< Mwanzo 36 >

1 Hivi ndivyo vizazi vya Esau (yaani Edomu).
and these generation Esau he/she/it Edom
2 Esau akaoa wake kutoka miongoni mwa wanawake wa Kanaani: Ada binti wa Eloni Mhiti, Oholibama binti wa Ana, mjukuu wa kike wa Sibeoni Mhivi,
Esau to take: take [obj] woman: wife his from daughter Canaan [obj] Adah daughter Elon [the] Hittite and [obj] Oholibamah daughter Anah daughter Zibeon [the] Hivite
3 pia akaoa Basemathi binti wa Ishmaeli, dada yake Nebayothi.
and [obj] Basemath daughter Ishmael sister Nebaioth
4 Ada akamzalia Esau Elifazi, Basemathi akamzaa Reueli,
and to beget Adah to/for Esau [obj] Eliphaz and Basemath to beget [obj] Reuel
5 Oholibama akamzaa Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wana wa Esau waliozaliwa kwake huko Kanaani.
and Oholibamah to beget [obj] (Jeush *Q(K)*) and [obj] Jalam and [obj] Korah these son: child Esau which to beget to/for him in/on/with land: country/planet Canaan
6 Esau akawachukua wake zake, watoto wake wa kiume na wa kike na wote wa nyumbani mwake, mifugo yake pamoja na wanyama wake wengine wote na mali yake yote ambayo alikuwa ameipata akiwa Kanaani, akahamia katika nchi iliyo mbali na Yakobo ndugu yake.
and to take: take Esau [obj] woman: wife his and [obj] son: child his and [obj] daughter his and [obj] all soul: person house: household his and [obj] livestock his and [obj] all animal his and [obj] all acquisition his which to gather in/on/with land: country/planet Canaan and to go: went to(wards) land: country/planet from face: before Jacob brother: male-sibling his
7 Mali zao zilikuwa nyingi sana kiasi kwamba haikuwa rahisi wao kuishi pamoja, nchi waliyokuwa wakiishi isingewatosha wote kwa ajili ya mifugo yao.
for to be property their many from to dwell together and not be able land: country/planet sojourning their to/for to lift: aid [obj] them from face: because livestock their
8 Kwa hiyo Esau (ambaye ni Edomu) aliishi katika nchi ya kilima huko Seiri.
and to dwell Esau in/on/with mountain: hill country Seir Esau he/she/it Edom
9 Hawa ndio wazao wa Esau, baba wa Waedomu, katika nchi ya kilima cha Seiri.
and these generation Esau father Edom in/on/with mountain: hill country Seir
10 Haya ndiyo majina ya wana wa Esau: Elifazi, mwana wa Esau ambaye mkewe Ada alimzalia; na Reueli, mwana wa Esau ambaye mkewe Basemathi alimzalia.
these name son: child Esau Eliphaz son: child Adah woman: wife Esau Reuel son: child Basemath woman: wife Esau
11 Wana wa Elifazi ni: Temani, Omari, Sefo, Gatamu na Kenazi.
and to be son: child Eliphaz Teman Omar Zepho and Gatam and Kenaz
12 Elifazi mwana wa Esau alikuwa pia na suria aliyeitwa Timna, ambaye alimzalia Amaleki. Hawa ndio waliokuwa wajukuu wa Ada mke wa Esau.
and Timna to be concubine to/for Eliphaz son: child Esau and to beget to/for Eliphaz [obj] Amalek these son: child Adah woman: wife Esau
13 Wana wa Reueli ni: Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio waliokuwa wajukuu wa Basemathi mkewe Esau.
and these son: child Reuel Nahath and Zerah Shammah and Mizzah these to be son: child Basemath woman: wife Esau
14 Wana wa Oholibama binti Ana, mkewe Esau, aliyekuwa mjukuu wa Sibeoni, aliomzalia Esau ni: Yeushi, Yalamu na Kora.
and these to be son: child Oholibamah daughter Anah daughter Zibeon woman: wife Esau and to beget to/for Esau [obj] (Jeush *Q(K)*) and [obj] Jalam and [obj] Korah
15 Hawa ndio waliokuwa wakuu miongoni mwa wazao wa Esau: Wakuu wa wana wa Elifazi, mzaliwa wa kwanza wa Esau ni: Temani, Omari, Sefo, Kenazi,
these chief son: child Esau son: child Eliphaz firstborn Esau chief Teman chief Omar chief Zepho chief Kenaz
16 Kora, Gatamu na Amaleki. Hawa ndio waliokuwa wakuu waliotoka kwa Elifazi huko Edomu, waliokuwa wajukuu wa kiume wa Ada.
chief Korah chief Gatam chief Amalek these chief Eliphaz in/on/with land: country/planet Edom these son: descendant/people Adah
17 Wakuu wa wana wa Reueli, mwana wa Esau ni: Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa Reueli huko Edomu, waliokuwa wajukuu wa kiume wa Basemathi mkewe Esau.
and these son: child Reuel son: child Esau chief Nahath chief Zerah chief Shammah chief Mizzah these chief Reuel in/on/with land: country/planet Edom these son: child Basemath woman: wife Esau
18 Wakuu wa wana wa Esau ambao mkewe Oholibama alimzalia ni: Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa mke wa Esau, Oholibama binti Ana.
