< Mwanzo 40 >
1 Baada ya muda, mnyweshaji na mwokaji wa mfalme wa Misri, wakamkosea bwana wao, mfalme wa Misri.
這些事以後,埃及王的司酒和司廚得罪了他們的主人埃及王。
2 Farao akawakasirikia hawa maafisa wake wawili, mnyweshaji mkuu na mwokaji mkuu,
法郎於是對那兩個內臣,司酒長和司廚長發了怒,
3 akawaweka chini ya ulinzi katika nyumba ya mkuu wa kikosi cha ulinzi katika gereza lile lile alimofungwa Yosefu.
將他們囚在衛隊長府內的拘留所內,若瑟被囚禁的地方。
4 Mkuu wa kikosi cha ulinzi akawakabidhi kwa Yosefu, naye akawahudumia. Walipokuwa wamekaa chini ya ulinzi kwa muda,
衛隊長將他們交給若瑟,若瑟就照管他們。他們在拘留所內過了一些時日,
5 kila mmoja wa hao wawili waliokuwa wamewekwa gerezani, yaani mnyweshaji na mwokaji wa mfalme wa Misri, waliota ndoto usiku mmoja, na kila ndoto ilikuwa na maana yake tofauti.
那兩個被囚在獄裏的埃及王的司酒和司廚,在同一夜裏,各作了一夢;每人的夢都有它的意義。
6 Yosefu alipowajia asubuhi yake, akawaona kwamba walikuwa na huzuni.
早晨若瑟到了他們那裏,見他們面有憂色,
7 Ndipo Yosefu akawauliza maafisa hao wa Farao waliokuwa chini ya ulinzi pamoja naye nyumbani mwa bwana wake, akasema, “Mbona nyuso zenu zimejaa huzuni leo?”
便問那與他同在自己主人府中監獄裏的法郎內臣說:「為什麼你們今天面帶憂色﹖」
8 Wakamjibu, “Sisi sote tuliota ndoto, lakini hapakuwa na mtu yeyote wa kuzifasiri.” Ndipo Yosefu akawaambia, “Je, kufasiri ndoto si kazi ya Mungu? Niambieni ndoto zenu.”
他們回答說:「我們各作了一夢,沒有人能夠解釋。」若瑟對他們說:「解夢不是天主的事嗎﹖請你們講給我聽! 」
9 Basi mkuu wa wanyweshaji akamweleza Yosefu ndoto yake. Akamwambia, “Katika ndoto yangu niliona mzabibu mbele yangu,
司酒長就將自己的夢講給若瑟聽,對他說:「我夢見在我前面有株葡萄樹。
10 nao mzabibu ulikuwa na matawi matatu. Mara tu ulipoanza kuchipua, maua yalichanua na vishada vyake vikawa zabibu zilizoiva.
樹上有三根枝子,剛發芽,就生出了花朵,花朵結了熟葡萄。
11 Kikombe cha Farao kilikuwa mkononi mwangu, nikazitwaa zabibu, nikazikamua katika kikombe cha Farao, na nikaweka kikombe mkononi mwake.”
我手拿著法郎的杯,將葡萄擠在法郎的杯中,將杯遞在法郎的手內。」
12 Yosefu akamwambia, “Hii ndiyo maana yake: Matawi matatu ni siku tatu.
若瑟對他說:「這夢的意義就是:三根枝子是指的三天。
13 Katika siku hizi tatu, Farao atakutoa gerezani na kukuweka tena kwenye nafasi yako, nawe utaweka kikombe cha Farao mikononi mwake, kama vile ulivyokuwa unafanya ulipokuwa mnyweshaji wake.
三天以內,法郎要高舉你,恢復你的職位:你仍將杯放在法郎的手中,像先前作他司酒時一樣;
14 Lakini wakati mambo yatakapokuwia mazuri, unikumbuke, unifanyie wema, useme mema juu yangu kwa Farao ili niondoke huku gerezani.
但是,當你得志時,請你記得我,望你對我施恩,為我告訴法郎,救我出離這監牢;
15 Kwa maana nilichukuliwa kwa nguvu kutoka nchi ya Waebrania, na hata hapa nilipo sikufanya lolote linalostahili niwekwe gerezani.”
因為我不但是由希伯來人地被拐來的,而且在這裏我也沒有做過什麼使他們將我放在這地牢裏的事。」
16 Yule mwokaji mkuu alipoona kuwa Yosefu amefasiri ikiwa na maana nzuri, akamwambia Yosefu, “Mimi pia niliota ndoto: Kichwani mwangu kulikuwepo vikapu vitatu vya mikate.
司廚長見他解得吉祥,便對若瑟說:「我也作了一夢,夢見在我的頭上有三筐白餅。
17 Katika kikapu cha juu kulikuwa na aina zote za vyakula vilivyookwa kwa ajili ya Farao, lakini ndege walikuwa wakivila kutoka kwenye kikapu nilichokuwa nimebeba kichwani.”
最上面的筐內,有為法郎預備的各種食物,有飛鳥來啄食我頭上筐裏的食物。」
18 Yosefu akamwambia, “Hii ndiyo maana yake: Vikapu vitatu ni siku tatu.
若瑟回答說:「這夢的意義就是:三筐是指的三天。
19 Katika siku hizi tatu, Farao atakata kichwa chako na kukutundika juu ya mti. Nao ndege watakula nyama ya mwili wako.”
三天以內,法郎要高舉你,將你懸在木架上,飛鳥要來啄食你的肉。」
20 Mnamo siku ya tatu, ilikuwa kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Farao, naye akawaandalia maafisa wake wote karamu. Akawatoa gerezani mnyweshaji mkuu na mwokaji mkuu, akawaweka mbele ya maafisa wake:
第三天,適逢法郎的生日,法郎為群臣擺設了盛宴,在群臣中將司酒長和司廚長提出來,
21 Ndipo akamrudisha mnyweshaji mkuu kwenye nafasi yake, ili aweke kikombe mikononi mwa Farao tena,
恢復了司酒長的司酒職,再將杯放在法郎手中;
22 lakini akamwangika yule mwokaji mkuu, sawasawa na jinsi Yosefu alivyowaambia katika tafsiri yake.
至於司廚長,卻被懸掛起來,正如若瑟對他們所解釋的。
23 Pamoja na hayo, mnyweshaji mkuu hakumkumbuka Yosefu, bali alimsahau.
司酒長卻沒有記得若瑟,竟將他忘了。