< Mwanzo 39 >

1 Wakati huu Yosefu alikuwa amechukuliwa mpaka Misri. Mmisri aliyeitwa Potifa aliyekuwa mmojawapo wa maafisa wa Farao, mkuu wa ulinzi, akamnunua Yosefu kutoka kwa Waishmaeli waliomleta Misri.
Naipan ni Jose iti Egipto. Ti Egipcio a ni Potifar, a maysa nga opisial iti Faraon ta isu ket kapitan dagiti guardia, ginatangna ni Jose manipud kadagiti Ismaelita a nangipan kenkuana sadiay.
2 Bwana alikuwa pamoja na Yosefu, naye akastawi, Yosefu akaishi nyumbani kwa bwana wake Mmisri.
Adda ni Yahweh kenni Jose. Isuna ket narang-ay a tao. Adda isuna iti balay ti amona nga Egipcio.
3 Potifa alipoona kuwa Bwana alikuwa pamoja na Yosefu na kwamba Bwana alimfanikisha kwa kila kitu alichokifanya,
Nakita ti apona nga adda ni Yahweh kenkuana ken pinarang-ay ni Yahweh ti tunggal banag nga inaramidna.
4 Yosefu alipata kibali machoni pa Potifa, akamfanya mhudumu wake. Potifa akamweka kuwa msimamizi wa nyumba yake, naye akamkabidhi kuwa mwangalizi wa kila kitu alichokuwa nacho.
Nagbalin ngarud ni Jose a makaay-ayo iti imatang ti apona. Nagserbianna ni Potifar. Pinagbalin ni Potifar ni Jose a mangimaton iti isuamin nga adda iti balayna, ket amin a sanikuana, impaaywanna kenni Jose.
5 Kuanzia wakati huo Potifa alipomweka Yosefu kuwa msimamizi wa nyumba na mali zake zote alizokuwa nazo, Bwana aliibariki nyumba ya Mmisri huyo kwa sababu ya Yosefu. Baraka ya Bwana ilikuwa juu ya kila kitu alichokuwa nacho Potifa, nyumbani na shambani.
Napasamak a manipud iti tiempo a pinagbalin ni Potifar ni Jose a mangimaton iti balayna ken iti amin a sanikuana, a binendisionan ni Yahweh ti balay ti Egipcio gapu kenni Jose. Ti bendision ni Yahweh ket adda kadagiti amin nga adda iti balay ken taltalon ni Potifar.
6 Kwa hiyo Potifa akamwachia Yosefu uangalizi wa kila kitu alichokuwa nacho, Yosefu alipokuwa katika uongozi, Potifa hakuwa na sababu ya kujishughulisha na kitu chochote isipokuwa chakula alichokula. Yosefu alikuwa mwenye umbo zuri na sura ya kuvutia;
Impaaywan ni Potifar dagiti amin nga adda kenkuana kenni Jose. Saannan a masapul a panunoten pay ti maipapan iti aniaman a banag malaksid ti taraon a kanenna. Ita, ni Jose ket nataer ken nabaked.
7 baada ya kitambo mke wa Potifa akamtamani Yosefu, akamwambia, “Njoo, ukutane nami kimwili!”
Napasamak kalpasan daytoy, a ni Jose ket pinaggarteman ti asawa ti apona. Kinunana, “Kaiddaennak.”
8 Lakini Yosefu akakataa. Akamwambia yule mwanamke, “Mimi nikiwa katika uongozi, bwana wangu hahusiki na kitu chochote katika nyumba hii, kila kitu alicho nacho amenikabidhi.
Ngem nagkedked isuna ket kinunana iti asawa ti apona, “Kitaem, saan a pakibibbiangan ti apok no ania ti aramidek iti balay, ken amin a sanikuana ket impaaywanna kaniak.
9 Hapa nyumbani hakuna aliye mkuu kuliko mimi. Bwana wangu hakunizuilia kitu chochote isipokuwa wewe, kwa kuwa wewe ni mke wake. Nitawezaje basi kufanya uovu huu na kutenda dhambi dhidi ya Mungu?”
Awan ti siasinoman a nangatngato kaniak iti daytoy a balay. Awan iti aniaman a saanna nga intalek kaniak malaksid kenka, gapu ta sika ket asawana. Apay ketdin nga aramidek daytoy a nakaro a kinadakes a pakabasulak iti Dios?”
10 Ingawa yule mwanamke aliendelea kumshawishi Yosefu siku baada ya siku, Yosefu alikataa kukutana naye kimwili wala kukaa karibu naye.
Inaldaw a makikisao isuna kenni Jose, ngem nagkedked isuna a makikaidda wenno makikaddua kenkuana.
