< Mwanzo 41 >
1 Baada ya miaka miwili kamili kupita, Farao aliota ndoto: Tazama alikuwa amesimama kando ya Mto Naili,
After two years, Pharaoh saw a dream. He thought himself to be standing above a river,
2 wakati ngʼombe saba, wazuri na wanono, walitokea mtoni wakajilisha kwenye matete.
from which ascended seven cows, exceedingly beautiful and stout. And they pastured in marshy places.
3 Baada yao ngʼombe wengine saba, wabaya na waliokonda, wakatokea mtoni Naili wakasimama kando ya wale wanono ukingoni mwa mto.
Likewise, another seven emerged from the river, filthy and thoroughly emaciated. And they pastured on the same bank of the river, in green places.
4 Wale ngʼombe wabaya na waliokonda wakawala wale saba wazuri na wanono. Kisha Farao akaamka.
And they devoured those whose appearance and condition of body was so wonderful. Pharaoh, having been awakened,
5 Farao akaingia usingizini tena akaota ndoto ya pili: Akaona masuke saba ya nafaka, yenye afya na mazuri, yanakua katika bua moja.
slept again, and he saw another dream. Seven ears of grain sprung up on one stalk, full and well-formed.
6 Baadaye, masuke mengine saba yakachipua, yakiwa membamba yaliyonyaushwa na upepo wa mashariki.
Likewise, other ears of grain, of the same number, rose up, thin and struck with blight,
7 Masuke yale membamba yakameza yale masuke saba yenye afya na yaliyojaa. Basi Farao akaamka kutoka usingizini, kumbe ilikuwa ndoto.
devouring all the beauty of the first. Pharaoh, when he awakened after his rest,
8 Asubuhi yake, alifadhaika akilini, hivyo akawaita waaguzi wote pamoja na watu wenye busara wa Misri. Walipokuja, Farao akawaeleza ndoto zake, lakini hakuna hata mmoja aliyeweza kumfasiria.
and when morning arrived, being terrified with fear, sent to all the interpreters of Egypt and to all of the wise men. And when they were summoned, he explained to them his dream; but there was no one who could interpret it.
9 Ndipo mnyweshaji mkuu alipomwambia Farao, “Leo nimekumbushwa kuhusu kosa langu.
Then at last the chief cupbearer, remembering, said, “I confess my sin.
10 Wakati fulani Farao aliwakasirikia watumishi wake, akanifunga mimi na mwokaji mkuu katika nyumba ya mkuu wa ulinzi.
The king, being angry with his servants, ordered me and the chief miller of grain to be forced into the prison of the leader of the military.
11 Kila mmoja wetu aliota ndoto katika usiku mmoja na kila ndoto ilikuwa na maana yake tofauti.
There, in one night, both of us saw a dream presaging the future.
12 Basi kijana wa Kiebrania aliyekuwa pamoja nasi huko, alikuwa mtumishi wa mkuu wa kikosi cha ulinzi. Tulimweleza ndoto zetu, naye akatufasiria, akitupa kila mtu tafsiri ya ndoto yake.
In that place, there was a Hebrew, a servant of the same commander of the military, to whom we explained our dreams.
13 Nayo mambo yakawa sawa kabisa na jinsi alivyotufasiria ndoto zetu: Mimi nilirudishwa kazini mwangu na huyo mtu mwingine akaangikwa.”
Whatever we heard was proven afterwards by the event of the matter. For I was restored to my office, and he was suspended on a cross.”
14 Basi, Farao akatuma Yosefu aitwe, naye akatolewa kifungoni haraka. Baada ya kunyoa na kubadilisha nguo zake akaenda mbele ya Farao.
Immediately, by the king’s authority, Joseph was led out of prison, and they shaved him. And changing his apparel, they presented him to him.
15 Farao akamwambia Yosefu, “Nimeota ndoto, wala hakuna mtu hata mmoja anayeweza kuifasiri. Lakini nimesikia ikisemwa kwa habari yako kwamba unapoelezwa ndoto waweza kuifasiri.”
