< Mwanzo 42 >

1 Wakati Yakobo alipofahamu kuwa kuna nafaka huko Misri, akawaambia wanawe, “Mbona mnakaa tu hapa mnatazamana?”
and to see: examine Jacob for there grain in/on/with Egypt and to say Jacob to/for son: child his to/for what? to see: see
2 Akaendelea kuwaambia, “Nimesikia kuwa huko Misri kuna nafaka. Telemkeni huko mkanunue chakula kwa ajili yetu, ili tuweze kuishi wala tusife.”
and to say behold to hear: hear for there grain in/on/with Egypt to go down there [to] and to buy grain to/for us from there and to live and not to die
3 Ndipo wale ndugu kumi wa Yosefu, wakateremka huko Misri kununua nafaka.
and to go down brother: male-sibling Joseph ten to/for to buy grain grain from Egypt
4 Lakini Yakobo hakumtuma Benyamini, ndugu yake Yosefu, pamoja na wengine, kwa sababu aliogopa asije akapatwa na madhara.
and [obj] Benjamin brother: male-sibling Joseph not to send: depart Jacob with brother: male-sibling his for to say lest to encounter: chanced him harm
5 Hivyo wana wa Israeli walikuwa miongoni mwa wale waliokwenda Misri kununua nafaka, kwani njaa ilikuwa katika nchi ya Kanaani pia.
and to come (in): come son: child Israel to/for to buy grain in/on/with midst [the] to come (in): come for to be [the] famine in/on/with land: country/planet Canaan
6 Wakati huo Yosefu alikuwa mtawala wa nchi ya Misri, naye alikuwa ndiye aliwauzia watu wote nafaka. Kwa hiyo wakati ndugu zake Yosefu walipofika, wakamsujudia hadi nyuso zao zikagusa ardhi.
and Joseph he/she/it [the] domineering upon [the] land: country/planet he/she/it [the] to buy grain to/for all people [the] land: country/planet and to come (in): come brother: male-sibling Joseph and to bow to/for him face land: soil [to]
7 Mara Yosefu alipowaona ndugu zake, akawatambua, lakini akajifanya mgeni na kuzungumza nao kwa ukali, akiwauliza, “Ninyi mnatoka wapi?” Wakamjibu, “Tumetoka katika nchi ya Kanaani kuja kununua chakula.”
and to see: see Joseph [obj] brother: male-sibling his and to recognize them and to alienate to(wards) them and to speak: speak with them severe and to say to(wards) them from where? to come (in): come and to say from land: country/planet Canaan to/for to buy grain food
8 Ingawa Yosefu aliwatambua ndugu zake, wao hawakumtambua.
and to recognize Joseph [obj] brother: male-sibling his and they(masc.) not to recognize him
9 Ndipo Yosefu alipokumbuka ndoto zake kuwahusu wao, akawaambia, “Ninyi ni wapelelezi! Mmekuja kuangalia mahali ambapo nchi yetu haina ulinzi.”
and to remember Joseph [obj] [the] dream which to dream to/for them and to say to(wards) them to spy you(m. p.) to/for to see: see [obj] nakedness [the] land: country/planet to come (in): come
10 Wakamjibu, “Sivyo bwana wangu. Watumishi wako wamekuja kununua chakula.
and to say to(wards) him not lord my and servant/slave your to come (in): come to/for to buy grain food
11 Sisi sote ni wana wa baba mmoja. Watumishi wako ni watu waaminifu, wala sio wapelelezi.”
all our son: child man one we right we not to be servant/slave your to spy
12 Akawaambia, “La hasha! Mmekuja kuangalia mahali ambapo nchi yetu haina ulinzi.”
and to say to(wards) them not for nakedness [the] land: country/planet to come (in): come to/for to see: see
13 Lakini wakamjibu, “Watumishi wako walikuwa kumi na wawili, wana wa mtu mmoja ambaye anaishi katika nchi ya Kanaani. Sasa mdogo wetu wa mwisho yupo na baba yetu na mwingine alikufa.”
and to say two ten servant/slave your brother: male-sibling we son: child man one in/on/with land: country/planet Canaan and behold [the] small: young with father our [the] day: today and [the] one nothing he
14 Yosefu akawaambia, “Ni sawa kabisa kama nilivyowaambia: Ninyi ni wapelelezi!
and to say to(wards) them Joseph he/she/it which to speak: speak to(wards) you to/for to say to spy you(m. p.)
