< Mwanzo 39 >

1 Wakati huu Yosefu alikuwa amechukuliwa mpaka Misri. Mmisri aliyeitwa Potifa aliyekuwa mmojawapo wa maafisa wa Farao, mkuu wa ulinzi, akamnunua Yosefu kutoka kwa Waishmaeli waliomleta Misri.
Therfor Joseph was led in to Egipt, and Putifar, `chast and onest seruaunt of Farao, prince of the oost, a man of Egipt, bouyte hym of the hondis of Ismaelitis, of which he was brouyt.
2 Bwana alikuwa pamoja na Yosefu, naye akastawi, Yosefu akaishi nyumbani kwa bwana wake Mmisri.
And the Lord was with hym, and he was a man doynge with prosperite in alle thingis. And Joseph dwellide in `the hows of his lord,
3 Potifa alipoona kuwa Bwana alikuwa pamoja na Yosefu na kwamba Bwana alimfanikisha kwa kila kitu alichokifanya,
which knew best that the Lord was with Joseph, and that alle thingis whiche he dide, weren dressid of the Lord in `the hond of hym.
4 Yosefu alipata kibali machoni pa Potifa, akamfanya mhudumu wake. Potifa akamweka kuwa msimamizi wa nyumba yake, naye akamkabidhi kuwa mwangalizi wa kila kitu alichokuwa nacho.
And Joseph foond grace bifor his lord, and `mynystride to hym, of whom Joseph was maad souereyn of alle thingis, and gouernede the hows bitaken to hym, and alle thingis that weren bitakun to hym.
5 Kuanzia wakati huo Potifa alipomweka Yosefu kuwa msimamizi wa nyumba na mali zake zote alizokuwa nazo, Bwana aliibariki nyumba ya Mmisri huyo kwa sababu ya Yosefu. Baraka ya Bwana ilikuwa juu ya kila kitu alichokuwa nacho Potifa, nyumbani na shambani.
And the Lord blesside the `hows of Egipcian for Joseph, and multipliede al his catel, as wel in howsis as in feeldis;
6 Kwa hiyo Potifa akamwachia Yosefu uangalizi wa kila kitu alichokuwa nacho, Yosefu alipokuwa katika uongozi, Potifa hakuwa na sababu ya kujishughulisha na kitu chochote isipokuwa chakula alichokula. Yosefu alikuwa mwenye umbo zuri na sura ya kuvutia;
nether he knew ony other thing no but `breed which he eet. Forsothe Joseph was fair in face, and schapli in siyt.
7 baada ya kitambo mke wa Potifa akamtamani Yosefu, akamwambia, “Njoo, ukutane nami kimwili!”
And so aftir many daies the ladi castide hir iyen in to Joseph, and seide, Slepe thou with me;
8 Lakini Yosefu akakataa. Akamwambia yule mwanamke, “Mimi nikiwa katika uongozi, bwana wangu hahusiki na kitu chochote katika nyumba hii, kila kitu alicho nacho amenikabidhi.
which assentide not to the vnleueful werk, and seide to hir, Lo! while alle thingis ben bitakun to me, my lord woot not what he hath in his hows,
9 Hapa nyumbani hakuna aliye mkuu kuliko mimi. Bwana wangu hakunizuilia kitu chochote isipokuwa wewe, kwa kuwa wewe ni mke wake. Nitawezaje basi kufanya uovu huu na kutenda dhambi dhidi ya Mungu?”
nether ony thing is, which is not in my power, ether which `he hath not bitake to me, outakun thee, which art his wijf; how therfor may Y do this yuel, and do synne ayens my lord?
10 Ingawa yule mwanamke aliendelea kumshawishi Yosefu siku baada ya siku, Yosefu alikataa kukutana naye kimwili wala kukaa karibu naye.
Thei spaken siche wordis `bi alle daies, and the womman was diseseful to the yong waxynge man, and he forsook auoutrie.