And he said to him, “I have seen dreams, and there is no one who can unfold them. I have heard that you are very wise at interpreting these.”
16 Yosefu akamjibu Farao, “Siwezi kuifasiri, lakini Mungu atampa Farao jibu analolihitaji.”
Joseph responded, “Apart from me, God will respond favorably to Pharaoh.”
17 Kisha Farao akamwambia Yosefu, “Katika ndoto yangu nilikuwa nimesimama ukingoni mwa Mto Naili,
Therefore, Pharaoh explained what he had seen: “I thought myself to be standing on the bank of a river,
18 nikawaona ngʼombe saba, wazuri na wanono, wakijitokeza kutoka mtoni wakaja kujilisha kwenye matete.
and seven cows climbed up from the river, exceedingly beautiful and full of flesh. And they grazed in a pasture of a marshy greenery.
19 Baada ya hao, ngʼombe wengine saba wadhaifu wakatokea, wabaya sana na waliokonda. Kamwe sikuwahi kuona ngʼombe wabaya jinsi hiyo katika nchi yote ya Misri.
And behold, there followed after these, another seven cows, with such deformity and emaciation as I had never seen in the land of Egypt.
20 Hao ngʼombe waliokonda na wabaya sana wakawala wale ngʼombe saba walionona waliojitokeza kwanza.
These devoured and consumed the first,
21 Lakini hata baada ya kuwala, hakuna mtu ambaye angeweza kusema kwamba wamekula, bado walionekana wabaya kama mwanzoni. Kisha nikaamka kutoka usingizini.
giving no indication of being full. But they remained in the same state of emaciation and squalor. Awakening, but being weighed down into sleep again,
22 “Pia katika ndoto zangu niliona masuke saba ya nafaka, yamejaa na mazuri, yanakua katika bua moja.
I saw a dream. Seven ears of grain sprang up on one stalk, full and very beautiful.
23 Baada ya hayo masuke mengine saba yakachipua, yaliyonyauka, membamba na yamekaushwa na upepo wa mashariki.
Likewise, another seven, thin and struck with blight, rose up from the stalk.
24 Yale masuke membamba ya nafaka yakayameza yale masuke saba mazuri yaliyojaa nafaka. Nimewaeleza waaguzi, wala hakuna yeyote aliyeweza kunifasiria.”
And they devoured the beauty of the first. I explained this dream to the interpreters, and there is no one who can unfold it.”
25 Ndipo Yosefu akamwambia Farao, “Ndoto za Farao ni ndoto iyo hiyo moja. Mungu amemfunulia Farao jambo analokusudia kufanya karibuni.
Joseph responded: “The dream of the king is one. What God will do, he has revealed to Pharaoh.
26 Ngʼombe saba wazuri ni miaka saba, nayo masuke saba mazuri yaliyojaa nafaka ni miaka saba, ni ndoto iyo hiyo moja.
The seven beautiful cows, and the seven full ears of grain, are seven years of abundance. And so the force of the dreams is understood to be the same.
27 Ngʼombe saba waliokonda na wabaya wale waliojitokeza baadaye ni miaka saba, vivyo hivyo masuke saba ya ngano yaliyodhoofika na kukaushwa na upepo wa mashariki, ni miaka saba ya njaa.
Likewise, the seven thin and emaciated cows, which ascended after them, and the seven thin ears of grain, which were struck with the burning wind, are seven approaching years of famine.
28 “Ni kama vile nilivyomwambia Farao: Mungu amemwonyesha Farao jambo analokusudia kufanya karibuni.
These will be fulfilled in this order.
29 Miaka saba ya neema inakuja katika nchi yote ya Misri,
Behold, there will arrive seven years of great fertility throughout the entire land of Egypt.
30 lakini itafuata miaka saba ya njaa. Ndipo neema yote ya Misri itasahaulika na njaa itaikumba nchi.
After this, there will follow another seven years, of such great barrenness that all the former abundance will be delivered into oblivion. For the famine will consume all the land,
31 “Neema iliyokuwa katika nchi haitakumbukwa, kwa sababu njaa itakayofuata itakuwa kali mno.
and the greatness of this destitution will cause the greatness of the abundance to be lost.
