< Mwanzo 36 >

1 Hivi ndivyo vizazi vya Esau (yaani Edomu).
Magi e joka Esau (ma tiende ni Edom).
2 Esau akaoa wake kutoka miongoni mwa wanawake wa Kanaani: Ada binti wa Eloni Mhiti, Oholibama binti wa Ana, mjukuu wa kike wa Sibeoni Mhivi,
Esau nokendo nyi Kanaan: Ada nyar Elon ja-Hiti, kod Oholibama nyar Ana ma nyakwar Zibeon ja-Hivi,
3 pia akaoa Basemathi binti wa Ishmaeli, dada yake Nebayothi.
gi Basemath nyar Ishmael kendo ma nyamin Nebayoth.
4 Ada akamzalia Esau Elifazi, Basemathi akamzaa Reueli,
Ada nonywolone Esau Elifaz, to Basemath nonywolo Reuel,
5 Oholibama akamzaa Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wana wa Esau waliozaliwa kwake huko Kanaani.
kendo Oholibama nonywolo Jeush, Jalam kod Kora. Magi ema ne yawuot Esau, mane onywol Kanaan.
6 Esau akawachukua wake zake, watoto wake wa kiume na wa kike na wote wa nyumbani mwake, mifugo yake pamoja na wanyama wake wengine wote na mali yake yote ambayo alikuwa ameipata akiwa Kanaani, akahamia katika nchi iliyo mbali na Yakobo ndugu yake.
Esau nokawo monde, yawuote, nyige kod joode duto kaachiel gi jambe duto kod mwandu duto mane oyudo Kanaan, kendo nodhi e piny moro mabor gi Jakobo owadgi.
7 Mali zao zilikuwa nyingi sana kiasi kwamba haikuwa rahisi wao kuishi pamoja, nchi waliyokuwa wakiishi isingewatosha wote kwa ajili ya mifugo yao.
Mwandugi ne ngʼeny makoro ne ok ginyal dak kamoro achiel; piny mane gidakie ne tin ma ok nyal romogi nikech kwethgi.
8 Kwa hiyo Esau (ambaye ni Edomu) aliishi katika nchi ya kilima huko Seiri.
Kuom mano Esau (ma tiende ni Edom) nodhi odak e piny gode man Seir.
9 Hawa ndio wazao wa Esau, baba wa Waedomu, katika nchi ya kilima cha Seiri.
Ma e nonro mar joka Esau ma kwar jo-Edom manodak e piny gode mar Seir.
10 Haya ndiyo majina ya wana wa Esau: Elifazi, mwana wa Esau ambaye mkewe Ada alimzalia; na Reueli, mwana wa Esau ambaye mkewe Basemathi alimzalia.
Magi e nying yawuot Esau: Elifaz wuod Esau mane Ada onywolone, kod Reuel wuod Esau mane Basemath onywolone.
11 Wana wa Elifazi ni: Temani, Omari, Sefo, Gatamu na Kenazi.
Elifaz nonywolo: Teman, Omar, Zefo, Gatam kod Kenaz.
12 Elifazi mwana wa Esau alikuwa pia na suria aliyeitwa Timna, ambaye alimzalia Amaleki. Hawa ndio waliokuwa wajukuu wa Ada mke wa Esau.
Elifaz wuod Esau bende ne nigi jatich madhako miluongo ni Timna mane onywolone Amalek. Magi ema ne nyikwa Ada chi Esau.
13 Wana wa Reueli ni: Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio waliokuwa wajukuu wa Basemathi mkewe Esau.
Yawuot Reuel ne gin: Nahath, Zera, Shama kod Miza. Magi ema ne nyikwa Basemath chi Esau.
14 Wana wa Oholibama binti Ana, mkewe Esau, aliyekuwa mjukuu wa Sibeoni, aliomzalia Esau ni: Yeushi, Yalamu na Kora.
Yawuot Oholibama, chi Esau ma nyar Ana kendo nyakwar Zibeon mane onywolone Esau ne gin: Jeush, Jalam kod Kora.
15 Hawa ndio waliokuwa wakuu miongoni mwa wazao wa Esau: Wakuu wa wana wa Elifazi, mzaliwa wa kwanza wa Esau ni: Temani, Omari, Sefo, Kenazi,
Magi ema ne jodong joka Esau: Yawuot Elifaz ma wuod Esau makayo gin: Jaduongʼ Teman, Omar, Zefo, Kenaz,
16 Kora, Gatamu na Amaleki. Hawa ndio waliokuwa wakuu waliotoka kwa Elifazi huko Edomu, waliokuwa wajukuu wa kiume wa Ada.
Kora, Gatam kod Amalek magi e jodongo ma nyikwa Elifaz mane odak Edom; bende ne gin nyikwa Ada.
17 Wakuu wa wana wa Reueli, mwana wa Esau ni: Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa Reueli huko Edomu, waliokuwa wajukuu wa kiume wa Basemathi mkewe Esau.
Yawuot Reuel wuod Esau ne gin: Jaduongʼ Nahath, Zera, Shama kod Miza. Magi e jodongo ma nyikwa Reuel mane odak Edom; bende ne gin nyikwa Basemath chi Esau.
18 Wakuu wa wana wa Esau ambao mkewe Oholibama alimzalia ni: Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa mke wa Esau, Oholibama binti Ana.
Yawuot Oholibama ma chi Esau gin: Jaduongʼ Jeush, Jalam kod Kora. Magi ema ne jodongo mowuok kuom Oholibama ma chi Esau nyar Ana.
