< Mwanzo 38 >

1 Wakati ule, Yuda akawaacha ndugu zake, akaenda kuishi na Hira Mwadulami.
Et il arriva, dans ce temps-là, que Juda descendit d’auprès de ses frères, et se retira vers un homme adullamite, nommé Hira.
2 Huko Yuda akakutana na binti wa Kikanaani aitwaye Shua, akamwoa na akakutana naye kimwili,
Et Juda y vit la fille d’un homme cananéen, et son nom était Shua; et il la prit, et vint vers elle.
3 akapata mimba, akamzaa mwana, ambaye alimwita Eri.
Et elle conçut, et enfanta un fils, et on appela son nom Er.
4 Akapata mimba tena, akamzaa mwana na kumwita Onani.
Et elle conçut encore, et enfanta un fils, et elle appela son nom Onan.
5 Akamzaa mwana mwingine tena, akamwita Shela. Huyu alimzalia mahali paitwapo Kezibu.
Et elle enfanta encore un fils, et elle appela son nom Shéla. Et [Juda] était à Kezib quand elle l’enfanta.
6 Yuda akampatia Eri, mzaliwa wake wa kwanza, mke aitwaye Tamari.
Et Juda prit pour Er, son premier-né, une femme qui se nommait Tamar.
7 Lakini Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mwovu machoni pa Bwana, kwa hiyo Bwana akamuua.
Et Er, premier-né de Juda, était méchant aux yeux de l’Éternel, et l’Éternel le fit mourir.
8 Kisha Yuda akamwambia Onani, “Kutana kimwili na mke wa ndugu yako, na utimize wajibu wako kwake kama mke wa ndugu yako, ili umpatie ndugu yako uzao.”
Et Juda dit à Onan: Va vers la femme de ton frère, et remplis envers elle le devoir de beau-frère, et suscite de la semence à ton frère.
9 Lakini Onani alijua kwamba uzao haungekuwa wake, kwa hiyo kila alipokutana kimwili na mke wa ndugu yake, alimwaga chini mbegu za kiume ili asimpatie ndugu yake uzao.
Et Onan savait que la semence ne serait pas à lui; et il arriva que lorsqu’il entra vers la femme de son frère, il perdit sur la terre, pour ne pas donner de semence à son frère.
10 Alichofanya kilikuwa kiovu machoni pa Bwana, hivyo, pia Bwana akamuua Onani.
Et ce qu’il faisait fut mauvais aux yeux de l’Éternel, et il le fit mourir aussi.
11 Kisha Yuda akamwambia Tamari mkwewe, “Ishi kama mjane nyumbani mwa baba yako mpaka mwanangu Shela atakapokua.” Kwa maana alifikiri, “Angeweza kufa pia kama ndugu zake.” Kwa hiyo Tamari alikwenda kuishi nyumbani kwa baba yake.
Et Juda dit à Tamar, sa belle-fille: Demeure veuve dans la maison de ton père, jusqu’à ce que Shéla, mon fils, soit devenu grand; car il dit: De peur qu’il ne meure, lui aussi, comme ses frères. Et Tamar s’en alla, et demeura dans la maison de son père.
12 Baada ya muda mrefu mke wa Yuda binti wa Shua akafariki. Baada ya msiba, Yuda alikwenda Timna, kwa watu waliokuwa wakikata kondoo wake manyoya, naye alifuatana na rafiki yake Hira Mwadulami.
Et les jours se multiplièrent, et la fille de Shua, femme de Juda, mourut; et Juda se consola, et monta à Thimna, lui et Hira, l’Adullamite, son ami, vers les tondeurs de son troupeau.
13 Tamari alipoambiwa, “Baba mkwe wako yuko njiani kwenda Timna kukata kondoo wake manyoya,”
Et on l’annonça à Tamar, en disant: Voici, ton beau-père monte à Thimna pour tondre son troupeau.
14 alivua mavazi yake ya ujane, akajifunika kwa shela ili asifahamike, akaketi kwenye mlango wa Enaimu, ambao upo njiani kuelekea Timna. Akafanya hivyo kwa sababu aliona kwamba, ingawa Shela amekua, lakini alikuwa hajakabidhiwa kwake kuwa mkewe.
Et elle ôta de dessus elle les vêtements de son veuvage, et se couvrit d’un voile, et s’enveloppa, et s’assit à l’entrée d’Énaïm, qui était sur le chemin de Thimna; car elle voyait que Shéla était devenu grand, et qu’elle ne lui était pas donnée pour femme.
15 Yuda alipomwona alifikiri ni kahaba, kwa sababu alikuwa amefunika uso wake.
Et Juda la vit, et la tint pour une prostituée, car elle avait couvert son visage.
16 Pasipo kutambua kwamba alikuwa mkwe wake, akamwendea kando ya njia na kumwambia, “Njoo sasa, nikutane na wewe kimwili.” Yule mkwewe akamuuliza, “Utanipa nini nikikutana nawe kimwili?”
Et il se détourna vers elle, dans le chemin, et dit: Permets, je te prie, que je vienne vers toi. Car il ne savait pas que c’était sa belle-fille. Et elle dit: Que me donneras-tu, afin que tu viennes vers moi?
17 Akamwambia, “Nitakutumia mwana-mbuzi kutoka kundi langu.” Akamuuliza, “Utanipa kitu chochote kama amana mpaka utakapompeleka?”
