< Mwanzo 38 >

1 Wakati ule, Yuda akawaacha ndugu zake, akaenda kuishi na Hira Mwadulami.
And it fortuned at that tyme that Iudas went from his brethren and gatt him to a man called Hira of Odollam
2 Huko Yuda akakutana na binti wa Kikanaani aitwaye Shua, akamwoa na akakutana naye kimwili,
and there he sawe the doughter of a man called Sua a Canaanyte. And he toke her ad went in vnto her.
3 akapata mimba, akamzaa mwana, ambaye alimwita Eri.
And she conceaued and bare a sonne and called his name Er.
4 Akapata mimba tena, akamzaa mwana na kumwita Onani.
And she conceaued agayne and bare a sonne and called him Onan.
5 Akamzaa mwana mwingine tena, akamwita Shela. Huyu alimzalia mahali paitwapo Kezibu.
And she conceaued the thyrde tyme and bare a sonne whom she called Scla: and he was at Chesyb when she bare hem.
6 Yuda akampatia Eri, mzaliwa wake wa kwanza, mke aitwaye Tamari.
And Iudas gaue Er his eldest sonne a wife whose name was Thamar.
7 Lakini Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mwovu machoni pa Bwana, kwa hiyo Bwana akamuua.
But this Er Iudas eldest sonne was wicked in the syghte of the LORde wherfore the LORde slewe him.
8 Kisha Yuda akamwambia Onani, “Kutana kimwili na mke wa ndugu yako, na utimize wajibu wako kwake kama mke wa ndugu yako, ili umpatie ndugu yako uzao.”
Than sayde Iudas vnto Onan: goo in to thi brothers wyfe and Marie her and styrre vp seed vnto thy brother.
9 Lakini Onani alijua kwamba uzao haungekuwa wake, kwa hiyo kila alipokutana kimwili na mke wa ndugu yake, alimwaga chini mbegu za kiume ili asimpatie ndugu yake uzao.
And when Onan perceaued that the seed shulde not be his: therfore when he went in to his brothers wife he spylled it on the grounde because he wold not geue seed vnto his brother.
10 Alichofanya kilikuwa kiovu machoni pa Bwana, hivyo, pia Bwana akamuua Onani.
And the thinge which he dyd displeased the LORde wherfore he slew him also.
11 Kisha Yuda akamwambia Tamari mkwewe, “Ishi kama mjane nyumbani mwa baba yako mpaka mwanangu Shela atakapokua.” Kwa maana alifikiri, “Angeweza kufa pia kama ndugu zake.” Kwa hiyo Tamari alikwenda kuishi nyumbani kwa baba yake.
Than sayde Iudas to Thamar his doughter in lawe: remayne a wydow at thi fathers house tyll Sela my sonne be growne: for he feared lest he shulde haue dyed also as his brethren did. Thus went Thamar and dwelt in hir fathers house.
12 Baada ya muda mrefu mke wa Yuda binti wa Shua akafariki. Baada ya msiba, Yuda alikwenda Timna, kwa watu waliokuwa wakikata kondoo wake manyoya, naye alifuatana na rafiki yake Hira Mwadulami.
And in processe of tyme the doughter of Sua Iudas wife dyed. Than Iudas when he had left mornynge went vnto his shepe sherers to Thimnath with his frende Hira of Odollam.
13 Tamari alipoambiwa, “Baba mkwe wako yuko njiani kwenda Timna kukata kondoo wake manyoya,”
And one told Thamar saynge: beholde thy father in lawe goth vp to Thimnath to shere his shepe.
14 alivua mavazi yake ya ujane, akajifunika kwa shela ili asifahamike, akaketi kwenye mlango wa Enaimu, ambao upo njiani kuelekea Timna. Akafanya hivyo kwa sababu aliona kwamba, ingawa Shela amekua, lakini alikuwa hajakabidhiwa kwake kuwa mkewe.
And she put hyr wydows garmetes of from her and couered her with a clooke and disgyssed herself: And sat her downe at the entrynge of Enaim which is by the hye wayes syde to Thimnath for because she sawe that Sela was growne and she was not geue vnto him to wife.
15 Yuda alipomwona alifikiri ni kahaba, kwa sababu alikuwa amefunika uso wake.
When Iuda sawe her he thought it had bene an hoore because she had couered hyr face.
16 Pasipo kutambua kwamba alikuwa mkwe wake, akamwendea kando ya njia na kumwambia, “Njoo sasa, nikutane na wewe kimwili.” Yule mkwewe akamuuliza, “Utanipa nini nikikutana nawe kimwili?”
And turned to her vnto the waye and sayde come I praye the let me lye with the for he knewe not that it was his doughter in lawe. And she sayde what wylt thou gyue me for to lye with me?
