< Mwanzo 36 >

1 Hivi ndivyo vizazi vya Esau (yaani Edomu).
Estas son las generaciones de Esaú, es decir, Edom.
2 Esau akaoa wake kutoka miongoni mwa wanawake wa Kanaani: Ada binti wa Eloni Mhiti, Oholibama binti wa Ana, mjukuu wa kike wa Sibeoni Mhivi,
Las mujeres de Esaú eran mujeres de Canaán: Ada, la hija de Elón el hitita, y Aholibama, hija de Aná, hija de Zibeón el heveo,
3 pia akaoa Basemathi binti wa Ishmaeli, dada yake Nebayothi.
Y Basemat, hija de Ismael, hermana de Nebaiot.
4 Ada akamzalia Esau Elifazi, Basemathi akamzaa Reueli,
Ada tenía un hijo Elifaz; y Basemat era la madre de Reuel;
5 Oholibama akamzaa Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wana wa Esau waliozaliwa kwake huko Kanaani.
Aholibama era la madre de Jeús, Jaalam y Coré; estos son los hijos de Esaú, cuyo nacimiento tuvo lugar en la tierra de Canaán.
6 Esau akawachukua wake zake, watoto wake wa kiume na wa kike na wote wa nyumbani mwake, mifugo yake pamoja na wanyama wake wengine wote na mali yake yote ambayo alikuwa ameipata akiwa Kanaani, akahamia katika nchi iliyo mbali na Yakobo ndugu yake.
Esaú tomó sus mujeres, sus hijos, sus hijas, y todo el pueblo de su casa, y sus bestias, y sus ganados, y todos sus bienes que había juntado en la tierra de Canaán, y se fue a la tierra de Seir, lejos de su hermano Jacob.
7 Mali zao zilikuwa nyingi sana kiasi kwamba haikuwa rahisi wao kuishi pamoja, nchi waliyokuwa wakiishi isingewatosha wote kwa ajili ya mifugo yao.
porque su riqueza era tan grande que la tierra no era lo suficientemente amplia para ellos dos y todo su ganado.
8 Kwa hiyo Esau (ambaye ni Edomu) aliishi katika nchi ya kilima huko Seiri.
Así edificó Esaú su lugar de residencia en la región montañosa de Seir (Esaú es Edom).
9 Hawa ndio wazao wa Esau, baba wa Waedomu, katika nchi ya kilima cha Seiri.
Y estas son las generaciones de Esaú, el padre de los edomitas en el monte de Seir:
10 Haya ndiyo majina ya wana wa Esau: Elifazi, mwana wa Esau ambaye mkewe Ada alimzalia; na Reueli, mwana wa Esau ambaye mkewe Basemathi alimzalia.
Estos son los nombres de los hijos de Esaú: Elifaz, hijo de la mujer de Esaú, Ada, y Reuel, hijo de Basemath, la mujer de Esaú.
11 Wana wa Elifazi ni: Temani, Omari, Sefo, Gatamu na Kenazi.
Los hijos de Elifaz fueron Temán, Omar, Zefo, Gatam y Cenaz.
12 Elifazi mwana wa Esau alikuwa pia na suria aliyeitwa Timna, ambaye alimzalia Amaleki. Hawa ndio waliokuwa wajukuu wa Ada mke wa Esau.
Y Elifaz, hijo de Esaú, tuvo una relación con una mujer llamada Timna, que dio a luz a Amalec; todos estos fueron hijos de Ada, la mujer de Esaú.
13 Wana wa Reueli ni: Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio waliokuwa wajukuu wa Basemathi mkewe Esau.
Y estos son los hijos de Reuel: Nahat, Zera, Sama, y Miza; fueron hijos de la mujer de Esaú, Basemat.
14 Wana wa Oholibama binti Ana, mkewe Esau, aliyekuwa mjukuu wa Sibeoni, aliomzalia Esau ni: Yeushi, Yalamu na Kora.
Y estos son los hijos de Aholibama, hija de Aná, hija de Zibeón, que fué madre de Jeús, Jalam y Coré.
15 Hawa ndio waliokuwa wakuu miongoni mwa wazao wa Esau: Wakuu wa wana wa Elifazi, mzaliwa wa kwanza wa Esau ni: Temani, Omari, Sefo, Kenazi,
Estos fueron los jefes entre los hijos de Esaú: los hijos de Elifaz, el primer hijo de Esaú: Temán, Omar, Zefo, Cenaz,
16 Kora, Gatamu na Amaleki. Hawa ndio waliokuwa wakuu waliotoka kwa Elifazi huko Edomu, waliokuwa wajukuu wa kiume wa Ada.
Coré, Gatam, Amalec: todos estos fueron los jefes en la tierra de Edom, los hijos de Elifaz, la simiente de Ada.
17 Wakuu wa wana wa Reueli, mwana wa Esau ni: Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa Reueli huko Edomu, waliokuwa wajukuu wa kiume wa Basemathi mkewe Esau.
Y estos son los hijos de Reuel, hijo de Esaú: Nahat, Zera, Sama, Miza; estos fueron los jefes de Reuel en la tierra de Edom, los hijos de Basemat, la mujer de Esaú.
18 Wakuu wa wana wa Esau ambao mkewe Oholibama alimzalia ni: Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa mke wa Esau, Oholibama binti Ana.
Y estos son los hijos de Aholibama, la mujer de Esaú: Jeús, Jalam y Coré: estos fueron los jefes que vinieron de la mujer de Esaú, Aholibama, hija de Ana.