15 Na hivi ndivyo mtakavyojaribiwa: Hakika kama Farao aishivyo, hamtaondoka mahali hapa mpaka ndugu yenu mdogo aje hapa.
in/on/with this to test alive Pharaoh if: surely no to come out: come from this that if: except if: except in/on/with to come (in): come brother: male-sibling your [the] small: young here/thus
16 Tumeni mmoja wenu akamlete huyo ndugu yenu, wengine mtawekwa gerezani, ili maneno yenu yajaribiwe kuona kama mnasema kweli. La sivyo, hakika kama Farao aishivyo ninyi ni wapelelezi!”
to send: depart from you one and to take: bring [obj] brother: male-sibling your and you(m. p.) to bind and to test word your truth: true with you and if not alive Pharaoh for to spy you(m. p.)
17 Akawaweka wote chini ya ulinzi kwa siku tatu.
and to gather [obj] them to(wards) custody three day
18 Siku ya tatu Yosefu akawaambia, “Fanyeni hili nanyi mtaishi, kwa maana namwogopa Mungu:
and to say to(wards) them Joseph in/on/with day [the] third this to make: do and to live [obj] [the] God I afraid
19 Ikiwa ninyi ni watu waaminifu, mmoja wa ndugu zenu na abaki kifungoni, nanyi wengine pelekeni nafaka kwa jamaa yenu wanaoteseka kwa njaa.
if right you(m. p.) brother: male-sibling your one to bind in/on/with house: home custody your and you(m. p.) to go: went to come (in): bring grain famine house: household your
20 Lakini ni lazima mniletee ndugu yenu mdogo hapa, ili maneno yenu yathibitike na kwamba msife.” Wakakubali kufanya hivyo.
and [obj] brother: male-sibling your [the] small: young to come (in): bring to(wards) me and be faithful word your and not to die and to make: do so
21 Wakaambiana wao kwa wao, “Hakika tunaadhibiwa kwa sababu ya ndugu yetu. Tuliona jinsi alivyohuzunika alipokuwa anatusihi kuponya maisha yake, lakini hatukumsikiliza, hiyo ndiyo sababu dhiki hii imetupata.”
and to say man: anyone to(wards) brother: compatriot his truly guilty we upon brother: male-sibling our which to see: see distress soul his in/on/with be gracious he to(wards) us and not to hear: hear upon so to come (in): come to(wards) us [the] distress [the] this
22 Reubeni akawajibu, “Sikuwaambieni msitende dhambi dhidi ya kijana? Lakini hamkunisikiliza! Sasa ni lazima tuadhibiwe kwa ajili ya damu yake.”
and to answer Reuben [obj] them to/for to say not to say to(wards) you to/for to say not to sin in/on/with youth and not to hear: hear and also blood his behold to seek
23 Hawakujua kuwa Yosefu angewaelewa, kwa sababu alitumia mkalimani.
and they(masc.) not to know for to hear: understand Joseph for [the] to mock between them
24 Yosefu akajitenga nao akaanza kulia, kisha akawarudia na kuzungumza nao tena. Akataka Simeoni akamatwe na kufungwa mbele yao.
and to turn: turn from upon them and to weep and to return: return to(wards) them and to speak: speak to(wards) them and to take: take from with them [obj] Simeon and to bind [obj] him to/for eye: before(the eyes) their
25 Yosefu akatoa amri ya kujaza magunia yao nafaka na kuweka fedha ya kila mmoja ndani ya gunia lake, kisha wapewe mahitaji ya njiani. Baada ya kufanyiwa hayo yote,
and to command Joseph and to fill [obj] article/utensil their grain and to/for to return: return silver: money their man: anyone to(wards) sackcloth his and to/for to give: give to/for them provision to/for way: journey and to make: do to/for them so
26 wakapakiza nafaka juu ya punda zao, wakaondoka.
and to lift: bear [obj] grain their upon donkey their and to go: went from there
27 Walipofika mahali pa kulala huko njiani mmoja wao akafungua gunia lake ili amlishe punda wake, akakuta fedha yake kwenye mdomo wa gunia lake.
and to open [the] one [obj] sackcloth his to/for to give: give fodder to/for donkey his in/on/with lodging and to see: see [obj] silver: money his and behold he/she/it in/on/with lip sack his
28 Akawaambia ndugu zake, “Fedha yangu imerudishwa. Iko ndani ya gunia langu.” Mioyo yao ikazimia, na kila mmoja akamgeukia mwenzake wakitetemeka, wakaulizana, “Ni nini hiki Mungu alichotufanyia?”
