< Mwanzo 37 >

1 Yakobo akaishi Kanaani katika nchi ambayo baba yake alikuwa ameishi.
and to dwell Jacob in/on/with land: country/planet sojourning father his in/on/with land: country/planet Canaan
2 Zifuatazo ni habari za Yakobo. Yosefu, kijana wa miaka kumi na saba, alikuwa akichunga makundi ya kondoo na mbuzi pamoja na ndugu zake wa mama wengine, yaani wana wa Bilha na wana wa Zilpa wake za baba yake, naye akawa akimletea baba yake taarifa mbaya kuhusu hao ndugu zake.
these generation Jacob Joseph son: aged seven ten year to be to pasture with brother: male-sibling his in/on/with flock and he/she/it youth with son: aged Bilhah and with son: child Zilpah woman: wife father his and to come (in): bring Joseph [obj] slander their bad: harmful to(wards) father their
3 Basi, Israeli akampenda Yosefu kuliko yeyote miongoni mwa kaka zake, kwani ni mwanawe wa uzeeni, akamshonea joho lililorembwa vizuri sana.
and Israel to love: lover [obj] Joseph from all son: child his for son: child extreme age he/she/it to/for him and to make to/for him tunic long-sleeved
4 Ndugu zake walipoona kwamba baba yao anampenda Yosefu kuliko yeyote mwingine miongoni mwao, walimchukia na hawakusema naye neno lolote jema.
and to see: see brother: male-sibling his for [obj] him to love: lover father their from all brother: male-sibling his and to hate [obj] him and not be able to speak: speak him to/for peace
5 Yosefu akaota ndoto, naye alipowaeleza ndugu zake, wakamchukia zaidi.
and to dream Joseph dream and to tell to/for brother: male-sibling his and to add still to hate [obj] him
6 Akawaambia, “Sikilizeni ndoto niliyoota:
and to say to(wards) them to hear: hear please [the] dream [the] this which to dream
7 Tulikuwa tukifunga miganda ya nafaka shambani, ghafula mganda wangu ukasimama wima, wakati miganda yenu ikiuzunguka na kuuinamia.”
and behold we be dumb sheaf in/on/with midst [the] land: country and behold to arise: rise sheaf my and also to stand and behold to turn: turn sheaf your and to bow to/for sheaf my
8 Ndugu zake wakamwambia, “Wewe unakusudia kututawala? Hivi kweli wewe utatutawala sisi?” Wakaongeza kumchukia zaidi kwa sababu ya ndoto yake pamoja na yale aliyowaambia.
and to say to/for him brother: male-sibling his to reign to reign upon us if to rule to rule in/on/with us and to add still to hate [obj] him upon dream his and upon word his
9 Kisha akaota ndoto nyingine, akawaambia ndugu zake akisema, “Sikilizeni, nimeota ndoto nyingine, wakati huu jua, mwezi na nyota kumi na moja zilikuwa zinanisujudia.”
and to dream still dream another and to recount [obj] him to/for brother: male-sibling his and to say behold to dream dream still and behold [the] sun and [the] moon and one ten star to bow to/for me
10 Alipomwambia baba yake pamoja na ndugu zake, baba yake akamkemea akisema, “Ni ndoto gani hii uliyoota? Hivi kweli mama yako na mimi na ndugu zako tutakuja kukusujudia wewe hadi nchi?”
and to recount to(wards) father his and to(wards) brother: male-sibling his and to rebuke in/on/with him father his and to say to/for him what? [the] dream [the] this which to dream to come (in): come to come (in): come I and mother your and brother: male-sibling your to/for to bow to/for you land: soil [to]
11 Ndugu zake wakamwonea wivu, lakini baba yake akaliweka jambo hilo moyoni.
and be jealous in/on/with him brother: male-sibling his and father his to keep: obey [obj] [the] word
12 Basi, ndugu zake walikuwa wamekwenda kuchunga makundi ya baba yao karibu na Shekemu,
and to go: went brother: male-sibling his to/for to pasture [obj] flock father their in/on/with Shechem
13 naye Israeli akamwambia Yosefu, “Kama ujuavyo, ndugu zako wanachunga makundi huko karibu na Shekemu. Njoo, nitakutuma kwao.” Yosefu akajibu, “Vema sana, niko tayari.”
