< Mwanzo 40 >

1 Baada ya muda, mnyweshaji na mwokaji wa mfalme wa Misri, wakamkosea bwana wao, mfalme wa Misri.
Nogen Tid efter hændte det, at Ægypterkongens Mundskænk og Bager forbrød sig mod deres Herre Ægypterkongen,
2 Farao akawakasirikia hawa maafisa wake wawili, mnyweshaji mkuu na mwokaji mkuu,
og Farao vrededes paa sine to Hofmænd, Overmundskænken og Overbageren,
3 akawaweka chini ya ulinzi katika nyumba ya mkuu wa kikosi cha ulinzi katika gereza lile lile alimofungwa Yosefu.
og lod dem sætte i Forvaring i Livvagtens Øverstes Hus, i samme Fængsel, hvor Josef sad fængslet;
4 Mkuu wa kikosi cha ulinzi akawakabidhi kwa Yosefu, naye akawahudumia. Walipokuwa wamekaa chini ya ulinzi kwa muda,
og Livvagtens Øverste gav dem Josef til Opvartning, og han gik dem til Haande. Da de nu havde været i Forvaring en Tid lang,
5 kila mmoja wa hao wawili waliokuwa wamewekwa gerezani, yaani mnyweshaji na mwokaji wa mfalme wa Misri, waliota ndoto usiku mmoja, na kila ndoto ilikuwa na maana yake tofauti.
drømte Ægypterkongens Mundskænk og Bager, som sad i Fængselet, samme Nat hver sin Drøm med sin særlige Betydning.
6 Yosefu alipowajia asubuhi yake, akawaona kwamba walikuwa na huzuni.
Da Josef om Morgenen kom ind til Faraos Hofmænd, der sammen med ham var i Forvaring i hans Herres Hus, og saa, at de var nedslaaede,
7 Ndipo Yosefu akawauliza maafisa hao wa Farao waliokuwa chini ya ulinzi pamoja naye nyumbani mwa bwana wake, akasema, “Mbona nyuso zenu zimejaa huzuni leo?”
spurgte han dem: »Hvorfor ser I saa ulykkelige ud i Dag?«
8 Wakamjibu, “Sisi sote tuliota ndoto, lakini hapakuwa na mtu yeyote wa kuzifasiri.” Ndipo Yosefu akawaambia, “Je, kufasiri ndoto si kazi ya Mungu? Niambieni ndoto zenu.”
Besvarede: »Vi har haft en Drøm, og her er ingen, som kan tyde den.« Da sagde Josef til dem: »Er det ikke Guds Sag at tyde Drømme? Fortæl mig det da!«
9 Basi mkuu wa wanyweshaji akamweleza Yosefu ndoto yake. Akamwambia, “Katika ndoto yangu niliona mzabibu mbele yangu,
Saa fortalte Overmundskænken Josef sin Drøm og sagde: »Jeg saa i Drømme en Vinstok for mig;
10 nao mzabibu ulikuwa na matawi matatu. Mara tu ulipoanza kuchipua, maua yalichanua na vishada vyake vikawa zabibu zilizoiva.
paa Vinstokken var der tre Ranker, og næppe havde den sat Skud, før Blomsterne sprang ud, og Klaserne bar modne Druer;
11 Kikombe cha Farao kilikuwa mkononi mwangu, nikazitwaa zabibu, nikazikamua katika kikombe cha Farao, na nikaweka kikombe mkononi mwake.”
og jeg havde Faraos Bæger i Haanden og tog Druerne og pressede dem i Faraos Bæger og rakte Farao det.«
12 Yosefu akamwambia, “Hii ndiyo maana yake: Matawi matatu ni siku tatu.
Da sagde Josef: »Det skal udtydes saaledes: De tre Ranker betyder tre Dage;
13 Katika siku hizi tatu, Farao atakutoa gerezani na kukuweka tena kwenye nafasi yako, nawe utaweka kikombe cha Farao mikononi mwake, kama vile ulivyokuwa unafanya ulipokuwa mnyweshaji wake.
om tre Dage skal Farao løfte dit Hoved og genindsætte dig i dit Embede, saa du atter rækker Farao Bægeret som før, da du var hans Mundskænk.
14 Lakini wakati mambo yatakapokuwia mazuri, unikumbuke, unifanyie wema, useme mema juu yangu kwa Farao ili niondoke huku gerezani.
Vilde du nu blot tænke paa mig, naar det gaar dig vel, og vise mig Godhed og omtale mig for Farao og saaledes hjælpe mig ud af dette Hus;
15 Kwa maana nilichukuliwa kwa nguvu kutoka nchi ya Waebrania, na hata hapa nilipo sikufanya lolote linalostahili niwekwe gerezani.”
thi jeg er stjaalet fra Hebræernes Land og har heller ikke her gjort noget, de kunde sætte mig i Fængsel for.«
16 Yule mwokaji mkuu alipoona kuwa Yosefu amefasiri ikiwa na maana nzuri, akamwambia Yosefu, “Mimi pia niliota ndoto: Kichwani mwangu kulikuwepo vikapu vitatu vya mikate.
Da nu Overbageren saa, at Josef gav Mundskænken en gunstig Tydning, sagde han til ham: »Jeg havde en lignende Drøm: Se, jeg bar tre Kurve Hvedebrød paa mit Hoved.
17 Katika kikapu cha juu kulikuwa na aina zote za vyakula vilivyookwa kwa ajili ya Farao, lakini ndege walikuwa wakivila kutoka kwenye kikapu nilichokuwa nimebeba kichwani.”
I den øverste Kurv var der alle Haande Bagværk til Faraos Bord, men Fuglene aad det af Kurven paa mit Hoved!«
18 Yosefu akamwambia, “Hii ndiyo maana yake: Vikapu vitatu ni siku tatu.
Da sagde Josef: »Det skal udtydes saaledes: De tre Kurve betyder tre Dage;
19 Katika siku hizi tatu, Farao atakata kichwa chako na kukutundika juu ya mti. Nao ndege watakula nyama ya mwili wako.”
om tre Dage skal Farao løfte dit Hoved og hænge dig op paa en Pæl, og Fuglene skal æde Kødet af din Krop!«
20 Mnamo siku ya tatu, ilikuwa kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Farao, naye akawaandalia maafisa wake wote karamu. Akawatoa gerezani mnyweshaji mkuu na mwokaji mkuu, akawaweka mbele ya maafisa wake:
Tre Dage efter, da det var Faraos Fødselsdag, gjorde han et Gæstebud for alle sine Tjenere, og da løftede han Overmundskænkens og Overbagerens, Hoveder iblandt sine Tjenere.
21 Ndipo akamrudisha mnyweshaji mkuu kwenye nafasi yake, ili aweke kikombe mikononi mwa Farao tena,
Overmundskænken genindsatte han i hans Embede, saa han atter rakte Farao Bægeret,
22 lakini akamwangika yule mwokaji mkuu, sawasawa na jinsi Yosefu alivyowaambia katika tafsiri yake.
og Overbageren lod han hænge, som Josef havde tydet det for dem.
23 Pamoja na hayo, mnyweshaji mkuu hakumkumbuka Yosefu, bali alimsahau.
Men Overmundskænken tænkte ikke paa Josef; han glemte ham.

< Mwanzo 40 >