32 Sababu ya ndoto kumjia Farao kwa namna mbili ni kwamba jambo hilo Mungu ameshaamua kwa hakika, naye Mungu atalifanya karibuni.
Now, as to what you saw the second time, it is a dream pertaining to the same thing. It is an indication of its firmness, because the word of God shall be done, and it shall be completed swiftly.
33 “Basi sasa Farao na atafute mtu mwenye akili na hekima ili amweke kuwa msimamizi wa nchi ya Misri.
Now therefore, let the king provide a wise and industrious man, and place him over the land of Egypt,
34 Farao na aweke wenye amri nchini kote wakusanye sehemu ya tano ya mavuno ya Misri katika miaka hii saba ya neema.
so that he may appoint overseers throughout all the regions. And let a fifth part of the fruits, throughout the seven fertile years
35 Wakusanye chakula chote katika miaka hii saba ya neema inayokuja na kuhifadhi nafaka chini ya mamlaka ya Farao, iwe akiba ya chakula katika miji.
that now have already begun to occur, be gathered into storehouses. And let all the grain be stored away, under the power of Pharaoh, and let it be kept in the cities.
36 Chakula hiki kitakuwa akiba ya tahadhari kwa ajili ya nchi, ili kitumike katika ile miaka saba ya njaa itakayokuja Misri, ili nchi isiharibiwe na njaa.”
And let it be prepared for the future famine of seven years, which will oppress Egypt, and then the land will not be consumed by destitution.”
37 Mpango huu ulionekana mzuri kwa Farao na kwa maafisa wake wote.
The counsel pleased Pharaoh and all his ministers.
38 Hivyo Farao akawauliza, “Je tunaweza kumpata yeyote kama mtu huyu, ambaye Roho wa Mungu yumo ndani yake?”
And he said to them, “Would we be able to find another such man, who is full of the Spirit of God?”
39 Ndipo Farao akamwambia Yosefu, “Maadamu Mungu amekufunulia yote haya, hakuna mwingine yeyote mwenye akili na hekima kama wewe.
Therefore, he said to Joseph: “Because God has revealed to you all that you have said, would I be able to find anyone wiser and as much like you?
40 Wewe utakuwa msimamizi wa jumba langu la kifalme, na watu wangu wote watatii amri zako. Ni kuhusu kiti cha ufalme tu nitakuwa mkuu kuliko wewe.”
You will be over my house, and to the authority of your mouth, all the people will show obedience. Only in one way, in the throne of the kingdom, will I go before you.”
41 Kwa hiyo Farao akamwambia Yosefu, “Sasa nakuweka uwe msimamizi wa nchi yote ya Misri.”
And again, Pharaoh said to Joseph, “Behold, I have appointed you over the entire land of Egypt.”
42 Ndipo Farao akaivua pete yake ya muhuri kutoka kidoleni mwake na kuivalisha katika kidole cha Yosefu. Akamvika majoho mazuri ya kitani safi na mkufu wa dhahabu shingoni mwake.
And he took the ring from his own hand, and he gave it into his hand. And he clothed him with a robe of fine linen, and he placed a necklace of gold around his neck.
43 Akampandisha katika gari lake la farasi kama msaidizi wake, watu wakatangulia wakishangilia, wakisema, “Fungueni njia!” Ndivyo Farao alivyomweka Yosefu kuwa msimamizi wa nchi yote ya Misri.
And he caused him to ascend upon his second swift chariot, with the herald proclaiming that everyone should bend their knee before him, and that they should know that he was governor over the entire land of Egypt.
44 Kisha Farao akamwambia Yosefu, “Mimi ni Farao, lakini pasipo neno lako, hakuna mtu mwenye ruhusa kuinua mkono au mguu katika nchi yote ya Misri.”
Likewise, the king said to Joseph: “I am Pharaoh: apart from your authority, no one will move hand or foot in all the land of Egypt.”