Et il dit: J’enverrai un chevreau du troupeau. Et elle dit: [Me] donneras-tu un gage, jusqu’à ce que tu l’envoies?
18 Akamuuliza, “Nikupe amana gani?” Akamjibu, “Pete yako na kamba yake pamoja na fimbo iliyo mkononi mwako.” Kwa hiyo akampa vitu hivyo kisha akakutana naye kimwili, naye akapata mimba yake.
Et il dit: Quel gage te donnerai-je? Et elle dit: Ton cachet, et ton cordon, et ton bâton qui est en ta main. Et il [les] lui donna; et il vint vers elle, et elle conçut de lui.
19 Tamari akaondoka, akavua shela yake akavaa tena nguo zake za ujane.
Et elle se leva et s’en alla, et ôta son voile de dessus elle, et revêtit les vêtements de son veuvage.
20 Wakati ule ule, Yuda akamtuma rafiki yake Mwadulami apeleke yule mwana-mbuzi ili arudishiwe amana yake kutoka kwa yule mwanamke, lakini yule rafiki yake hakumkuta yule mwanamke.
Et Juda envoya le chevreau par la main de son ami, l’Adullamite, pour recevoir le gage de la main de la femme; mais il ne la trouva pas.
21 Akawauliza watu wanaoishi mahali pale, “Yuko wapi yule kahaba wa mahali pa kuabudia miungu aliyekuwa kando ya barabara hapa Enaimu?” Wakamjibu, “Hajawahi kuwepo mwanamke yeyote kahaba wa mahali pa kuabudia miungu hapa.”
Et il interrogea les hommes du lieu, disant: Où est cette prostituée qui était à Énaïm, sur le chemin? Et ils dirent: Il n’y a pas eu ici de prostituée.
22 Kwa hiyo akamrudia Yuda na kumwambia, “Sikumpata. Zaidi ya hayo, watu wanaoishi mahali pale walisema ‘Hapakuwahi kuwepo mwanamke yeyote kahaba wa mahali pa kuabudia miungu hapa.’”
Et il retourna vers Juda, et dit: Je ne l’ai pas trouvée, et aussi les gens du lieu m’ont dit: Il n’y a pas eu ici de prostituée.
23 Kisha Yuda akasema, “Mwache avichukue vitu hivyo, ama sivyo tutakuwa kichekesho. Hata hivyo, nilimpelekea mwana-mbuzi, lakini hukumkuta.”
Et Juda dit: Qu’elle prenne le [gage] pour elle, de peur que nous ne soyons en mépris. Voici, j’ai envoyé ce chevreau, et toi tu ne l’as pas trouvée.
24 Baada ya miezi mitatu Yuda akaambiwa, “Tamari mkweo ana hatia ya kuwa kahaba, na matokeo yake ana mimba.” Yuda akasema, “Mtoeni nje na achomwe moto hadi afe!”
Et il arriva, environ trois mois après, qu’on informa Juda, en disant: Tamar, ta belle-fille, s’est prostituée, et voici, elle est même enceinte par la prostitution. Et Juda dit: Faites-la sortir, et qu’elle soit brûlée.
25 Alipokuwa akitolewa nje, akatuma ujumbe kwa baba mkwe wake kusema, “Nina mimba ya mtu mwenye vitu hivi.” Akaongeza kusema, “Angalia kama utatambua kwamba pete hii na kamba yake pamoja na fimbo hii ni vya nani.”
Comme on la faisait sortir, elle envoya vers son beau-père, disant: C’est de l’homme à qui appartiennent ces choses que je suis enceinte. Et elle dit: Reconnais, je te prie, à qui est ce cachet, et ce cordon, et ce bâton.
26 Yuda akavitambua na kusema, “Yeye ana haki kuliko mimi, kwa kuwa sikumkabidhi kwa mwanangu Shela ili awe mkewe.” Tangu hapo hakukutana naye kimwili tena.
Et Juda [les] reconnut, et dit: Elle est plus juste que moi; parce que je ne l’ai pas donnée à Shéla, mon fils. Et il ne la connut plus.
27 Wakati ulipofika wa kujifungua, kukawa na wana mapacha tumboni mwake.
Et il arriva, au temps où elle enfanta, que voici, des jumeaux étaient dans son ventre;
28 Alipokuwa akijifungua, mmoja akatoa mkono wake nje, kwa hiyo mkunga akachukua uzi mwekundu na kuufunga mkononi mwa yule mtoto, akasema, “Huyu ametoka kwanza.”
et il arriva, comme elle enfantait, que [l’un d’eux] tendit la main; et la sage-femme la prit, et lia sur sa main un fil écarlate, en disant: Celui-ci sort le premier.
29 Lakini alipourudisha mkono wake ndugu yake akaanza kutoka, naye akasema, “Hivi ndivyo ulivyotoka kwa nguvu!” Akaitwa Peresi.
Et il arriva, comme il retira sa main, que voici, son frère sortit; et elle dit: Quelle brèche tu as faite! La brèche est sur toi. Et on appela son nom Pérets.
30 Kisha ndugu yake, aliyekuwa na uzi mwekundu mkononi, akatoka, naye akaitwa Zera.
Et ensuite sortit son frère, sur la main duquel était le fil écarlate; et on appela son nom Zérakh.

< Mwanzo 38 >