< Mwanzo 38 >

1 Wakati ule, Yuda akawaacha ndugu zake, akaenda kuishi na Hira Mwadulami.
Pripetilo se je ob tistem času, da je Juda šel dol od svojih bratov in vstopil k nekemu Adulámcu, katerega ime je bilo Hirá.
2 Huko Yuda akakutana na binti wa Kikanaani aitwaye Shua, akamwoa na akakutana naye kimwili,
Juda je tam videl hčer nekega Kánaanca, katerega ime je bilo Šua in vzel jo je ter šel noter k njej.
3 akapata mimba, akamzaa mwana, ambaye alimwita Eri.
Ta je spočela in rodila sina in njegovo ime je imenoval Er.
4 Akapata mimba tena, akamzaa mwana na kumwita Onani.
Ponovno je spočela ter rodila sina in njegovo ime je imenovala Onán.
5 Akamzaa mwana mwingine tena, akamwita Shela. Huyu alimzalia mahali paitwapo Kezibu.
Spet je spočela in rodila sina in njegovo ime je imenovala Šelá. Bil je pri Kezíbu, ko ga je rodila.
6 Yuda akampatia Eri, mzaliwa wake wa kwanza, mke aitwaye Tamari.
Juda je vzel ženo za svojega prvorojenca Era, ki ji je bilo ime Tamara.
7 Lakini Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mwovu machoni pa Bwana, kwa hiyo Bwana akamuua.
Judov prvorojenec Er pa je bil zloben v Gospodovih očeh in Gospod ga je usmrtil.
8 Kisha Yuda akamwambia Onani, “Kutana kimwili na mke wa ndugu yako, na utimize wajibu wako kwake kama mke wa ndugu yako, ili umpatie ndugu yako uzao.”
Juda je rekel Onánu: »Pojdi noter k ženi svojega brata in jo poroči ter svojemu bratu obudi potomca.«
9 Lakini Onani alijua kwamba uzao haungekuwa wake, kwa hiyo kila alipokutana kimwili na mke wa ndugu yake, alimwaga chini mbegu za kiume ili asimpatie ndugu yake uzao.
Onán pa je vedel, da potomec ne bo njegov in pripetilo se je, ko je šel noter k ženi svojega brata, da je to izlil na tla, da svojemu bratu ne bi dal potomca.
10 Alichofanya kilikuwa kiovu machoni pa Bwana, hivyo, pia Bwana akamuua Onani.
Stvar, ki jo je storil, je razžalila Gospoda, zaradi česar je tudi njega usmrtil.
11 Kisha Yuda akamwambia Tamari mkwewe, “Ishi kama mjane nyumbani mwa baba yako mpaka mwanangu Shela atakapokua.” Kwa maana alifikiri, “Angeweza kufa pia kama ndugu zake.” Kwa hiyo Tamari alikwenda kuishi nyumbani kwa baba yake.
Potem je Juda rekel svoji snahi Tamari: »Ostani vdova, v hiši svojega očeta, dokler moj sin Šelá ne odraste, « kajti rekel je: »Da ne bi morda tudi on umrl, kakor sta njegova brata.« Tamara je odšla in prebivala v hiši svojega očeta.
12 Baada ya muda mrefu mke wa Yuda binti wa Shua akafariki. Baada ya msiba, Yuda alikwenda Timna, kwa watu waliokuwa wakikata kondoo wake manyoya, naye alifuatana na rafiki yake Hira Mwadulami.
Tekom časa je Šuova hči, Judova žena, umrla in Juda je bil potolažen in se dvignil k svojim strižcem ovc v Timno, on in njegov prijatelj Adulámec Hirá.
13 Tamari alipoambiwa, “Baba mkwe wako yuko njiani kwenda Timna kukata kondoo wake manyoya,”
To je bilo povedano Tamari, rekoč: »Glej, tvoj tast gre v Timno, da ostriže svoje ovce.«
14 alivua mavazi yake ya ujane, akajifunika kwa shela ili asifahamike, akaketi kwenye mlango wa Enaimu, ambao upo njiani kuelekea Timna. Akafanya hivyo kwa sababu aliona kwamba, ingawa Shela amekua, lakini alikuwa hajakabidhiwa kwake kuwa mkewe.
Iz sebe je odložila svoje vdovske obleke, se pokrila z zagrinjalom, se ogrnila in sedla na odprt kraj, ki je na poti v Timno, kajti videla je, da je Šelá odrastel, pa mu ni bila dana za ženo.
15 Yuda alipomwona alifikiri ni kahaba, kwa sababu alikuwa amefunika uso wake.
Ko jo je Juda zagledal, je mislil, da je pocestnica, ker je imela svoj obraz zakrit.
16 Pasipo kutambua kwamba alikuwa mkwe wake, akamwendea kando ya njia na kumwambia, “Njoo sasa, nikutane na wewe kimwili.” Yule mkwewe akamuuliza, “Utanipa nini nikikutana nawe kimwili?”
Na poti se je obrnil k njej in rekel: »Daj, prosim te, naj pridem noter vate, « (kajti ni vedel, da je bila njegova snaha.) Ona pa je rekla: »Kaj mi hočeš dati, da lahko prideš vame?«
17 Akamwambia, “Nitakutumia mwana-mbuzi kutoka kundi langu.” Akamuuliza, “Utanipa kitu chochote kama amana mpaka utakapompeleka?”
