< Mwanzo 41 >

1 Baada ya miaka miwili kamili kupita, Farao aliota ndoto: Tazama alikuwa amesimama kando ya Mto Naili,
Un pēc diviem gadiem Faraons redzēja sapni un redzi, viņš stāvēja upes malā.
2 wakati ngʼombe saba, wazuri na wanono, walitokea mtoni wakajilisha kwenye matete.
Un redzi, no upes izkāpa septiņas govis krāšņu augumu un treknām miesām, un tās ganījās niedrēs.
3 Baada yao ngʼombe wengine saba, wabaya na waliokonda, wakatokea mtoni Naili wakasimama kando ya wale wanono ukingoni mwa mto.
Un redzi, septiņas citas govis izkāpa pēc šīm no upes, nejauku augumu un liesām miesām, un piestājās pie tām citām govīm upes malā.
4 Wale ngʼombe wabaya na waliokonda wakawala wale saba wazuri na wanono. Kisha Farao akaamka.
Un tās govis nejauku izskatu un liesām miesām ierija tās septiņas treknās govis krāšņu izskatu; - tad Faraons atmodās.
5 Farao akaingia usingizini tena akaota ndoto ya pili: Akaona masuke saba ya nafaka, yenye afya na mazuri, yanakua katika bua moja.
Pēc viņš atkal aizmiga un sapņoja otrkārt. Un redzi, septiņas vārpas auga uz viena stiebra, briedušas un brangas.
6 Baadaye, masuke mengine saba yakachipua, yakiwa membamba yaliyonyaushwa na upepo wa mashariki.
Un redzi, septiņas tievas un austriņa kaltētas vārpas radās pēc tām.
7 Masuke yale membamba yakameza yale masuke saba yenye afya na yaliyojaa. Basi Farao akaamka kutoka usingizini, kumbe ilikuwa ndoto.
Un tās tievās vārpas ierija tās septiņas briedušās un pilnās vārpas. Tad Faraons atmodās, un redzi, tas bija sapnis.
8 Asubuhi yake, alifadhaika akilini, hivyo akawaita waaguzi wote pamoja na watu wenye busara wa Misri. Walipokuja, Farao akawaeleza ndoto zake, lakini hakuna hata mmoja aliyeweza kumfasiria.
Un notikās no rīta, tad viņš bija bēdīgs savā garā, un sūtīja un aicināja visus ēģiptiešu zīlniekus un visus gudros, kas tur bija, un Faraons tiem teica savus sapņus, bet neviena nebija, kas tos Faraonam izstāstītu.
9 Ndipo mnyweshaji mkuu alipomwambia Farao, “Leo nimekumbushwa kuhusu kosa langu.
Tad dzēriena devēju virsnieks runāja uz Faraonu un sacīja: es pieminu šodien savu noziegumu.
10 Wakati fulani Farao aliwakasirikia watumishi wake, akanifunga mimi na mwokaji mkuu katika nyumba ya mkuu wa ulinzi.
Kad Faraons bija apskaities par saviem kalpiem un mani ielika cietumā, sargu virsnieka namā, mani un maizes cepēju virsnieku,
11 Kila mmoja wetu aliota ndoto katika usiku mmoja na kila ndoto ilikuwa na maana yake tofauti.
Tad mums bija vienā naktī sapnis, ikvienam savs sapnis, savādi izstāstāms.
12 Basi kijana wa Kiebrania aliyekuwa pamoja nasi huko, alikuwa mtumishi wa mkuu wa kikosi cha ulinzi. Tulimweleza ndoto zetu, naye akatufasiria, akitupa kila mtu tafsiri ya ndoto yake.
Un tur bija pie mums viens Ebreju jauneklis, sargu virsnieka kalps, un mēs tam tos pasacījām, un viņš mums mūsu sapņus izstāstīja, ikvienam tas to izstāstīja pēc viņa sapņošanas.
