< Mwanzo 41 >
1 Baada ya miaka miwili kamili kupita, Farao aliota ndoto: Tazama alikuwa amesimama kando ya Mto Naili,
Och tu år derefter hade Pharao en dröm, såsom han hade ståndit vid älfvena,
2 wakati ngʼombe saba, wazuri na wanono, walitokea mtoni wakajilisha kwenye matete.
Och sett af älfvene uppstiga sju nöt skön och fet; och de gingo i goda bet.
3 Baada yao ngʼombe wengine saba, wabaya na waliokonda, wakatokea mtoni Naili wakasimama kando ya wale wanono ukingoni mwa mto.
Sedan såg han annor sju nöt uppstiga af älfvene, vanskapeliga och magra; och gingo jemte de andra på strandene vid älfvena.
4 Wale ngʼombe wabaya na waliokonda wakawala wale saba wazuri na wanono. Kisha Farao akaamka.
Och de sju vanskapeliga och magra nöten åto upp de sju sköna och feta nöten. Då vaknade Pharao.
5 Farao akaingia usingizini tena akaota ndoto ya pili: Akaona masuke saba ya nafaka, yenye afya na mazuri, yanakua katika bua moja.
Och han somnade åter, och åter drömde honom, och såg, att sju ax full och tjock växte på enom stjelk.
6 Baadaye, masuke mengine saba yakachipua, yakiwa membamba yaliyonyaushwa na upepo wa mashariki.
Derefter såg han sju tunn förvissen ax uppgå.
7 Masuke yale membamba yakameza yale masuke saba yenye afya na yaliyojaa. Basi Farao akaamka kutoka usingizini, kumbe ilikuwa ndoto.
Och de sju magra axen uppslukte de sju stora och fulla axen. Då vaknade Pharao, och såg, att det var en dröm.
8 Asubuhi yake, alifadhaika akilini, hivyo akawaita waaguzi wote pamoja na watu wenye busara wa Misri. Walipokuja, Farao akawaeleza ndoto zake, lakini hakuna hata mmoja aliyeweza kumfasiria.
Och då det vardt morgon, var hans ande bedröfvad; och skickade ut, och lät kalla alla spåmän i Egypten, och alla visa, och förtäljde dem sin dröm: Men der var ingen, som honom kunde uttyda för Pharao.
9 Ndipo mnyweshaji mkuu alipomwambia Farao, “Leo nimekumbushwa kuhusu kosa langu.
Då talade den öfverste skänken med Pharao, och sade: Jag kommer ihåg i dag mina synder.
10 Wakati fulani Farao aliwakasirikia watumishi wake, akanifunga mimi na mwokaji mkuu katika nyumba ya mkuu wa ulinzi.
Då Pharao var förtörnad på sina tjenare, och lade mig med den öfversta bakaren i fängelse, i hofmästarens hus;
11 Kila mmoja wetu aliota ndoto katika usiku mmoja na kila ndoto ilikuwa na maana yake tofauti.
Då drömde oss bådom i ene natt, hvar sin dröm, hvars uttydning hvarjom för sig pågalt.
12 Basi kijana wa Kiebrania aliyekuwa pamoja nasi huko, alikuwa mtumishi wa mkuu wa kikosi cha ulinzi. Tulimweleza ndoto zetu, naye akatufasiria, akitupa kila mtu tafsiri ya ndoto yake.
Då var när oss en Ebreisk ung man, hofmästarens tjenare; honom förtäljde vi det, och han uttydde oss våra drömmar, hvarjom efter sinom dröm.
13 Nayo mambo yakawa sawa kabisa na jinsi alivyotufasiria ndoto zetu: Mimi nilirudishwa kazini mwangu na huyo mtu mwingine akaangikwa.”
Och som han oss uttydde, så är det gånget; ty jag är åter satt till mitt ämbete, och han är hängder.
14 Basi, Farao akatuma Yosefu aitwe, naye akatolewa kifungoni haraka. Baada ya kunyoa na kubadilisha nguo zake akaenda mbele ya Farao.
Då sände Pharao bort, och lät kalla Joseph, och de hade honom utu fängslet. Och han lät raka sig, och förvandla sin kläder, och kom in till Pharao.
15 Farao akamwambia Yosefu, “Nimeota ndoto, wala hakuna mtu hata mmoja anayeweza kuifasiri. Lakini nimesikia ikisemwa kwa habari yako kwamba unapoelezwa ndoto waweza kuifasiri.”