and to say to(wards) brother: male-sibling his to return: return silver: money my and also behold in/on/with sack my and to come out: surrender heart their and to tremble man: anyone to(wards) brother: compatriot his to/for to say what? this to make: do God to/for us
29 Walipofika kwa Yakobo baba yao katika nchi ya Kanaani, wakamweleza mambo yote yaliyowapata. Wakasema,
and to come (in): come to(wards) Jacob father their land: country/planet [to] Canaan and to tell to/for him [obj] all [the] to meet [obj] them to/for to say
30 “Huyo mtu ambaye ndiye bwana katika nchi hiyo alisema nasi kwa ukali, akatutendea kana kwamba sisi tulikuwa tunaipeleleza nchi.
to speak: speak [the] man lord [the] land: country/planet with us severe and to give: make [obj] us like/as to spy [obj] [the] land: country/planet
31 Lakini tulimwambia, ‘Sisi ni watu waaminifu, sio wapelelezi.
and to say to(wards) him right we not to be to spy
32 Tulizaliwa ndugu kumi na wawili, wana wa baba mmoja. Mmoja alikufa, na mdogo wetu wa mwisho yupo na baba yetu huko Kanaani.’
two ten we brother: male-sibling son: child father our [the] one nothing he and [the] small: young [the] day: today with father our in/on/with land: country/planet Canaan
33 “Ndipo huyo mtu aliye bwana katika nchi hiyo alipotuambia, ‘Hivi ndivyo nitafahamu kuwa ninyi ni watu waaminifu: Mwacheni mmoja wa ndugu zenu pamoja nami hapa, kisha nendeni mpeleke chakula kwa ajili ya jamaa yenu inayoteseka kwa njaa.
and to say to(wards) us [the] man lord [the] land: country/planet in/on/with this to know for right you(m. p.) brother: male-sibling your [the] one to rest with me and [obj] famine house: household your to take: take and to go: went
34 Lakini mleteni huyo ndugu yenu mdogo kwangu, ndipo nitajua kuwa ninyi sio wapelelezi, ila ni watu waaminifu. Kisha nitamrudisha ndugu yenu, nanyi mtaweza kufanya biashara katika nchi hii.’”
and to come (in): bring [obj] brother: male-sibling your [the] small: young to(wards) me and to know for not to spy you(m. p.) for right you(m. p.) [obj] brother: male-sibling your to give: give to/for you and [obj] [the] land: country/planet to trade
35 Walipokuwa wanamimina nafaka kutoka kwenye magunia yao, ndani ya gunia la kila mtu kulikuwa na mfuko wa fedha! Wakati wao na baba yao walipoona mifuko ya fedha, wakaogopa.
and to be they(masc.) to empty sackcloth their and behold man: anyone bundle silver: money his in/on/with sackcloth his and to see: see [obj] bundle silver: money their they(masc.) and father their and to fear
36 Yakobo baba yao akawaambia, “Ninyi mmenipokonya watoto wangu. Yosefu hayupo na Simeoni hayupo tena na sasa mnataka kumchukua Benyamini. Kila kitu ni kinyume nami!”
and to say to(wards) them Jacob father their [obj] me be bereaved Joseph nothing he and Simeon nothing he and [obj] Benjamin to take: take upon me to be all their
37 Ndipo Reubeni akamwambia baba yake, “Waweza kuwaua wanangu wote wawili, ikiwa sitamrudisha Benyamini kwako. Mkabidhi Benyamini katika uangalizi wangu, nami nitamrudisha.”
and to say Reuben to(wards) father his to/for to say [obj] two son: child my to die if not to come (in): bring him to(wards) you to give: put [emph?] [obj] him upon hand my and I to return: return him to(wards) you
38 Lakini Yakobo akasema, “Mwanangu hatashuka huko pamoja nanyi; ndugu yake amekufa naye ndiye peke yake aliyebaki. Ikiwa atapatwa na madhara katika safari mnayoiendea, mtashusha kichwa changu chenye mvi kaburini kwa masikitiko.” (Sheol h7585)
and to say not to go down son: child my with you for brother: male-sibling his to die and he/she/it to/for alone him to remain and to encounter: chanced him harm in/on/with way: journey which to go: continue in/on/with her and to go down [obj] greyheaded my in/on/with sorrow hell: Sheol [to] (Sheol h7585)

< Mwanzo 42 >