< Mwanzo 35 >
1 Kisha Mungu akamwambia Yakobo, “Panda uende Betheli ukakae huko na ukamjengee Mungu madhabahu huko, Yeye aliyekutokea ulipokuwa unamkimbia Esau ndugu yako.”
2 Hivyo Yakobo akawaambia watu wa nyumbani mwake pamoja na wote waliokuwa naye, “Iondoeni miungu ya kigeni ile iliyoko katikati yenu, jitakaseni na mkabadilishe nguo zenu.
3 Kisha njooni, twende Betheli, mahali nitakapomjengea Mungu madhabahu, aliyenijibu katika siku ya shida yangu, ambaye amekuwa pamoja nami popote nilipokwenda.”
4 Kwa hiyo wakampa Yakobo miungu yote ya kigeni waliyokuwa nayo, pamoja na pete zilizokuwa masikioni mwao. Yakobo akavizika chini ya mti wa mwaloni huko Shekemu.
5 Kisha wakaondoka, na hofu ya Mungu ikawapata miji yote iliyowazunguka. Kwa hiyo hakuna aliyewafuatia wana wa Yakobo.
6 Yakobo na watu wote waliokuwa pamoja naye wakafika Luzu (ndio Betheli), katika nchi ya Kanaani.
7 Huko akajenga madhabahu na akapaita mahali pale El-Betheli, kwa sababu mahali pale ndipo Mungu alipojifunua kwake alipokuwa akimkimbia ndugu yake.
8 Wakati huu Debora, mlezi wa Rebeka, akafa na akazikwa chini ya mti wa mwaloni ulioko chini ya Betheli. Kwa hiyo pakaitwa Alon-Bakuthi.
9 Baada ya Yakobo kurudi kutoka Padan-Aramu, Mungu alimtokea tena na kumbariki.
Yaaq'ub Paddan-Arameençe siyk'alang'a Allah mang'us dyagu, xayir-düə huvu,
10 Mungu akamwambia, “Jina lako ni Yakobo, lakini hutaitwa tena Yakobo, jina lako utakuwa Israeli.” Kwa hiyo akamwita Israeli.
eyhen: – Yiğın do Yaaq'ub vodun. Həşdiyle valqa Yaaq'ubva ona'as deş. G'iyniyke şaqa yiğın do İzrail ixhes. İnəxüd mang'un do İzrail eyxhe.
11 Mungu akamwambia, “Mimi ndimi Mungu Mwenyezi, ukazae na kuongezeka. Taifa na jamii ya mataifa itatoka kwako, nao wafalme watatoka viunoni mwako.
Qiyğa Allahee mang'uk'le eyhen: – Gırgın əxəna Allah Zı vorna. Ğunab yiğna nasıl hexxee'e, geeb qee'e. Vake sa millet deş, geedın milletbı g'ales. Yiğne nasıleab paççaharıb vuxhesınbı.
12 Nchi niliyowapa Abrahamu na Isaki nakupa wewe pia, nami nitawapa wazao wako baada yako.”
İbrahimısiy I'saq'ıs huvuyn ç'iyebı Zı vasıd helesınbı. Valed qiyğa yiğne nasılıs heles.
13 Kisha Mungu akapanda juu kutoka kwake mahali pale alipozungumza naye.
Allah Yaaq'ubne k'anençe – yuşana'ane cigeençe ooqa ts'ıts'axhxhe.
14 Yakobo akasimamisha nguzo ya jiwe mahali pale Mungu alipozungumza naye, akamimina sadaka ya kinywaji juu yake, pia akamimina mafuta juu yake.
Yaaq'ubee Allah cuka yuşan hı'iyne cigee sa g'aye ulyoozaraa'a. Qiyğad Allahne doyule çilqa zeytunun q'ışiy kya'an k'ı'ı.
15 Yakobo akapaita mahali pale Mungu alipozungumza naye Betheli.
Yaaq'ubee Allah cuka yuşan hı'iyne cigayn do Bet-El (Allahın xav) giyxhe.
16 Kisha wakaondoka Betheli. Walipokuwa umbali fulani kabla ya kufika Efrathi, Raheli akaanza kusikia uchungu na alipata shida kuu.