19 Hawa ndio waliokuwa wana wa Esau (ndiye Edomu), na hawa ndio waliokuwa wakuu wao.
Magi ema ne yawuot Esau (ma tiende ni Edom), kendo magi ema ne jodong-gi.
20 Hawa ndio walikuwa wana wa Seiri, Mhori, waliokuwa wakiishi katika nchi ile: Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana,
Magi ema ne yawuot Seir ja-Hori, mane odak e gwengʼno: Lotan, Shobal, Zibeon, Ana,
21 Dishoni, Eseri na Dishani. Hawa ndio wana wa Seiri huko Edomu waliokuwa wakuu kwa Wahori.
Dishon, Ezer, kod Dishan. Yawuot Seir gi, mane odak Edom ema ne jodong jo-Hori.
22 Wana wa Lotani walikuwa: Hori na Homamu. Timna alikuwa dada yake Lotani.
Lotan nonywolo: Hori kod Homam. Timna ne en nyamin Lotan.
23 Wana wa Shobali walikuwa: Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo na Onamu.
Shobal nonywolo: Alvan, Manahath, Ebal, Shefo kod Onam.
24 Wana wa Sibeoni walikuwa: Aiya na Ana. Huyu Ana ndiye aligundua chemchemi ya maji moto jangwani alipokuwa akichunga punda za Sibeoni baba yake.
Zibeon nonywolo: Aiya, kod Ana. (Ma e Ana mane ofwenyo thidhna mar pi maliet e thim kane oyudo okwayo punde wuon mare Zibeon.)
25 Watoto wa Ana walikuwa: Dishoni na Oholibama binti wa Ana.
Ana nonywolo: Dishon, kod Oholibama nyar Ana.
26 Wana wa Dishoni walikuwa: Hemdani, Eshbani, Ithrani na Kerani.
Dishon nonywolo: Hemdan, Eshban, Ithran kod Keran.
27 Wana wa Eseri walikuwa: Bilhani, Zaavani na Akani.
Ezer nonywolo: Bilhan, Zavan kod Akan.
28 Wana wa Dishani walikuwa: Usi na Arani.
Dishan nonywolo: Uz kod Aran.
29 Hawa ndio waliokuwa wakuu wa Wahori: Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana,
Magi ema ne jodong jo-Hori: Lotan, Shobal, Zibeon, Ana,
30 Dishoni, Eseri na Dishani. Hawa ndio walikuwa wakuu wa Wahori, kufuatana na makundi yao, katika nchi ya Seiri.
Dishon, Ezer kod Dishan. Magi ema ne jodong jo-Hori, kaluwore gi dhoutgi e piny mar Seir.
31 Wafuatao ni wafalme waliotawala Edomu kabla ya mfalme yeyote wa Israeli kutawala:
Magi e ruodhi mane orito piny Edom kane jo-Israel ne pod onge kod ruodhi:
32 Bela mwana wa Beori alikuwa mfalme wa Edomu. Mji wake uliitwa Dinhaba.
Bela wuod Beor nobedo ruodh Edom. Dalane maduongʼ niluongo ni Dinhaba.
33 Bela alipofariki, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosra akawa mfalme baada yake.
Kane Bela otho, Jobab wuod Zera mane ja-Bozra nobedo ruoth kare.
34 Yobabu alipofariki, Hushamu kutoka nchi ya Watemani akawa mfalme baada yake.
Kane Jobab otho, Husham mane oa e piny jo-Teman nobedo ruoth kare.
35 Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi, aliyeshinda Midiani katika nchi ya Moabu, akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Avithi.
Kane Husham otho, Hadad wuod Bedad, mane oloyo jo-Midian e piny jo-Moab nobedo ruoth kare. Dalane maduongʼ niluongo ni Avith.
36 Hadadi alipofariki, Samla kutoka Masreka akawa mfalme baada yake.
Kane Hadad otho, Samla ja-Masreka nobedo ruoth kare.
37 Samla alipofariki, Shauli kutoka Rehobothi ngʼambo ya Mto Frati akawa mfalme baada yake.
Kane Samla otho, Shaul ja-Rehoboth man but aora nobedo ruoth kare.
38 Shauli alipofariki, Baal-Hanani mwana wa Akbori akawa mfalme baada yake.
Kane Shaul otho, Baal-Hanan wuod Akbor nobedo ruoth kare.
39 Baal-Hanani mwana wa Akbori alipofariki, Hadadi akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Pau, na mkewe aliitwa Mehetabeli binti Matredi, binti Me-Zahabu.
Kane Baal-Hanan wuod Akbor otho, Hadad nobedo ruoth kare. Dalane maduongʼ niluongo ni Pau, kendo chiege niluongo ni Mehetabel nyar Matred, ma nyar Me-Zahab.
40 Hawa ndio wakuu waliotokana na Esau, kwa majina, kufuatana na koo zao na nchi zao: Timna, Alva, Yethethi,
Koro magi e jodong joka Esau gi nying-gi, kaluwore gi dhoutgi kod pinjegi: Timna, Alva, Jetheth,
41 Oholibama, Ela, Pinoni,
Oholibama, Ela, Pinon,
42 Kenazi, Temani, Mibsari,
Kenaz, Teman, Mibzar,
43 Magdieli na Iramu. Hawa ndio walikuwa wakuu wa Edomu, kufuatana na makazi yao katika nchi waliyoimiliki. Huyu ndiye alikuwa Esau, baba wa Waedomu.
Magdiel kod Iram. Magi ema ne jodong Edom, kaluwore gi dakgi e piny mane gikawo kaka margi. Ma e chal Esau, kwar jo-Edom.

< Mwanzo 36 >