Då sade Pharao till honom: Mig hafver drömt en dröm, och ingen är, som honom uttyder: Men jag hafver hört af dig sägas, att när du hörer en dröm, då uttyder du honom.
16 Yosefu akamjibu Farao, “Siwezi kuifasiri, lakini Mungu atampa Farao jibu analolihitaji.”
Joseph svarade Pharao, och sade: Det står icke mig till; men Gud skall dock förkunna Pharao det godt är.
17 Kisha Farao akamwambia Yosefu, “Katika ndoto yangu nilikuwa nimesimama ukingoni mwa Mto Naili,
Pharao sade till Joseph: Mig drömde, jag stod på strandene vid älfvena,
18 nikawaona ngʼombe saba, wazuri na wanono, wakijitokeza kutoka mtoni wakaja kujilisha kwenye matete.
Och såg uppstiga af älfvene sju nöt, fet och skön, och de gingo i goda bet;
19 Baada ya hao, ngʼombe wengine saba wadhaifu wakatokea, wabaya sana na waliokonda. Kamwe sikuwahi kuona ngʼombe wabaya jinsi hiyo katika nchi yote ya Misri.
Och efter dem såg jag sju annor nöt uppstiga, tunn och fast vanskapeliga och magra; jag hafver icke i hela Egypten sett så vanskapeliga.
20 Hao ngʼombe waliokonda na wabaya sana wakawala wale ngʼombe saba walionona waliojitokeza kwanza.
Och de sju vanskapeliga och magra nöten åto upp de sju första feta nöten.
21 Lakini hata baada ya kuwala, hakuna mtu ambaye angeweza kusema kwamba wamekula, bado walionekana wabaya kama mwanzoni. Kisha nikaamka kutoka usingizini.
Och då de hade ätit dem upp, syntes intet på dem, att de hade ätit dem, och voro vanskapeliga såsom tillförene. Då vaknade jag.
22 “Pia katika ndoto zangu niliona masuke saba ya nafaka, yamejaa na mazuri, yanakua katika bua moja.
Och såg åter i minom dröm sju ax vuxen på enom stjelk full och tjock.
23 Baada ya hayo masuke mengine saba yakachipua, yaliyonyauka, membamba na yamekaushwa na upepo wa mashariki.
Derefter gingo upp sju torr ax tunn och förvissen.
24 Yale masuke membamba ya nafaka yakayameza yale masuke saba mazuri yaliyojaa nafaka. Nimewaeleza waaguzi, wala hakuna yeyote aliyeweza kunifasiria.”
Och de sju tunna axen uppslöko de sju torra axen. Och jag hafver sagt det mina spåmän; men de kunna icke tyda mig det ut.
25 Ndipo Yosefu akamwambia Farao, “Ndoto za Farao ni ndoto iyo hiyo moja. Mungu amemfunulia Farao jambo analokusudia kufanya karibuni.
Joseph svarade Pharao: Båda drömmarne, Pharao, äro ens. Gud förkunnar Pharao, hvad han göra vill.
26 Ngʼombe saba wazuri ni miaka saba, nayo masuke saba mazuri yaliyojaa nafaka ni miaka saba, ni ndoto iyo hiyo moja.
De sju sköna nöten äro sju år, och de sju fulla axen äro ock de sju åren: Det är allt enahanda dröm.
27 Ngʼombe saba waliokonda na wabaya wale waliojitokeza baadaye ni miaka saba, vivyo hivyo masuke saba ya ngano yaliyodhoofika na kukaushwa na upepo wa mashariki, ni miaka saba ya njaa.
De sju magra nöten och vanskapeliga, som efter de andra uppstigna äro, äro sju år; och de sju magra och förvissnade axen skola vara sju hård år.
28 “Ni kama vile nilivyomwambia Farao: Mungu amemwonyesha Farao jambo analokusudia kufanya karibuni.
Det är nu det jag sagt hafver till Pharao, att Gud undervisar Pharao, hvad han göra vill.
29 Miaka saba ya neema inakuja katika nchi yote ya Misri,
Si, sju år varda kommande med stor ymnoghet i hela Egypti lande.
30 lakini itafuata miaka saba ya njaa. Ndipo neema yote ya Misri itasahaulika na njaa itaikumba nchi.
