< Mwanzo 37 >

1 Yakobo akaishi Kanaani katika nchi ambayo baba yake alikuwa ameishi.
And Jacob dwelt in the land of his father's sojourning, in the land of Canaan.
2 Zifuatazo ni habari za Yakobo. Yosefu, kijana wa miaka kumi na saba, alikuwa akichunga makundi ya kondoo na mbuzi pamoja na ndugu zake wa mama wengine, yaani wana wa Bilha na wana wa Zilpa wake za baba yake, naye akawa akimletea baba yake taarifa mbaya kuhusu hao ndugu zake.
These are the generations of Jacob. Joseph, being seventeen years old, was feeding the flock with his brothers. And he was a lad with the sons of Bilhah, and with the sons of Zilpah, his father's wives, and Joseph brought the evil report of them to their father.
3 Basi, Israeli akampenda Yosefu kuliko yeyote miongoni mwa kaka zake, kwani ni mwanawe wa uzeeni, akamshonea joho lililorembwa vizuri sana.
Now Israel loved Joseph more than all his sons, because he was the son of his old age. And he made for him a coat of many colors.
4 Ndugu zake walipoona kwamba baba yao anampenda Yosefu kuliko yeyote mwingine miongoni mwao, walimchukia na hawakusema naye neno lolote jema.
And his brothers saw that their father loved him more than all his brothers. And they hated him, and could not speak peaceably to him.
5 Yosefu akaota ndoto, naye alipowaeleza ndugu zake, wakamchukia zaidi.
And Joseph dreamed a dream, and he told it to his brothers, and they hated him yet the more.
6 Akawaambia, “Sikilizeni ndoto niliyoota:
And he said to them, Hear, I pray you, this dream which I have dreamed.
7 Tulikuwa tukifunga miganda ya nafaka shambani, ghafula mganda wangu ukasimama wima, wakati miganda yenu ikiuzunguka na kuuinamia.”
For, behold, we were binding sheaves in the field, and, lo, my sheaf arose, and also stood upright. And, behold, your sheaves came round about, and made obeisance to my sheaf.
8 Ndugu zake wakamwambia, “Wewe unakusudia kututawala? Hivi kweli wewe utatutawala sisi?” Wakaongeza kumchukia zaidi kwa sababu ya ndoto yake pamoja na yale aliyowaambia.
And his brothers said to him, Shall thou indeed reign over us? Or shall thou indeed have dominion over us? And they hated him yet the more for his dreams, and for his words.
9 Kisha akaota ndoto nyingine, akawaambia ndugu zake akisema, “Sikilizeni, nimeota ndoto nyingine, wakati huu jua, mwezi na nyota kumi na moja zilikuwa zinanisujudia.”
And he dreamed yet another dream, and told it to his brothers. And said, Behold, I have dreamed a dream again. And, behold, the sun and the moon and eleven stars made obeisance to me.
10 Alipomwambia baba yake pamoja na ndugu zake, baba yake akamkemea akisema, “Ni ndoto gani hii uliyoota? Hivi kweli mama yako na mimi na ndugu zako tutakuja kukusujudia wewe hadi nchi?”
And he told it to his father, and to his brothers. And his father rebuked him, and said to him, What is this dream that thou have dreamed? Shall I and thy mother and thy brothers indeed come to bow down ourselves to thee to the earth?
11 Ndugu zake wakamwonea wivu, lakini baba yake akaliweka jambo hilo moyoni.
And his brothers envied him, but his father kept the saying in mind.
12 Basi, ndugu zake walikuwa wamekwenda kuchunga makundi ya baba yao karibu na Shekemu,
And his brothers went to feed their father's flock in Shechem.
13 naye Israeli akamwambia Yosefu, “Kama ujuavyo, ndugu zako wanachunga makundi huko karibu na Shekemu. Njoo, nitakutuma kwao.” Yosefu akajibu, “Vema sana, niko tayari.”
And Israel said to Joseph, Are not thy brothers feeding the flock in Shechem? Come, and I will send thee to them. And he said to him, Here I am.
14 Kwa hiyo akamwambia, “Nenda uone kama mambo yote ni salama kwa ndugu zako na makundi, kisha uniletee habari.” Ndipo akamtuma Yosefu kutoka Bonde la Hebroni. Yosefu alipofika Shekemu,
And he said to him, Go now, see whether it is well with thy brothers, and well with the flock, and bring me word again. So he sent him out of the valley of Hebron, and he came to Shechem.
15 mtu mmoja akamkuta akizungukazunguka mashambani na akamuuliza, “Unatafuta nini?”
And a certain man found him, and, behold, he was wandering in the field. And the man asked him, saying, What do thou seek?
16 Akajibu, “Ninawatafuta ndugu zangu. Unaweza kuniambia wanachunga wapi makundi yao?”
And he said, I am seeking my brothers. Tell me, I pray thee, where they are feeding.
17 Yule mtu akajibu, “Wamehama hapa. Nilisikia wakisema, ‘Twende Dothani.’” Kwa hiyo Yosefu akawafuatilia ndugu zake na kuwakuta karibu na Dothani.
And the man said, They are departed from here, for I heard them say, Let us go to Dothan. And Joseph went after his brothers, and found them in Dothan.
18 Ndugu zake walipomwona akiwa mbali, kabla hajawafikia, wakapanga shauri baya la kumuua.
And they saw him afar off. And before he came near to them, they conspired against him to kill him.
