< Mwanzo 37 >

1 Yakobo akaishi Kanaani katika nchi ambayo baba yake alikuwa ameishi.
Jakob je prebival v deželi, v kateri je bil njegov oče tujec, v kánaanski deželi.
2 Zifuatazo ni habari za Yakobo. Yosefu, kijana wa miaka kumi na saba, alikuwa akichunga makundi ya kondoo na mbuzi pamoja na ndugu zake wa mama wengine, yaani wana wa Bilha na wana wa Zilpa wake za baba yake, naye akawa akimletea baba yake taarifa mbaya kuhusu hao ndugu zake.
To so Jakobovi rodovi. Jožef je bil star sedemnajst let, ko je s svojimi brati pasel trop in deček je bil s sinovi Bilhe in s sinovi Zilpe, ženama svojega očeta. Jožef je svojemu očetu prinesel njihovo zlo poročilo.
3 Basi, Israeli akampenda Yosefu kuliko yeyote miongoni mwa kaka zake, kwani ni mwanawe wa uzeeni, akamshonea joho lililorembwa vizuri sana.
Torej Izrael je bolj ljubil Jožefa kakor vse svoje otroke, ker je bil sin njegove visoke starosti. Naredil mu je plašč iz mnogih barv.
4 Ndugu zake walipoona kwamba baba yao anampenda Yosefu kuliko yeyote mwingine miongoni mwao, walimchukia na hawakusema naye neno lolote jema.
Ko so njegovi bratje videli, da ga je njihov oče bolj ljubil kakor vse njegove brate, so ga zasovražili in niso mogli miroljubno govoriti z njim.
5 Yosefu akaota ndoto, naye alipowaeleza ndugu zake, wakamchukia zaidi.
Jožef je sanjal sanje in te je povedal svojim bratom, oni pa so ga še bolj sovražili.
6 Akawaambia, “Sikilizeni ndoto niliyoota:
Rekel jim je: »Poslušajte, prosim vas, te sanje, ki sem jih sanjal.
7 Tulikuwa tukifunga miganda ya nafaka shambani, ghafula mganda wangu ukasimama wima, wakati miganda yenu ikiuzunguka na kuuinamia.”
Kajti, glejte, na polju smo vezali snope in glejte, moj snop je vstal in tudi stal pokončno. Glejte, vaši snopi so stali naokoli in se globoko priklanjali mojemu snopu.«
8 Ndugu zake wakamwambia, “Wewe unakusudia kututawala? Hivi kweli wewe utatutawala sisi?” Wakaongeza kumchukia zaidi kwa sababu ya ndoto yake pamoja na yale aliyowaambia.
Njegovi bratje so mu rekli: »Ali boš zares kraljeval nad nami? Ali boš zares imel gospostvo nad nami?« In še bolj so ga zasovražili zaradi njegovih sanj in zaradi njegovih besed.
9 Kisha akaota ndoto nyingine, akawaambia ndugu zake akisema, “Sikilizeni, nimeota ndoto nyingine, wakati huu jua, mwezi na nyota kumi na moja zilikuwa zinanisujudia.”
Sanjal je še druge sanje in te povedal svojim bratom in rekel: »Glejte, še sem sanjal sanje. Glejte globoko so se mi priklanjali sonce in luna in enajst zvezd.«
10 Alipomwambia baba yake pamoja na ndugu zake, baba yake akamkemea akisema, “Ni ndoto gani hii uliyoota? Hivi kweli mama yako na mimi na ndugu zako tutakuja kukusujudia wewe hadi nchi?”
Te je povedal svojemu očetu in svojim bratom. Njegov oče pa ga je oštel in mu rekel: »Kaj so te sanje, ki si jih sanjal? Naj zares pridemo jaz, tvoja mati in tvoji bratje, da se ti priklonimo k zemlji?«
11 Ndugu zake wakamwonea wivu, lakini baba yake akaliweka jambo hilo moyoni.
Njegovi bratje so mu zavidali, toda njegov oče je obeležil besede.
12 Basi, ndugu zake walikuwa wamekwenda kuchunga makundi ya baba yao karibu na Shekemu,
Njegovi bratje so odšli, da pasejo trop svojega očeta v Sihemu.