and to say Israel to(wards) Joseph not brother: male-sibling your to pasture in/on/with Shechem to go: come! [emph?] and to send: depart you to(wards) them and to say to/for him behold I
14 Kwa hiyo akamwambia, “Nenda uone kama mambo yote ni salama kwa ndugu zako na makundi, kisha uniletee habari.” Ndipo akamtuma Yosefu kutoka Bonde la Hebroni. Yosefu alipofika Shekemu,
and to say to/for him to go: went please to see: see [obj] peace: well-being brother: male-sibling your and [obj] peace: well-being [the] flock and to return: return me word and to send: depart him from Valley (of Hebron) Hebron (Valley) and to come (in): come Shechem [to]
15 mtu mmoja akamkuta akizungukazunguka mashambani na akamuuliza, “Unatafuta nini?”
and to find him man and behold to go astray in/on/with land: country and to ask him [the] man to/for to say what? to seek
16 Akajibu, “Ninawatafuta ndugu zangu. Unaweza kuniambia wanachunga wapi makundi yao?”
and to say [obj] brother: male-sibling my I to seek to tell [emph?] please to/for me where? they(masc.) to pasture
17 Yule mtu akajibu, “Wamehama hapa. Nilisikia wakisema, ‘Twende Dothani.’” Kwa hiyo Yosefu akawafuatilia ndugu zake na kuwakuta karibu na Dothani.
and to say [the] man to set out from this for to hear: hear to say to go: follow Dothan [to] and to go: follow Joseph after brother: male-sibling his and to find them in/on/with Dothan
18 Ndugu zake walipomwona akiwa mbali, kabla hajawafikia, wakapanga shauri baya la kumuua.
and to see: see [obj] him from distant and in/on/with before to present: come to(wards) them and to plot [obj] him to/for to die him
19 Wakaambiana, “Yule mwota ndoto anakuja!
and to say man: anyone to(wards) brother: compatriot his behold master: [master of] [the] dream this to come (in): come
20 Njooni sasa, tumuue na kumtupa katika shimo mojawapo na tuseme kwamba mnyama mkali amemrarua. Kisha tutaona matokeo ya ndoto zake.”
and now to go: come! and to kill him and to throw him in/on/with one [the] pit and to say living thing bad: harmful to eat him and to see: see what? to be dream his
21 Reubeni aliposikia jambo hili, akajaribu kumwokoa kutoka mikononi mwao akasema, “Tusiutoe uhai wake.
and to hear: hear Reuben and to rescue him from hand their and to say not to smite him soul: life
22 Tusimwage damu yoyote. Mtupeni katika shimo lililoko hapa jangwani, lakini msimguse.” Reubeni alisema hivyo ili amwokoe kutoka mikononi mwao, kisha amrudishe nyumbani kwa baba yake.
and to say to(wards) them Reuben not to pour: kill blood to throw [obj] him to(wards) [the] pit [the] this which in/on/with wilderness and hand not to send: reach in/on/with him because to rescue [obj] him from hand their to/for to return: rescue him to(wards) father his
23 Kwa hiyo Yosefu alipowafikia ndugu zake, walimvua lile joho lake, lile joho lililorembwa vizuri alilokuwa amevaa.
and to be like/as as which to come (in): come Joseph to(wards) brother: male-sibling his and to strip [obj] Joseph [obj] tunic his [obj] tunic [the] long-sleeved which upon him
24 Kisha wakamchukua wakamtupa katika shimo. Wakati huo shimo lilikuwa tupu, halikuwa na maji ndani yake.
and to take: take him and to throw [obj] him [the] pit [to] and [the] pit worthless nothing in/on/with him water
25 Walipokaa ili wale chakula chao, wakainua macho wakaona msafara wa Waishmaeli ukija kutoka Gileadi. Ngamia wao walikuwa wamepakizwa mizigo ya vikolezo, uvumba na manemane, nao walikuwa njiani kuvipeleka Misri.
