< Mwanzo 38 >

1 Wakati ule, Yuda akawaacha ndugu zake, akaenda kuishi na Hira Mwadulami.
And it comes to pass, at that time, that Judah goes down from his brothers, and turns aside to a man, an Adullamite, whose name [is] Hirah;
2 Huko Yuda akakutana na binti wa Kikanaani aitwaye Shua, akamwoa na akakutana naye kimwili,
and Judah sees there the daughter of a man, a Canaanite, whose name [is] Shuah, and takes her, and goes in to her.
3 akapata mimba, akamzaa mwana, ambaye alimwita Eri.
And she conceives, and bears a son, and he calls his name Er;
4 Akapata mimba tena, akamzaa mwana na kumwita Onani.
and she conceives again, and bears a son, and calls his name Onan;
5 Akamzaa mwana mwingine tena, akamwita Shela. Huyu alimzalia mahali paitwapo Kezibu.
and she adds again, and bears a son, and calls his name Shelah; and he was in Chezib in her bearing him.
6 Yuda akampatia Eri, mzaliwa wake wa kwanza, mke aitwaye Tamari.
And Judah takes a wife for Er, his firstborn, and her name [is] Tamar;
7 Lakini Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mwovu machoni pa Bwana, kwa hiyo Bwana akamuua.
and Er, Judah’s firstborn, is evil in the eyes of YHWH, and YHWH puts him to death.
8 Kisha Yuda akamwambia Onani, “Kutana kimwili na mke wa ndugu yako, na utimize wajibu wako kwake kama mke wa ndugu yako, ili umpatie ndugu yako uzao.”
And Judah says to Onan, “Go in to the wife of your brother, and marry her, and raise up seed to your brother”;
9 Lakini Onani alijua kwamba uzao haungekuwa wake, kwa hiyo kila alipokutana kimwili na mke wa ndugu yake, alimwaga chini mbegu za kiume ili asimpatie ndugu yake uzao.
and Onan knows that the seed is not [reckoned] his; and it has come to pass, if he has gone in to his brother’s wife, that he has destroyed [it] to the earth, so as not to give seed to his brother;
10 Alichofanya kilikuwa kiovu machoni pa Bwana, hivyo, pia Bwana akamuua Onani.
and that which he has done is evil in the eyes of YHWH, and He puts him also to death.
11 Kisha Yuda akamwambia Tamari mkwewe, “Ishi kama mjane nyumbani mwa baba yako mpaka mwanangu Shela atakapokua.” Kwa maana alifikiri, “Angeweza kufa pia kama ndugu zake.” Kwa hiyo Tamari alikwenda kuishi nyumbani kwa baba yake.
And Judah says to his daughter-in-law Tamar, “Abide [as] a widow at your father’s house, until my son Shelah grows up”; for he said, “Lest he die—even he—like his brothers”; and Tamar goes and dwells at her father’s house.
12 Baada ya muda mrefu mke wa Yuda binti wa Shua akafariki. Baada ya msiba, Yuda alikwenda Timna, kwa watu waliokuwa wakikata kondoo wake manyoya, naye alifuatana na rafiki yake Hira Mwadulami.
And the days are multiplied, and the daughter of Shuah, Judah’s wife, dies; and Judah is comforted, and goes up to his sheep-shearers, he and Hirah his friend the Adullamite, to Timnath.
13 Tamari alipoambiwa, “Baba mkwe wako yuko njiani kwenda Timna kukata kondoo wake manyoya,”
And it is declared to Tamar, saying, “Behold, your husband’s father is going up to Timnath to shear his flock”;
14 alivua mavazi yake ya ujane, akajifunika kwa shela ili asifahamike, akaketi kwenye mlango wa Enaimu, ambao upo njiani kuelekea Timna. Akafanya hivyo kwa sababu aliona kwamba, ingawa Shela amekua, lakini alikuwa hajakabidhiwa kwake kuwa mkewe.
and she turns aside the garments of her widowhood from off her, and covers herself with a veil, and wraps herself up, and sits in the opening of Enayim, which [is] by the way to Timnath, for she has seen that Shelah has grown up, and she has not been given to him for a wife.
15 Yuda alipomwona alifikiri ni kahaba, kwa sababu alikuwa amefunika uso wake.
And Judah sees her, and reckons her for a harlot, for she has covered her face,
16 Pasipo kutambua kwamba alikuwa mkwe wake, akamwendea kando ya njia na kumwambia, “Njoo sasa, nikutane na wewe kimwili.” Yule mkwewe akamuuliza, “Utanipa nini nikikutana nawe kimwili?”
and he turns aside to her by the way and says, “Please come, let me come in to you,” for he has not known that she [is] his daughter-in-law; and she says, “What do you give to me, that you may come in to me?”
17 Akamwambia, “Nitakutumia mwana-mbuzi kutoka kundi langu.” Akamuuliza, “Utanipa kitu chochote kama amana mpaka utakapompeleka?”
