< Mwanzo 42 >

1 Wakati Yakobo alipofahamu kuwa kuna nafaka huko Misri, akawaambia wanawe, “Mbona mnakaa tu hapa mnatazamana?”
و اما یعقوب چون دید که غله درمصر است، پس یعقوب به پسران خودگفت: «چرا به یکدیگر می‌نگرید؟»۱
2 Akaendelea kuwaambia, “Nimesikia kuwa huko Misri kuna nafaka. Telemkeni huko mkanunue chakula kwa ajili yetu, ili tuweze kuishi wala tusife.”
و گفت: «اینک شنیده‌ام که غله در مصر است، بدانجابروید و برای ما از آنجا بخرید، تا زیست کنیم ونمیریم.»۲
3 Ndipo wale ndugu kumi wa Yosefu, wakateremka huko Misri kununua nafaka.
پس ده برادر یوسف برای خریدن غله به مصر فرود آمدند.۳
4 Lakini Yakobo hakumtuma Benyamini, ndugu yake Yosefu, pamoja na wengine, kwa sababu aliogopa asije akapatwa na madhara.
و اما بنیامین، برادر یوسف رایعقوب با برادرانش نفرستاد، زیرا گفت مبادازیانی بدو رسد.۴
5 Hivyo wana wa Israeli walikuwa miongoni mwa wale waliokwenda Misri kununua nafaka, kwani njaa ilikuwa katika nchi ya Kanaani pia.
پس بنی‌اسرائیل در میان آنانی که می‌آمدند، به جهت خرید آمدند، زیرا که قحطدر زمین کنعان بود.۵
6 Wakati huo Yosefu alikuwa mtawala wa nchi ya Misri, naye alikuwa ndiye aliwauzia watu wote nafaka. Kwa hiyo wakati ndugu zake Yosefu walipofika, wakamsujudia hadi nyuso zao zikagusa ardhi.
و یوسف حاکم ولایت بود، و خود به همه اهل زمین غله می‌فروخت. و برادران یوسف آمده، رو به زمین نهاده، او را سجده کردند.۶
7 Mara Yosefu alipowaona ndugu zake, akawatambua, lakini akajifanya mgeni na kuzungumza nao kwa ukali, akiwauliza, “Ninyi mnatoka wapi?” Wakamjibu, “Tumetoka katika nchi ya Kanaani kuja kununua chakula.”
چون یوسف برادران خود را دید، ایشان را بشناخت، وخود را بدیشان بیگانه نموده، آنها را به درشتی، سخن گفت و از ایشان پرسید: «از کجا آمده‌اید؟» گفتند: «از زمین کنعان تا خوراک بخریم.»۷
8 Ingawa Yosefu aliwatambua ndugu zake, wao hawakumtambua.
و یوسف برادران خود را شناخت، لیکن ایشان او را نشناختند.۸
9 Ndipo Yosefu alipokumbuka ndoto zake kuwahusu wao, akawaambia, “Ninyi ni wapelelezi! Mmekuja kuangalia mahali ambapo nchi yetu haina ulinzi.”
و یوسف خوابها را که درباره ایشان دیده بود، بیاد آورد. پس بدیشان گفت: «شما جاسوسانید، و به جهت دیدن عریانی زمین آمده‌اید.»۹
10 Wakamjibu, “Sivyo bwana wangu. Watumishi wako wamekuja kununua chakula.
بدو گفتند: «نه، یا سیدی! بلکه غلامانت به جهت خریدن خوراک آمده‌اند.۱۰
11 Sisi sote ni wana wa baba mmoja. Watumishi wako ni watu waaminifu, wala sio wapelelezi.”
ماهمه پسران یک شخص هستیم. ما مردمان صادقیم؛ غلامانت، جاسوس نیستند.»۱۱
12 Akawaambia, “La hasha! Mmekuja kuangalia mahali ambapo nchi yetu haina ulinzi.”
بدیشان گفت: «نه، بلکه به جهت دیدن عریانی زمین آمده‌اید.»۱۲
13 Lakini wakamjibu, “Watumishi wako walikuwa kumi na wawili, wana wa mtu mmoja ambaye anaishi katika nchi ya Kanaani. Sasa mdogo wetu wa mwisho yupo na baba yetu na mwingine alikufa.”