13 naye Israeli akamwambia Yosefu, “Kama ujuavyo, ndugu zako wanachunga makundi huko karibu na Shekemu. Njoo, nitakutuma kwao.” Yosefu akajibu, “Vema sana, niko tayari.”
Izrael je rekel Jožefu: »Mar tvoji bratje ne pasejo tropa v Sihemu? Pridi in poslal te bom k njim.« Ta mu je rekel: »Tukaj sem.«
14 Kwa hiyo akamwambia, “Nenda uone kama mambo yote ni salama kwa ndugu zako na makundi, kisha uniletee habari.” Ndipo akamtuma Yosefu kutoka Bonde la Hebroni. Yosefu alipofika Shekemu,
Rekel mu je: »Pojdi, prosim te, poglej če je dobro s tvojimi brati in dobro s tropi in besedo mi ponovno prinesi nazaj.« Tako ga je poslal iz hebrónske doline in je prišel v Sihem.
15 mtu mmoja akamkuta akizungukazunguka mashambani na akamuuliza, “Unatafuta nini?”
Našel pa ga je nek mož in glej, taval je po polju in človek ga je vprašal, rekoč: »Kaj iščeš?«
16 Akajibu, “Ninawatafuta ndugu zangu. Unaweza kuniambia wanachunga wapi makundi yao?”
Rekel je: »Iščem svoje brate. Povej mi, prosim te, kje pasejo svoje trope.«
17 Yule mtu akajibu, “Wamehama hapa. Nilisikia wakisema, ‘Twende Dothani.’” Kwa hiyo Yosefu akawafuatilia ndugu zake na kuwakuta karibu na Dothani.
Človek je rekel: »Odpravili so se od tod, kajti slišal sem jih reči: ›Pojdimo v Dotán.‹« Jožef je odšel za svojimi brati in jih našel v Dotánu.
18 Ndugu zake walipomwona akiwa mbali, kabla hajawafikia, wakapanga shauri baya la kumuua.
Ko so ga od daleč zagledali, celo preden se jim je približal, so se zoper njega zarotili, da ga ubijejo.
19 Wakaambiana, “Yule mwota ndoto anakuja!
Drug drugemu so rekli: »Glejte, ta sanjač prihaja.
20 Njooni sasa, tumuue na kumtupa katika shimo mojawapo na tuseme kwamba mnyama mkali amemrarua. Kisha tutaona matokeo ya ndoto zake.”
Pridimo torej, ubijmo ga in ga vrzimo v neko jamo in bomo rekli: ›Neka zla žival ga je požrla‹ in bomo videli, kaj bo nastalo iz njegovih sanj.«
21 Reubeni aliposikia jambo hili, akajaribu kumwokoa kutoka mikononi mwao akasema, “Tusiutoe uhai wake.
Ruben pa je to slišal in ga osvobodil iz njihovih rok in rekel: »Naj ga ne ubijemo mi.«
22 Tusimwage damu yoyote. Mtupeni katika shimo lililoko hapa jangwani, lakini msimguse.” Reubeni alisema hivyo ili amwokoe kutoka mikononi mwao, kisha amrudishe nyumbani kwa baba yake.
Ruben jim je rekel: »Ne prelijmo krvi, temveč ga vrzimo v tole jamo, ki je v divjini in ne položimo roke nanj, « da bi ga lahko osvobodil iz njihovih rok, da ga ponovno izroči njegovemu očetu.
23 Kwa hiyo Yosefu alipowafikia ndugu zake, walimvua lile joho lake, lile joho lililorembwa vizuri alilokuwa amevaa.
Pripetilo pa se je, ko je Jožef prišel k svojim bratom, da so Jožefa slekli iz njegovega plašča, njegovega plašča iz mnogih barv, ki je bil na njem
24 Kisha wakamchukua wakamtupa katika shimo. Wakati huo shimo lilikuwa tupu, halikuwa na maji ndani yake.
in ga prijeli ter vrgli v jamo. Jama pa je bila prazna, v njej ni bilo vode.
