< Mwanzo 39 >

1 Wakati huu Yosefu alikuwa amechukuliwa mpaka Misri. Mmisri aliyeitwa Potifa aliyekuwa mmojawapo wa maafisa wa Farao, mkuu wa ulinzi, akamnunua Yosefu kutoka kwa Waishmaeli waliomleta Misri.
And Joseph was brought down to Egypt. And Potiphar, an officer of Pharaoh's, the captain of the guard, an Egyptian, bought him from the hand of the Ishmaelites, who had brought him down there.
2 Bwana alikuwa pamoja na Yosefu, naye akastawi, Yosefu akaishi nyumbani kwa bwana wake Mmisri.
And Jehovah was with Joseph. And he was a man who succeeds. And he was in the house of his master the Egyptian.
3 Potifa alipoona kuwa Bwana alikuwa pamoja na Yosefu na kwamba Bwana alimfanikisha kwa kila kitu alichokifanya,
And his master saw that Jehovah was with him, and that Jehovah made all that he did to prosper in his hand.
4 Yosefu alipata kibali machoni pa Potifa, akamfanya mhudumu wake. Potifa akamweka kuwa msimamizi wa nyumba yake, naye akamkabidhi kuwa mwangalizi wa kila kitu alichokuwa nacho.
And Joseph found favor in his sight, and he ministered to him. And he made him overseer over his house, and all that he had he put into his hand.
5 Kuanzia wakati huo Potifa alipomweka Yosefu kuwa msimamizi wa nyumba na mali zake zote alizokuwa nazo, Bwana aliibariki nyumba ya Mmisri huyo kwa sababu ya Yosefu. Baraka ya Bwana ilikuwa juu ya kila kitu alichokuwa nacho Potifa, nyumbani na shambani.
And it came to pass from the time that he made him overseer in his house, and over all that he had, that Jehovah blessed the Egyptian's house for Joseph's sake. And the blessing of Jehovah was upon all that he had, in the house and in the field.
6 Kwa hiyo Potifa akamwachia Yosefu uangalizi wa kila kitu alichokuwa nacho, Yosefu alipokuwa katika uongozi, Potifa hakuwa na sababu ya kujishughulisha na kitu chochote isipokuwa chakula alichokula. Yosefu alikuwa mwenye umbo zuri na sura ya kuvutia;
And he left all that he had in Joseph's hand, and he knew nothing that was with him, save the bread which he ate. And Joseph was comely, and well-favored.
7 baada ya kitambo mke wa Potifa akamtamani Yosefu, akamwambia, “Njoo, ukutane nami kimwili!”
And it came to pass, after these things, that his master's wife cast her eyes upon Joseph, and she said, Lie with me.
8 Lakini Yosefu akakataa. Akamwambia yule mwanamke, “Mimi nikiwa katika uongozi, bwana wangu hahusiki na kitu chochote katika nyumba hii, kila kitu alicho nacho amenikabidhi.
But he refused, and said to his master's wife, Behold, my master does not know what is with me in the house, and he has put all that he has into my hand.
9 Hapa nyumbani hakuna aliye mkuu kuliko mimi. Bwana wangu hakunizuilia kitu chochote isipokuwa wewe, kwa kuwa wewe ni mke wake. Nitawezaje basi kufanya uovu huu na kutenda dhambi dhidi ya Mungu?”
He is not greater in this house than I, nor has he kept back anything from me but thee, because thou are his wife. How then can I do this great wickedness, and sin against God?
10 Ingawa yule mwanamke aliendelea kumshawishi Yosefu siku baada ya siku, Yosefu alikataa kukutana naye kimwili wala kukaa karibu naye.
And it came to pass, as she spoke to Joseph day by day, that he did not hearken to her, to lie by her, or to be with her.
11 Siku moja Yosefu akaingia ndani ya nyumba kufanya kazi zake, wala hapakuwepo na mfanyakazi yeyote ndani ya nyumba.
And it came to pass, about this time, that he went into the house to do his work, and there was none of the men of the house there inside.
12 Mke wa Potifa akashika vazi Yosefu alilokuwa amevaa, akamwambia, “Njoo tukutane kimwili!” Lakini Yosefu akaacha vazi lake mkononi mwa huyo mwanamke, akatoka nje ya nyumba akikimbia.
And she caught him by his garment, saying, Lie with me. And he left his garment in her hand, and fled, and got out.
13 Yule mwanamke alipoona kwamba Yosefu amemwachia vazi lake mkononi na kukimbilia nje ya nyumba,
And it came to pass, when she saw that he had left his garment in her hand, and was fled forth,
14 akawaita watumishi wake wa nyumbani, akawaambia, “Tazameni! Huyu Mwebrania ameletwa hapa kutudhihaki! Aliingia hapa ndani ili akutane nami kimwili, lakini nikapiga kelele.
that she called to the men of her house, and spoke to them, saying, See, he has brought in a Hebrew to us to mock us. He came in to me to lie with me, and I cried with a loud voice.
15 Aliposikia kelele za kuomba msaada, akaacha vazi lake kando yangu akakimbilia nje.”
And it came to pass, when he heard that I lifted up my voice and cried, that he left his garment by me, and fled, and got out.
16 Yule mwanamke akaliweka lile vazi karibu naye mpaka Potifa aliporudi nyumbani.
And she laid up his garment by her until his master came home.
17 Ndipo akamweleza kisa hiki, akisema: “Yule mtumwa wa Kiebrania uliyetuletea alinijia ili kunidhihaki.
And she spoke to him according to these words, saying, The Hebrew servant, whom thou have brought to us, came in to me to mock me.
18 Lakini mara nilipopiga kelele kuomba msaada, akaliacha vazi lake kando yangu akakimbia nje ya nyumba.”
And it came to pass, as I lifted up my voice and cried, that he left his garment by me, and fled out.
19 Potifa aliposikia kisa hiki mkewe alichomweleza, akisema, “Hivi ndivyo mtumwa wako alivyonitenda.” Hasira ya Potifa ikawaka.
And it came to pass, when his master heard the words of his wife, which she spoke to him, saying, After this manner did thy servant to me, that his wrath was kindled.
20 Potifa akamchukua Yosefu na kumweka gerezani, mahali ambapo wahalifu wa mfalme walikuwa wamefungwa. Lakini wakati Yosefu alipokuwa huko gerezani,
And Joseph's master took him, and put him into the prison, the place where the king's prisoners were bound. And he was there in the prison.
21 Bwana alikuwa pamoja naye, akamhurumia na kumpa kibali mbele ya msimamizi wa gereza.
But Jehovah was with Joseph, and showed kindness to him, and gave him favor in the sight of the keeper of the prison.
22 Kwa hiyo msimamizi wa gereza akamweka Yosefu awe mkuu wa wafungwa pamoja na kusimamia yote ambayo yalitendeka mle gerezani.
And the keeper of the prison committed to Joseph's hand all the prisoners who were in the prison. And whatever they did there, he was the doer of it.
23 Msimamizi wa gereza hakujishughulisha tena na kitu chochote kilichokuwa chini ya uangalizi wa Yosefu, kwa sababu Bwana alikuwa pamoja na Yosefu akimfanikisha kwa kila alichofanya.
The keeper of the prison did not look to anything that was under his hand, because Jehovah was with him, and that which he did, Jehovah made it prosper.

< Mwanzo 39 >