گفتند: «غلامانت دوازده برادرند، پسران یک مرد در زمین کنعان. و اینک کوچکتر، امروز نزد پدر ماست، و یکی نایاب شده است.»۱۳
14 Yosefu akawaambia, “Ni sawa kabisa kama nilivyowaambia: Ninyi ni wapelelezi!
یوسف بدیشان گفت: «همین است آنچه به شما گفتم که جاسوسانید!۱۴
15 Na hivi ndivyo mtakavyojaribiwa: Hakika kama Farao aishivyo, hamtaondoka mahali hapa mpaka ndugu yenu mdogo aje hapa.
بدینطور آزموده می‌شوید: به حیات فرعون از اینجا بیرون نخواهید رفت، جز اینکه برادر کهتر شما در اینجابیاید.۱۵
16 Tumeni mmoja wenu akamlete huyo ndugu yenu, wengine mtawekwa gerezani, ili maneno yenu yajaribiwe kuona kama mnasema kweli. La sivyo, hakika kama Farao aishivyo ninyi ni wapelelezi!”
یک نفر از خودتان بفرستید، تا برادر شمارا بیاورد، و شما اسیر بمانید تا سخن شما آزموده شود که صدق با شماست یا نه، والا به حیات فرعون جاسوسانید!»۱۶
17 Akawaweka wote chini ya ulinzi kwa siku tatu.
پس ایشان را با هم سه روز در زندان انداخت.۱۷
18 Siku ya tatu Yosefu akawaambia, “Fanyeni hili nanyi mtaishi, kwa maana namwogopa Mungu:
و روز سوم یوسف بدیشان گفت: «این رابکنید و زنده باشید، زیرا من از خدا می‌ترسم:۱۸
19 Ikiwa ninyi ni watu waaminifu, mmoja wa ndugu zenu na abaki kifungoni, nanyi wengine pelekeni nafaka kwa jamaa yenu wanaoteseka kwa njaa.
هر گاه شما صادق هستید، یک برادر از شما درزندان شما اسیر باشد، و شما رفته، غله برای گرسنگی خانه های خود ببرید.۱۹
20 Lakini ni lazima mniletee ndugu yenu mdogo hapa, ili maneno yenu yathibitike na kwamba msife.” Wakakubali kufanya hivyo.
و برادر کوچک خود را نزد من آرید، تا سخنان شما تصدیق شودو نمیرید.» پس چنین کردند.۲۰
21 Wakaambiana wao kwa wao, “Hakika tunaadhibiwa kwa sababu ya ndugu yetu. Tuliona jinsi alivyohuzunika alipokuwa anatusihi kuponya maisha yake, lakini hatukumsikiliza, hiyo ndiyo sababu dhiki hii imetupata.”
و به یکدیگر گفتند: «هر آینه به برادر خودخطا کردیم، زیرا تنگی جان او را دیدیم وقتی که به ما استغاثه می‌کرد، و نشنیدیم. از این‌رو این تنگی بر ما رسید.»۲۱
22 Reubeni akawajibu, “Sikuwaambieni msitende dhambi dhidi ya kijana? Lakini hamkunisikiliza! Sasa ni lazima tuadhibiwe kwa ajili ya damu yake.”
و روبین در جواب ایشان گفت: «آیا به شما نگفتم که به پسر خطا مورزید؟۲۲
23 Hawakujua kuwa Yosefu angewaelewa, kwa sababu alitumia mkalimani.
و ایشان ندانستند که یوسف می‌فهمد، زیرا که ترجمانی در میان ایشان بود.۲۳
24 Yosefu akajitenga nao akaanza kulia, kisha akawarudia na kuzungumza nao tena. Akataka Simeoni akamatwe na kufungwa mbele yao.
پس از ایشان کناره جسته، بگریست و نزدایشان برگشته، با ایشان گفتگو کرد، و شمعون را ازمیان ایشان گرفته، او را روبروی ایشان دربند نهاد.۲۴
25 Yosefu akatoa amri ya kujaza magunia yao nafaka na kuweka fedha ya kila mmoja ndani ya gunia lake, kisha wapewe mahitaji ya njiani. Baada ya kufanyiwa hayo yote,
و یوسف فرمود تا جوالهای ایشان را از غله پر سازند، و نقد ایشان را در عدل هر کس نهند، وزاد سفر بدیشان دهند، و به ایشان چنین کردند.۲۵
26 wakapakiza nafaka juu ya punda zao, wakaondoka.
پس غله را بر حماران خود بار کرده، از آنجاروانه شدند.۲۶
27 Walipofika mahali pa kulala huko njiani mmoja wao akafungua gunia lake ili amlishe punda wake, akakuta fedha yake kwenye mdomo wa gunia lake.
و چون یکی، عدل خود را در منزل باز کرد، تا خوراک به الاغ دهد، نقد خود را دید که اینک در دهن عدل او بود.۲۷
28 Akawaambia ndugu zake, “Fedha yangu imerudishwa. Iko ndani ya gunia langu.” Mioyo yao ikazimia, na kila mmoja akamgeukia mwenzake wakitetemeka, wakaulizana, “Ni nini hiki Mungu alichotufanyia?”
