< Mwanzo 36 >
1 Hivi ndivyo vizazi vya Esau (yaani Edomu).
These were the descendants of Esau (also called Edom).
2 Esau akaoa wake kutoka miongoni mwa wanawake wa Kanaani: Ada binti wa Eloni Mhiti, Oholibama binti wa Ana, mjukuu wa kike wa Sibeoni Mhivi,
Esau took his wives from the Canaanites. These were his wives: Adah the daughter of Elon the Hittite; Oholibamah the daughter of Anah, the granddaughter of Zibeon the Hivite;
3 pia akaoa Basemathi binti wa Ishmaeli, dada yake Nebayothi.
and Basemath, Ishmael's daughter, sister of Nebaioth.
4 Ada akamzalia Esau Elifazi, Basemathi akamzaa Reueli,
Adah bore Eliphaz to Esau, and Basemath bore Reuel.
5 Oholibama akamzaa Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wana wa Esau waliozaliwa kwake huko Kanaani.
Oholibamah bore Jeush, Jalam, and Korah. These were the sons of Esau who were born to him in the land of Canaan.
6 Esau akawachukua wake zake, watoto wake wa kiume na wa kike na wote wa nyumbani mwake, mifugo yake pamoja na wanyama wake wengine wote na mali yake yote ambayo alikuwa ameipata akiwa Kanaani, akahamia katika nchi iliyo mbali na Yakobo ndugu yake.
Esau took his wives, his sons, his daughters, and all the members of his household, his livestock—all his animals, and all his possessions, which he had gathered in the land of Canaan, and went into a land away from his brother Jacob.
7 Mali zao zilikuwa nyingi sana kiasi kwamba haikuwa rahisi wao kuishi pamoja, nchi waliyokuwa wakiishi isingewatosha wote kwa ajili ya mifugo yao.
He did this because their possessions were too many for them to stay together. The land where they had settled could not support them because of their livestock.
8 Kwa hiyo Esau (ambaye ni Edomu) aliishi katika nchi ya kilima huko Seiri.
So Esau, also known as Edom, settled in the hill country of Seir.
9 Hawa ndio wazao wa Esau, baba wa Waedomu, katika nchi ya kilima cha Seiri.
These were the descendants of Esau, the ancestor of the Edomites in the hill country of Seir.
10 Haya ndiyo majina ya wana wa Esau: Elifazi, mwana wa Esau ambaye mkewe Ada alimzalia; na Reueli, mwana wa Esau ambaye mkewe Basemathi alimzalia.
These were the names of Esau's sons: Eliphaz son of Adah, the wife of Esau; Reuel son of Basemath, the wife of Esau.
11 Wana wa Elifazi ni: Temani, Omari, Sefo, Gatamu na Kenazi.
The sons of Eliphaz were Teman, Omar, Zepho, Gatam, and Kenaz.
12 Elifazi mwana wa Esau alikuwa pia na suria aliyeitwa Timna, ambaye alimzalia Amaleki. Hawa ndio waliokuwa wajukuu wa Ada mke wa Esau.
Timna, a concubine of Eliphaz, Esau's son, bore Amalek. These were the grandsons of Adah, Esau's wife.
13 Wana wa Reueli ni: Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio waliokuwa wajukuu wa Basemathi mkewe Esau.
These were the sons of Reuel: Nahath, Zerah, Shammah, and Mizzah. These were the grandsons of Basemath, Esau's wife.
14 Wana wa Oholibama binti Ana, mkewe Esau, aliyekuwa mjukuu wa Sibeoni, aliomzalia Esau ni: Yeushi, Yalamu na Kora.
These were the sons of Oholibamah, Esau's wife, who was the daughter of Anah and the granddaughter of Zibeon. She bore to Esau Jeush, Jalam, and Korah.
15 Hawa ndio waliokuwa wakuu miongoni mwa wazao wa Esau: Wakuu wa wana wa Elifazi, mzaliwa wa kwanza wa Esau ni: Temani, Omari, Sefo, Kenazi,
These were the clans among Esau's descendants: the descendants of Eliphaz, the firstborn of Esau: Teman, Omar, Zepho, Kenaz,
16 Kora, Gatamu na Amaleki. Hawa ndio waliokuwa wakuu waliotoka kwa Elifazi huko Edomu, waliokuwa wajukuu wa kiume wa Ada.
Korah, Gatam, and Amalek. These were the clans descended from Eliphaz in the land of Edom. They were the grandsons of Adah.
17 Wakuu wa wana wa Reueli, mwana wa Esau ni: Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa Reueli huko Edomu, waliokuwa wajukuu wa kiume wa Basemathi mkewe Esau.
These were the clans from Reuel, Esau's son: Nahath, Zerah, Shammah, Mizzah. These were the clans descended from Reuel in the land of Edom. They were the grandsons of Basemath, Esau's wife.
18 Wakuu wa wana wa Esau ambao mkewe Oholibama alimzalia ni: Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa mke wa Esau, Oholibama binti Ana.
These were the clans of Oholibamah, Esau's wife: Jeush, Jalam, Korah. These are the clans that descended from Esau's wife Oholibamah, daughter of Anah.