and to dwell to/for to eat food and to lift: look eye: seeing their and to see: see and behold caravan Ishmaelite to come (in): come from Gilead and camel their to lift: bear tragacanth gum and balsam and myrrh to go: journey to/for to go down Egypt [to]
26 Yuda akawaambia ndugu zake, “Tutafaidi nini ikiwa tutamuua ndugu yetu na kuificha damu yake?
and to say Judah to(wards) brother: male-sibling his what? unjust-gain for to kill [obj] brother: male-sibling our and to cover [obj] blood his
27 Njooni, tumuuze kwa hawa Waishmaeli. Tusimguse, kwa kuwa hata hivyo yeye ni ndugu yetu, nyama yetu na damu yetu wenyewe.” Ndugu zake wakakubali.
to go: come! and to sell him to/for Ishmaelite and hand our not to be in/on/with him for brother: male-sibling our flesh our he/she/it and to hear: hear brother: male-sibling his
28 Kwa hiyo wale wafanyabiashara Wamidiani walipofika pale, ndugu zake wakamtoa Yosefu kutoka kwenye lile shimo, na kumuuza kwa shekeli ishirini za fedha kwa wale Waishmaeli, ambao walimpeleka Misri.
and to pass human Midianite to trade and to draw and to ascend: establish [obj] Joseph from [the] pit and to sell [obj] Joseph to/for Ishmaelite in/on/with twenty silver: money and to come (in): bring [obj] Joseph Egypt [to]
29 Reubeni aliporudi kutazama kwenye lile shimo na kuona kwamba Yosefu hayupo, alirarua nguo zake.
and to return: return Reuben to(wards) [the] pit and behold nothing Joseph in/on/with pit and to tear [obj] garment his
30 Akawarudia ndugu zake na kusema, “Kijana hayuko mle! Nielekee wapi sasa?”
and to return: return to(wards) brother: male-sibling his and to say [the] youth nothing he and I where? I to come (in): come
31 Kisha wakalichukua lile joho la Yosefu, wakachinja mbuzi na kulichovya katika damu.
and to take: take [obj] tunic Joseph and to slaughter he-goat goat and to dip [obj] [the] tunic in/on/with blood
32 Wakalichukua lile joho lililorembwa vizuri na kulipeleka kwa baba yao na kusema, “Tumeliokota hili joho. Uchunguze uone kama ni la mwanao.”
and to send: depart [obj] tunic [the] long-sleeved and to come (in): bring to(wards) father their and to say this to find to recognize please tunic son: child your he/she/it if not
33 Baba yao akalitambua akasema, “Hili ni joho la mwanangu! Mnyama mkali amemrarua. Hakika Yosefu ameraruliwa vipande vipande.”
and to recognize her and to say tunic son: child my living thing bad: harmful to eat him to tear to tear Joseph
34 Kisha Yakobo akararua nguo zake, akavaa nguo ya gunia na kumwombolezea mwanawe kwa siku nyingi.
and to tear Jacob mantle his and to set: put sackcloth in/on/with loin his and to mourn upon son: child his day many
35 Wanawe wote na binti zake wakaja kumfariji, lakini hakukubali kufarijiwa. Akasema, “Hapana, nitamwombolezea mwanangu mpaka nimfikie kaburini.” Kwa hiyo baba yake akaendelea kumlilia. (Sheol h7585)
and to arise: rise all son: child his and all daughter his to/for to be sorry: comfort him and to refuse to/for to be sorry: comfort and to say for to go down to(wards) son: child my mourning hell: Sheol [to] and to weep [obj] him father his (Sheol h7585)
36 Wakati ule ule, Wamidiani wakamuuza Yosefu huko Misri kwa Potifa, mmojawapo wa maafisa wa Farao, aliyekuwa mkuu wa ulinzi.
(and [the] Midianite *L(E)*) to sell [obj] him to(wards) Egypt to/for Potiphar eunuch Pharaoh ruler [the] guard

< Mwanzo 37 >