13 Nayo mambo yakawa sawa kabisa na jinsi alivyotufasiria ndoto zetu: Mimi nilirudishwa kazini mwangu na huyo mtu mwingine akaangikwa.”
Un kā tas mums ir izstāstījis, tāpat tas noticis; mani Faraons atkal iecēlis manā vietā un viņu pakāris.
14 Basi, Farao akatuma Yosefu aitwe, naye akatolewa kifungoni haraka. Baada ya kunyoa na kubadilisha nguo zake akaenda mbele ya Farao.
Tad Faraons sūtīja un aicināja Jāzepu, un tie tam ātri lika iziet no bedres, un viņš apcirpās un apvilka citas drēbes un nāca pie Faraona.
15 Farao akamwambia Yosefu, “Nimeota ndoto, wala hakuna mtu hata mmoja anayeweza kuifasiri. Lakini nimesikia ikisemwa kwa habari yako kwamba unapoelezwa ndoto waweza kuifasiri.”
Tad Faraons sacīja uz Jāzepu: es esmu sapņojis sapni, un neviena nav, kas to izstāsta; bet es esmu dzirdējis par tevi sakām, kad tu sapni dzirdot, tad tu to varot izstāstīt.
16 Yosefu akamjibu Farao, “Siwezi kuifasiri, lakini Mungu atampa Farao jibu analolihitaji.”
Un Jāzeps atbildēja Faraonam un sacīja: tas nestāv pie manis; Dievs Faraonam sludinās labu.
17 Kisha Farao akamwambia Yosefu, “Katika ndoto yangu nilikuwa nimesimama ukingoni mwa Mto Naili,
Un Faraons sacīja uz Jāzepu: redzi, es sapnī stāvēju upes malā.
18 nikawaona ngʼombe saba, wazuri na wanono, wakijitokeza kutoka mtoni wakaja kujilisha kwenye matete.
Un redzi, tur izkāpa no upes septiņas govis treknām miesām un krāšņu izskatu un ganījās niedrēs.
19 Baada ya hao, ngʼombe wengine saba wadhaifu wakatokea, wabaya sana na waliokonda. Kamwe sikuwahi kuona ngʼombe wabaya jinsi hiyo katika nchi yote ya Misri.
Un redzi, septiņas citas govis izkāpa pēc tām, liesu un ļoti nejauku augumu un izdēdējušām miesām, es tik nejaukas, kā šās, visā Ēģiptes zemē neesmu redzējis.
20 Hao ngʼombe waliokonda na wabaya sana wakawala wale ngʼombe saba walionona waliojitokeza kwanza.
Un tās izdēdējušās un nejaukās govis ierija tās septiņas pirmās treknās govis.
21 Lakini hata baada ya kuwala, hakuna mtu ambaye angeweza kusema kwamba wamekula, bado walionekana wabaya kama mwanzoni. Kisha nikaamka kutoka usingizini.
Un kad tās no viņām bija ierītas, nevarēja manīt, ka tās bija viņu iekšās, un tās izskatījās nejaukas tāpat kā papriekš. Tad es atmodos.
22 “Pia katika ndoto zangu niliona masuke saba ya nafaka, yamejaa na mazuri, yanakua katika bua moja.
Pēc tam es redzēju savā sapnī, un redzi, septiņas vārpas izauga no viena stiebra, pilnas un brangas.
23 Baada ya hayo masuke mengine saba yakachipua, yaliyonyauka, membamba na yamekaushwa na upepo wa mashariki.
Un redzi, septiņas sakaltušas, tievas un austriņa kaltētas vārpas izplauka pēc tām.
24 Yale masuke membamba ya nafaka yakayameza yale masuke saba mazuri yaliyojaa nafaka. Nimewaeleza waaguzi, wala hakuna yeyote aliyeweza kunifasiria.”