19 Hawa ndio waliokuwa wana wa Esau (ndiye Edomu), na hawa ndio waliokuwa wakuu wao.
Estos fueron los hijos de Esaú (es decir, Edom), y éstos fueron sus jefes.
20 Hawa ndio walikuwa wana wa Seiri, Mhori, waliokuwa wakiishi katika nchi ile: Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana,
Estos son los hijos de Seir el horeo que vivían en ese país; Lotán, Sobal, Zibeon, Ana,
21 Dishoni, Eseri na Dishani. Hawa ndio wana wa Seiri huko Edomu waliokuwa wakuu kwa Wahori.
Disón, Ezer y Disán: estos son los jefes de los horeos, hijos de Seir, en la tierra de Edom.
22 Wana wa Lotani walikuwa: Hori na Homamu. Timna alikuwa dada yake Lotani.
Los hijos de Lotán fueron Hori y Hemam; La hermana de Lotan era Timna.
23 Wana wa Shobali walikuwa: Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo na Onamu.
Y estos son los hijos de Sobal: Alvan, Manahat, Ebal, Sefo y Onam.
24 Wana wa Sibeoni walikuwa: Aiya na Ana. Huyu Ana ndiye aligundua chemchemi ya maji moto jangwani alipokuwa akichunga punda za Sibeoni baba yake.
Y estos son los hijos de Zibeón: Aja y Aná; el mismo Ana que hizo el descubrimiento de los manantiales en la tierra baldía, cuando estaba cuidando los asnos de su padre Zibeon.
25 Watoto wa Ana walikuwa: Dishoni na Oholibama binti wa Ana.
Y estos son los hijos de Aná: Disón y Aholibama su hija.
26 Wana wa Dishoni walikuwa: Hemdani, Eshbani, Ithrani na Kerani.
Estos son los hijos de Disón: Hemdan, Esban, Itran y Queran.
27 Wana wa Eseri walikuwa: Bilhani, Zaavani na Akani.
Estos son los hijos de Ezer: Bilhan, Zaavan y Acan.
28 Wana wa Dishani walikuwa: Usi na Arani.
Estos son los hijos de Disán: Uz y Arán.
29 Hawa ndio waliokuwa wakuu wa Wahori: Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana,
Estos fueron los jefes de los horeos: Lotán, Sobal, Zibeón, Aná,
30 Dishoni, Eseri na Dishani. Hawa ndio walikuwa wakuu wa Wahori, kufuatana na makundi yao, katika nchi ya Seiri.
Disón, Ezer y Disán. Tales fueron los jefes horeos en su orden en la tierra de Seir.
31 Wafuatao ni wafalme waliotawala Edomu kabla ya mfalme yeyote wa Israeli kutawala:
Y estos son los reyes que gobernaban en la tierra de Edom antes que hubiera rey sobre los hijos de Israel.
32 Bela mwana wa Beori alikuwa mfalme wa Edomu. Mji wake uliitwa Dinhaba.
Bela, hijo de Beor, fue rey en Edom, y el nombre de su ciudad principal fue Dinaba.
33 Bela alipofariki, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosra akawa mfalme baada yake.
En su muerte, Jobab, hijo de Zera de Bosra, fue rey en su lugar.
34 Yobabu alipofariki, Hushamu kutoka nchi ya Watemani akawa mfalme baada yake.
Y a la muerte de Jobab, Husam, de la tierra de los temanitas, llegó a ser rey en su lugar.
35 Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi, aliyeshinda Midiani katika nchi ya Moabu, akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Avithi.
Y a la muerte de Husam, Hadad, hijo de Bedad, que venció a los madianitas en el campo de Moab, llegó a ser rey; su ciudad principal fue llamada Avit.
36 Hadadi alipofariki, Samla kutoka Masreka akawa mfalme baada yake.
Y a la muerte de Hadad, Samlat de Masreca se convirtió en rey.
37 Samla alipofariki, Shauli kutoka Rehobothi ngʼambo ya Mto Frati akawa mfalme baada yake.
Y a la muerte de Samla, Saúl de Rehobot junto al río se hizo rey en su lugar.
38 Shauli alipofariki, Baal-Hanani mwana wa Akbori akawa mfalme baada yake.
Y a la muerte de Saúl, Baal-hanán, hijo de Acbor, se hizo rey.
39 Baal-Hanani mwana wa Akbori alipofariki, Hadadi akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Pau, na mkewe aliitwa Mehetabeli binti Matredi, binti Me-Zahabu.
Y en la muerte de Baal-hanan, Hadar se hizo rey en su lugar; su ciudad principal se llamaba Pau, y el nombre de su esposa era Mehetabel; ella era la hija de Matred, la hija de Mezaab.
40 Hawa ndio wakuu waliotokana na Esau, kwa majina, kufuatana na koo zao na nchi zao: Timna, Alva, Yethethi,
Estos son los nombres de los jefes de Esaú por orden de sus familias y sus lugares: Timna, Alva, Jetet,
41 Oholibama, Ela, Pinoni,
Aholibama, Elah, Pinón,
42 Kenazi, Temani, Mibsari,
Cenaz, Teman, Mibzar,
43 Magdieli na Iramu. Hawa ndio walikuwa wakuu wa Edomu, kufuatana na makazi yao katika nchi waliyoimiliki. Huyu ndiye alikuwa Esau, baba wa Waedomu.
Magdiel, Iram; estos son los jefes edomitas, en sus lugares en su herencia; este es Esaú, el padre de los edomitas.

< Mwanzo 36 >