25 Walipokaa ili wale chakula chao, wakainua macho wakaona msafara wa Waishmaeli ukija kutoka Gileadi. Ngamia wao walikuwa wamepakizwa mizigo ya vikolezo, uvumba na manemane, nao walikuwa njiani kuvipeleka Misri.
Usedli so se, da jedo kruh in povzdignili so svoje oči, pogledali in glej, skupina Izmaelcev je prihajala iz Gileáda, s svojimi kamelami, nesoč dišave, balzam in miro, da to odnesejo dol v Egipt.
26 Yuda akawaambia ndugu zake, “Tutafaidi nini ikiwa tutamuua ndugu yetu na kuificha damu yake?
Juda je rekel svojim bratom: »Kakšna korist je to, če ubijemo svojega brata in prikrijemo njegovo kri?
27 Njooni, tumuuze kwa hawa Waishmaeli. Tusimguse, kwa kuwa hata hivyo yeye ni ndugu yetu, nyama yetu na damu yetu wenyewe.” Ndugu zake wakakubali.
Pridite in prodajmo ga Izmaelcem in naj naša roka ne bo nad njim, kajti on je naš brat in naše meso.« Njegovi bratje so bili zadovoljni.
28 Kwa hiyo wale wafanyabiashara Wamidiani walipofika pale, ndugu zake wakamtoa Yosefu kutoka kwenye lile shimo, na kumuuza kwa shekeli ishirini za fedha kwa wale Waishmaeli, ambao walimpeleka Misri.
Potem so šli mimo midjánski trgovci in Jožefa so potegnili ter dvignili iz jame in Jožefa prodali Izmaelcem za dvajset koščkov srebra in ti so Jožefa pripeljali v Egipt.
29 Reubeni aliporudi kutazama kwenye lile shimo na kuona kwamba Yosefu hayupo, alirarua nguo zake.
Ruben pa se je vrnil k jami in glej, Jožefa ni bilo v jami. Raztrgal je svoja oblačila
30 Akawarudia ndugu zake na kusema, “Kijana hayuko mle! Nielekee wapi sasa?”
in se vrnil k svojim bratom ter rekel: »Otroka ni in kam naj grem jaz?«
31 Kisha wakalichukua lile joho la Yosefu, wakachinja mbuzi na kulichovya katika damu.
Vzeli so Jožefov plašč, zaklali kozlička izmed koz in plašč pomočili v kri
32 Wakalichukua lile joho lililorembwa vizuri na kulipeleka kwa baba yao na kusema, “Tumeliokota hili joho. Uchunguze uone kama ni la mwanao.”
in poslali so plašč iz mnogih barv in ga prinesli k svojemu očetu ter rekli: »To smo našli. Védi torej, ali je to plašč tvojega sina ali ne.«
33 Baba yao akalitambua akasema, “Hili ni joho la mwanangu! Mnyama mkali amemrarua. Hakika Yosefu ameraruliwa vipande vipande.”
Prepoznal ga je in rekel: » To je plašč mojega sina. Zla žival ga je požrla. Jožef je brez dvoma raztrgan na koščke.«
34 Kisha Yakobo akararua nguo zake, akavaa nguo ya gunia na kumwombolezea mwanawe kwa siku nyingi.
Jakob je raztrgal svoja oblačila in na svoja ledja oblekel vrečevino in mnogo dni žaloval za svojim sinom.
35 Wanawe wote na binti zake wakaja kumfariji, lakini hakukubali kufarijiwa. Akasema, “Hapana, nitamwombolezea mwanangu mpaka nimfikie kaburini.” Kwa hiyo baba yake akaendelea kumlilia. (Sheol h7585)
Vsi njegovi sinovi in vse njegove hčere so vstali, da ga potolažijo, toda odklonil je, da bi bil potolažen in rekel je: »Kajti žalujoč bom šel v grob k svojemu sinu.« Tako je njegov oče jokal za njim. (Sheol h7585)
36 Wakati ule ule, Wamidiani wakamuuza Yosefu huko Misri kwa Potifa, mmojawapo wa maafisa wa Farao, aliyekuwa mkuu wa ulinzi.
Midjánci pa so ga prodali v Egipt k Potifárju, faraonovemu častniku in poveljniku straže.

< Mwanzo 37 >