Un tās septiņas tievās vārpas ierija tās septiņas brangās vārpas. Un es to tiem zīlniekiem esmu teicis, bet neviena nav, kas to var izstāstīt.
25 Ndipo Yosefu akamwambia Farao, “Ndoto za Farao ni ndoto iyo hiyo moja. Mungu amemfunulia Farao jambo analokusudia kufanya karibuni.
Tad Jāzeps sacīja uz Faraonu. Faraona sapņi ir vienādi. Dievs Faraonam ir darījis zināmu, ko Viņš apņēmies darīt.
26 Ngʼombe saba wazuri ni miaka saba, nayo masuke saba mazuri yaliyojaa nafaka ni miaka saba, ni ndoto iyo hiyo moja.
Tās septiņas krāšņās govis ir septiņi gadi, un tās septiņas brangās vārpas ir septiņi gadi, - tie sapņi ir vienādi.
27 Ngʼombe saba waliokonda na wabaya wale waliojitokeza baadaye ni miaka saba, vivyo hivyo masuke saba ya ngano yaliyodhoofika na kukaushwa na upepo wa mashariki, ni miaka saba ya njaa.
Un tās septiņas izdēdējušās un nejaukās govis, kas pēc tām izkāpa, ir septiņi gadi, un tās septiņas tievās un austriņa kaltētās vārpas būs septiņi bada gadi.
28 “Ni kama vile nilivyomwambia Farao: Mungu amemwonyesha Farao jambo analokusudia kufanya karibuni.
Šis ir tas vārds, ko es uz Faraonu esmu runājis: Dievs Faraonam ir parādījis, ko Viņš apņēmies.
29 Miaka saba ya neema inakuja katika nchi yote ya Misri,
Redzi, septiņi it auglīgi gadi nāks pār visu Ēģiptes zemi.
30 lakini itafuata miaka saba ya njaa. Ndipo neema yote ya Misri itasahaulika na njaa itaikumba nchi.
Bet pēc tiem nāks septiņi bada gadi; tad tas pilnums Ēģiptes zemē taps aizmirsts, un bads klaji apēdīs zemi.
31 “Neema iliyokuwa katika nchi haitakumbukwa, kwa sababu njaa itakayofuata itakuwa kali mno.
Un to pilnumu vairs nemanīs tai zemē aiz tā bada pēc tam, jo tas būs pārlieku grūts.
32 Sababu ya ndoto kumjia Farao kwa namna mbili ni kwamba jambo hilo Mungu ameshaamua kwa hakika, naye Mungu atalifanya karibuni.
Un, ka tas sapnis Faraonam divreiz ir rādījies, tas ir tāpēc, ka Dievs to stipri apņēmies un Dievs steigšus to darīs.
33 “Basi sasa Farao na atafute mtu mwenye akili na hekima ili amweke kuwa msimamizi wa nchi ya Misri.
Un nu lai Faraons lūko pēc viena prātīga un gudra vīra un to lai ieceļ pār Ēģiptes zemi.
34 Farao na aweke wenye amri nchini kote wakusanye sehemu ya tano ya mavuno ya Misri katika miaka hii saba ya neema.
Lai Faraons tā dara un lai ieceļ uzraugus pār zemi un lai ņem piekto tiesu no Ēģiptes zemes pa tiem septiņiem bagātiem gadiem, un lai tie sakrāj visādu barību pa šiem nākamiem auglīgiem gadiem.
35 Wakusanye chakula chote katika miaka hii saba ya neema inayokuja na kuhifadhi nafaka chini ya mamlaka ya Farao, iwe akiba ya chakula katika miji.
Un lai tie saber labību apakš Faraona rokas par barību pilsētā, un lai to paglabā.
36 Chakula hiki kitakuwa akiba ya tahadhari kwa ajili ya nchi, ili kitumike katika ile miaka saba ya njaa itakayokuja Misri, ili nchi isiharibiwe na njaa.”