11 Siku moja Yosefu akaingia ndani ya nyumba kufanya kazi zake, wala hapakuwepo na mfanyakazi yeyote ndani ya nyumba.
Forsothe it bifelde in a dai, that Joseph entride in to the hows, and dide sum werk with out witnessis.
12 Mke wa Potifa akashika vazi Yosefu alilokuwa amevaa, akamwambia, “Njoo tukutane kimwili!” Lakini Yosefu akaacha vazi lake mkononi mwa huyo mwanamke, akatoka nje ya nyumba akikimbia.
And sche took `the hem of his clooth, and sche seide, Slepe thou with me; and he lefte the mentil in hir hoond, and he fledde, and yede out.
13 Yule mwanamke alipoona kwamba Yosefu amemwachia vazi lake mkononi na kukimbilia nje ya nyumba,
And whanne the womman hadde seyn the clooth in hir hondis, and that sche was dispisid,
14 akawaita watumishi wake wa nyumbani, akawaambia, “Tazameni! Huyu Mwebrania ameletwa hapa kutudhihaki! Aliingia hapa ndani ili akutane nami kimwili, lakini nikapiga kelele.
sche clepide to hir the men of hir hows, and seide to hem, Lo! my lord hath brouyt in an Ebrew man, that he schulde scorn vs; he entride to me to do leccherie with me, and whanne Y criede, and he herde my vois,
15 Aliposikia kelele za kuomba msaada, akaacha vazi lake kando yangu akakimbilia nje.”
he lefte the mentil which Y helde, and he fledde out.
16 Yule mwanamke akaliweka lile vazi karibu naye mpaka Potifa aliporudi nyumbani.
Therfor in to the preuyng of trouthe, sche schewide the mantil, holdun to the hosebonde turnynge ayen hoom.
17 Ndipo akamweleza kisa hiki, akisema: “Yule mtumwa wa Kiebrania uliyetuletea alinijia ili kunidhihaki.
And she seide, The Ebrew seruaunt, whom thou brouytist, entride to me to scorne me; and whanne he siy me crye,
18 Lakini mara nilipopiga kelele kuomba msaada, akaliacha vazi lake kando yangu akakimbia nje ya nyumba.”
he lefte the mentil which Y helde, and he fledde out.
19 Potifa aliposikia kisa hiki mkewe alichomweleza, akisema, “Hivi ndivyo mtumwa wako alivyonitenda.” Hasira ya Potifa ikawaka.
And whanne these thingis weren herd, the lord bileuyde ouer myche to the wordis of the wijf, and was ful wrooth;
20 Potifa akamchukua Yosefu na kumweka gerezani, mahali ambapo wahalifu wa mfalme walikuwa wamefungwa. Lakini wakati Yosefu alipokuwa huko gerezani,
and he bitook Joseph in to prisoun, where the bounden men of the kyng weren kept, and he was closid there.
21 Bwana alikuwa pamoja naye, akamhurumia na kumpa kibali mbele ya msimamizi wa gereza.
Forsothe the Lord was with Joseph, and hadde mercy on hym, and yaf grace to hym in the siyt of the prince of the prisoun,
22 Kwa hiyo msimamizi wa gereza akamweka Yosefu awe mkuu wa wafungwa pamoja na kusimamia yote ambayo yalitendeka mle gerezani.
which bitook in the hond of Joseph alle prisoneris that weren holdun in kepyng, and what euer thing was doon, it was vndur Joseph, nethir the prince knewe ony thing,
23 Msimamizi wa gereza hakujishughulisha tena na kitu chochote kilichokuwa chini ya uangalizi wa Yosefu, kwa sababu Bwana alikuwa pamoja na Yosefu akimfanikisha kwa kila alichofanya.
for alle thingis weren bitakun to Joseph; for the Lord was with hym, and dresside alle his werkis.

< Mwanzo 39 >