< Mwanzo 35 >

1 Kisha Mungu akamwambia Yakobo, “Panda uende Betheli ukakae huko na ukamjengee Mungu madhabahu huko, Yeye aliyekutokea ulipokuwa unamkimbia Esau ndugu yako.”
Yn the mene tyme the Lord spak to Jacob, Ryse thou, and stie to Bethel, and dwelle thou there, and make thou an auter to the Lord, that apperide to thee whanne thou fleddist Esau, thi brother.
2 Hivyo Yakobo akawaambia watu wa nyumbani mwake pamoja na wote waliokuwa naye, “Iondoeni miungu ya kigeni ile iliyoko katikati yenu, jitakaseni na mkabadilishe nguo zenu.
Forsothe Jacob seide, whanne al his hous was clepid to gidere, Caste ye a wei alien goddis, that ben `in the myddis of you, and be ye clensid, and chaunge ye youre clothis;
3 Kisha njooni, twende Betheli, mahali nitakapomjengea Mungu madhabahu, aliyenijibu katika siku ya shida yangu, ambaye amekuwa pamoja nami popote nilipokwenda.”
rise ye, and stie we into Bethel, that we make there an auter to the Lord, which herde me in the dai of my tribulacioun, and was felowe of my weie.
4 Kwa hiyo wakampa Yakobo miungu yote ya kigeni waliyokuwa nayo, pamoja na pete zilizokuwa masikioni mwao. Yakobo akavizika chini ya mti wa mwaloni huko Shekemu.
Therfor thei yauen to hym alle alien goddis which thei hadden, and eere ryngis, that weren in `the eeris of hem; and he deluyde tho vndur a `tre, clepid therubynte, which is bihynde the citee of Sichem.
5 Kisha wakaondoka, na hofu ya Mungu ikawapata miji yote iliyowazunguka. Kwa hiyo hakuna aliyewafuatia wana wa Yakobo.
And whanne thei yeden, drede assailide alle men by cumpas of the citee, and thei weren not hardi to pursue hem goynge a wei.
6 Yakobo na watu wote waliokuwa pamoja naye wakafika Luzu (ndio Betheli), katika nchi ya Kanaani.
Therfor Jacob cam to Lusa, which is in the lond of Canaan, bi `sire name Bethel, he and al his puple with hym.
7 Huko akajenga madhabahu na akapaita mahali pale El-Betheli, kwa sababu mahali pale ndipo Mungu alipojifunua kwake alipokuwa akimkimbia ndugu yake.
And he bildide there an auter to the Lord, and clepide the name of that place The hows of God, for God apperide there to hym, whanne he fledde his brothir.
8 Wakati huu Debora, mlezi wa Rebeka, akafa na akazikwa chini ya mti wa mwaloni ulioko chini ya Betheli. Kwa hiyo pakaitwa Alon-Bakuthi.
Delbora, the nurische of Rebecca, diede in the same tyme, and sche was biried at the roote of Bethel, vndir an ook, and the name of the place was clepid The ook of wepyng.
9 Baada ya Yakobo kurudi kutoka Padan-Aramu, Mungu alimtokea tena na kumbariki.
Forsothe God apperide eft to Jacob, aftir that he turnede ayen fro Mesopotanye of Sirie, and cam into Bethel, and blesside hym,
10 Mungu akamwambia, “Jina lako ni Yakobo, lakini hutaitwa tena Yakobo, jina lako utakuwa Israeli.” Kwa hiyo akamwita Israeli.
and seide, Thou schalt no more be clepid Jacob, but Israel schal be thi name. And God clepide hym Israel, and seide to hym,
11 Mungu akamwambia, “Mimi ndimi Mungu Mwenyezi, ukazae na kuongezeka. Taifa na jamii ya mataifa itatoka kwako, nao wafalme watatoka viunoni mwako.
Y am God Almyyti, encreesse thou, and be thou multiplied, folkis and puplis of naciouns schulen be of thee, kyngis schulen go out of thi leendis;
12 Nchi niliyowapa Abrahamu na Isaki nakupa wewe pia, nami nitawapa wazao wako baada yako.”
and Y shal yyue to thee, and to thi seed after thee, the lond which Y yaf to Abraham, and Ysaac.
13 Kisha Mungu akapanda juu kutoka kwake mahali pale alipozungumza naye.
And God departide fro hym.
