< Mwanzo 42 >
1 Wakati Yakobo alipofahamu kuwa kuna nafaka huko Misri, akawaambia wanawe, “Mbona mnakaa tu hapa mnatazamana?”
Then Jacob, hearing that food was being sold in Egypt, said to his sons: “Why are you negligent?
2 Akaendelea kuwaambia, “Nimesikia kuwa huko Misri kuna nafaka. Telemkeni huko mkanunue chakula kwa ajili yetu, ili tuweze kuishi wala tusife.”
I have heard that wheat is being sold in Egypt. Go down and buy necessities for us, so that we may be able to live, and not be consumed by destitution.”
3 Ndipo wale ndugu kumi wa Yosefu, wakateremka huko Misri kununua nafaka.
And so, when ten brothers of Joseph went down to buy grain in Egypt,
4 Lakini Yakobo hakumtuma Benyamini, ndugu yake Yosefu, pamoja na wengine, kwa sababu aliogopa asije akapatwa na madhara.
Benjamin was kept at home by Jacob, who said to his brothers, “Lest perhaps he may suffer harm on the journey.”
5 Hivyo wana wa Israeli walikuwa miongoni mwa wale waliokwenda Misri kununua nafaka, kwani njaa ilikuwa katika nchi ya Kanaani pia.
And they entered into the land of Egypt with the others who traveled to buy. For the famine was in the land of Canaan.
6 Wakati huo Yosefu alikuwa mtawala wa nchi ya Misri, naye alikuwa ndiye aliwauzia watu wote nafaka. Kwa hiyo wakati ndugu zake Yosefu walipofika, wakamsujudia hadi nyuso zao zikagusa ardhi.
And Joseph was governor in the land of Egypt, and grain was sold under his direction to the people. And when his brothers had reverenced him
7 Mara Yosefu alipowaona ndugu zake, akawatambua, lakini akajifanya mgeni na kuzungumza nao kwa ukali, akiwauliza, “Ninyi mnatoka wapi?” Wakamjibu, “Tumetoka katika nchi ya Kanaani kuja kununua chakula.”
and he had recognized them, he spoke harshly, as if to foreigners, questioning them: “Where did you come from?” And they responded, “From the land of Canaan, to buy necessary provisions.”
8 Ingawa Yosefu aliwatambua ndugu zake, wao hawakumtambua.
And although he knew his brothers, he was not known by them.
9 Ndipo Yosefu alipokumbuka ndoto zake kuwahusu wao, akawaambia, “Ninyi ni wapelelezi! Mmekuja kuangalia mahali ambapo nchi yetu haina ulinzi.”
And remembering the dreams, which he had seen in another time, he said to them: “You are scouts. You have come in order to see which parts of the land are weaker.”
10 Wakamjibu, “Sivyo bwana wangu. Watumishi wako wamekuja kununua chakula.
And they said: “It is not so, my lord. But your servants have arrived in order to buy food.
11 Sisi sote ni wana wa baba mmoja. Watumishi wako ni watu waaminifu, wala sio wapelelezi.”
We are all sons of one man. We have come in peace, nor do any of your subjects devise evil.”
12 Akawaambia, “La hasha! Mmekuja kuangalia mahali ambapo nchi yetu haina ulinzi.”
And he answered them: “It is otherwise. You have come to examine the unguarded parts of this land.”
13 Lakini wakamjibu, “Watumishi wako walikuwa kumi na wawili, wana wa mtu mmoja ambaye anaishi katika nchi ya Kanaani. Sasa mdogo wetu wa mwisho yupo na baba yetu na mwingine alikufa.”
But they said: “We, your servants, are twelve brothers, the sons of one man in the land of Canaan. The youngest is with our father; the other is not living.”
14 Yosefu akawaambia, “Ni sawa kabisa kama nilivyowaambia: Ninyi ni wapelelezi!
He said: “This is just as I have said. You are scouts.