Och efter dem varda sju hård år kommande, att man varder förgätandes all sådana ymnoghet i Egypti lande: Och den dyre tiden varder förtärandes landet;
31 “Neema iliyokuwa katika nchi haitakumbukwa, kwa sababu njaa itakayofuata itakuwa kali mno.
Att man intet skall veta af den ymnoghetene i landena, för den dyra tidens skull, som efter kommer; förty han skall varda ganska svår.
32 Sababu ya ndoto kumjia Farao kwa namna mbili ni kwamba jambo hilo Mungu ameshaamua kwa hakika, naye Mungu atalifanya karibuni.
Men det Pharao hafver andra resona drömt betyder, att Gud skall sådant visserliga och snarliga göra.
33 “Basi sasa Farao na atafute mtu mwenye akili na hekima ili amweke kuwa msimamizi wa nchi ya Misri.
Nu må Pharao se efter en förståndig och vis man, den han sätta må öfver Egypti land;
34 Farao na aweke wenye amri nchini kote wakusanye sehemu ya tano ya mavuno ya Misri katika miaka hii saba ya neema.
Och skaffa, att han förskickar ämbetsmän i landena, och taga den femte delen i Egypti lande i de sju rika åren.
35 Wakusanye chakula chote katika miaka hii saba ya neema inayokuja na kuhifadhi nafaka chini ya mamlaka ya Farao, iwe akiba ya chakula katika miji.
Och församle alla spisning af de goda åren, som komma skola, att de låta inkomma säd uti Pharaos kornhus till förråd i städerna, och förvara det:
36 Chakula hiki kitakuwa akiba ya tahadhari kwa ajili ya nchi, ili kitumike katika ile miaka saba ya njaa itakayokuja Misri, ili nchi isiharibiwe na njaa.”
På det man finner landena spisning i de sju hårda åren, som komma skola öfver Egypti land; att landet icke förderfvas af hunger.
37 Mpango huu ulionekana mzuri kwa Farao na kwa maafisa wake wote.
Det talet behagade Pharao och alla hans tjenare väl.
38 Hivyo Farao akawauliza, “Je tunaweza kumpata yeyote kama mtu huyu, ambaye Roho wa Mungu yumo ndani yake?”
Och Pharao sade till sina tjenare: Huru kunne vi finna en sådana man, som Guds Ande är uti?
39 Ndipo Farao akamwambia Yosefu, “Maadamu Mungu amekufunulia yote haya, hakuna mwingine yeyote mwenye akili na hekima kama wewe.
Och sade till Joseph: Efter Gud hafver allt sådant kundgjort dig, är ingen så klok och förståndig, som du.
40 Wewe utakuwa msimamizi wa jumba langu la kifalme, na watu wangu wote watatii amri zako. Ni kuhusu kiti cha ufalme tu nitakuwa mkuu kuliko wewe.”
Du skall vara öfver mitt hus, och efter dino orde skall allt mitt folk lydigt vara: Allena i mitt Konungsliga säte vill jag vara mer än du.
41 Kwa hiyo Farao akamwambia Yosefu, “Sasa nakuweka uwe msimamizi wa nchi yote ya Misri.”
Och sade: Si, jag hafver satt dig öfver hela Egypti land.
42 Ndipo Farao akaivua pete yake ya muhuri kutoka kidoleni mwake na kuivalisha katika kidole cha Yosefu. Akamvika majoho mazuri ya kitani safi na mkufu wa dhahabu shingoni mwake.
Och tog sin ring af sine hand, och gaf honom Joseph på sina hand, och klädde honom Joseph i hvitt silke, och hängde en guldkedjo på hans hals;
43 Akampandisha katika gari lake la farasi kama msaidizi wake, watu wakatangulia wakishangilia, wakisema, “Fungueni njia!” Ndivyo Farao alivyomweka Yosefu kuwa msimamizi wa nchi yote ya Misri.
Och lät honom sitta på den andra vagnen, och lät utropa honom: Denne är landsens fader: Och satte honom öfver hela Egypti land.
44 Kisha Farao akamwambia Yosefu, “Mimi ni Farao, lakini pasipo neno lako, hakuna mtu mwenye ruhusa kuinua mkono au mguu katika nchi yote ya Misri.”
Och Pharao sade till Joseph: Jag är Pharao; utan din vilja skall ingen, i hela Egypti lande, röra sin hand eller fot.
