< Mwanzo 36 >
1 Hivi ndivyo vizazi vya Esau (yaani Edomu).
This is the account of Esau (that is, Edom).
2 Esau akaoa wake kutoka miongoni mwa wanawake wa Kanaani: Ada binti wa Eloni Mhiti, Oholibama binti wa Ana, mjukuu wa kike wa Sibeoni Mhivi,
Esau took his wives from the daughters of Canaan: Adah daughter of Elon the Hittite, Oholibamah daughter of Anah and granddaughter of Zibeon the Hivite,
3 pia akaoa Basemathi binti wa Ishmaeli, dada yake Nebayothi.
and Basemath daughter of Ishmael and sister of Nebaioth.
4 Ada akamzalia Esau Elifazi, Basemathi akamzaa Reueli,
And Adah bore Eliphaz to Esau, Basemath gave birth to Reuel,
5 Oholibama akamzaa Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wana wa Esau waliozaliwa kwake huko Kanaani.
and Oholibamah gave birth to Jeush, Jalam, and Korah. These were the sons of Esau, who were born to him in the land of Canaan.
6 Esau akawachukua wake zake, watoto wake wa kiume na wa kike na wote wa nyumbani mwake, mifugo yake pamoja na wanyama wake wengine wote na mali yake yote ambayo alikuwa ameipata akiwa Kanaani, akahamia katika nchi iliyo mbali na Yakobo ndugu yake.
Later, Esau took his wives and sons and daughters and all the people of his household, along with his livestock, all his other animals, and all the property he had acquired in Canaan, and he moved to a land far away from his brother Jacob.
7 Mali zao zilikuwa nyingi sana kiasi kwamba haikuwa rahisi wao kuishi pamoja, nchi waliyokuwa wakiishi isingewatosha wote kwa ajili ya mifugo yao.
For their possessions were too great for them to dwell together; the land where they stayed could not support them because of their livestock.
8 Kwa hiyo Esau (ambaye ni Edomu) aliishi katika nchi ya kilima huko Seiri.
So Esau (that is, Edom) settled in the area of Mount Seir.
9 Hawa ndio wazao wa Esau, baba wa Waedomu, katika nchi ya kilima cha Seiri.
This is the account of Esau, the father of the Edomites, in the area of Mount Seir.
10 Haya ndiyo majina ya wana wa Esau: Elifazi, mwana wa Esau ambaye mkewe Ada alimzalia; na Reueli, mwana wa Esau ambaye mkewe Basemathi alimzalia.
These are the names of Esau’s sons: Eliphaz son of Esau’s wife Adah, and Reuel son of Esau’s wife Basemath.
11 Wana wa Elifazi ni: Temani, Omari, Sefo, Gatamu na Kenazi.
The sons of Eliphaz were Teman, Omar, Zepho, Gatam, and Kenaz.
12 Elifazi mwana wa Esau alikuwa pia na suria aliyeitwa Timna, ambaye alimzalia Amaleki. Hawa ndio waliokuwa wajukuu wa Ada mke wa Esau.
Additionally, Timna, a concubine of Esau’s son Eliphaz, gave birth to Amalek. These are the grandsons of Esau’s wife Adah.
13 Wana wa Reueli ni: Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio waliokuwa wajukuu wa Basemathi mkewe Esau.
These are the sons of Reuel: Nahath, Zerah, Shammah, and Mizzah. They are the grandsons of Esau’s wife Basemath.
14 Wana wa Oholibama binti Ana, mkewe Esau, aliyekuwa mjukuu wa Sibeoni, aliomzalia Esau ni: Yeushi, Yalamu na Kora.
These are the sons of Esau’s wife Oholibamah (daughter of Anah and granddaughter of Zibeon) whom she bore to Esau: Jeush, Jalam, and Korah.
15 Hawa ndio waliokuwa wakuu miongoni mwa wazao wa Esau: Wakuu wa wana wa Elifazi, mzaliwa wa kwanza wa Esau ni: Temani, Omari, Sefo, Kenazi,
These are the chiefs among the sons of Esau. The sons of Eliphaz the firstborn of Esau: Chiefs Teman, Omar, Zepho, Kenaz,
16 Kora, Gatamu na Amaleki. Hawa ndio waliokuwa wakuu waliotoka kwa Elifazi huko Edomu, waliokuwa wajukuu wa kiume wa Ada.
Korah, Gatam, and Amalek. They are the chiefs of Eliphaz in the land of Edom, and they are the grandsons of Adah.
17 Wakuu wa wana wa Reueli, mwana wa Esau ni: Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa Reueli huko Edomu, waliokuwa wajukuu wa kiume wa Basemathi mkewe Esau.
These are the sons of Esau’s son Reuel: Chiefs Nahath, Zerah, Shammah, and Mizzah. They are the chiefs descended from Reuel in the land of Edom, and they are the grandsons of Esau’s wife Basemath.
18 Wakuu wa wana wa Esau ambao mkewe Oholibama alimzalia ni: Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa mke wa Esau, Oholibama binti Ana.
These are the sons of Esau’s wife Oholibamah: Chiefs Jeush, Jalam, and Korah. They are the chiefs descended from Esau’s wife Oholibamah, the daughter of Anah.