45 Farao akamwita Yosefu Safenath-Panea, pia akampa Asenathi binti Potifera, kuhani wa mji wa Oni, kuwa mke wake. Ndipo Yosefu akaitembelea nchi yote ya Misri.
And he changed his name and called him, in the Egyptian tongue: ‘Savior of the world.’ And he gave him as a wife, Asenath, the daughter of Potiphera, priest of Heliopolis. And so Joseph went out into the land of Egypt.
46 Yosefu alikuwa na miaka thelathini alipoingia katika utumishi wa Farao mfalme wa Misri. Naye Yosefu akatoka mbele ya Farao akasafiri katika nchi yote ya Misri.
(Now he was thirty years old when he stood in the sight of king Pharaoh.) And he traveled throughout the regions of Egypt.
47 Katika ile miaka saba ya neema nchi ilizaa mazao kwa wingi sana.
And the fertility of the seven years arrived. And when the grain fields were reduced to sheaves, these were gathered into the storehouses of Egypt.
48 Yosefu akakusanya chakula chote kilichozalishwa katika ile miaka saba ya neema nchini Misri, akakihifadhi katika ghala za miji. Katika kila mji kulihifadhiwa chakula kilichozalishwa katika mashamba yaliyouzunguka mji huo.
And now all the abundance of grain was stored away in every city.
49 Yosefu alihifadhi nafaka nyingi, mfano wa mchanga wa bahari, ilikuwa nyingi mno kiasi kwamba walishindwa kuweka kumbukumbu kwa sababu akiba ilizidi sana kupita kipimo.
And there was such a great abundance of wheat that it was comparable to the sands of the sea, and its bounty exceeded all measure.
50 Kabla ya miaka ya njaa kuanza, Asenathi binti Potifera, kuhani wa mji wa Oni, alikuwa amemzalia Yosefu wana wawili wa kiume.
Then, before the famine arrived, Joseph had two sons born, whom Asenath, the daughter of Potiphera, priest of Heliopolis, bore for him.
51 Yosefu akamwita mzaliwa wake wa kwanza Manase, akisema, “Ni kwa sababu Mungu amenifanya nisahau taabu zangu zote pamoja na jamaa yote ya nyumba ya baba yangu.”
And he called the name of the firstborn Manasseh, saying, “God has caused me to forget all my labors and the house of my father.”
52 Mwana wa pili akamwita Efraimu, akisema, “Ni kwa sababu Mungu amenistawisha katika nchi ya mateso yangu.”
Likewise, he named the second Ephraim, saying, “God has caused me to increase in the land of my poverty.”
53 Ile miaka saba ya neema huko Misri ikaisha,
And so, when the seven years of fertility that occurred in Egypt had passed,
54 nayo miaka ile saba ya njaa ikaanza, sawasawa na alivyosema Yosefu. Kulikuwa na njaa katika nchi nyingine zote, bali katika nchi yote ya Misri kulikuwa na chakula.
the seven years of destitution, which Joseph had predicted, began to arrive. And the famine prevailed throughout the whole world, but there was bread in all the land of Egypt.
55 Wakati nchi yote ya Misri ilipopatwa na njaa, watu wakamlilia Farao ili awape chakula. Ndipo Farao alipowaagiza Wamisri wote, akisema, “Nendeni kwa Yosefu, nanyi mfanye anachowaambia.”
And being hungry, the people cried out to Pharaoh, asking for provisions. And he said to them: “Go to Joseph. And do whatever he will tell you.”
56 Wakati njaa ilipokuwa imeenea katika nchi yote, Yosefu akafungua ghala za vyakula na kuwauzia Wamisri nafaka, kwa sababu njaa ilikuwa kali mno katika nchi yote ya Misri.
Then the famine increased daily in all the land. And Joseph opened all of the storehouses and sold to the Egyptians. For the famine had oppressed them also.
57 Pia nchi nyingine zote zilikuja Misri kununua nafaka kutoka kwa Yosefu, kwa sababu njaa ilikuwa kali mno duniani kote.
And all the provinces came to Egypt, to buy food and to temper the misfortune of their destitution.