< Mwanzo 42 >

1 Wakati Yakobo alipofahamu kuwa kuna nafaka huko Misri, akawaambia wanawe, “Mbona mnakaa tu hapa mnatazamana?”
When someone told Jacob that there was grain in Egypt that people could buy, he said to his sons, “(Why do you just sit there looking at each other?/Do not just sit there looking at each other!) [RHQ] We need some grain!”
2 Akaendelea kuwaambia, “Nimesikia kuwa huko Misri kuna nafaka. Telemkeni huko mkanunue chakula kwa ajili yetu, ili tuweze kuishi wala tusife.”
He said to them, “Someone told me that there is grain for sale in Egypt. Go down there and buy some for us, in order that we will not die!”
3 Ndipo wale ndugu kumi wa Yosefu, wakateremka huko Misri kununua nafaka.
So Joseph’s ten [older] brothers went down to Egypt to buy some grain.
4 Lakini Yakobo hakumtuma Benyamini, ndugu yake Yosefu, pamoja na wengine, kwa sababu aliogopa asije akapatwa na madhara.
But Jacob did not send Benjamin, Joseph’s [younger] brother, to go with the others, because he was afraid/worried that something terrible might happen to him like what happened to Joseph.
5 Hivyo wana wa Israeli walikuwa miongoni mwa wale waliokwenda Misri kununua nafaka, kwani njaa ilikuwa katika nchi ya Kanaani pia.
So Jacob’s other sons went down from Canaan to Egypt to buy grain, and others from there went too, because there was a famine in Canaan also.
6 Wakati huo Yosefu alikuwa mtawala wa nchi ya Misri, naye alikuwa ndiye aliwauzia watu wote nafaka. Kwa hiyo wakati ndugu zake Yosefu walipofika, wakamsujudia hadi nyuso zao zikagusa ardhi.
At that time Joseph was the governor of Egypt. He was the one who sold grain to people who came from all over Egypt and from many other countries [HYP] to buy grain. So when Joseph’s brothers arrived, [they were told that it was necessary for them to talk with Joseph. So they went to him and] prostrated themselves before him with their faces to the ground.
7 Mara Yosefu alipowaona ndugu zake, akawatambua, lakini akajifanya mgeni na kuzungumza nao kwa ukali, akiwauliza, “Ninyi mnatoka wapi?” Wakamjibu, “Tumetoka katika nchi ya Kanaani kuja kununua chakula.”
As soon as Joseph saw his brothers, he recognized them. But he pretended that he did not know them. He spoke harshly to them, saying, “Where do you come from?” One of them replied, “We have come from Canaan, to buy some grain.”
8 Ingawa Yosefu aliwatambua ndugu zake, wao hawakumtambua.
Although Joseph recognized his brothers, they did not recognize him.
9 Ndipo Yosefu alipokumbuka ndoto zake kuwahusu wao, akawaambia, “Ninyi ni wapelelezi! Mmekuja kuangalia mahali ambapo nchi yetu haina ulinzi.”
And then Joseph remembered what he had dreamed about them many years previously. [But he decided not to tell them yet that he was their younger brother]. He said to them, “You are spies! You have come to find out whether we will be able to defend ourselves [if you attack us]!”
10 Wakamjibu, “Sivyo bwana wangu. Watumishi wako wamekuja kununua chakula.
One of them replied, “No, sir! We have come to buy grain.
11 Sisi sote ni wana wa baba mmoja. Watumishi wako ni watu waaminifu, wala sio wapelelezi.”
We are all sons of one man. We are honest men, not spies.”
12 Akawaambia, “La hasha! Mmekuja kuangalia mahali ambapo nchi yetu haina ulinzi.”
He said to them, “[I do not believe you]. You have come just to see whether we would be able to defend ourselves if we were attacked!”
13 Lakini wakamjibu, “Watumishi wako walikuwa kumi na wawili, wana wa mtu mmoja ambaye anaishi katika nchi ya Kanaani. Sasa mdogo wetu wa mwisho yupo na baba yetu na mwingine alikufa.”
But one of them replied, “No, that is not true! Originally there were twelve of us who were brothers, the sons of one man. Our younger brother is with our father. One [younger] brother has died. [EUP]”
14 Yosefu akawaambia, “Ni sawa kabisa kama nilivyowaambia: Ninyi ni wapelelezi!
Joseph replied, “[You are lying! I think] it is just as I told you. You are spies!