15 Na hivi ndivyo mtakavyojaribiwa: Hakika kama Farao aishivyo, hamtaondoka mahali hapa mpaka ndugu yenu mdogo aje hapa.
I will now continue to put you to the test. By the health of Pharaoh, you will not depart from here, until your youngest brother arrives.
16 Tumeni mmoja wenu akamlete huyo ndugu yenu, wengine mtawekwa gerezani, ili maneno yenu yajaribiwe kuona kama mnasema kweli. La sivyo, hakika kama Farao aishivyo ninyi ni wapelelezi!”
Send one of you and bring him. But you will be in chains, until what you have said is proven to be either true or false. Otherwise, by the health of Pharaoh, you are scouts.”
17 Akawaweka wote chini ya ulinzi kwa siku tatu.
Therefore, he delivered them into custody for three days.
18 Siku ya tatu Yosefu akawaambia, “Fanyeni hili nanyi mtaishi, kwa maana namwogopa Mungu:
Then, on the third day, he brought them out of prison, and he said: “Do as I have said, and you will live. For I fear God.
19 Ikiwa ninyi ni watu waaminifu, mmoja wa ndugu zenu na abaki kifungoni, nanyi wengine pelekeni nafaka kwa jamaa yenu wanaoteseka kwa njaa.
If you are peaceful, let one of your brothers be bound in prison. Then you may go away and carry the grain that you have bought to your houses.
20 Lakini ni lazima mniletee ndugu yenu mdogo hapa, ili maneno yenu yathibitike na kwamba msife.” Wakakubali kufanya hivyo.
And bring your youngest brother to me, so that I may be able to test your words, and you may not die.” They did as he had said,
21 Wakaambiana wao kwa wao, “Hakika tunaadhibiwa kwa sababu ya ndugu yetu. Tuliona jinsi alivyohuzunika alipokuwa anatusihi kuponya maisha yake, lakini hatukumsikiliza, hiyo ndiyo sababu dhiki hii imetupata.”
and they spoke to one another: “We deserve to suffer these things, because we have sinned against our brother, seeing the anguish of his soul, when he begged us and we would not listen. For that reason, this tribulation has come upon us.”
22 Reubeni akawajibu, “Sikuwaambieni msitende dhambi dhidi ya kijana? Lakini hamkunisikiliza! Sasa ni lazima tuadhibiwe kwa ajili ya damu yake.”
And Reuben, one of them, said: “Did not I say to you, ‘Do not sin against the boy,’ and you would not listen to me? See, his blood is exacted.”
23 Hawakujua kuwa Yosefu angewaelewa, kwa sababu alitumia mkalimani.
But they did not know that Joseph understood, because he was speaking to them through an interpreter.
24 Yosefu akajitenga nao akaanza kulia, kisha akawarudia na kuzungumza nao tena. Akataka Simeoni akamatwe na kufungwa mbele yao.
And he turned himself away briefly and wept. And returning, he spoke to them.
25 Yosefu akatoa amri ya kujaza magunia yao nafaka na kuweka fedha ya kila mmoja ndani ya gunia lake, kisha wapewe mahitaji ya njiani. Baada ya kufanyiwa hayo yote,
And taking Simeon, and binding him in their presence, he ordered his ministers to fill their sacks with wheat, and to replace each one’s money in their sacks, and to give them, in addition, provisions for the way. And they did so.
26 wakapakiza nafaka juu ya punda zao, wakaondoka.
Then, having loaded their donkeys with the grain, they set out.
27 Walipofika mahali pa kulala huko njiani mmoja wao akafungua gunia lake ili amlishe punda wake, akakuta fedha yake kwenye mdomo wa gunia lake.