19 Wakaambiana, “Yule mwota ndoto anakuja!
And they said one to another, Behold, this dreamer comes.
20 Njooni sasa, tumuue na kumtupa katika shimo mojawapo na tuseme kwamba mnyama mkali amemrarua. Kisha tutaona matokeo ya ndoto zake.”
Come now therefore, and let us kill him, and cast him into one of the pits. And we will say, An evil beast has devoured him. And we shall see what will become of his dreams.
21 Reubeni aliposikia jambo hili, akajaribu kumwokoa kutoka mikononi mwao akasema, “Tusiutoe uhai wake.
And Reuben heard it, and delivered him out of their hand, and said, Let us not take his life.
22 Tusimwage damu yoyote. Mtupeni katika shimo lililoko hapa jangwani, lakini msimguse.” Reubeni alisema hivyo ili amwokoe kutoka mikononi mwao, kisha amrudishe nyumbani kwa baba yake.
And Reuben said to them, Shed no blood. Cast him into this pit that is in the wilderness, but lay no hand upon him, that he might deliver him out of their hand, to restore him to his father.
23 Kwa hiyo Yosefu alipowafikia ndugu zake, walimvua lile joho lake, lile joho lililorembwa vizuri alilokuwa amevaa.
And it came to pass, when Joseph came to his brothers, that they stripped Joseph of his coat, the coat of many colors that was on him,
24 Kisha wakamchukua wakamtupa katika shimo. Wakati huo shimo lilikuwa tupu, halikuwa na maji ndani yake.
and they took him, and cast him into the pit. And the pit was empty; there was no water in it.
25 Walipokaa ili wale chakula chao, wakainua macho wakaona msafara wa Waishmaeli ukija kutoka Gileadi. Ngamia wao walikuwa wamepakizwa mizigo ya vikolezo, uvumba na manemane, nao walikuwa njiani kuvipeleka Misri.
And they sat down to eat bread. And they lifted up their eyes and looked, and, behold, a caravan of Ishmaelites was coming from Gilead, with their camels bearing spicery and balm and myrrh, going to carry it down to Egypt.
26 Yuda akawaambia ndugu zake, “Tutafaidi nini ikiwa tutamuua ndugu yetu na kuificha damu yake?
And Judah said to his brothers, What profit is it if we kill our brother and conceal his blood?
27 Njooni, tumuuze kwa hawa Waishmaeli. Tusimguse, kwa kuwa hata hivyo yeye ni ndugu yetu, nyama yetu na damu yetu wenyewe.” Ndugu zake wakakubali.
Come, and let us sell him to the Ishmaelites, and let not our hand be upon him, for he is our brother, our flesh. And his brothers hearkened to him.
28 Kwa hiyo wale wafanyabiashara Wamidiani walipofika pale, ndugu zake wakamtoa Yosefu kutoka kwenye lile shimo, na kumuuza kwa shekeli ishirini za fedha kwa wale Waishmaeli, ambao walimpeleka Misri.
And there passed by Midianites, merchantmen, and they drew and lifted Joseph up out of the pit, and sold Joseph to the Ishmaelites for twenty pieces of silver. And they brought Joseph into Egypt.
29 Reubeni aliporudi kutazama kwenye lile shimo na kuona kwamba Yosefu hayupo, alirarua nguo zake.
And Reuben returned to the pit, and, behold, Joseph was not in the pit. And he tore his clothes,
30 Akawarudia ndugu zake na kusema, “Kijana hayuko mle! Nielekee wapi sasa?”
and he returned to his brothers, and said, The child is not, and I, where shall I go?
31 Kisha wakalichukua lile joho la Yosefu, wakachinja mbuzi na kulichovya katika damu.
And they took Joseph's coat, and killed a he-goat, and dipped the coat in the blood.
32 Wakalichukua lile joho lililorembwa vizuri na kulipeleka kwa baba yao na kusema, “Tumeliokota hili joho. Uchunguze uone kama ni la mwanao.”
And they sent the coat of many colors, and they brought it to their father, and said, We have found this. Know now whether it is thy son's coat or not.
33 Baba yao akalitambua akasema, “Hili ni joho la mwanangu! Mnyama mkali amemrarua. Hakika Yosefu ameraruliwa vipande vipande.”
And he knew it, and said, It is my son's coat. An evil beast has devoured him; Joseph is without doubt torn in pieces.
34 Kisha Yakobo akararua nguo zake, akavaa nguo ya gunia na kumwombolezea mwanawe kwa siku nyingi.
And Jacob tore his garments, and put sackcloth upon his loins, and mourned for his son many days.
35 Wanawe wote na binti zake wakaja kumfariji, lakini hakukubali kufarijiwa. Akasema, “Hapana, nitamwombolezea mwanangu mpaka nimfikie kaburini.” Kwa hiyo baba yake akaendelea kumlilia. (Sheol h7585)
And all his sons and all his daughters rose up to comfort him, but he refused to be comforted, and he said, For I will go down to Sheol to my son mourning. And his father wept for him. (Sheol h7585)
36 Wakati ule ule, Wamidiani wakamuuza Yosefu huko Misri kwa Potifa, mmojawapo wa maafisa wa Farao, aliyekuwa mkuu wa ulinzi.
And the Midianites sold him into Egypt to Potiphar, an officer of Pharaoh's, the captain of the guard.

< Mwanzo 37 >