45 Farao akamwita Yosefu Safenath-Panea, pia akampa Asenathi binti Potifera, kuhani wa mji wa Oni, kuwa mke wake. Ndipo Yosefu akaitembelea nchi yote ya Misri.
Och kallade honom det hemligaste rådet; och gaf honom till hustru Asnath Potiphera dotter Prestens i On. Så for Joseph ut till att bese Egypti land.
46 Yosefu alikuwa na miaka thelathini alipoingia katika utumishi wa Farao mfalme wa Misri. Naye Yosefu akatoka mbele ya Farao akasafiri katika nchi yote ya Misri.
Och han var tretio år gammal, då han stod för Pharao. Och for ut ifrå Pharao, och for omkring hela Egypti land.
47 Katika ile miaka saba ya neema nchi ilizaa mazao kwa wingi sana.
Och landet gjorde allt så i de sju rika åren.
48 Yosefu akakusanya chakula chote kilichozalishwa katika ile miaka saba ya neema nchini Misri, akakihifadhi katika ghala za miji. Katika kila mji kulihifadhiwa chakula kilichozalishwa katika mashamba yaliyouzunguka mji huo.
Och församlade i de sju åren alla spisning i Egypti land, och läto det i städerna: Ehvad spisning som växte på markene vid hvar och en stad allt omkring, det läto de komma der in.
49 Yosefu alihifadhi nafaka nyingi, mfano wa mchanga wa bahari, ilikuwa nyingi mno kiasi kwamba walishindwa kuweka kumbukumbu kwa sababu akiba ilizidi sana kupita kipimo.
Så lade Joseph tillhopa sädena öfver måtto mycket, som sandkornen i hafvet, så att han vände igen att räkna; ty man kunde det icke räkna.
50 Kabla ya miaka ya njaa kuanza, Asenathi binti Potifera, kuhani wa mji wa Oni, alikuwa amemzalia Yosefu wana wawili wa kiume.
Och Joseph vordo födde två söner, förra än den dyre tiden kom, hvilka honom födde Asnath Potiphera dotter Prestens i On.
51 Yosefu akamwita mzaliwa wake wa kwanza Manase, akisema, “Ni kwa sababu Mungu amenifanya nisahau taabu zangu zote pamoja na jamaa yote ya nyumba ya baba yangu.”
Och kallade den första Manasse; förty, sade han, Gud hafver låtit mig förgäta alla mina olycko, och mins faders hus.
52 Mwana wa pili akamwita Efraimu, akisema, “Ni kwa sababu Mungu amenistawisha katika nchi ya mateso yangu.”
Den andra kallade han Ephraim; förty, sade han, Gud hafver låtit mig växa till i mins eländes lande.
53 Ile miaka saba ya neema huko Misri ikaisha,
Då nu de sju rika åren voro framliden i Egypten,
54 nayo miaka ile saba ya njaa ikaanza, sawasawa na alivyosema Yosefu. Kulikuwa na njaa katika nchi nyingine zote, bali katika nchi yote ya Misri kulikuwa na chakula.
Så begynte de sju hårda åren gå uppå, som Joseph hade omtalat. Och vardt en dyr tid i all land; men i hela Egypti lande var bröd.
55 Wakati nchi yote ya Misri ilipopatwa na njaa, watu wakamlilia Farao ili awape chakula. Ndipo Farao alipowaagiza Wamisri wote, akisema, “Nendeni kwa Yosefu, nanyi mfanye anachowaambia.”
Då nu Egypti land ock led hunger, ropade folket till Pharao om bröd. Men Pharao sade till alla Egyptier: Går bort till Joseph, hvad han säger eder, det görer.
56 Wakati njaa ilipokuwa imeenea katika nchi yote, Yosefu akafungua ghala za vyakula na kuwauzia Wamisri nafaka, kwa sababu njaa ilikuwa kali mno katika nchi yote ya Misri.
När nu dyr tid var öfver allt landet, slog Joseph kornhusen upp allestäds, och sålde de Egyptier; förty som dyre tiden vardt ju längre ju större i landena.
57 Pia nchi nyingine zote zilikuja Misri kununua nafaka kutoka kwa Yosefu, kwa sababu njaa ilikuwa kali mno duniani kote.
Och all land kommo till Egypten, till att köpa när Joseph; förty den dyre tiden fick öfverhandena i all land.