And he says, “I send a kid of the goats from the flock.” And she says, “Do you give a pledge until you send [it]?”
18 Akamuuliza, “Nikupe amana gani?” Akamjibu, “Pete yako na kamba yake pamoja na fimbo iliyo mkononi mwako.” Kwa hiyo akampa vitu hivyo kisha akakutana naye kimwili, naye akapata mimba yake.
And he says, “What [is] the pledge that I give to you?” And she says, “Your seal, and your ribbon, and your staff which [is] in your hand”; and he gives to her, and goes in to her, and she conceives to him;
19 Tamari akaondoka, akavua shela yake akavaa tena nguo zake za ujane.
and she rises, and goes, and turns aside her veil from off her, and puts on the garments of her widowhood.
20 Wakati ule ule, Yuda akamtuma rafiki yake Mwadulami apeleke yule mwana-mbuzi ili arudishiwe amana yake kutoka kwa yule mwanamke, lakini yule rafiki yake hakumkuta yule mwanamke.
And Judah sends the kid of the goats by the hand of his friend the Adullamite, to receive the pledge from the hand of the woman, and he has not found her.
21 Akawauliza watu wanaoishi mahali pale, “Yuko wapi yule kahaba wa mahali pa kuabudia miungu aliyekuwa kando ya barabara hapa Enaimu?” Wakamjibu, “Hajawahi kuwepo mwanamke yeyote kahaba wa mahali pa kuabudia miungu hapa.”
And he asks the men of her place, saying, “Where [is] the separated one—she in Enayim, by the way?” And they say, “There has not been in this [place] a separated one.”
22 Kwa hiyo akamrudia Yuda na kumwambia, “Sikumpata. Zaidi ya hayo, watu wanaoishi mahali pale walisema ‘Hapakuwahi kuwepo mwanamke yeyote kahaba wa mahali pa kuabudia miungu hapa.’”
And he turns back to Judah and says, “I have not found her; and the men of the place also have said, There has not been in this [place] a separated one,”
23 Kisha Yuda akasema, “Mwache avichukue vitu hivyo, ama sivyo tutakuwa kichekesho. Hata hivyo, nilimpelekea mwana-mbuzi, lakini hukumkuta.”
and Judah says, “Let her take to herself, lest we become despised; behold, I sent this kid, and you have not found her.”
24 Baada ya miezi mitatu Yuda akaambiwa, “Tamari mkweo ana hatia ya kuwa kahaba, na matokeo yake ana mimba.” Yuda akasema, “Mtoeni nje na achomwe moto hadi afe!”
And it comes to pass about three months [after], that it is declared to Judah, saying, “Your daughter-in-law Tamar has committed fornication; and also, behold, she has conceived by fornication”: and Judah says, “Bring her out—and she is burned.”
25 Alipokuwa akitolewa nje, akatuma ujumbe kwa baba mkwe wake kusema, “Nina mimba ya mtu mwenye vitu hivi.” Akaongeza kusema, “Angalia kama utatambua kwamba pete hii na kamba yake pamoja na fimbo hii ni vya nani.”
She is brought out, and she has sent to her husband’s father, saying, “To a man whose these [are], I [am] pregnant”; and she says, “Please discern whose these [are]—the seal, and the ribbons, and the staff.”
26 Yuda akavitambua na kusema, “Yeye ana haki kuliko mimi, kwa kuwa sikumkabidhi kwa mwanangu Shela ili awe mkewe.” Tangu hapo hakukutana naye kimwili tena.
And Judah discerns and says, “She has been more righteous than I, because that I did not give her to my son Shelah”; and he has not added to know her again.
27 Wakati ulipofika wa kujifungua, kukawa na wana mapacha tumboni mwake.
And it comes to pass in the time of her bearing, that behold, twins [are] in her womb;
28 Alipokuwa akijifungua, mmoja akatoa mkono wake nje, kwa hiyo mkunga akachukua uzi mwekundu na kuufunga mkononi mwa yule mtoto, akasema, “Huyu ametoka kwanza.”
and it comes to pass in her bearing, that [one] gives out a hand, and the midwife takes and binds on his hand a scarlet thread, saying, “This has come out first.”
29 Lakini alipourudisha mkono wake ndugu yake akaanza kutoka, naye akasema, “Hivi ndivyo ulivyotoka kwa nguvu!” Akaitwa Peresi.
And it comes to pass as he draws back his hand, that behold, his brother has come out, and she says, “What! You have broken forth—the breach [is] on you”; and he calls his name Perez;
30 Kisha ndugu yake, aliyekuwa na uzi mwekundu mkononi, akatoka, naye akaitwa Zera.
and afterward his brother has come out, on whose hand [is] the scarlet thread, and he calls his name Zerah.

< Mwanzo 38 >