Tad būs barība zemei par padomu, kamēr tie septiņi bada gadi būs Ēģiptes zemē, ka zeme no bada netop izdeldēta.
37 Mpango huu ulionekana mzuri kwa Farao na kwa maafisa wake wote.
Un šie vārdi patika Faraonam un visiem viņa kalpiem.
38 Hivyo Farao akawauliza, “Je tunaweza kumpata yeyote kama mtu huyu, ambaye Roho wa Mungu yumo ndani yake?”
Un Faraons sacīja uz saviem kalpiem: kur mēs atrastu tādu vīru, iekš kā ir Dieva Gars?
39 Ndipo Farao akamwambia Yosefu, “Maadamu Mungu amekufunulia yote haya, hakuna mwingine yeyote mwenye akili na hekima kama wewe.
Tad Faraons sacīja uz Jāzepu: tāpēc ka Dievs tev visas šīs lietas ir darījis zināmas, nav neviena tik prātīga un gudra, kā tu.
40 Wewe utakuwa msimamizi wa jumba langu la kifalme, na watu wangu wote watatii amri zako. Ni kuhusu kiti cha ufalme tu nitakuwa mkuu kuliko wewe.”
Tev būs būt pār manu namu, un visiem maniem ļaudīm būs klausīt tavam vārdam; pēc tā goda krēsla vien es būšu lielāks nekā tu.
41 Kwa hiyo Farao akamwambia Yosefu, “Sasa nakuweka uwe msimamizi wa nchi yote ya Misri.”
Un Faraons sacīja uz Jāzepu: redzi, es tevi esmu iecēlis pār visu Ēģiptes zemi.
42 Ndipo Farao akaivua pete yake ya muhuri kutoka kidoleni mwake na kuivalisha katika kidole cha Yosefu. Akamvika majoho mazuri ya kitani safi na mkufu wa dhahabu shingoni mwake.
Un Faraons novilka savu gredzenu no savas rokas un deva to Jāzepam rokā, un to apģērba ar dārga audekla drēbēm un apkāra zelta ķēdes ap viņa kaklu,
43 Akampandisha katika gari lake la farasi kama msaidizi wake, watu wakatangulia wakishangilia, wakisema, “Fungueni njia!” Ndivyo Farao alivyomweka Yosefu kuwa msimamizi wa nchi yote ya Misri.
Un tam lika braukt uz saviem otrajiem ratiem, kas viņam bija, un viņa priekšā sauca: klanāties! Un viņš to iecēla pār visu Ēģiptes zemi.
44 Kisha Farao akamwambia Yosefu, “Mimi ni Farao, lakini pasipo neno lako, hakuna mtu mwenye ruhusa kuinua mkono au mguu katika nchi yote ya Misri.”
Un Faraons sacīja uz Jāzepu: es esmu Faraons, tomēr bez tavas ziņas nevienam ne roku, ne kāju nebūs pacelt visā Ēģiptes zemē.
45 Farao akamwita Yosefu Safenath-Panea, pia akampa Asenathi binti Potifera, kuhani wa mji wa Oni, kuwa mke wake. Ndipo Yosefu akaitembelea nchi yote ya Misri.
Un Faraons Jāzepu nosauca Capnat-Paneak (pasaules glābējs) un tam deva par sievu Asnatu, Potifera, Onna priestera, meitu. Un Jāzeps devās ceļā pa visu Ēģiptes zemi.
46 Yosefu alikuwa na miaka thelathini alipoingia katika utumishi wa Farao mfalme wa Misri. Naye Yosefu akatoka mbele ya Farao akasafiri katika nchi yote ya Misri.
Un Jāzeps bija trīsdesmit gadus vecs, kad viņš priekš Ēģiptes ķēniņa Faraona stāvēja. Un Jāzeps aizgāja no Faraona un pārstaigāja visu Ēģiptes zemi.