و به برادران خود گفت: «نقد من رد شده است، و اینک در عدل من است. آنگاه دل ایشان طپیدن گرفت، و به یکدیگر لرزان شده، گفتند: «این چیست که خدا به ما کرده است.»۲۸
29 Walipofika kwa Yakobo baba yao katika nchi ya Kanaani, wakamweleza mambo yote yaliyowapata. Wakasema,
پس نزد پدر خود، یعقوب، به زمین کنعان آمدند، و از آنچه بدیشان واقع شده بود، خبرداده، گفتند:۲۹
30 “Huyo mtu ambaye ndiye bwana katika nchi hiyo alisema nasi kwa ukali, akatutendea kana kwamba sisi tulikuwa tunaipeleleza nchi.
«آن مرد که حاکم زمین است، با مابه سختی سخن گفت، و ما را جاسوسان زمین پنداشت.۳۰
31 Lakini tulimwambia, ‘Sisi ni watu waaminifu, sio wapelelezi.
و بدو گفتیم ما صادقیم و جاسوس نی.۳۱
32 Tulizaliwa ndugu kumi na wawili, wana wa baba mmoja. Mmoja alikufa, na mdogo wetu wa mwisho yupo na baba yetu huko Kanaani.’
ما دوازده برادر، پسران پدر خود هستیم، یکی نایاب شده است، و کوچکتر، امروز نزد پدرما در زمین کنعان می‌باشد.۳۲
33 “Ndipo huyo mtu aliye bwana katika nchi hiyo alipotuambia, ‘Hivi ndivyo nitafahamu kuwa ninyi ni watu waaminifu: Mwacheni mmoja wa ndugu zenu pamoja nami hapa, kisha nendeni mpeleke chakula kwa ajili ya jamaa yenu inayoteseka kwa njaa.
و آن مرد که حاکم زمین است، به ما گفت: از این خواهم فهمید که شما راستگو هستید که یکی از برادران خود را نزدمن گذارید، و برای گرسنگی خانه های خودگرفته، بروید.۳۳
34 Lakini mleteni huyo ndugu yenu mdogo kwangu, ndipo nitajua kuwa ninyi sio wapelelezi, ila ni watu waaminifu. Kisha nitamrudisha ndugu yenu, nanyi mtaweza kufanya biashara katika nchi hii.’”
و برادر کوچک خود را نزد من آرید، و خواهم یافت که شما جاسوس نیستیدبلکه صادق. آنگاه برادر شما را به شما رد کنم، ودر زمین داد و ستد نمایید.»۳۴
35 Walipokuwa wanamimina nafaka kutoka kwenye magunia yao, ndani ya gunia la kila mtu kulikuwa na mfuko wa fedha! Wakati wao na baba yao walipoona mifuko ya fedha, wakaogopa.
و واقع شد که چون عدلهای خود را خالی می‌کردند، اینک کیسه پول هر کس در عدلش بود. و چون ایشان و پدرشان، کیسه های پول را دیدند، بترسیدند.۳۵
36 Yakobo baba yao akawaambia, “Ninyi mmenipokonya watoto wangu. Yosefu hayupo na Simeoni hayupo tena na sasa mnataka kumchukua Benyamini. Kila kitu ni kinyume nami!”
و پدر ایشان، یعقوب، بدیشان گفت: «مرا بی‌اولاد ساختید، یوسف نیست و شمعون نیست و بنیامین را می‌خواهید ببرید. این همه برمن است؟»۳۶
37 Ndipo Reubeni akamwambia baba yake, “Waweza kuwaua wanangu wote wawili, ikiwa sitamrudisha Benyamini kwako. Mkabidhi Benyamini katika uangalizi wangu, nami nitamrudisha.”
روبین به پدر خود عرض کرده، گفت: «هر دو پسر مرا بکش، اگر او را نزد تو بازنیاورم. او را به‌دست من بسپار، و من او را نزد توباز خواهم آورد.»۳۷
38 Lakini Yakobo akasema, “Mwanangu hatashuka huko pamoja nanyi; ndugu yake amekufa naye ndiye peke yake aliyebaki. Ikiwa atapatwa na madhara katika safari mnayoiendea, mtashusha kichwa changu chenye mvi kaburini kwa masikitiko.” (Sheol h7585)
گفت: «پسرم با شما نخواهد آمد زیرا که برادرش مرده است، و او تنها باقی است. و هر گاه در راهی که می‌روید زیانی بدو رسد، همانامویهای سفید مرا با حزن به گور فرود خواهیدبرد.» (Sheol h7585)۳۸

< Mwanzo 42 >