11 Siku moja Yosefu akaingia ndani ya nyumba kufanya kazi zake, wala hapakuwepo na mfanyakazi yeyote ndani ya nyumba.
Napasamak iti maysa nga aldaw a simrek isuna iti balay tapno aramidenna ti trabahona. Awan kadagiti lallaki iti balay ti adda iti balay.
12 Mke wa Potifa akashika vazi Yosefu alilokuwa amevaa, akamwambia, “Njoo tukutane kimwili!” Lakini Yosefu akaacha vazi lake mkononi mwa huyo mwanamke, akatoka nje ya nyumba akikimbia.
Ginammatanna isuna babaen kadagiti kawesna ket kinunana, “Kaidddaennak.” Timmaray ni Jose a napan iti ruar, ket nabatina ti kawesna iti ima ti babai.
13 Yule mwanamke alipoona kwamba Yosefu amemwachia vazi lake mkononi na kukimbilia nje ya nyumba,
Napasamak nga idi nakita ti asawa ni Potifar a nabati ni Jose ti kawesna iti ima daytoy ken timmaray iti ruar,
14 akawaita watumishi wake wa nyumbani, akawaambia, “Tazameni! Huyu Mwebrania ameletwa hapa kutudhihaki! Aliingia hapa ndani ili akutane nami kimwili, lakini nikapiga kelele.
immawag isuna kadagiti lallaki iti balayna ket imbagana kadakuada, “Kitaenyo, nangiserrek ditoy ni Potifar iti Hebreo a manglais kadatayo. Sinerreknak tapno kaiddaenak, ket nagikkisak.
15 Aliposikia kelele za kuomba msaada, akaacha vazi lake kando yangu akakimbilia nje.”
Napasamak nga idi nangngegna a nagikkisak, timmaray iti ruwar ket nabatina ti kawesna kaniak.”
16 Yule mwanamke akaliweka lile vazi karibu naye mpaka Potifa aliporudi nyumbani.
Inkabilna ti kawesna iti sibayna agingga a nagawid ti apona.
17 Ndipo akamweleza kisa hiki, akisema: “Yule mtumwa wa Kiebrania uliyetuletea alinijia ili kunidhihaki.
Imbagana kenkuana daytoy a palawag, “Ti adipen a Hebreo nga inyegmo kadakami, sinerreknak tapno gundawayannak.
18 Lakini mara nilipopiga kelele kuomba msaada, akaliacha vazi lake kando yangu akakimbia nje ya nyumba.”
Ket napamasak nga idi nagikkisak, timmaray iti ruar ket nabatina ti kawesna kaniak.”
19 Potifa aliposikia kisa hiki mkewe alichomweleza, akisema, “Hivi ndivyo mtumwa wako alivyonitenda.” Hasira ya Potifa ikawaka.
Napasamak nga idi nangngeg ni Potifar ti palawag nga imbaga ti asawana kenkuana a kunana, “Kastoy ti inaramid kaniak ti adipenmo,” nakapungtot iti kasta unay ni Potifar.
20 Potifa akamchukua Yosefu na kumweka gerezani, mahali ambapo wahalifu wa mfalme walikuwa wamefungwa. Lakini wakati Yosefu alipokuwa huko gerezani,
Innala ni Potifar ni Jose ket pinaibaludna, iti lugar a nakaibaludan dagiti balud ti ari. Ket adda ngarud isunan iti pagbaludan.
21 Bwana alikuwa pamoja naye, akamhurumia na kumpa kibali mbele ya msimamizi wa gereza.
Ngem adda ni Yahweh kenni Jose ken impakitana kenkuana a napudno isuna iti tulagna. Nagtignay ni Yahweh iti agbanbantay iti pagbaludan isu a nakasarak ni Jose iti pabor iti imatang daytoy.
22 Kwa hiyo msimamizi wa gereza akamweka Yosefu awe mkuu wa wafungwa pamoja na kusimamia yote ambayo yalitendeka mle gerezani.
Intalek ti agbanbantay iti pagbaludan dagiti amin a balud nga adda iti pagbaludan kenni Jose. Aniaman nga ar-aramidenda idiay, naitalek kenni Jose dagitoy.
23 Msimamizi wa gereza hakujishughulisha tena na kitu chochote kilichokuwa chini ya uangalizi wa Yosefu, kwa sababu Bwana alikuwa pamoja na Yosefu akimfanikisha kwa kila alichofanya.
Awan ti pagdanagan ti agbanbantay iti pagbaludan maipapan iti aniaman a banag a naitalek kenni Jose, gapu ta adda ni Yahweh kenkuana. Pinarang-ay ni Yahweh ti aniaman nga inaramidna.

< Mwanzo 39 >