< Mwanzo 40 >
1 Baada ya muda, mnyweshaji na mwokaji wa mfalme wa Misri, wakamkosea bwana wao, mfalme wa Misri.
Después de estas cosas, el siervo principal que tenía el cuidado del vino, y el jefe de los panaderos en la casa de Faraón, hicieron algo contra las órdenes de Faraón;
2 Farao akawakasirikia hawa maafisa wake wawili, mnyweshaji mkuu na mwokaji mkuu,
Y el Faraón se enojó con sus dos siervos, con el siervo principal y el jefe de la panadería;
3 akawaweka chini ya ulinzi katika nyumba ya mkuu wa kikosi cha ulinzi katika gereza lile lile alimofungwa Yosefu.
Y los puso en la cárcel bajo el cuidado del capitán del ejército, en la misma prisión donde el propio José estaba encerrado.
4 Mkuu wa kikosi cha ulinzi akawakabidhi kwa Yosefu, naye akawahudumia. Walipokuwa wamekaa chini ya ulinzi kwa muda,
y el capitán los puso a cargo de José, e hizo lo que se necesitaba; y estuvieron en prisión por algún tiempo.
5 kila mmoja wa hao wawili waliokuwa wamewekwa gerezani, yaani mnyweshaji na mwokaji wa mfalme wa Misri, waliota ndoto usiku mmoja, na kila ndoto ilikuwa na maana yake tofauti.
Y estos dos tuvieron un sueño en la misma noche; el principal sirviente de vino y el principal panadero del rey de Egipto, que estaban en la cárcel, los dos tenían sueños con un sentido especial.
6 Yosefu alipowajia asubuhi yake, akawaona kwamba walikuwa na huzuni.
Y a la mañana cuando José llegó a ellos, vio que estaban tristes.
7 Ndipo Yosefu akawauliza maafisa hao wa Farao waliokuwa chini ya ulinzi pamoja naye nyumbani mwa bwana wake, akasema, “Mbona nyuso zenu zimejaa huzuni leo?”
Y dijo a los siervos de Faraón que estaban en la cárcel con él: ¿Por qué te ves tan triste?
8 Wakamjibu, “Sisi sote tuliota ndoto, lakini hapakuwa na mtu yeyote wa kuzifasiri.” Ndipo Yosefu akawaambia, “Je, kufasiri ndoto si kazi ya Mungu? Niambieni ndoto zenu.”
Entonces ellos le dijeron: Hemos tenido un sueño, y nadie puede darnos el sentido. Y José dijo: ¿Acaso el sentido de los sueños no proviene de Dios? ¿Cuál fue tu sueño?
9 Basi mkuu wa wanyweshaji akamweleza Yosefu ndoto yake. Akamwambia, “Katika ndoto yangu niliona mzabibu mbele yangu,
Entonces el siervo principal dio a José cuenta de su sueño, y dijo: En mi sueño vi una vid delante de mí;
10 nao mzabibu ulikuwa na matawi matatu. Mara tu ulipoanza kuchipua, maua yalichanua na vishada vyake vikawa zabibu zilizoiva.
Y en la vid tres ramas; y parecía que sacaba brotes y flores, y de ellos salían uvas listas para cortar.
11 Kikombe cha Farao kilikuwa mkononi mwangu, nikazitwaa zabibu, nikazikamua katika kikombe cha Farao, na nikaweka kikombe mkononi mwake.”
Y la copa de Faraón estaba en mi mano, y tomé las uvas y las trituré en la copa de Faraón, y puse la copa en la mano de Faraón.
12 Yosefu akamwambia, “Hii ndiyo maana yake: Matawi matatu ni siku tatu.
Entonces dijo José: Este es el sentido de tu sueño: las tres ramas son tres días;
13 Katika siku hizi tatu, Farao atakutoa gerezani na kukuweka tena kwenye nafasi yako, nawe utaweka kikombe cha Farao mikononi mwake, kama vile ulivyokuwa unafanya ulipokuwa mnyweshaji wake.
Después de tres días, Faraón te dará honor, y te hará volver a tu lugar, y le darás su copa como lo hiciste antes, cuando eras su siervo.
14 Lakini wakati mambo yatakapokuwia mazuri, unikumbuke, unifanyie wema, useme mema juu yangu kwa Farao ili niondoke huku gerezani.
Pero ten en cuenta cuando las cosas te vayan bien, y sé bueno conmigo y di una buena palabra para mí a Faraón y sácame de esta prisión:
15 Kwa maana nilichukuliwa kwa nguvu kutoka nchi ya Waebrania, na hata hapa nilipo sikufanya lolote linalostahili niwekwe gerezani.”
Porque en verdad fui tomado por la fuerza de la tierra de los hebreos; y no he hecho nada por lo que pueda ser encarcelado.
16 Yule mwokaji mkuu alipoona kuwa Yosefu amefasiri ikiwa na maana nzuri, akamwambia Yosefu, “Mimi pia niliota ndoto: Kichwani mwangu kulikuwepo vikapu vitatu vya mikate.
Y cuando el jefe de los panaderos vio que el primer sueño tenía buen sentido, dijo a José: Tuve un sueño; y en mi sueño había tres canastas de pan blanco en mi cabeza;
17 Katika kikapu cha juu kulikuwa na aina zote za vyakula vilivyookwa kwa ajili ya Farao, lakini ndege walikuwa wakivila kutoka kwenye kikapu nilichokuwa nimebeba kichwani.”
Y en la canasta superior había toda clase de carnes cocidas para Faraón; y los pájaros los sacaban de las canastas en mi cabeza.
18 Yosefu akamwambia, “Hii ndiyo maana yake: Vikapu vitatu ni siku tatu.
Entonces dijo José: Este es el sentido de tu sueño: las tres cestas son tres días;
19 Katika siku hizi tatu, Farao atakata kichwa chako na kukutundika juu ya mti. Nao ndege watakula nyama ya mwili wako.”
Después de tres días, el Faraón te sacará de la cárcel, colgándote de un árbol, para que tu carne sea alimento para las aves.
20 Mnamo siku ya tatu, ilikuwa kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Farao, naye akawaandalia maafisa wake wote karamu. Akawatoa gerezani mnyweshaji mkuu na mwokaji mkuu, akawaweka mbele ya maafisa wake:
Ahora bien, el tercer día era el cumpleaños de Faraón, y él dio una fiesta a todos sus siervos; y dio honor al principal sirviente de vino y al principal panadero entre los demás.
21 Ndipo akamrudisha mnyweshaji mkuu kwenye nafasi yake, ili aweke kikombe mikononi mwa Farao tena,
Y volvió a poner al siervo principal en su lugar antiguo; y él dio la copa en la mano de Faraón.
22 lakini akamwangika yule mwokaji mkuu, sawasawa na jinsi Yosefu alivyowaambia katika tafsiri yake.
Pero el principal panadero fue muerto ahorcándolo, como José había dicho.
23 Pamoja na hayo, mnyweshaji mkuu hakumkumbuka Yosefu, bali alimsahau.
Pero el siervo no tuvo a José en mente sino que lo olvido.