< Mwanzo 41 >

1 Baada ya miaka miwili kamili kupita, Farao aliota ndoto: Tazama alikuwa amesimama kando ya Mto Naili,
Aftir twei yeer Farao seiy a dreem; he gesside that he stood on a flood,
2 wakati ngʼombe saba, wazuri na wanono, walitokea mtoni wakajilisha kwenye matete.
fro which seuene faire kiyn and ful fatte stieden, and weren fed in the places of mareis;
3 Baada yao ngʼombe wengine saba, wabaya na waliokonda, wakatokea mtoni Naili wakasimama kando ya wale wanono ukingoni mwa mto.
and othere seuene, foule and leene, camen out of the flood, and weren fed in thilk brenke of the watir, in grene places;
4 Wale ngʼombe wabaya na waliokonda wakawala wale saba wazuri na wanono. Kisha Farao akaamka.
and tho deuoureden thilke kien of whiche the fairnesse and comelynesse of bodies was wondurful.
5 Farao akaingia usingizini tena akaota ndoto ya pili: Akaona masuke saba ya nafaka, yenye afya na mazuri, yanakua katika bua moja.
Farao wakide, and slepte eft, and seiy another dreem; seuen eeris of corn ful and faire camen forth in o stalke,
6 Baadaye, masuke mengine saba yakachipua, yakiwa membamba yaliyonyaushwa na upepo wa mashariki.
and othere as many eeris of corn, thinne and smytun with corrupcioun of brennynge wynd,
7 Masuke yale membamba yakameza yale masuke saba yenye afya na yaliyojaa. Basi Farao akaamka kutoka usingizini, kumbe ilikuwa ndoto.
camen forth, deuourynge al the fairenesse of the firste. Farao wakide aftir reste,
8 Asubuhi yake, alifadhaika akilini, hivyo akawaita waaguzi wote pamoja na watu wenye busara wa Misri. Walipokuja, Farao akawaeleza ndoto zake, lakini hakuna hata mmoja aliyeweza kumfasiria.
and whanne morewtid was maad, he was aferd bi inward drede, and he sente to alle the expowneris of Egipt, and to alle wise men; and whanne thei weren clepid, he telde the dreem, and noon was that expownede.
9 Ndipo mnyweshaji mkuu alipomwambia Farao, “Leo nimekumbushwa kuhusu kosa langu.
Thanne at the laste the maistir `of boteleris bithouyte, and seide, Y knowleche my synne;
10 Wakati fulani Farao aliwakasirikia watumishi wake, akanifunga mimi na mwokaji mkuu katika nyumba ya mkuu wa ulinzi.
the kyng was wrooth to hise seruauntis, and comaundide me and the maister `of bakeris to be cast doun in to the prisoun of the prince of knyytis,
11 Kila mmoja wetu aliota ndoto katika usiku mmoja na kila ndoto ilikuwa na maana yake tofauti.
where we bothe saien a dreem in o nyyt, biforeschewynge of thingis to comynge.
12 Basi kijana wa Kiebrania aliyekuwa pamoja nasi huko, alikuwa mtumishi wa mkuu wa kikosi cha ulinzi. Tulimweleza ndoto zetu, naye akatufasiria, akitupa kila mtu tafsiri ya ndoto yake.
An Ebrew child, seruaunt of the same duk of knyytis was there, to whom we telden the dremes,
13 Nayo mambo yakawa sawa kabisa na jinsi alivyotufasiria ndoto zetu: Mimi nilirudishwa kazini mwangu na huyo mtu mwingine akaangikwa.”
and herden what euer thing the bifallyng of thing preuede afterward; for Y am restorid to myn office, and he was hangid in a cros.
14 Basi, Farao akatuma Yosefu aitwe, naye akatolewa kifungoni haraka. Baada ya kunyoa na kubadilisha nguo zake akaenda mbele ya Farao.
Anoon at the comaundement of the kyng thei polliden Joseph led out of prisoun, and whanne `the clooth was chaungid, thei brouyten Joseph to the kyng.
15 Farao akamwambia Yosefu, “Nimeota ndoto, wala hakuna mtu hata mmoja anayeweza kuifasiri. Lakini nimesikia ikisemwa kwa habari yako kwamba unapoelezwa ndoto waweza kuifasiri.”