Rekel je: »Poslal ti bom kozlička od tropa.« Rekla je: »Ali mi boš dal jamstvo, dokler ga ne pošlješ?«
18 Akamuuliza, “Nikupe amana gani?” Akamjibu, “Pete yako na kamba yake pamoja na fimbo iliyo mkononi mwako.” Kwa hiyo akampa vitu hivyo kisha akakutana naye kimwili, naye akapata mimba yake.
Rekel je: »Kakšno jamstvo naj ti dam?« Rekla je: »Svoj pečat in svoje okrasne vrvice in svojo palico, ki je v tvoji roki.« To ji je dal in prišel noter vanjo in ta je spočela z njim.
19 Tamari akaondoka, akavua shela yake akavaa tena nguo zake za ujane.
Vstala je ter odšla proč in poleg sebe položila svoje zagrinjalo iz sebe in si nadela obleke svojega vdovstva.
20 Wakati ule ule, Yuda akamtuma rafiki yake Mwadulami apeleke yule mwana-mbuzi ili arudishiwe amana yake kutoka kwa yule mwanamke, lakini yule rafiki yake hakumkuta yule mwanamke.
Juda je poslal kozlička po roki svojega prijatelja Adulámca, da prejme svoje jamstvo iz roke ženske, toda ta je ni našel.
21 Akawauliza watu wanaoishi mahali pale, “Yuko wapi yule kahaba wa mahali pa kuabudia miungu aliyekuwa kando ya barabara hapa Enaimu?” Wakamjibu, “Hajawahi kuwepo mwanamke yeyote kahaba wa mahali pa kuabudia miungu hapa.”
Potem je vprašal ljudi tega kraja, rekoč: »Kje je pocestnica, ki je bila javno poleg poti?« Rekli so: »Na tem kraju ni bilo nobene pocestnice.«
22 Kwa hiyo akamrudia Yuda na kumwambia, “Sikumpata. Zaidi ya hayo, watu wanaoishi mahali pale walisema ‘Hapakuwahi kuwepo mwanamke yeyote kahaba wa mahali pa kuabudia miungu hapa.’”
Vrnil se je k Judu in rekel: »Ne morem je najti in tudi ljudje tega kraja so rekli, da na tem kraju ni bilo nobene pocestnice.«
23 Kisha Yuda akasema, “Mwache avichukue vitu hivyo, ama sivyo tutakuwa kichekesho. Hata hivyo, nilimpelekea mwana-mbuzi, lakini hukumkuta.”
Juda je rekel: »Naj si ona to vzame k sebi, da ne bova osramočena. Glej, poslal sem tega kozlička, ti pa je nisi našel.«
24 Baada ya miezi mitatu Yuda akaambiwa, “Tamari mkweo ana hatia ya kuwa kahaba, na matokeo yake ana mimba.” Yuda akasema, “Mtoeni nje na achomwe moto hadi afe!”
Pripetilo se je približno tri mesece kasneje, da je bilo Judu povedano, rekoč: »Tvoja snaha Tamara je igrala pocestnico in prav tako poglej, ona je z otrokom od vlačugarstva.« Juda je rekel: »Privedite jo naprej in naj bo sežgana.«
25 Alipokuwa akitolewa nje, akatuma ujumbe kwa baba mkwe wake kusema, “Nina mimba ya mtu mwenye vitu hivi.” Akaongeza kusema, “Angalia kama utatambua kwamba pete hii na kamba yake pamoja na fimbo hii ni vya nani.”
Ko je bila privedena naprej, je poslala k svojemu tastu, rekoč: »Po moškem, čigar [last] je to, sem z otrokom.« Rekla je: »Razpoznaj, prosim te, čigav je ta pečat, okrasne vrvice in palica.«
26 Yuda akavitambua na kusema, “Yeye ana haki kuliko mimi, kwa kuwa sikumkabidhi kwa mwanangu Shela ili awe mkewe.” Tangu hapo hakukutana naye kimwili tena.
Juda jim je priznal in rekel: »Bolj pravična je bila kakor jaz, zato ker je nisem dal svojemu sinu Šeláju.« In ni je več ponovno spoznal.
27 Wakati ulipofika wa kujifungua, kukawa na wana mapacha tumboni mwake.
Pripetilo pa se je v času njenih porodnih muk, glej, da sta bila v njeni maternici dvojčka.
28 Alipokuwa akijifungua, mmoja akatoa mkono wake nje, kwa hiyo mkunga akachukua uzi mwekundu na kuufunga mkononi mwa yule mtoto, akasema, “Huyu ametoka kwanza.”
Ko je bila v porodnih mukah se je pripetilo, da je eden iztegnil svojo roko in babica je prijela ter na njegovo roko privezala škrlatno nit, rekoč: »Ta je prvi prišel ven.«
29 Lakini alipourudisha mkono wake ndugu yake akaanza kutoka, naye akasema, “Hivi ndivyo ulivyotoka kwa nguvu!” Akaitwa Peresi.
Pripetilo pa se je, ko je svojo roko potegnil nazaj, glej, je prišel ven njegov brat. Rekla je: »Kako si izbruhnil? Ta prodor bodi na tebi.« Zato je bilo njegovo ime imenovano Parec.
30 Kisha ndugu yake, aliyekuwa na uzi mwekundu mkononi, akatoka, naye akaitwa Zera.
Nato je prišel ven njegov brat, ki je imel na svoji roki škrlatno nit in njegovo ime je bilo imenovano Zerah.

< Mwanzo 38 >