni nani aliziweka fedha hizo katika magunia yetu.”
And silver other we have brought down in hand our to buy food not we know who? did he put silver our in sacks our.
23 Akawaambia, “Vema, msiogope. Mungu wenu, Mungu wa baba yenu, amewapa ninyi hazina katika magunia yenu; mimi nilipokea fedha yenu.” Ndipo akawaletea Simeoni.
And he said peace [be] to you may not you fear God your and [the] God of father your he gave to you treasure in sacks your silver your it came to me and he brought out to them Simeon.
24 Msimamizi akawapeleka wale watu katika nyumba ya Yosefu, akawapa maji ya kunawa miguu na kuwapa punda wao majani.
And he brought the man the men [the] house of towards Joseph and he gave water and they washed feet their and he gave fodder to donkeys their.
25 Wakaandaa zawadi zao ili wampe Yosefu wakati atakapofika adhuhuri, kwa kuwa walikuwa wamesikia kwamba watakula chakula huko.
And they prepared the gift until came Joseph at noon for they had heard that there they will eat food.
26 Yosefu alipokuja nyumbani, walimkabidhi zile zawadi walizokuwa nazo, ambazo walikuwa wamezileta mle nyumbani, nao wakamsujudia hadi nchi.
And he came Joseph the house towards and they brought to him the gift which [was] in hand their the house towards and they bowed down to him [the] ground towards.
27 Akawauliza kuhusu hali yao, kisha akawaambia, “Yule baba yenu mzee mliyeniambia habari zake, yu hali gani? Je, bado yu hai?”
And he asked of them to welfare and he said ¿ health [is] father your old whom you spoke ¿ [is] still he alive.
28 Wakamjibu, “Mtumishi wako baba yetu bado anaishi na ni mzima.” Kisha wakainama chini kumpa heshima.
And they said health [belongs] to servant your to father our still he [is] alive and they bowed low (and they bowed down. *Q(K)*)
29 Alipotazama na kumwona Benyamini ndugu yake, mwana wa mama yake hasa, akauliza, “Je, huyu ndiye ndugu yenu wa mwisho, ambaye mlinieleza habari zake?” Ndipo akasema, “Mungu na akufadhili, mwanangu.”
And he lifted up eyes his and he saw Benjamin brother his [the] son of mother his and he said ¿ [is] this brother your young whom you spoke to me and he said God may he show favor to you O son my.
30 Akiwa ameguswa sana kwa kumwona ndugu yake, Yosefu akatoka nje kwa haraka na kutafuta mahali pa kulilia. Akaingia kwenye chumba chake cha pekee na kulilia humo.
And he hurried Joseph for they grew warm compassion his to brother his and he sought to weep and he went the inner room towards and he wept there.
31 Baada ya kunawa uso wake, akatoka nje na huku akijizuia akasema, “Pakueni chakula.”
And he washed face his and he came out and he restrained himself and he said set food.
32 Wakampakulia Yosefu peke yake, ndugu zake peke yao na Wamisri waliokula pamoja naye peke yao, kwa sababu Wamisri wasingeweza kula pamoja na Waebrania, kwa maana ilikuwa ni chukizo kwa Wamisri.
And they set for him to only him and to them to alone them and for the Egyptians who were eating with him to alone them for not they were able! the Egyptians to eat with the Hebrews food for [is] an abomination it to Egypt.
33 Watu hao walikuwa wameketi mbele yake kwa mfuatano wa umri wao, kuanzia mzaliwa wa kwanza hadi mzaliwa wa mwisho, wakatazamana wao kwa wao kwa mshangao.
And they sat down before him the firstborn according to birthright his and the young [brother] according to youth his and they looked in astonishment the men each to neighbor his.
34 Wakati walipelekewa sehemu ya chakula kutoka mezani mwa Yosefu, sehemu ya Benyamini ilikuwa mara tano zaidi ya sehemu ya wale wengine. Kwa hiyo wakanywa na kufurahi pamoja naye.
And someone took portions from with face his to them and it was great [the] portion of Benjamin more than [the] portions of all of them five hands and they drank and they became drunk with him.

< Mwanzo 43 >