To whom the kyng seide, Y seiye dremes, and noon is that expowneth tho thingis that Y seiy, I haue herd that thou expownest moost prudentli.
16 Yosefu akamjibu Farao, “Siwezi kuifasiri, lakini Mungu atampa Farao jibu analolihitaji.”
Joseph answerde, With out me, God schal answere prosperitees to Farao.
17 Kisha Farao akamwambia Yosefu, “Katika ndoto yangu nilikuwa nimesimama ukingoni mwa Mto Naili,
Therfor Farao telde that that he seiy; Y gesside that Y stood on the brenke of the flood,
18 nikawaona ngʼombe saba, wazuri na wanono, wakijitokeza kutoka mtoni wakaja kujilisha kwenye matete.
and seuene kiyn, ful faire and with fleischis able to etyng, stieden fro the watir, whiche kiyn gaderiden grene seggis in the pasture of the marreis;
19 Baada ya hao, ngʼombe wengine saba wadhaifu wakatokea, wabaya sana na waliokonda. Kamwe sikuwahi kuona ngʼombe wabaya jinsi hiyo katika nchi yote ya Misri.
and lo! seuene othere kiyn, so foule and leene, sueden these, that Y seiy neuere siche in the lond of Egipt;
20 Hao ngʼombe waliokonda na wabaya sana wakawala wale ngʼombe saba walionona waliojitokeza kwanza.
and whanne the formere kien weren deuourid and wastid, tho secounde yauen no steppe of fulnesse,
21 Lakini hata baada ya kuwala, hakuna mtu ambaye angeweza kusema kwamba wamekula, bado walionekana wabaya kama mwanzoni. Kisha nikaamka kutoka usingizini.
but weren slowe bi lijk leenesse and palenesse. I wakide, and eft Y was oppressid bi sleep, and Y seiy a dreem;
22 “Pia katika ndoto zangu niliona masuke saba ya nafaka, yamejaa na mazuri, yanakua katika bua moja.
seuene eeris of corn, ful and faireste, camen forth in o stalke,
23 Baada ya hayo masuke mengine saba yakachipua, yaliyonyauka, membamba na yamekaushwa na upepo wa mashariki.
and othere seuene, thinne and smytun with `corrupcioun of brennynge wynd, camen forth of the stobil,
24 Yale masuke membamba ya nafaka yakayameza yale masuke saba mazuri yaliyojaa nafaka. Nimewaeleza waaguzi, wala hakuna yeyote aliyeweza kunifasiria.”
whiche deuouriden the fairenesse of the formere;
25 Ndipo Yosefu akamwambia Farao, “Ndoto za Farao ni ndoto iyo hiyo moja. Mungu amemfunulia Farao jambo analokusudia kufanya karibuni.
Y telde the dreem to expowneris, and no man is that expowneth. Joseph answerde, The dreem of the king is oon; God schewide to Farao what thingis he schal do.
26 Ngʼombe saba wazuri ni miaka saba, nayo masuke saba mazuri yaliyojaa nafaka ni miaka saba, ni ndoto iyo hiyo moja.
Seuene faire kiyn, and seuene ful eeris of corn, ben seuene yeeris of plentee, and tho comprehenden the same strengthe of dreem;
27 Ngʼombe saba waliokonda na wabaya wale waliojitokeza baadaye ni miaka saba, vivyo hivyo masuke saba ya ngano yaliyodhoofika na kukaushwa na upepo wa mashariki, ni miaka saba ya njaa.
and seuene kiyn thinne and leene, that stieden aftir tho, and seuene thinne eeris of corn and smytun with brennynge wynd, ben seuene yeer of hungur to comynge,
28 “Ni kama vile nilivyomwambia Farao: Mungu amemwonyesha Farao jambo analokusudia kufanya karibuni.
whiche schulen be fillid bi this ordre.
29 Miaka saba ya neema inakuja katika nchi yote ya Misri,
Lo! seuene yeer of greet plentee in al the lond of Egipt schulen come,
30 lakini itafuata miaka saba ya njaa. Ndipo neema yote ya Misri itasahaulika na njaa itaikumba nchi.
and seuene othre yeer of so greet bareynesse schulen sue tho, that al the abundaunce bifore be youun to foryetyng; for the hungur schal waste al the lond,
31 “Neema iliyokuwa katika nchi haitakumbukwa, kwa sababu njaa itakayofuata itakuwa kali mno.
and the greetnesse of pouert schal leese the greetnesse of plentee.