17 Akamwambia, “Nitakutumia mwana-mbuzi kutoka kundi langu.” Akamuuliza, “Utanipa kitu chochote kama amana mpaka utakapompeleka?”
Tha sayde he I will sende the a kydd fro the flocke. She answered Than geue me a pledge till thou sende it.
18 Akamuuliza, “Nikupe amana gani?” Akamjibu, “Pete yako na kamba yake pamoja na fimbo iliyo mkononi mwako.” Kwa hiyo akampa vitu hivyo kisha akakutana naye kimwili, naye akapata mimba yake.
Than sayde he what pledge shall I geue the? And she sayde: they sygnett thy necke lace and thy staffe that is in thy hande. And he gaue it her and lay by her and she was with child by him.
19 Tamari akaondoka, akavua shela yake akavaa tena nguo zake za ujane.
And she gatt her vp and went and put her mantell from her ad put on hir widowes rayment agayne.
20 Wakati ule ule, Yuda akamtuma rafiki yake Mwadulami apeleke yule mwana-mbuzi ili arudishiwe amana yake kutoka kwa yule mwanamke, lakini yule rafiki yake hakumkuta yule mwanamke.
And Iudas sent the kydd by his neybure of Odollam for to fetch out his pledge agayne from the wifes hande. But he fownde her not.
21 Akawauliza watu wanaoishi mahali pale, “Yuko wapi yule kahaba wa mahali pa kuabudia miungu aliyekuwa kando ya barabara hapa Enaimu?” Wakamjibu, “Hajawahi kuwepo mwanamke yeyote kahaba wa mahali pa kuabudia miungu hapa.”
Than asked he the men of the same place saynge: where is the whoore that satt at Enaim in the waye? And they sayde: there was no whoore here.
22 Kwa hiyo akamrudia Yuda na kumwambia, “Sikumpata. Zaidi ya hayo, watu wanaoishi mahali pale walisema ‘Hapakuwahi kuwepo mwanamke yeyote kahaba wa mahali pa kuabudia miungu hapa.’”
And he came to Iuda agayne saynge: I can not fynde her and also the men of the place sayde: that there was no whoore there.
23 Kisha Yuda akasema, “Mwache avichukue vitu hivyo, ama sivyo tutakuwa kichekesho. Hata hivyo, nilimpelekea mwana-mbuzi, lakini hukumkuta.”
And Iuda sayde: let her take it to her lest we be shamed: for I sente the kydd and thou coudest not fynde her.
24 Baada ya miezi mitatu Yuda akaambiwa, “Tamari mkweo ana hatia ya kuwa kahaba, na matokeo yake ana mimba.” Yuda akasema, “Mtoeni nje na achomwe moto hadi afe!”
And it came to passe that after. iij. monethes one tolde Iuda saynge: Thamar thy doughter in lawe hath played the whoore and with playnge the whoore is become great with childe. And Iuda sayde: brynge her forth ad let her be brente.
25 Alipokuwa akitolewa nje, akatuma ujumbe kwa baba mkwe wake kusema, “Nina mimba ya mtu mwenye vitu hivi.” Akaongeza kusema, “Angalia kama utatambua kwamba pete hii na kamba yake pamoja na fimbo hii ni vya nani.”
And when they brought her forth she sent to her father in lawe saynge: by the ma vnto whome these thinges pertayne am I with childe. And sayd also: loke whose are this seall necklace and staffe.
26 Yuda akavitambua na kusema, “Yeye ana haki kuliko mimi, kwa kuwa sikumkabidhi kwa mwanangu Shela ili awe mkewe.” Tangu hapo hakukutana naye kimwili tena.
And Iuda knewe them saynge: she is more rightwes tha I because I gaue her not to Sela my sone. But he laye with her nomore.
27 Wakati ulipofika wa kujifungua, kukawa na wana mapacha tumboni mwake.
When tyme was come that she shulde be delyuered beholde there was. ij. twynnes in hyr wobe.
28 Alipokuwa akijifungua, mmoja akatoa mkono wake nje, kwa hiyo mkunga akachukua uzi mwekundu na kuufunga mkononi mwa yule mtoto, akasema, “Huyu ametoka kwanza.”
And as she traveled the one put out his hande and the mydwife toke and bownde a reed threde aboute it saynge: this wyll come out fyrst.
29 Lakini alipourudisha mkono wake ndugu yake akaanza kutoka, naye akasema, “Hivi ndivyo ulivyotoka kwa nguvu!” Akaitwa Peresi.
But he plucked his hande backe agayne and his brother came out. And she sayde: wherfore hast thou rent a rent vppon the? and called him Pharez.
30 Kisha ndugu yake, aliyekuwa na uzi mwekundu mkononi, akatoka, naye akaitwa Zera.
And afterward came out his brother that had the reade threde about his hade which was called Zarah.

< Mwanzo 38 >