15 Na hivi ndivyo mtakavyojaribiwa: Hakika kama Farao aishivyo, hamtaondoka mahali hapa mpaka ndugu yenu mdogo aje hapa.
But this is how I will determine whether what you are saying is true. I think that as surely as the king lives, you are spies. And you will not leave this place until your youngest brother comes here!
16 Tumeni mmoja wenu akamlete huyo ndugu yenu, wengine mtawekwa gerezani, ili maneno yenu yajaribiwe kuona kama mnasema kweli. La sivyo, hakika kama Farao aishivyo ninyi ni wapelelezi!”
Send one of your group to go and get your younger brother and bring him here. I will put the rest of you in prison, in order that I may test what you have said to find out whether what you are telling me is true. If the one who goes does not bring your younger brother here, then, just as surely as the king lives, it will be clear that you are lying and that you are spies.”
17 Akawaweka wote chini ya ulinzi kwa siku tatu.
Then Joseph put them all in prison for three days.
18 Siku ya tatu Yosefu akawaambia, “Fanyeni hili nanyi mtaishi, kwa maana namwogopa Mungu:
On the third day, Joseph went to the prison and said to them, “I am a man who fears that God [will punish me if I do not do what I promise]. So do what I tell you, and I will spare your lives.
19 Ikiwa ninyi ni watu waaminifu, mmoja wa ndugu zenu na abaki kifungoni, nanyi wengine pelekeni nafaka kwa jamaa yenu wanaoteseka kwa njaa.
If you are honest men, let one of your brothers stay here in prison, and the rest of you can take some grain back to your families who are very hungry because of the famine.
20 Lakini ni lazima mniletee ndugu yenu mdogo hapa, ili maneno yenu yathibitike na kwamba msife.” Wakakubali kufanya hivyo.
But if you come back here again, you must bring your youngest brother to me, so that you can prove that what you told me is true, and as a result I will not have you executed.” So they agreed to do that.
21 Wakaambiana wao kwa wao, “Hakika tunaadhibiwa kwa sababu ya ndugu yetu. Tuliona jinsi alivyohuzunika alipokuwa anatusihi kuponya maisha yake, lakini hatukumsikiliza, hiyo ndiyo sababu dhiki hii imetupata.”
They said to each other, “It is surely because of what we did to our [younger] brother that (we are being punished/God is punishing us)! We saw that he [SYN] was very distressed when he pleaded with us not to harm him. But we did not pay any attention to him, and that is why we are having this trouble!”
22 Reubeni akawajibu, “Sikuwaambieni msitende dhambi dhidi ya kijana? Lakini hamkunisikiliza! Sasa ni lazima tuadhibiwe kwa ajili ya damu yake.”
Reuben said to them, “I told you not to harm the boy [RHQ], but you did not pay attention to what I said! Now we are being (paid back/punished) for killing him [MTY]!”
23 Hawakujua kuwa Yosefu angewaelewa, kwa sababu alitumia mkalimani.
While they were talking with Joseph, they were speaking through (an interpreter/someone who knew their language and the Egyptian language), but when they said these things among themselves, they were speaking in their own language, and they did not know that Joseph could understand their language, and that he could understand what they were saying.
24 Yosefu akajitenga nao akaanza kulia, kisha akawarudia na kuzungumza nao tena. Akataka Simeoni akamatwe na kufungwa mbele yao.
[Because of what they said, Joseph realized that they admitted that what they had done to him many years previously was wrong]. He could not keep from crying, [and he did not want them to see him crying], so he left them and went outside the room and began to cry. But then he returned to them and talked to them again. Then he took Simeon, and while they were watching, he told his servants to tie him up. He left Simeon in the prison and told the others that they could go.
25 Yosefu akatoa amri ya kujaza magunia yao nafaka na kuweka fedha ya kila mmoja ndani ya gunia lake, kisha wapewe mahitaji ya njiani. Baada ya kufanyiwa hayo yote,
Joseph told his servants to fill the men’s sacks with grain, but he also told them to put the money that each one had paid for the grain in the top of his sack. He also told them to give them food to eat along the way. After the servants did those things for Joseph’s older brothers,
26 wakapakiza nafaka juu ya punda zao, wakaondoka.
his older brothers loaded the sacks of grain on their donkeys and left.
27 Walipofika mahali pa kulala huko njiani mmoja wao akafungua gunia lake ili amlishe punda wake, akakuta fedha yake kwenye mdomo wa gunia lake.