19 Hawa ndio waliokuwa wana wa Esau (ndiye Edomu), na hawa ndio waliokuwa wakuu wao.
All these are the sons of Esau (that is, Edom), and they were their chiefs.
20 Hawa ndio walikuwa wana wa Seiri, Mhori, waliokuwa wakiishi katika nchi ile: Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana,
These are the sons of Seir the Horite, who were living in the land: Lotan, Shobal, Zibeon, Anah,
21 Dishoni, Eseri na Dishani. Hawa ndio wana wa Seiri huko Edomu waliokuwa wakuu kwa Wahori.
Dishon, Ezer, and Dishan. They are the chiefs of the Horites, the descendants of Seir in the land of Edom.
22 Wana wa Lotani walikuwa: Hori na Homamu. Timna alikuwa dada yake Lotani.
The sons of Lotan were Hori and Hemam. Timna was Lotan’s sister.
23 Wana wa Shobali walikuwa: Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo na Onamu.
These are the sons of Shobal: Alvan, Manahath, Ebal, Shepho, and Onam.
24 Wana wa Sibeoni walikuwa: Aiya na Ana. Huyu Ana ndiye aligundua chemchemi ya maji moto jangwani alipokuwa akichunga punda za Sibeoni baba yake.
These are the sons of Zibeon: Aiah and Anah. (This is the Anah who found the hot springs in the wilderness as he was pasturing the donkeys of his father Zibeon.)
25 Watoto wa Ana walikuwa: Dishoni na Oholibama binti wa Ana.
These are the children of Anah: Dishon and Oholibamah daughter of Anah.
26 Wana wa Dishoni walikuwa: Hemdani, Eshbani, Ithrani na Kerani.
These are the sons of Dishon: Hemdan, Eshban, Ithran, and Cheran.
27 Wana wa Eseri walikuwa: Bilhani, Zaavani na Akani.
These are the sons of Ezer: Bilhan, Zaavan, and Akan.
28 Wana wa Dishani walikuwa: Usi na Arani.
These are the sons of Dishan: Uz and Aran.
29 Hawa ndio waliokuwa wakuu wa Wahori: Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana,
These are the chiefs of the Horites: Chiefs Lotan, Shobal, Zibeon, Anah,
30 Dishoni, Eseri na Dishani. Hawa ndio walikuwa wakuu wa Wahori, kufuatana na makundi yao, katika nchi ya Seiri.
Dishon, Ezer, and Dishan. They are the chiefs of the Horites, according to their divisions in the land of Seir.
31 Wafuatao ni wafalme waliotawala Edomu kabla ya mfalme yeyote wa Israeli kutawala:
These are the kings who reigned in the land of Edom before any king reigned over the Israelites:
32 Bela mwana wa Beori alikuwa mfalme wa Edomu. Mji wake uliitwa Dinhaba.
Bela son of Beor reigned in Edom; the name of his city was Dinhabah.
33 Bela alipofariki, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosra akawa mfalme baada yake.
When Bela died, Jobab son of Zerah from Bozrah reigned in his place.
34 Yobabu alipofariki, Hushamu kutoka nchi ya Watemani akawa mfalme baada yake.
When Jobab died, Husham from the land of the Temanites reigned in his place.
35 Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi, aliyeshinda Midiani katika nchi ya Moabu, akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Avithi.
When Husham died, Hadad son of Bedad, who defeated Midian in the country of Moab, reigned in his place. And the name of his city was Avith.
36 Hadadi alipofariki, Samla kutoka Masreka akawa mfalme baada yake.
When Hadad died, Samlah from Masrekah reigned in his place.
37 Samla alipofariki, Shauli kutoka Rehobothi ngʼambo ya Mto Frati akawa mfalme baada yake.
When Samlah died, Shaul from Rehoboth on the Euphrates reigned in his place.
38 Shauli alipofariki, Baal-Hanani mwana wa Akbori akawa mfalme baada yake.
When Shaul died, Baal-hanan son of Achbor reigned in his place.
39 Baal-Hanani mwana wa Akbori alipofariki, Hadadi akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Pau, na mkewe aliitwa Mehetabeli binti Matredi, binti Me-Zahabu.
When Baal-hanan son of Achbor died, Hadad reigned in his place. His city was named Pau, and his wife’s name was Mehetabel daughter of Matred, the daughter of Me-zahab.
40 Hawa ndio wakuu waliotokana na Esau, kwa majina, kufuatana na koo zao na nchi zao: Timna, Alva, Yethethi,
These are the names of Esau’s chiefs, according to their families and regions, by their names: Chiefs Timna, Alvah, Jetheth,
41 Oholibama, Ela, Pinoni,
Oholibamah, Elah, Pinon,
42 Kenazi, Temani, Mibsari,
Kenaz, Teman, Mibzar,
43 Magdieli na Iramu. Hawa ndio walikuwa wakuu wa Edomu, kufuatana na makazi yao katika nchi waliyoimiliki. Huyu ndiye alikuwa Esau, baba wa Waedomu.
Magdiel, and Iram. These were the chiefs of Edom, according to their settlements in the land they possessed. Esau was the father of the Edomites.