32 Sababu ya ndoto kumjia Farao kwa namna mbili ni kwamba jambo hilo Mungu ameshaamua kwa hakika, naye Mungu atalifanya karibuni.
Forsothe this that thou siyest the secunde tyme a dreem, perteynynge to the same thing, is a `schewyng of sadnesse, for the word of God schal be doon, and schal be fillid ful swiftli.
33 “Basi sasa Farao na atafute mtu mwenye akili na hekima ili amweke kuwa msimamizi wa nchi ya Misri.
Now therfor puruey the kyng a wijs man and a redi, and make the kyng hym souereyn to the lond of Egipt,
34 Farao na aweke wenye amri nchini kote wakusanye sehemu ya tano ya mavuno ya Misri katika miaka hii saba ya neema.
which man ordeyne gouernouris bi alle cuntreis, and gadere he in to bernys the fyuethe part of fruytis bi seuene yeer of plentee,
35 Wakusanye chakula chote katika miaka hii saba ya neema inayokuja na kuhifadhi nafaka chini ya mamlaka ya Farao, iwe akiba ya chakula katika miji.
that schulen come now; and al the wheete be kept vndur the power of Farao, and be it kept in citees,
36 Chakula hiki kitakuwa akiba ya tahadhari kwa ajili ya nchi, ili kitumike katika ile miaka saba ya njaa itakayokuja Misri, ili nchi isiharibiwe na njaa.”
and be it maad redi to the hungur to comynge of seuene yeer that schal oppresse Egipt, and the lond be not wastid bi pouert.
37 Mpango huu ulionekana mzuri kwa Farao na kwa maafisa wake wote.
The counsel pleside Farao,
38 Hivyo Farao akawauliza, “Je tunaweza kumpata yeyote kama mtu huyu, ambaye Roho wa Mungu yumo ndani yake?”
and alle his mynystris, and he spak to hem, Wher we moun fynde sich a man which is ful of Goddis spirit?
39 Ndipo Farao akamwambia Yosefu, “Maadamu Mungu amekufunulia yote haya, hakuna mwingine yeyote mwenye akili na hekima kama wewe.
Therfor Farao seide to Joseph, For God hath schewid to thee alle thingis whiche thou hast spoke, wher Y mai fynde a wisere man and lijk thee?
40 Wewe utakuwa msimamizi wa jumba langu la kifalme, na watu wangu wote watatii amri zako. Ni kuhusu kiti cha ufalme tu nitakuwa mkuu kuliko wewe.”
Therfor thou schalt be ouer myn hous, and al the puple schal obeie to the comaundement of thi mouth; Y schal passe thee onely by o trone of the rewme.
41 Kwa hiyo Farao akamwambia Yosefu, “Sasa nakuweka uwe msimamizi wa nchi yote ya Misri.”
And eft Farao seide to Joseph, Lo! Y haue ordeyned thee on al the lond of Egipt.
42 Ndipo Farao akaivua pete yake ya muhuri kutoka kidoleni mwake na kuivalisha katika kidole cha Yosefu. Akamvika majoho mazuri ya kitani safi na mkufu wa dhahabu shingoni mwake.
And Farao took the ryng fro his hond, and yaf it in the hond of Joseph, and he clothide Joseph with a stoole of bijs, and puttide a goldun wrethe aboute the necke;
43 Akampandisha katika gari lake la farasi kama msaidizi wake, watu wakatangulia wakishangilia, wakisema, “Fungueni njia!” Ndivyo Farao alivyomweka Yosefu kuwa msimamizi wa nchi yote ya Misri.
and Farao made Joseph to `stie on his secounde chare, while a bidele criede, that alle men schulden knele bifore hym, and schulden knowe that he was souereyn of al the lond of Egipt.
44 Kisha Farao akamwambia Yosefu, “Mimi ni Farao, lakini pasipo neno lako, hakuna mtu mwenye ruhusa kuinua mkono au mguu katika nchi yote ya Misri.”
And the kyng seide to Joseph, Y am Farao, without thi comaundement no man shal stire hond ether foot in al the lond of Egipt.