14 Yakobo akasimamisha nguzo ya jiwe mahali pale Mungu alipozungumza naye, akamimina sadaka ya kinywaji juu yake, pia akamimina mafuta juu yake.
Forsothe Jacob reiside a title ether memorial of stoonys, in the place where ynne God spak to hym, and he sacrifiede ther onne fletynge sacrifices, and schedde out oile,
15 Yakobo akapaita mahali pale Mungu alipozungumza naye Betheli.
and clepide the name of that place Bethel.
16 Kisha wakaondoka Betheli. Walipokuwa umbali fulani kabla ya kufika Efrathi, Raheli akaanza kusikia uchungu na alipata shida kuu.
Forsothe Jacob yede out fro thennus, and cam in the bigynnynge of somer to the lond that ledith to Effrata; in which lond whanne Rachel trauelide in child beryng,
17 Alipokuwa katika shida hii katika kujifungua, mkunga akamwambia, “Usiogope, kwa sababu umempata mwana mwingine.”
sche bigan to be in perel for the hardnesse of childberyng; and the medewijf seide to hir, Nyle thou drede, for thou schalt haue also this sone.
18 Hapo alipopumua pumzi yake ya mwisho, kwa maana alikuwa akifa, akamwita mwanawe Benoni. Lakini babaye akamwita Benyamini.
Forsothe while the soule yede out for sorew, and deeth neiyede thanne, she clepide the name of hir sone Bennony, that is, the sone of my sorewe; forsothe the fadir clepide hym Beniamyn, that is the sone of the riyt side.
19 Kwa hiyo Raheli akafa, akazikwa kando ya njia iendayo Efrathi (ndio Bethlehemu).
Therfor Rachel diede, and was biriede in the weie that ledith to Effrata, this is Bethleem.
20 Juu ya kaburi lake, Yakobo akasimamisha nguzo, ambayo mpaka leo inatambulisha kaburi la Raheli.
And Jacob bildide a title on the sepulcre of hir; this is the title of biriel of Rachel `til into present dai.
21 Israeli akaendelea tena na safari yake na kupiga hema mbele mnara wa Ederi.
Jacob yede fro thennus, and settide tabernacle ouer the tour of the flok.
22 Wakati Israeli alipokuwa akiishi katika nchi ile, Reubeni mwanawe alikutana kimwili na suria wa baba yake aitwaye Bilha, naye Israeli akasikia jambo hili. Yakobo alikuwa na wana kumi na wawili:
And while he dwellide in that cuntrei, Ruben yede, and slepte with Bala, the secundarie wijf of his fadir, which thing was not hid fro hym. Forsothe the sones of Jacob weren twelue;
23 Wana wa Lea walikuwa: Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Yakobo, Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari na Zabuloni.
the sones of Lia weren, the firste gendrid Ruben, and Symeon, and Leuy, and Judas, and Isachar, and Zabulon;
24 Wana wa Raheli walikuwa: Yosefu na Benyamini.
the sones of Rachel weren, Joseph and Beniamyn;
25 Wana waliozaliwa na Bilha mtumishi wa kike wa Raheli walikuwa: Dani na Naftali.
the sones of Bala, handmayde of Rachel, weren Dan, and Neptalym;
26 Wana waliozaliwa na Zilpa mtumishi wa kike wa Lea walikuwa: Gadi na Asheri. Hawa walikuwa wana wa Yakobo, waliozaliwa kwake akiwa Padan-Aramu.
the sones of Zelfa, handmayde of Lya, weren Gad, and Aser. These weren the sones of Jacob, that weren borun to hym in Mesopotanye of Sirie.
27 Yakobo akarudi nyumbani kwa baba yake Isaki huko Mamre, karibu na Kiriath-Arba (yaani Hebroni), ambapo walikuwa wameishi Abrahamu na Isaki.
Also Jacob came to Isaac, his fadir, in to Manbre, a citee Arabee, this is Ebron, in which Manbre Abraham `and Isaac was a pylgrym.
28 Isaki aliishi miaka 180.
And the daies of Isaac weren fillid an hundrid and foure scoore of yeris;
29 Kisha Isaki akapumua pumzi yake ya mwisho akafa, akakusanywa pamoja na watu wake akiwa mzee wa miaka mingi. Nao wanawe Esau na Yakobo wakamzika.
and he was wastid in age, and diede, and he was put to his puple, and was eeld, and ful of daies; and Esau and Jacob his sones birieden hym.

< Mwanzo 35 >