Yaaq'ubiy cuna xizan Bet-Eleençe avayk'ananbı. Efratısqa hiviyxharang'a Raahileys uşax eyxhe. Uxooxang'a məng'ee xəppa k'ov ts'ıts'av'u. Məng'ı'n uxuy dağamda ılğeç'ee.
17 Alipokuwa katika shida hii katika kujifungua, mkunga akamwambia, “Usiogope, kwa sababu umempata mwana mwingine.”
Məng'ee k'ov ts'ıts'a'ane, uxooxane gahıl kumag ha'ane xhunaşşee eyhen: – Qimeeq'ən, vas meer dix ıxha.
18 Hapo alipopumua pumzi yake ya mwisho, kwa maana alikuwa akifa, akamwita mwanawe Benoni. Lakini babaye akamwita Benyamini.
Mana qeek'aniy vor, duxays Ben-Oni (yizde uts'urna dix) do giyxheng'a. Qiyğa dekkeme mang'un do badal hı'ı Benyamin (sağne xıleena dix) giyxhe.
19 Kwa hiyo Raheli akafa, akazikwa kando ya njia iendayo Efrathi (ndio Bethlehemu).
Raahile qeek'ana. Efratne (Bet-Lexemne) yəqqə mana k'eyxhı.
20 Juu ya kaburi lake, Yakobo akasimamisha nguzo, ambayo mpaka leo inatambulisha kaburi la Raheli.
Yaaq'ubee Raahileynee nyuq'nelqa sa g'aye giviyxhe. Mana g'aye g'iyniyne yiğılqamee Raahileyne nyuq'nel guts xhinne avxuna.
21 Israeli akaendelea tena na safari yake na kupiga hema mbele mnara wa Ederi.
İzrail mançe ark'ın, Migdal-Ederne şene aq'val çadır güvxü.
22 Wakati Israeli alipokuwa akiishi katika nchi ile, Reubeni mwanawe alikutana kimwili na suria wa baba yake aitwaye Bilha, naye Israeli akasikia jambo hili. Yakobo alikuwa na wana kumi na wawili:
İzrail maa'ar axvang'a, Ruven dekkıne nukarıka Bilyhayka g'ılexha. İzrailik'le man ats'axhxhen. Yaaq'ubuqa yits'ıq'vər dixniy vor.
23 Wana wa Lea walikuwa: Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Yakobo, Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari na Zabuloni.
Manbı Leaye vuxuynbıniy vob: Yaaq'ubna ts'erriyna dix Ruven, qihnanbıb Şimon, Levi, Yahud, İssaxariy Zevulun vuxha.
24 Wana wa Raheli walikuwa: Yosefu na Benyamini.
İnbıb Raahilee vuxuynbıniy vob: Yusuf, Benyamin.
25 Wana waliozaliwa na Bilha mtumishi wa kike wa Raheli walikuwa: Dani na Naftali.
İnsabıme Raahileyne nukaree Bilyhanee vuxuynbıniy vob: Dani, Naftali.
26 Wana waliozaliwa na Zilpa mtumishi wa kike wa Lea walikuwa: Gadi na Asheri. Hawa walikuwa wana wa Yakobo, waliozaliwa kwake akiwa Padan-Aramu.
Leayeyne nukaree Zilypaneeyib inbıniy vuxu: Qad, Aşer. Yaaq'ubus Paddan-Aramee vuxhayn dixbı inbı vuxha.
27 Yakobo akarudi nyumbani kwa baba yake Isaki huko Mamre, karibu na Kiriath-Arba (yaani Hebroni), ambapo walikuwa wameishi Abrahamu na Isaki.
Yaaq'ub Mamreeqa Kiryat-Arbenne (Xevronne) k'anyaqa, dekkıne I'saq'ne k'aneqa qarayle. İbrahimiy I'saq' Mamreab menne cigaynbı xhinne vuxha.
28 Isaki aliishi miaka 180.
I'saq'ee vəşşe molts'al sen hı'ı.
29 Kisha Isaki akapumua pumzi yake ya mwisho akafa, akakusanywa pamoja na watu wake akiwa mzee wa miaka mingi. Nao wanawe Esau na Yakobo wakamzika.
Mana ine dyunyeyle ats'ı q'əs qıxha qek'a. Mana dixbışe Esaveeyiy Yaaq'ubee k'eyxha.