45 Farao akamwita Yosefu Safenath-Panea, pia akampa Asenathi binti Potifera, kuhani wa mji wa Oni, kuwa mke wake. Ndipo Yosefu akaitembelea nchi yote ya Misri.
And he turnede the name of Joseph, and clepide him bi Egipcian langage, the sauyour of the world; and he yaf to Joseph a wijf, Asenech, the douyter of Potifar, preest of Heliopoleos. And so Joseph yede out to the lond of Egipt.
46 Yosefu alikuwa na miaka thelathini alipoingia katika utumishi wa Farao mfalme wa Misri. Naye Yosefu akatoka mbele ya Farao akasafiri katika nchi yote ya Misri.
Forsothe Joseph was of thretti yeer, whanne he stood in the siyt of kyng Farao, and cumpasside alle the cuntreis of Egipt.
47 Katika ile miaka saba ya neema nchi ilizaa mazao kwa wingi sana.
And the plente of seuene yeer cam, and ripe corn weren bounden into handfuls, and weren gaderid into the bernys of Egipt,
48 Yosefu akakusanya chakula chote kilichozalishwa katika ile miaka saba ya neema nchini Misri, akakihifadhi katika ghala za miji. Katika kila mji kulihifadhiwa chakula kilichozalishwa katika mashamba yaliyouzunguka mji huo.
also al the aboundaunce of cornes weren kept in alle citeis,
49 Yosefu alihifadhi nafaka nyingi, mfano wa mchanga wa bahari, ilikuwa nyingi mno kiasi kwamba walishindwa kuweka kumbukumbu kwa sababu akiba ilizidi sana kupita kipimo.
and so greet aboundaunce was of wheete, that it was maad euene to the grauel of the see, and the plente passide mesure.
50 Kabla ya miaka ya njaa kuanza, Asenathi binti Potifera, kuhani wa mji wa Oni, alikuwa amemzalia Yosefu wana wawili wa kiume.
Sotheli twei sones were born to Joseph bifor that the hungur came, whiche Asenech, douytir of Putifar, preest of Heliopoleos, childide to hym.
51 Yosefu akamwita mzaliwa wake wa kwanza Manase, akisema, “Ni kwa sababu Mungu amenifanya nisahau taabu zangu zote pamoja na jamaa yote ya nyumba ya baba yangu.”
And he clepide the name of the firste gendrid sone, Manasses, and seide, God hath maad me to foryete alle my traueilis, and the hous of my fadir;
52 Mwana wa pili akamwita Efraimu, akisema, “Ni kwa sababu Mungu amenistawisha katika nchi ya mateso yangu.”
and he clepide the name of the secunde sone Effraym, and seide, God hath maad me to encreesse in the lond of my pouert.
53 Ile miaka saba ya neema huko Misri ikaisha,
Therfor whanne seuene yeer of plentee that weren in Egipt weren passid,
54 nayo miaka ile saba ya njaa ikaanza, sawasawa na alivyosema Yosefu. Kulikuwa na njaa katika nchi nyingine zote, bali katika nchi yote ya Misri kulikuwa na chakula.
seuene yeer of pouert bigunnen to come, whiche Joseph bifore seide, and hungur hadde the maistri in al the world; also hungur was in al the lond of Egipt;
55 Wakati nchi yote ya Misri ilipopatwa na njaa, watu wakamlilia Farao ili awape chakula. Ndipo Farao alipowaagiza Wamisri wote, akisema, “Nendeni kwa Yosefu, nanyi mfanye anachowaambia.”
and whanne that lond hungride, the puple criede to Farao, and axide metis; to whiche he answeride, Go ye to Joseph, and do ye what euer thing he seith to you.
56 Wakati njaa ilipokuwa imeenea katika nchi yote, Yosefu akafungua ghala za vyakula na kuwauzia Wamisri nafaka, kwa sababu njaa ilikuwa kali mno katika nchi yote ya Misri.
Forsothe hungur encreesside ech dai in al the lond, and Joseph openyde alle the bernys, and seelde to Egipcians, for also hungur oppresside hem;
57 Pia nchi nyingine zote zilikuja Misri kununua nafaka kutoka kwa Yosefu, kwa sababu njaa ilikuwa kali mno duniani kote.
and alle prouynces camen in to Egipt to bie metis, and to abate the yuel of nedynesse.

< Mwanzo 41 >