And one of them, opening a sack to give his beast of burden fodder at the inn, looked upon the money at the sack’s mouth,
28 Akawaambia ndugu zake, “Fedha yangu imerudishwa. Iko ndani ya gunia langu.” Mioyo yao ikazimia, na kila mmoja akamgeukia mwenzake wakitetemeka, wakaulizana, “Ni nini hiki Mungu alichotufanyia?”
and he said to his brothers: “My money has returned to me. See, it is held in the sack.” And they were astonished and troubled, and they said to one another, “What is this that God has done to us?”
29 Walipofika kwa Yakobo baba yao katika nchi ya Kanaani, wakamweleza mambo yote yaliyowapata. Wakasema,
And they went to their father Jacob in the land of Canaan, and they explained to him all the things that had befallen them, saying:
30 “Huyo mtu ambaye ndiye bwana katika nchi hiyo alisema nasi kwa ukali, akatutendea kana kwamba sisi tulikuwa tunaipeleleza nchi.
“The lord of the land spoke harshly to us, and he considered us to be scouts of the province.
31 Lakini tulimwambia, ‘Sisi ni watu waaminifu, sio wapelelezi.
And we answered him: ‘We are peaceful, and we do not intend any treachery.
32 Tulizaliwa ndugu kumi na wawili, wana wa baba mmoja. Mmoja alikufa, na mdogo wetu wa mwisho yupo na baba yetu huko Kanaani.’
We are twelve brothers conceived of one father. One is not living; the youngest is with our father in the land of Canaan.’
33 “Ndipo huyo mtu aliye bwana katika nchi hiyo alipotuambia, ‘Hivi ndivyo nitafahamu kuwa ninyi ni watu waaminifu: Mwacheni mmoja wa ndugu zenu pamoja nami hapa, kisha nendeni mpeleke chakula kwa ajili ya jamaa yenu inayoteseka kwa njaa.
And he said to us: ‘Thus will I prove that you are peaceful. Release one of your brothers to me, and take necessary provisions for your houses, and go away,
34 Lakini mleteni huyo ndugu yenu mdogo kwangu, ndipo nitajua kuwa ninyi sio wapelelezi, ila ni watu waaminifu. Kisha nitamrudisha ndugu yenu, nanyi mtaweza kufanya biashara katika nchi hii.’”
and bring your youngest brother to me, so that I may know that you are not scouts. And this one, who is held in chains, you may be able to receive again. And thereafter, you shall have permission to buy what you want.’”
35 Walipokuwa wanamimina nafaka kutoka kwenye magunia yao, ndani ya gunia la kila mtu kulikuwa na mfuko wa fedha! Wakati wao na baba yao walipoona mifuko ya fedha, wakaogopa.
Having said this, when they poured out their grain, each found his money tied to the mouth of his sack. And all were terrified together.
36 Yakobo baba yao akawaambia, “Ninyi mmenipokonya watoto wangu. Yosefu hayupo na Simeoni hayupo tena na sasa mnataka kumchukua Benyamini. Kila kitu ni kinyume nami!”
Their father Jacob said, “You have caused me to be without children. Joseph is not living, Simeon is held in chains, and Benjamin you would carry away. All these evils have fallen back upon me.”
37 Ndipo Reubeni akamwambia baba yake, “Waweza kuwaua wanangu wote wawili, ikiwa sitamrudisha Benyamini kwako. Mkabidhi Benyamini katika uangalizi wangu, nami nitamrudisha.”
And Reuben answered him, “Put my two sons to death, if I do not lead him back to you. Deliver him into my hand, and I will restore him to you.”
38 Lakini Yakobo akasema, “Mwanangu hatashuka huko pamoja nanyi; ndugu yake amekufa naye ndiye peke yake aliyebaki. Ikiwa atapatwa na madhara katika safari mnayoiendea, mtashusha kichwa changu chenye mvi kaburini kwa masikitiko.” (Sheol )
But he said: “My son will not go down with you. His brother is dead, and he is left alone. If any adversity will befall him in the land to which you travel, you would lead my grey hairs down with sorrow to the grave.” (Sheol )