At the place where they stopped to sleep that night, one of them opened his sack to get some grain for his donkey. He was amazed to see his money in the top of the sack.
28 Akawaambia ndugu zake, “Fedha yangu imerudishwa. Iko ndani ya gunia langu.” Mioyo yao ikazimia, na kila mmoja akamgeukia mwenzake wakitetemeka, wakaulizana, “Ni nini hiki Mungu alichotufanyia?”
He exclaimed to his brothers, “Someone has returned my money! Here it is in my sack!” They started shaking with fear, and said to each other, “What is this that God has done to us?”
29 Walipofika kwa Yakobo baba yao katika nchi ya Kanaani, wakamweleza mambo yote yaliyowapata. Wakasema,
When they returned to their father in Canaan land, they told him all that had happened to them. One of them said,
30 “Huyo mtu ambaye ndiye bwana katika nchi hiyo alisema nasi kwa ukali, akatutendea kana kwamba sisi tulikuwa tunaipeleleza nchi.
“The man who governs the whole land of Egypt talked very harshly to us. He acted toward us as though we were spying on his country.
31 Lakini tulimwambia, ‘Sisi ni watu waaminifu, sio wapelelezi.
But we told him, ‘We are honest men! We are not spies.
32 Tulizaliwa ndugu kumi na wawili, wana wa baba mmoja. Mmoja alikufa, na mdogo wetu wa mwisho yupo na baba yetu huko Kanaani.’
Originally there were twelve of us who were brothers, the sons of one father. One has died [EUP], and our youngest brother is with our father in Canaan.’
33 “Ndipo huyo mtu aliye bwana katika nchi hiyo alipotuambia, ‘Hivi ndivyo nitafahamu kuwa ninyi ni watu waaminifu: Mwacheni mmoja wa ndugu zenu pamoja nami hapa, kisha nendeni mpeleke chakula kwa ajili ya jamaa yenu inayoteseka kwa njaa.
The man who is the governor of the land [did not believe us], so he said to us, ‘This is how I will know if you are truly honest men: Leave one of your brothers here with me. Then the rest of you can take some grain for your families that are starving from hunger and go.
34 Lakini mleteni huyo ndugu yenu mdogo kwangu, ndipo nitajua kuwa ninyi sio wapelelezi, ila ni watu waaminifu. Kisha nitamrudisha ndugu yenu, nanyi mtaweza kufanya biashara katika nchi hii.’”
But when you return, bring your youngest brother to me, in order that I will know that you are not spies, but instead, that you are honest men. Then I will release your brother for you. And then you can buy whatever you want in this country.’”
35 Walipokuwa wanamimina nafaka kutoka kwenye magunia yao, ndani ya gunia la kila mtu kulikuwa na mfuko wa fedha! Wakati wao na baba yao walipoona mifuko ya fedha, wakaogopa.
As they were emptying their sacks, they were surprised that in each man’s sack was his pouch of money! When they and their father saw all the pouches of money, they were frightened.
36 Yakobo baba yao akawaambia, “Ninyi mmenipokonya watoto wangu. Yosefu hayupo na Simeoni hayupo tena na sasa mnataka kumchukua Benyamini. Kila kitu ni kinyume nami!”
Their father Jacob said to them, “You have caused two of my children to be taken from me! Joseph is dead, and Simeon is gone! And now you want to take Benjamin from me! It is I who am suffering because of all these things that are happening!”
37 Ndipo Reubeni akamwambia baba yake, “Waweza kuwaua wanangu wote wawili, ikiwa sitamrudisha Benyamini kwako. Mkabidhi Benyamini katika uangalizi wangu, nami nitamrudisha.”
Reuben said to his father, “I will be responsible for Benjamin. [I will take him to Egypt and] bring him back to you. Let me take care of him. If I do not bring Benjamin back to you, you may kill both of my sons.”
38 Lakini Yakobo akasema, “Mwanangu hatashuka huko pamoja nanyi; ndugu yake amekufa naye ndiye peke yake aliyebaki. Ikiwa atapatwa na madhara katika safari mnayoiendea, mtashusha kichwa changu chenye mvi kaburini kwa masikitiko.” (Sheol h7585)
But Jacob said, “No, I will not let my son go down there with you. His [older] brother is dead, and he is the only [one of my wife Rachel’s] sons who is left! If something harms him while you are traveling, you would cause me, a gray-haired old man, to die because of sorrow.” (Sheol h7585)

< Mwanzo 42 >