47 Katika ile miaka saba ya neema nchi ilizaa mazao kwa wingi sana.
Un zeme tanīs septiņos bagātos gados izdeva bagātus augļus.
48 Yosefu akakusanya chakula chote kilichozalishwa katika ile miaka saba ya neema nchini Misri, akakihifadhi katika ghala za miji. Katika kila mji kulihifadhiwa chakula kilichozalishwa katika mashamba yaliyouzunguka mji huo.
Un viņš sakrāja to septiņu gadu labību, kas bija Ēģiptes zemē, visu un lika to labību pilsētās; to labību no ikvienas pilsētas tīruma, kas ap to bija, viņš tanī nolika.
49 Yosefu alihifadhi nafaka nyingi, mfano wa mchanga wa bahari, ilikuwa nyingi mno kiasi kwamba walishindwa kuweka kumbukumbu kwa sababu akiba ilizidi sana kupita kipimo.
Tā Jāzeps sabēra pārlieku daudz labības, kā smiltis jūrmalā, ka beidzot mitējās skaitīt, jo tā bija neskaitāma.
50 Kabla ya miaka ya njaa kuanza, Asenathi binti Potifera, kuhani wa mji wa Oni, alikuwa amemzalia Yosefu wana wawili wa kiume.
Un Jāzepam piedzima divi dēli, pirms nekā tie bada gadi nāca; tos Asnata, Potifera, Onna priestera, meita, viņam dzemdēja.
51 Yosefu akamwita mzaliwa wake wa kwanza Manase, akisema, “Ni kwa sababu Mungu amenifanya nisahau taabu zangu zote pamoja na jamaa yote ya nyumba ya baba yangu.”
Un Jāzeps tā pirmdzimtā vārdu nosauca Manasu, jo Dievs man ir licis aizmirst visu manu grūtumu un visu mana tēva namu.
52 Mwana wa pili akamwita Efraimu, akisema, “Ni kwa sababu Mungu amenistawisha katika nchi ya mateso yangu.”
Un tā otrā vārdu viņš nosauca Efraīm, jo Dievs man licis augt manā bēdu zemē.
53 Ile miaka saba ya neema huko Misri ikaisha,
Un tie septiņi bagātie gadi beidzās, kas bija Ēģiptes zemē.
54 nayo miaka ile saba ya njaa ikaanza, sawasawa na alivyosema Yosefu. Kulikuwa na njaa katika nchi nyingine zote, bali katika nchi yote ya Misri kulikuwa na chakula.
Un tie septiņi bada gadi sāka nākt, tā kā Jāzeps bija sacījis, un tur bija bads visapkārt, bet pa visu Ēģiptes zemi bija maize.
55 Wakati nchi yote ya Misri ilipopatwa na njaa, watu wakamlilia Farao ili awape chakula. Ndipo Farao alipowaagiza Wamisri wote, akisema, “Nendeni kwa Yosefu, nanyi mfanye anachowaambia.”
Kad nu visa Ēģiptes zeme arī badu cieta, tad tie ļaudis brēca uz Faraonu pēc maizes. Un Faraons sacīja visiem ēģiptiešiem: ejat pie Jāzepa, - ko tas jums sacīs, to dariet.
56 Wakati njaa ilipokuwa imeenea katika nchi yote, Yosefu akafungua ghala za vyakula na kuwauzia Wamisri nafaka, kwa sababu njaa ilikuwa kali mno katika nchi yote ya Misri.
Un bads bija pa visu zemi, un Jāzeps atvēra visas klētis un pārdeva ēģiptiešiem, jo bads palika jo dienas jo lielāks Ēģiptes zemē.
57 Pia nchi nyingine zote zilikuja Misri kununua nafaka kutoka kwa Yosefu, kwa sababu njaa ilikuwa kali mno duniani kote.
Un visas citas zemes nāca uz Ēģiptes zemi pie Jāzepa pirkt, jo bads bija liels pa visām zemēm.

< Mwanzo 41 >