< Mwanzo 4 >

1 Adamu akakutana kimwili na mkewe Eva, naye akapata mimba, akamzaa Kaini. Eva akasema, “Kwa msaada wa Bwana nimemzaa mwanaume.”
And the man he knew Eve wife his and she conceived and she bore Cain and she said I have acquired a man with Yahweh.
2 Baadaye akamzaa Abeli ndugu yake. Basi Abeli akawa mfugaji, na Kaini akawa mkulima.
And she repeated to give birth to brother his Abel and he was Abel a herder of sheep and Cain he was a tiller of [the] ground.
3 Baada ya muda Kaini akaleta baadhi ya mazao ya shamba kama sadaka kwa Bwana.
And it happened from [the] end of days and he brought Cain some of [the] fruit of the ground an offering to Yahweh.
4 Lakini Abeli akaleta fungu nono kutoka baadhi ya wazaliwa wa kwanza wa mifugo yake. Bwana akamkubali Abeli pamoja na sadaka yake,
And Abel he brought also he some of [the] firstborn of flock his and some of fat their and he looked Yahweh to Abel and to offering his.
5 lakini Mungu hakumkubali Kaini pamoja na sadaka yake. Kwa hiyo Kaini akakasirika sana, uso wake ukawa na huzuni.
And to Cain and to offering his not he looked and burned to Cain exceedingly and they fell face his.
6 Kisha Bwana akamwambia Kaini, “Kwa nini umekasirika? Kwa nini uso wako una huzuni?
And he said Yahweh to Cain why? does it burn to you and why? have they fallen face your.
7 Ukifanya lililo sawa, je, hutakubalika? Lakini usipofanya lililo sawa, dhambi inakuvizia mlangoni mwako, inakutamani wewe, lakini inakupasa uishinde.”
¿ Not if you will do well lifting up and if not you will do well to the door sin [is] crouching and [is] to you desire its and you you will rule over it.
8 Basi Kaini akamwambia ndugu yake Abeli, “Twende shambani.” Walipokuwa shambani, Kaini akamshambulia Abeli ndugu yake, akamuua.
And he said Cain to Abel brother his (let us go [into] the field *X*) and it was when were they in the field and he rose up Cain against Abel brother his and he killed him.
9 Kisha Bwana akamuuliza Kaini, “Ndugu yako Abeli yuko wapi?” Akamjibu, “Sijui, je, mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?”
And he said Yahweh to Cain where? [is] Abel brother your and he said not I know ¿ [the] keeper of brother my [am] I.
10 Bwana akasema, “Umefanya nini? Sikiliza! Damu ya ndugu yako inanililia mimi kutoka ardhini.
And he said what? have you done [the] voice of [the] blood of brother your [are] crying out to me from the ground.
11 Sasa umelaaniwa na umehamishwa kutoka ardhi, ambayo imefungua kinywa chake na kupokea damu ya ndugu yako kutoka mkononi mwako.
And now [are] cursed you from the ground which has opened mouth its to receive [the] blood of brother your from hand your.
12 Utakapoilima ardhi, haitakupa tena mazao yake. Utakuwa mtu wa kutangatanga duniani asiye na utulivu.”
For you will till the ground not will repeat to give produce its to you a wanderer and a fugitive you will be on the earth.
13 Kaini akamwambia Bwana, “Adhabu yangu ni zaidi ya niwezavyo kustahimili.
And he said Cain to Yahweh [is too] great punishment my for bearing.
14 Leo unanifukuza kutoka nchi, nami nitafichwa mbali na uwepo wako. Nitakuwa mtu wa kutangatanga asiyetulia duniani na yeyote anionaye ataniua.”
Here! you have driven away me this day from on [the] surface of the ground and from before you I will be hidden and I will be a wanderer and a fugitive on the earth and it will be every [one who] finds me he will kill me.
15 Lakini Bwana akamwambia, “La sivyo, ikiwa mtu yeyote atamuua Kaini atalipizwa kisasi mara saba zaidi.” Kisha Bwana akamwekea Kaini alama ili mtu yeyote ambaye angemwona asimuue.
And he said to him Yahweh therefore any [one who] kills Cain sevenfold he will be avenged and he appointed Yahweh for Cain a sign to not to strike him any [one who] found him.
16 Kwa hiyo Kaini akaondoka mbele za Bwana akaenda kuishi katika nchi ya Nodi, iliyoko mashariki ya Edeni.
And he went out Cain from to before Yahweh and he dwelt in [the] land of Nod [the] east of Eden.
17 Kaini akakutana kimwili na mkewe, naye akapata mimba na akamzaa Enoki. Wakati huo Kaini alikuwa anajenga mji, akauita Enoki jina la mtoto wake.
And he knew Cain wife his and she conceived and she bore Enoch and he was building a city and he called [the] name of the city according to [the] name of son his Enoch.
18 Enoki akamzaa Iradi, Iradi akamzaa Mehuyaeli, Mehuyaeli akamzaa Methushaeli, na Methushaeli akamzaa Lameki.
And he was born to Enoch Irad and Irad he fathered Mehujael and Mehujael he fathered Methushael and Methushael he fathered Lamech.
19 Lameki alioa wanawake wawili, mmoja aliitwa Ada, na mwingine Sila.
And he took for himself Lamech two wives [the] name of the one [was] Adah and [the] name of the second [was] Zillah.
20 Ada akamzaa Yabali ambaye ni baba wa wale walioishi katika mahema na kufuga wanyama.
And she bore Adah Jabal he he was [the] father of dweller[s] of tent and livestock.
21 Kaka yake aliitwa Yubali, aliyekuwa baba wa wote wapigao zeze na filimbi.
And [the] name of brother his [was] Jubal he he was [the] father of every player of harp and flute.
22 Pia Sila alikuwa na mtoto wa kiume aliyeitwa Tubali-Kaini ambaye alifua vifaa vya aina mbalimbali vya shaba na chuma. Naama alikuwa dada wa Tubali-Kaini.
And Zillah also she she bore Tubal-Cain a sharpener of every worker of bronze and iron and [was] [the] sister of Tubal-Cain Naamah.
23 Lameki akawaambia wake zake, “Ada na Sila nisikilizeni mimi; wake wa Lameki sikieni maneno yangu. Nimemuua mtu kwa kunijeruhi, kijana mdogo kwa kuniumiza.
And he said Lamech to wives his O Adah and Zillah listen to voice my O wives of Lamech give ear to speech my that a man I have killed for bruise my and a young man for wound my.
24 Kama Kaini atalipizwa kisasi mara saba, basi Lameki itakuwa mara sabini na saba.”
For sevenfold he will be avenged Cain and Lamech seventy and seven.
25 Adamu akakutana kimwili na mke wake tena, akamzaa mwana, akamwita Sethi, akisema, “Mungu amenijalia mwana mwingine badala ya Abeli, kwa kuwa Kaini alimuua.”
And he knew Adam again wife his and she bore a son and she called name his Seth for he has appointed for me God of spring another in place of Abel for he killed him Cain.
26 Naye Sethi akamzaa mwana, akamwita Enoshi. Wakati huo watu wakaanza kuliitia jina la Bwana.
And to Seth also he he was born a son and he called name his Enosh then it was begun to call on [the] name of Yahweh.

< Mwanzo 4 >