< Mwanzo 40 >

1 Baada ya muda, mnyweshaji na mwokaji wa mfalme wa Misri, wakamkosea bwana wao, mfalme wa Misri.
Sabara gah ılğevç'uyle qiyğa, Misirne paççahne insanaaşee, ulyoğan helenbışde xərıng'veyiy gıney qecenbışde xərıng'vee paççah qəllamişxhesın kar ha'a.
2 Farao akawakasirikia hawa maafisa wake wawili, mnyweshaji mkuu na mwokaji mkuu,
3 akawaweka chini ya ulinzi katika nyumba ya mkuu wa kikosi cha ulinzi katika gereza lile lile alimofungwa Yosefu.
Manbı avqu g'aravulyçeeşine xərıng'une xaane, Yusuf aqqıne zindaneeqa qoole.
4 Mkuu wa kikosi cha ulinzi akawakabidhi kwa Yosefu, naye akawahudumia. Walipokuwa wamekaa chini ya ulinzi kwa muda,
G'aravulyçeeşine xərıng'vee manbı qoolenbı Yusufusqa, Yusufee manbışis k'ılvalla hee'ecenva. Misirne paççahna ulyoğan helenayiy gıney qecena sabara gahna zindanee avxuyle qiyğa,
5 kila mmoja wa hao wawili waliokuwa wamewekwa gerezani, yaani mnyweshaji na mwokaji wa mfalme wa Misri, waliota ndoto usiku mmoja, na kila ndoto ilikuwa na maana yake tofauti.
sa xəmde manbışik'le curayn-curayn mə'nabınan nyak'bı g'ece.
6 Yosefu alipowajia asubuhi yake, akawaona kwamba walikuwa na huzuni.
Yusuf miç'eer manbışisqa qarımee, manbışe aq'vabı havaxanı'ı g'ece.
7 Ndipo Yosefu akawauliza maafisa hao wa Farao waliokuwa chini ya ulinzi pamoja naye nyumbani mwa bwana wake, akasema, “Mbona nyuso zenu zimejaa huzuni leo?”
Yusufee cuka sacigee xərıng'une xaa, zindanee havaacene fironne insanaaşike qidghın ha'an: – Nya'a g'iyna aq'vabı havaxanı'ı?
8 Wakamjibu, “Sisi sote tuliota ndoto, lakini hapakuwa na mtu yeyote wa kuzifasiri.” Ndipo Yosefu akawaambia, “Je, kufasiri ndoto si kazi ya Mungu? Niambieni ndoto zenu.”
Manbışe mang'uk'le eyhen: – Nyak' g'acu, man nyak' nen eyheniy, eyhes əxəna deşur. Yusufee manbışik'le eyhen: – Nya'a Allahee dişde ats'al hele, nyak' hucoova eyheniyva eyhesın? Hinnalan man zas yuşan he'e.
9 Basi mkuu wa wanyweshaji akamweleza Yosefu ndoto yake. Akamwambia, “Katika ndoto yangu niliona mzabibu mbele yangu,
Ulyoğan helenbışde xərıng'vee cun nyak' yuşan hı'ı eyhen: – Zak'le nik'ek yizde ögee t'ımılena tayang g'avcu.
10 nao mzabibu ulikuwa na matawi matatu. Mara tu ulipoanza kuchipua, maua yalichanua na vishada vyake vikawa zabibu zilizoiva.
Mane t'ımılene tayangıl xheyible tübəəyiy. T'ur qı'ğə-qı'ğə mançin t'et' g'avhu, t'ımıl aleyli'ı.
11 Kikombe cha Farao kilikuwa mkononi mwangu, nikazitwaa zabibu, nikazikamua katika kikombe cha Farao, na nikaweka kikombe mkononi mwake.”
Yizde xıle fironun k'olaniy vod, zı man ts'ets'ybı fironne k'oleeqa hoç'un, yicid fironusqa q'uvu.
12 Yosefu akamwambia, “Hii ndiyo maana yake: Matawi matatu ni siku tatu.
Yusufee mang'uk'le eyhen: – Man in eyhen vodun: xheyible tübəə xhebılle yiğ eyhen vodun.