19 Hawa ndio waliokuwa wana wa Esau (ndiye Edomu), na hawa ndio waliokuwa wakuu wao.
These were the sons of Esau (who was known as Edom), and these were their chiefs.
20 Hawa ndio walikuwa wana wa Seiri, Mhori, waliokuwa wakiishi katika nchi ile: Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana,
These were the sons of Seir the Horite, the inhabitants of the land: Lotan, Shobal, Zibeon, Anah,
21 Dishoni, Eseri na Dishani. Hawa ndio wana wa Seiri huko Edomu waliokuwa wakuu kwa Wahori.
Dishon, Ezer, and Dishan. These were the clans of the Horites, the inhabitants of Seir in the land of Edom.
22 Wana wa Lotani walikuwa: Hori na Homamu. Timna alikuwa dada yake Lotani.
The sons of Lotan were Hori and Heman, and Timna was Lotan's sister.
23 Wana wa Shobali walikuwa: Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo na Onamu.
These were the sons of Shobal: Alvan, Manahath, Ebal, Shepho, and Onam.
24 Wana wa Sibeoni walikuwa: Aiya na Ana. Huyu Ana ndiye aligundua chemchemi ya maji moto jangwani alipokuwa akichunga punda za Sibeoni baba yake.
These were the sons of Zibeon: Aiah and Anah. This is Anah who found the hot springs in the wilderness, as he was pasturing donkeys of Zibeon his father.
25 Watoto wa Ana walikuwa: Dishoni na Oholibama binti wa Ana.
These were the children of Anah: Dishon and Oholibamah, the daughter of Anah.
26 Wana wa Dishoni walikuwa: Hemdani, Eshbani, Ithrani na Kerani.
These were the sons of Dishon: Hemdan, Eshban, Ithran, and Keran.
27 Wana wa Eseri walikuwa: Bilhani, Zaavani na Akani.
These were the sons of Ezer: Bilhan, Zaavan, and Akan.
28 Wana wa Dishani walikuwa: Usi na Arani.
These were the sons of Dishan: Uz and Aran.
29 Hawa ndio waliokuwa wakuu wa Wahori: Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana,
These were the clans of the Horites: Lotan, Shobal, Zibeon, and Anah,
30 Dishoni, Eseri na Dishani. Hawa ndio walikuwa wakuu wa Wahori, kufuatana na makundi yao, katika nchi ya Seiri.
Dishon, Ezer, Dishan: These were clans of the Horites, according to their clan lists in the land of Seir.
31 Wafuatao ni wafalme waliotawala Edomu kabla ya mfalme yeyote wa Israeli kutawala:
These were the kings who reigned in the land of Edom before any king reigned over the Israelites:
32 Bela mwana wa Beori alikuwa mfalme wa Edomu. Mji wake uliitwa Dinhaba.
Bela son of Beor, reigned in Edom, and the name of his city was Dinhabah.
33 Bela alipofariki, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosra akawa mfalme baada yake.
When Bela died, then Jobab son of Zerah of Bozrah, reigned in his place.
34 Yobabu alipofariki, Hushamu kutoka nchi ya Watemani akawa mfalme baada yake.
When Jobab died, Husham who was of the land of the Temanites, reigned in his place.
35 Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi, aliyeshinda Midiani katika nchi ya Moabu, akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Avithi.
When Husham died, Hadad son of Bedad who defeated the Midianites in the land of Moab, reigned in his place. The name of his city was Avith.
36 Hadadi alipofariki, Samla kutoka Masreka akawa mfalme baada yake.
When Hadad died, then Samlah of Masrekah reigned in his place.
37 Samla alipofariki, Shauli kutoka Rehobothi ngʼambo ya Mto Frati akawa mfalme baada yake.
When Samlah died, then Shaul of Rehoboth by the river reigned in his place.
38 Shauli alipofariki, Baal-Hanani mwana wa Akbori akawa mfalme baada yake.
When Shaul died, then Baal-Hanan son of Akbor reigned in his place.
39 Baal-Hanani mwana wa Akbori alipofariki, Hadadi akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Pau, na mkewe aliitwa Mehetabeli binti Matredi, binti Me-Zahabu.
When Baal-Hanan son of Akbor, died, then Hadar reigned in his place. The name of his city was Pau. His wife's name was Mehetabel, the daughter of Matred, the granddaughter of Me Zahab.
40 Hawa ndio wakuu waliotokana na Esau, kwa majina, kufuatana na koo zao na nchi zao: Timna, Alva, Yethethi,
These were the names of the heads of clans from Esau's descendants, according to their clans and their regions, by their names: Timna, Alvah, Jetheth,
41 Oholibama, Ela, Pinoni,
Oholibamah, Elah, Pinon,
42 Kenazi, Temani, Mibsari,
Kenaz, Teman, Mibzar,
43 Magdieli na Iramu. Hawa ndio walikuwa wakuu wa Edomu, kufuatana na makazi yao katika nchi waliyoimiliki. Huyu ndiye alikuwa Esau, baba wa Waedomu.
Magdiel, and Iram. These were the clan heads of Edom, according to their settlements in the land they possessed. This was Esau, the father of the Edomites.