and these son: child Oholibamah woman: wife Esau chief Jeush chief Jalam chief Korah these chief Oholibamah daughter Anah woman: wife Esau
19 Hawa ndio waliokuwa wana wa Esau (ndiye Edomu), na hawa ndio waliokuwa wakuu wao.
these son: child Esau and these chief their he/she/it Edom
20 Hawa ndio walikuwa wana wa Seiri, Mhori, waliokuwa wakiishi katika nchi ile: Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana,
these son: child Seir [the] Horite to dwell [the] land: country/planet Lotan and Shobal and Zibeon and Anah
21 Dishoni, Eseri na Dishani. Hawa ndio wana wa Seiri huko Edomu waliokuwa wakuu kwa Wahori.
and Dishon and Ezer and Dishan these chief [the] Horite son: child Seir in/on/with land: country/planet Edom
22 Wana wa Lotani walikuwa: Hori na Homamu. Timna alikuwa dada yake Lotani.
and to be son: child Lotan Hori and Hemam and sister Lotan Timna
23 Wana wa Shobali walikuwa: Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo na Onamu.
and these son: child Shobal Alvan and Manahath and Ebal Shepho and Onam
24 Wana wa Sibeoni walikuwa: Aiya na Ana. Huyu Ana ndiye aligundua chemchemi ya maji moto jangwani alipokuwa akichunga punda za Sibeoni baba yake.
and these son: child Zibeon and Aiah and Anah he/she/it Anah which to find [obj] [the] hot spring in/on/with wilderness in/on/with to pasture he [obj] [the] donkey to/for Zibeon father his
25 Watoto wa Ana walikuwa: Dishoni na Oholibama binti wa Ana.
and these son: child Anah Dishon and Oholibamah daughter Anah
26 Wana wa Dishoni walikuwa: Hemdani, Eshbani, Ithrani na Kerani.
and these son: child Dishon Hemdan and Eshban and Ithran and Cheran
27 Wana wa Eseri walikuwa: Bilhani, Zaavani na Akani.
these son: child Ezer Bilhan and Zaavan and Akan
28 Wana wa Dishani walikuwa: Usi na Arani.
these son: child Dishan Uz and Aran
29 Hawa ndio waliokuwa wakuu wa Wahori: Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana,
these chief [the] Horite chief Lotan chief Shobal chief Zibeon chief Anah
30 Dishoni, Eseri na Dishani. Hawa ndio walikuwa wakuu wa Wahori, kufuatana na makundi yao, katika nchi ya Seiri.
chief Dishon chief Ezer chief Dishan these chief [the] Hori to/for chief their in/on/with land: country/planet Seir
31 Wafuatao ni wafalme waliotawala Edomu kabla ya mfalme yeyote wa Israeli kutawala:
and these [the] king which to reign in/on/with land: country/planet Edom to/for face: before to reign king to/for son: descendant/people Israel
32 Bela mwana wa Beori alikuwa mfalme wa Edomu. Mji wake uliitwa Dinhaba.
and to reign in/on/with Edom Bela son: child Beor and name city his Dinhabah
33 Bela alipofariki, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosra akawa mfalme baada yake.
and to die Bela and to reign underneath: instead him Jobab son: child Zerah from Bozrah
34 Yobabu alipofariki, Hushamu kutoka nchi ya Watemani akawa mfalme baada yake.
and to die Jobab and to reign underneath: instead him Husham from land: country/planet [the] Temanite
35 Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi, aliyeshinda Midiani katika nchi ya Moabu, akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Avithi.
and to die Husham and to reign underneath: instead him Hadad son: child Bedad [the] to smite [obj] Midian in/on/with land: country Moab and name city his Avith
36 Hadadi alipofariki, Samla kutoka Masreka akawa mfalme baada yake.
and to die Hadad and to reign underneath: instead him Samlah from Masrekah
37 Samla alipofariki, Shauli kutoka Rehobothi ngʼambo ya Mto Frati akawa mfalme baada yake.
and to die Samlah and to reign underneath: instead him Shaul from Rehoboth [the] River
38 Shauli alipofariki, Baal-Hanani mwana wa Akbori akawa mfalme baada yake.
and to die Shaul and to reign underneath: instead him Baal-hanan Baal-hanan son: child Achbor
39 Baal-Hanani mwana wa Akbori alipofariki, Hadadi akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Pau, na mkewe aliitwa Mehetabeli binti Matredi, binti Me-Zahabu.
and to die Baal-hanan Baal-hanan son: child Achbor and to reign underneath: instead him Hadar and name city his Pau and name woman: wife his Mehetabel daughter Matred daughter Mezahab Mezahab
40 Hawa ndio wakuu waliotokana na Esau, kwa majina, kufuatana na koo zao na nchi zao: Timna, Alva, Yethethi,
and these name chief Esau to/for family their to/for place their in/on/with name their chief Timna chief Alvah chief Jetheth
41 Oholibama, Ela, Pinoni,
chief Oholibamah chief Elah chief Pinon
42 Kenazi, Temani, Mibsari,
chief Kenaz chief Teman chief Mibzar
43 Magdieli na Iramu. Hawa ndio walikuwa wakuu wa Edomu, kufuatana na makazi yao katika nchi waliyoimiliki. Huyu ndiye alikuwa Esau, baba wa Waedomu.
chief Magdiel chief Iram these chief Edom to/for seat their in/on/with land: country/planet possession their he/she/it Esau father Edom

< Mwanzo 36 >