< Mwanzo 4 >

1 Adamu akakutana kimwili na mkewe Eva, naye akapata mimba, akamzaa Kaini. Eva akasema, “Kwa msaada wa Bwana nimemzaa mwanaume.”
Afterward the man knew Heuah his wife, which conceiued and bare Kain, and said, I haue obteined a man by the Lord.
2 Baadaye akamzaa Abeli ndugu yake. Basi Abeli akawa mfugaji, na Kaini akawa mkulima.
And againe she brought foorth his brother Habel, and Habel was a keeper of sheepe, and Kain was a tiller of the ground.
3 Baada ya muda Kaini akaleta baadhi ya mazao ya shamba kama sadaka kwa Bwana.
And in processe of time it came to passe, that Kain brought an oblation vnto the Lord of the fruite of the ground.
4 Lakini Abeli akaleta fungu nono kutoka baadhi ya wazaliwa wa kwanza wa mifugo yake. Bwana akamkubali Abeli pamoja na sadaka yake,
And Habel also him selfe brought of the first fruites of his sheepe, and of the fat of them, and the Lord had respect vnto Habel, and to his offering,
5 lakini Mungu hakumkubali Kaini pamoja na sadaka yake. Kwa hiyo Kaini akakasirika sana, uso wake ukawa na huzuni.
But vnto Kain and to his offering he had no regarde: wherefore Kain was exceeding wroth, and his countenance fell downe.
6 Kisha Bwana akamwambia Kaini, “Kwa nini umekasirika? Kwa nini uso wako una huzuni?
Then ye Lord said vnto Kain, Why art thou wroth? and why is thy countenance cast downe?
7 Ukifanya lililo sawa, je, hutakubalika? Lakini usipofanya lililo sawa, dhambi inakuvizia mlangoni mwako, inakutamani wewe, lakini inakupasa uishinde.”
If thou do well, shalt thou not be accepted? and if thou doest not well, sinne lieth at the doore: also vnto thee his desire shalbe subiect, and thou shalt rule ouer him.
8 Basi Kaini akamwambia ndugu yake Abeli, “Twende shambani.” Walipokuwa shambani, Kaini akamshambulia Abeli ndugu yake, akamuua.
Then Kain spake to Habel his brother. And when they were in the fielde, Kain rose vp against Habel his brother, and slewe him.
9 Kisha Bwana akamuuliza Kaini, “Ndugu yako Abeli yuko wapi?” Akamjibu, “Sijui, je, mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?”
Then the Lord said vnto Kain, Where is Habel thy brother? Who answered, I cannot tell. Am I my brothers keeper?
10 Bwana akasema, “Umefanya nini? Sikiliza! Damu ya ndugu yako inanililia mimi kutoka ardhini.
Againe he said, What hast thou done? the voyce of thy brothers blood cryeth vnto me from the earth.
11 Sasa umelaaniwa na umehamishwa kutoka ardhi, ambayo imefungua kinywa chake na kupokea damu ya ndugu yako kutoka mkononi mwako.
Now therefore thou art cursed from the earth, which hath opened her mouth to receiue thy brothers blood from thine hand.
12 Utakapoilima ardhi, haitakupa tena mazao yake. Utakuwa mtu wa kutangatanga duniani asiye na utulivu.”
When thou shalt till the grounde, it shall not henceforth yeelde vnto thee her strength: a vagabond and a runnagate shalt thou be in the earth.
13 Kaini akamwambia Bwana, “Adhabu yangu ni zaidi ya niwezavyo kustahimili.
Then Kain said to the Lord, My punishment is greater, then I can beare.
14 Leo unanifukuza kutoka nchi, nami nitafichwa mbali na uwepo wako. Nitakuwa mtu wa kutangatanga asiyetulia duniani na yeyote anionaye ataniua.”
Behold, thou hast cast me out this day from the earth, and from thy face shall I be hid, and shalbe a vagabond, and a runnagate in the earth, and whosoeuer findeth me, shall slay me.
15 Lakini Bwana akamwambia, “La sivyo, ikiwa mtu yeyote atamuua Kaini atalipizwa kisasi mara saba zaidi.” Kisha Bwana akamwekea Kaini alama ili mtu yeyote ambaye angemwona asimuue.
Then the Lord said vnto him, Doubtlesse whosoeuer slayeth Kain, he shalbe punished seue folde. And the Lord set a marke vpon Kain, lest any man finding him should kill him.
16 Kwa hiyo Kaini akaondoka mbele za Bwana akaenda kuishi katika nchi ya Nodi, iliyoko mashariki ya Edeni.
Then Kain went out from the presence of the Lord, and dwelt in the land of Nod towarde the Eastside of Eden.
17 Kaini akakutana kimwili na mkewe, naye akapata mimba na akamzaa Enoki. Wakati huo Kaini alikuwa anajenga mji, akauita Enoki jina la mtoto wake.
Kain also knewe his wife, which conceiued and bare Henoch: and he built a citie, and called the name of the citie by ye name of his sonne, Henoch.
18 Enoki akamzaa Iradi, Iradi akamzaa Mehuyaeli, Mehuyaeli akamzaa Methushaeli, na Methushaeli akamzaa Lameki.
And to Henoch was borne Irad, and Irad begate Mehuiael, and Mehuiael begate Methushael, and Methushael begate Lamech.
19 Lameki alioa wanawake wawili, mmoja aliitwa Ada, na mwingine Sila.
And Lamech tooke him two wiues: the name of the one was Adah, and the name of the other Zillah.
20 Ada akamzaa Yabali ambaye ni baba wa wale walioishi katika mahema na kufuga wanyama.
And Adah bare Iabal, who was the father of such as dwell in the tents, and of such as haue cattell.
21 Kaka yake aliitwa Yubali, aliyekuwa baba wa wote wapigao zeze na filimbi.
And his brothers name was Iubal, who was the father of all that play on the harpe and organes.
22 Pia Sila alikuwa na mtoto wa kiume aliyeitwa Tubali-Kaini ambaye alifua vifaa vya aina mbalimbali vya shaba na chuma. Naama alikuwa dada wa Tubali-Kaini.
And Zillah also bare Tubal-kain, who wrought cunningly euery craft of brasse and of yron: and the sister of Tubal-kain was Naamah.
23 Lameki akawaambia wake zake, “Ada na Sila nisikilizeni mimi; wake wa Lameki sikieni maneno yangu. Nimemuua mtu kwa kunijeruhi, kijana mdogo kwa kuniumiza.
Then Lamech saide vnto his wiues Adah and Zillah, Heare my voyce, ye wiues of Lamech: hearken vnto my speach: for I would slay a man in my wound, and a yong man in mine hurt.
24 Kama Kaini atalipizwa kisasi mara saba, basi Lameki itakuwa mara sabini na saba.”
If Kain shalbe auenged seuen folde, truely Lamech, seuentie times seuen folde.
25 Adamu akakutana kimwili na mke wake tena, akamzaa mwana, akamwita Sethi, akisema, “Mungu amenijalia mwana mwingine badala ya Abeli, kwa kuwa Kaini alimuua.”
And Adam knewe his wife againe, and she bare a sonne, and she called his name Sheth: for God, saide she, hath appointed me another seede for Habel, because Kain slewe him.
26 Naye Sethi akamzaa mwana, akamwita Enoshi. Wakati huo watu wakaanza kuliitia jina la Bwana.
And to ye same Sheth also there was borne a sonne, and he called his name Enosh. Then beganne men to call vpon the name of the Lord.

< Mwanzo 4 >