13 Katika siku hizi tatu, Farao atakutoa gerezani na kukuweka tena kwenye nafasi yako, nawe utaweka kikombe cha Farao mikononi mwake, kama vile ulivyokuwa unafanya ulipokuwa mnyweshaji wake.
Xhebne yiğıle fironee ğu zindaneençe qığavhu yisseyne işilqa sak'ala'as. Şenkiyn xhinne mang'us ulyoğan helena ixhes.
14 Lakini wakati mambo yatakapokuwia mazuri, unikumbuke, unifanyie wema, useme mema juu yangu kwa Farao ili niondoke huku gerezani.
Hucoon ixhes, gırgın kar yəqqı'lqa gitxhumee, zı yik'el qale'e. Zas sa yugvalla hee'e, fironusne yizın do ağmiş he'e. Zı ine zindaneençe g'attixhan he'e.
15 Kwa maana nilichukuliwa kwa nguvu kutoka nchi ya Waebrania, na hata hapa nilipo sikufanya lolote linalostahili niwekwe gerezani.”
Zı cühüt'yaaşine cigeençe qöqüna vor, inyayıd zı zindaneeqa gixhasın vuççud hı'ı deş.
16 Yule mwokaji mkuu alipoona kuwa Yosefu amefasiri ikiwa na maana nzuri, akamwambia Yosefu, “Mimi pia niliota ndoto: Kichwani mwangu kulikuwepo vikapu vitatu vya mikate.
Gıney qeceng'uk'le Yusufee nyak' yugvalis yuşan ha'a g'acu eyhen: – Zak'leme nik'ek yizde vuk'lel oo xheyible ç'emç'e cagvarane gıneyna g'avcu.
17 Katika kikapu cha juu kulikuwa na aina zote za vyakula vilivyookwa kwa ajili ya Farao, lakini ndege walikuwa wakivila kutoka kwenye kikapu nilichokuwa nimebeba kichwani.”
Oğane ç'emç'ee fironusva hı'iyn curayn-curayn gıney ıxha. Mane ç'emç'eеnçis şit'yaaşe k'ufarniy ı'xiyxə.
18 Yosefu akamwambia, “Hii ndiyo maana yake: Vikapu vitatu ni siku tatu.
Yusufee inəxüd eyhe: – Man in eyhen vod: xheyible ç'emç'e, xhebılle yiğ eyhen vod.
19 Katika siku hizi tatu, Farao atakata kichwa chako na kukutundika juu ya mti. Nao ndege watakula nyama ya mwili wako.”
Xhebne yiğıle fironee ğu zindaneençe qığavhu, yiğna vuk'ul candakike curav'u, candak yivele qı'xəs. Şit'yaaşed cis k'ufar ı'xəs.
20 Mnamo siku ya tatu, ilikuwa kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Farao, naye akawaandalia maafisa wake wote karamu. Akawatoa gerezani mnyweshaji mkuu na mwokaji mkuu, akawaweka mbele ya maafisa wake:
Xhebne yiğıle fironun yedike ıxhayn yiğ eyxhe. Mang'vee cune insanaaşis otxhun-ulyodğuy hele. Ulyoğan helenayiy gıney qecena zindaneençe qığav'u, cune insanaaşine hiqa qavayle.
21 Ndipo akamrudisha mnyweshaji mkuu kwenye nafasi yake, ili aweke kikombe mikononi mwa Farao tena,
Ulyoğan helenbışda xərna şenkiyn xhinne cune işilqa sak'ala'a, mang'veyid ögiylin xhinne k'ola fironne xıleqa qele.
22 lakini akamwangika yule mwokaji mkuu, sawasawa na jinsi Yosefu alivyowaambia katika tafsiri yake.
Gıney qecenabışda xərnar givayxanna. Gırgın kar Yusufee uvhuyn xhinne eyxhe.
23 Pamoja na hayo, mnyweshaji mkuu hakumkumbuka Yosefu, bali alimsahau.
Ulyoğan helenbışde xərıng'vee Yusuf yik'el qalya'a deş, yik'el hixanı'ına.

< Mwanzo 40 >